Hivi unafikiri Ripoti hiyo utaisoma muda huo huo Rais anapoisoma? Rais anapata taarifa mapema sana hivyo kuhoji Ripoti imetoka au laah ni kukosa maarifa kwenyewe.
Je, uliambiwa upimaji usingefanyika kipindi wanafanya huo uchunguzi?
Raia wa aina yako ndio laana ya nchi hii. Unaambiwa kuna tume inachunguza. Imemaliza kazi yake halafu unakuja kumshutumu mtu anayetaka tu kufahamu mambo yaliyojulikana! Unadhani utawahi kuhoji matumizi ya kodi unayolipa??
Umeambiwa vipimo ni feki. Ripoti ya tume ingeonesha ukweli au uongo wa hilo na tukajua kipi kinaendelea baada ya hapo. Toka tangazo la vipimo feki hata takwimu hakuna kwa sababu maabara ilifungwa kwa maelezo ya Ummy kuwa inafanyiwa ukarabati na wakati huo huo uchunguzi. Kweli kuhoji hili nalo ni jambo baya??
Raia wa hovyo sana wewe!!