Mbowe: Niliona John Heche anapotea kisiasa, nikamteua Mjumbe wa Kamati Kuu

Mbowe: Niliona John Heche anapotea kisiasa, nikamteua Mjumbe wa Kamati Kuu

Heche tumsamehe, kaingia katika kundi ambako silo bila kujua athali zake binafsi za kisiasa.
Siasa za chuki, kudhalilishana, kusengenyana hazina afya kwa chama. Wajumbe tusaidieni genge hili likataeni kwa kauli moja kama tulivyoukataa ugonjwa wa ukoma miaka ile ya 70.
Unausungo wewe
 
Halafu kitu kibaya zaidi wafuasi wake wanasema Heche kaongea vizuri sana kwa kumuheshimisha yeye MWAMBA, lakini MWAMBA Mwenyewe anasema HECHE anamtukana.
Huyu Mzee kawehuka!

Anacheza michezo ambayo ya kijinga na anadhani ataonekana smart kumbe ni kuwehuka.

Kila ninapomsikiliza naona anaongea ujinga.

Kila anachoongea kisha nikimsikiliza na Lissu anachokiongea, huyu Mzee ni muongo!

Na ndiyo maana kakimbia mdahalo!
 
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, amesema aliamua kumteua John Heche kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho ili kumuepusha na hatari ya kupotea kwenye siasa za juu za chama.

Mbowe aemetoa kauli hiyo jana, Januari 17, 2025, wakati wa mahojiano maalum na wahariri na waandishi wa habari kutoka kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) jijini Dar es Salaam.

Mbowe amesema kuwa, nafasi yake kama Mwenyekiti wa chama ni kuhakikisha kuwa chama kinakuwa na viongozi wenye nguvu na uwezo wa kulijenga.

Pia amebainisha kuwa Heche, aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti na Mjumbe wa Kamati Kuu, alishindwa kurejea kwenye nafasi hiyo baada ya kushindwa na Esther Matiko katika uchaguzi wa kanda.

“Nikaona kwamba mtu huyu atapotea kwenye siasa za juu za chama. Kwa hiyo, Heche ndiye mtu pekee niliyemteua kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu kwa miaka mitano ambayo sasa inakaribia kuisha,” alisema Mbowe.

Kwa mujibu wa Mbowe, Katiba ya CHADEMA inampa Mwenyekiti nafasi ya kuteua wajumbe sita wa Kamati Kuu, nafasi ambazo mara nyingi huzijaza kwa uangalifu mkubwa.

Sambamba na hilo, Mbowe ameeleza kuwa alimuheshimu Heche kwa mchango wake na hivyo alimchagua tena kuwa Mjumbe wa Kamati ya Maridhiano wakati chama kilipokuwa kinashiriki mchakato wa maridhiano.

“Tulivyokuwa tunaenda kwenye maridhiano, Kamati Kuu ilinipa jukumu la kuchagua wajumbe wa kwenda nao, nikamchagua tena Heche,” alisema.

Hata hivyo, Mbowe ameelezea masikitiko yake kuhusu hatua ya Heche kutoa taarifa za uongo kuhusu mchakato wa maridhiano.

Miongoni mwa madai hayo ni kwamba wajumbe wa Kamati ya Maridhiano walikuwa wakilipwa Shilingi milioni tatu kwa kila kikao, madai ambayo yalikanushwa.

“Tulivyombana kuhusu kauli hiyo, Heche alisema alikuwa anatania tu. Lakini shutuma kama hizo ni za uongo na zinaweza kudhoofisha imani ya wanachama na umma kwa ujumla,” aliongeza Mbowe.

Mbowe alihitimisha kwa kusisitiza kuwa uongozi ndani ya chama unapaswa kuzingatia ukweli, mshikamano, na nidhamu, akionyesha dhamira yake ya kuendelea kulijenga chama kwa kushirikiana na viongozi wote.

Jambo TV
Hizo hoja mbona hakuzipeleka kwenye mdaharo.
Aache unafiki wa kiccm
 
Hatuwezi kuwapa chama watu wa fitna ambao hawathamini kazi walizofanya wenzao hadi chama kikafikia hapo kilipo.

NIDHAMU ndiyo inakwenda kummaliza Lissu kesho kutwa.
Sasa ataamua mwenyewe kubakia ama kuondoka, ila tunamshauri abaki ajirekebishe na ashiriki kuijenga CDM baada ya uhalibifu mkubwa alioufanya yeye wa genge lake.
Hizi hoja mbona hakuzipeleka kwenye mdaharo?
Mbowe anapenda umbea ndio maana anaogopa midaharo.
 
Huyu Mzee kawehuka!

Anacheza michezo ambayo ya kijinga na anadhani ataonekana smart kumbe ni kuwehuka.

Kila ninapomsikiliza naona anaongea ujinga.

Kila anachoongea kisha nikimsikiliza na Lissu anachokiongea, huyu Mzee ni muongo!

Na ndiyo maana kakimbia mdahalo!
Mbowe na watu wa CCM hawana utofauti, nimeelewa sasa kwa nini Wana CCM huwa wanasema wanatukanwa na vyama vya upinzani.
 
Kambi ya Mbowe mbona maharage yarukaruka sana juu ya sufuria la moto kwenye jiko lililokolea moto mkali?.
 
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, amesema aliamua kumteua John Heche kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho ili kumuepusha na hatari ya kupotea kwenye siasa za juu za chama.

Mbowe aemetoa kauli hiyo jana, Januari 17, 2025, wakati wa mahojiano maalum na wahariri na waandishi wa habari kutoka kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) jijini Dar es Salaam.

Mbowe amesema kuwa, nafasi yake kama Mwenyekiti wa chama ni kuhakikisha kuwa chama kinakuwa na viongozi wenye nguvu na uwezo wa kulijenga.

Pia amebainisha kuwa Heche, aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti na Mjumbe wa Kamati Kuu, alishindwa kurejea kwenye nafasi hiyo baada ya kushindwa na Esther Matiko katika uchaguzi wa kanda.

“Nikaona kwamba mtu huyu atapotea kwenye siasa za juu za chama. Kwa hiyo, Heche ndiye mtu pekee niliyemteua kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu kwa miaka mitano ambayo sasa inakaribia kuisha,” alisema Mbowe.

Kwa mujibu wa Mbowe, Katiba ya CHADEMA inampa Mwenyekiti nafasi ya kuteua wajumbe sita wa Kamati Kuu, nafasi ambazo mara nyingi huzijaza kwa uangalifu mkubwa.

Sambamba na hilo, Mbowe ameeleza kuwa alimuheshimu Heche kwa mchango wake na hivyo alimchagua tena kuwa Mjumbe wa Kamati ya Maridhiano wakati chama kilipokuwa kinashiriki mchakato wa maridhiano.

“Tulivyokuwa tunaenda kwenye maridhiano, Kamati Kuu ilinipa jukumu la kuchagua wajumbe wa kwenda nao, nikamchagua tena Heche,” alisema.

Hata hivyo, Mbowe ameelezea masikitiko yake kuhusu hatua ya Heche kutoa taarifa za uongo kuhusu mchakato wa maridhiano.

Miongoni mwa madai hayo ni kwamba wajumbe wa Kamati ya Maridhiano walikuwa wakilipwa Shilingi milioni tatu kwa kila kikao, madai ambayo yalikanushwa.

“Tulivyombana kuhusu kauli hiyo, Heche alisema alikuwa anatania tu. Lakini shutuma kama hizo ni za uongo na zinaweza kudhoofisha imani ya wanachama na umma kwa ujumla,” aliongeza Mbowe.

Mbowe alihitimisha kwa kusisitiza kuwa uongozi ndani ya chama unapaswa kuzingatia ukweli, mshikamano, na nidhamu, akionyesha dhamira yake ya kuendelea kulijenga chama kwa kushirikiana na viongozi wote.

Jambo TV
Duuuh!!! Jamaaa Kila kukicha sera yake ni namna alivyowasaidia wapinzani wake kwenye kinyang'anyiro hiki Cha uchaguzi.
 
Katika wapiga debe wa Lissu, ni Heche peke yake ndiye amekuwa akimpa heshima zake Mbowe. Pamoja na kumtaka apumzike, amekataa kumpaka matope. Amesema pia kwa uwazi tu kuwa mchango wa Mbowe ni muhimu na bado unahitajika. Ameonyesha ukomavu wa hali ya juu.
Mimi ningependa awe Makamu Mwenyekiti chini ya Mbowe ili 2030 agombee uenyekiti.
Bahati mbaya Wenje amechafuliwa mno na hana charisma ya Heche.
Kumchagua Heche na Mbowe kutakuwa hatua ya kwanza ya kutibu majeraha ya kampeni hii maana kila upande utakuwa na mtu wake. Alternative ya Lissu na Wenje haiwezi kufanya kazi vizuri kwa pamoja.

Amandla....


..Mbowe angekuwa pro-active namna hii wakati wa maridhiano, chama kisingetumbukia ktk matatizo waliyonayo.

..pia wakati umefika kwa yeye kama mgombea kuunga mkono mabadiliko yote aliyoyapendekeza Tundu Lissu.

..Tundu Lissu anaweza kuwa wrong katika uwasilishaji wa hoja zake, lakini hajakosea ktk uhalali wa hoja hizo.

..Jambo lingine ni kuacha mizengwe. Kuna malalamiko mengi ya Mbowe kuumiza wenzake. Suala hili limejirudia sana, Mbowe ajirekebishe.
 
Hatuwezi kuwapa chama watu wa fitna ambao hawathamini kazi walizofanya wenzao hadi chama kikafikia hapo kilipo.

NIDHAMU ndiyo inakwenda kummaliza Lissu kesho kutwa.
Sasa ataamua mwenyewe kubakia ama kuondoka, ila tunamshauri abaki ajirekebishe na ashiriki kuijenga CDM baada ya uhalibifu mkubwa alioufanya yeye wa genge lake.
Huyo lisu nae alikua apotezwe kwenye siasa za chadema, Mungu saidia akastuka, ndio yate haya yakatokea. Hata la Wenje na Abdu alikua haliweki wazi. Alopostukia sinema anayoletewa akacharuka.
 
Alimuhonga Ujumbe wa kamati Kuu 🐼
Kwahiyo Lowassa,Sumaye na Kingunge walihongwa.
Sijui kwanini unapenda kujizima data.
Mwenyekiti wa CDM ana nafasi sita za uteuzi wajumbe wa Kamati kuu.
Huko CCM mwenyekiti anateua Makamu mwenyekiti,Katibu mkuu,wajumbe wa kamati kifupi huko hakuna uchaguzi ni mwendo wa kuteuana tu.
 
Heche tumsamehe, kaingia katika kundi ambako silo bila kujua athali zake binafsi za kisiasa.
Siasa za chuki, kudhalilishana, kusengenyana hazina afya kwa chama. Wajumbe tusaidieni genge hili likataeni kwa kauli moja kama tulivyoukataa ugonjwa wa ukoma miaka ile ya 70.
Hilo kundi bila kuvuta bangi na kunywa ulanzi unatengwa.
 
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, amesema aliamua kumteua John Heche kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho ili kumuepusha na hatari ya kupotea kwenye siasa za juu za chama.

Mbowe aemetoa kauli hiyo jana, Januari 17, 2025, wakati wa mahojiano maalum na wahariri na waandishi wa habari kutoka kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) jijini Dar es Salaam.

Mbowe amesema kuwa, nafasi yake kama Mwenyekiti wa chama ni kuhakikisha kuwa chama kinakuwa na viongozi wenye nguvu na uwezo wa kulijenga.

Pia amebainisha kuwa Heche, aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Kanda ya Serengeti na Mjumbe wa Kamati Kuu, alishindwa kurejea kwenye nafasi hiyo baada ya kushindwa na Esther Matiko katika uchaguzi wa kanda.

“Nikaona kwamba mtu huyu atapotea kwenye siasa za juu za chama. Kwa hiyo, Heche ndiye mtu pekee niliyemteua kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu kwa miaka mitano ambayo sasa inakaribia kuisha,” alisema Mbowe.

Kwa mujibu wa Mbowe, Katiba ya CHADEMA inampa Mwenyekiti nafasi ya kuteua wajumbe sita wa Kamati Kuu, nafasi ambazo mara nyingi huzijaza kwa uangalifu mkubwa.

Sambamba na hilo, Mbowe ameeleza kuwa alimuheshimu Heche kwa mchango wake na hivyo alimchagua tena kuwa Mjumbe wa Kamati ya Maridhiano wakati chama kilipokuwa kinashiriki mchakato wa maridhiano.

“Tulivyokuwa tunaenda kwenye maridhiano, Kamati Kuu ilinipa jukumu la kuchagua wajumbe wa kwenda nao, nikamchagua tena Heche,” alisema.

Hata hivyo, Mbowe ameelezea masikitiko yake kuhusu hatua ya Heche kutoa taarifa za uongo kuhusu mchakato wa maridhiano.

Miongoni mwa madai hayo ni kwamba wajumbe wa Kamati ya Maridhiano walikuwa wakilipwa Shilingi milioni tatu kwa kila kikao, madai ambayo yalikanushwa.

“Tulivyombana kuhusu kauli hiyo, Heche alisema alikuwa anatania tu. Lakini shutuma kama hizo ni za uongo na zinaweza kudhoofisha imani ya wanachama na umma kwa ujumla,” aliongeza Mbowe.

Mbowe alihitimisha kwa kusisitiza kuwa uongozi ndani ya chama unapaswa kuzingatia ukweli, mshikamano, na nidhamu, akionyesha dhamira yake ya kuendelea kulijenga chama kwa kushirikiana na viongozi wote.

Jambo TV
Huyu John Heche au Wegesa Charles ni mhuni tu. Nimesoma nae SAUT (EDUCHE) 2006/2009 namjua na sio mtu wa kuamini hata kidogo.
 
Kwahiyo Lowassa,Sumaye na Kingunge walihongwa.
Sijui kwanini unapenda kujizima data.
Mwenyekiti wa CDM ana nafasi sita za uteuzi wajumbe wa Kamati kuu.
Huko CCM mwenyekiti anateua Makamu mwenyekiti,Katibu mkuu,wajumbe wa kamati kifupi huko hakuna uchaguzi ni mwendo wa kuteuana tu.
Kama Heche alishindwa huko Kanda sasa YEYE kumteua Kamati Kuu ndio aanze kumsimanga?
Mbowe ni Dini gani kwani? 🐼
 
Back
Top Bottom