Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 40,455
- 73,145
Tatizo sio RAIA kuwa na nani Bali ni kuwa wako sahihi na wanakoelekezwa? Rais anasema ugonjwa unaisha, lakini madereva wetu kwa idadi kubwa wakifika mipakani wanagundulika wagonjwa kwa nini?Kwa hilo la Covid 19 mheshimiwa Mbowe angekubali tu matokeo kwamba kazidiwa.Upamoja wa wananchi na raisi Magufuli katika hili ni ushahidi tosha kwamba Raia wapo pamoja na raisi wao.
Maadamu yeye mheshimiwa Mbowe alishalizungumza basi na aliache na hata km madhara yatakuwepo huko mbele atakuwa shujaa kwa sababu historia itamlinda.
Kwa yeye kuendelea kulisemea mara kwa mara italeta picha km analibeba hilo kama agenda ya kisiasa.
Na hao wote wanatoka kwenye jamii huku mitaani ambako hatupimwi!
US embassy wameonya RAIA wao kuwa hali ya Dar inatisha, nchi jirani wanafunga mipaka bado hatuamini, lakini tunamuamini Magufuli tokea huko mafichoni?
Sent using Jamii Forums mobile app