Mbowe: Utawala wa Magufuli uliwatesa sana watu wa Kilimanjaro na Arusha!

Mbowe: Utawala wa Magufuli uliwatesa sana watu wa Kilimanjaro na Arusha!

Kuzuia mikutano ya nje ya vyama vya siasa ilikuwa ni moja ya sera yao?

Kusitisha mchakato wa katiba mpya ilikuwa ni moja ya sera yao?

Kuitupa kapuni sekta ya gesi kusini ilikuwa ni moja ya sera zao?
Uwe muelewa nimesema sera zao sasa hizo kama hazikuwa sera zao kwa nini uzilete?
 
Siku kiti Cha uwenyekiti kiamie Kanda ya Kati au hata kusini nitakuwa na imani na chdem ila kwa uchagaa huu hpn

Hawa ndugu zangu Ni makabila mbayaaa ukabila Na wabaguzi mbaya

Cdm chini ya mbowe Bado Sana [emoji38]
 
Kabila usilolipenda ndo unatoa huko mkuu wako wa usalama wa Taifa...mtu anaengalia usalama wako 24×7 kutoka kwa watu unaowachukia na kuwakandamiza...he must be crazy or tunayoambiwa ndo tuchanganye na zetu...
 
Sasa ndugu yangu Ile barabara ingepanuliwaje? You guys are so selfish, kwamba watanzania ni Bora tuwe na barabara ya sentimita mbili ili kuwanufaisha nyie?

..hakuna anayepinga barabara kupanuliwa.

..kinachopingwa ni kukataa kuwalipa fidia waliobomolewa nyumba zao ili kupisha mradi.
 
Kabila usilolipenda ndo unatoa huko mkuu wako wa usalama wa Taifa...mtu anaengalia usalama wako 24×7 kutoka kwa watu unaowachukia na kuwakandamiza...he must be crazy or tunayoambiwa ndo tuchanganye na zetu...
Yule ni mpare majina yasikupe jeuli tangu yule mpuuzi auwawe kipindi cha mkapa hakuna mchaga kupewa tena

USSR
 
Hii kauli ya Kiongozi huyu amekuwa akiirudia rudia sana naona kama haina afya kwa taifa!
Inabidi asamehe asonge mbele maisha ndo yalivyo! Yeye anaona utawala wa Magufuli uliwatesa lakini kuna watu hawaoni hivo!
Inabidi aondokane na hizi chembechembe za ubaguzi yeye kwanza!

Ukimkatia mchagga mirija ya upigaji, unakuwa umemtesa sana!
 
Tunataka Mbowe na CHADEMA watuambie watanzania watalifanyia nini taifa hili endapo watapata madaraka ya kuongoza nchi. Haya mengine ni utumbo kama utumbo!
 
Hii kauli ya Kiongozi huyu amekuwa akiirudia rudia sana naona kama haina afya kwa taifa!
Inabidi asamehe asonge mbele maisha ndo yalivyo! Yeye anaona utawala wa Magufuli uliwatesa lakini kuna watu hawaoni hivo!
Inabidi aondokane na hizi chembechembe za ubaguzi yeye kwanza!
Mbowe anaongea ukweli pamoja na kwamba sio wachagga tu japo wengi ni wao issue ni kwamba aliwachukia wafanya biashara wakubw walio chuma awamu zilizopita akiamini wezi hivyo ukiongea wafanya biashara kundi kubwa ni wao.ukweli usemwe mwendazake amevunja rekodi.kwamambo ya kikatili.
 
Hii kauli ya Kiongozi huyu amekuwa akiirudia rudia sana naona kama haina afya kwa taifa!
Inabidi asamehe asonge mbele maisha ndo yalivyo! Yeye anaona utawala wa Magufuli uliwatesa lakini kuna watu hawaoni hivo!
Inabidi aondokane na hizi chembechembe za ubaguzi yeye kwanza!
Unawezaje kuita ubaguzi ingali umesema asonge mbele huoni Kama wewe mwenyewe Kuna kitu hautaki kuadmit?

Kwanza tuweke mambo wazi Kama mama alivyosema then itasaidia sana kumove on sababu haitakuwa jambo jipya na ndipo kila mmoja wetu atakubaliana na hii suggestion yako kwamba he should move on otherwise ni ndoto za alinacha.

Mama mwenyewe alisema jambo la msingi ni kuponya makovu yaliyopo mioyoni mwa baadhi ya watu na kuunda umoja wa kitaifa Sasa ni vema mambo yawe wazi then mengine yanajadilika kuliko kubumba maneno tu wakati yanajulikana tu.

Kwani shida ipo wapi? Mbona yanazungumzika? Ila yakiendelea kubumbwa basi itaendelea hivyo na haitatusaidia kiukweli.

Ukweli ni kwamba kuna wakati siasa yetu ilienda mlama kidogo japo yanazungumzika tu.
 
Kabila usilolipenda ndo unatoa huko mkuu wako wa usalama wa Taifa...mtu anaengalia usalama wako 24×7 kutoka kwa watu unaowachukia na kuwakandamiza...he must be crazy or tunayoambiwa ndo tuchanganye na zetu...

..hiyo isikupe shida.

..kuna interahamwe walikuwa wameoa watutsi lakini hiyo haikuwazuia kushiriki mauaji ya halaiki.
 
Jitahidi kuvumilia ukweli hata kama unauma. Aliyekuwa anafanya huo uhayawani mliona yuko sawa, kwanini hamkumwambia matendo yake hayana afya kwa taifa?
Ni ukweli usiofichika Magufuli alwachukia sana na watu wa Kilimanjaro na Arusha

Chuki yake ilipitiliza kiasi cha kutamka akiwa Iringa ''....watu wa kaskazini sasa watusubiri''
Akapanda chuki nyingine watu wa kanda ya ziwa wakisema ''...ni zamu yetu''

Legacy ya Magufuli ni pamoja na kuvunja umoja wa kitaifa, kupanda mbegu za kikanda, kikabila na kuendekeza udini.

Marehemu Mkapa alimwambia kidiplomasia kupitia kitabu chake kwamba, alipomwambia Nyerere nani awe katika baraza lake Mwl alimjibu hatamshauri, isipokuwa atambue nchi ina makabila na dini tofuati na hilo azingatie. Magufuli hakuzingatia

Kile kinachoitwa ''kutumbua majibu' kilikuwa kiini macho tu, Magufuli alilenga makabila na dini na baada ya kumaliza hatukusikia tena kutumbua.

Katika watu waliojaribu sana kuvunja umoja wa kitaifa , mshikamano na upendo Magufuli alikuwa kiongozi wao, hilo lisemwe bila haya wala soni.

Kwasababu ya legacy yake hutawasikia watu wakizungumzia mambo kadhaa ikiwemo rekodi ya Utu, haki, utawala wa sheria, demokrasia, uhuru wa wananchi n.k. Utawasikia wetetezi wakizungumzia kajenga flyover n.k. kuficha madhaifu yake

Kwa miaka zaidi ya 20 Nyerere anachambuliwa , ni haki kumchambua Magufuli kwa mema na mabaya yake, si kutueleza flyover .

Pascal Mayalla JokaKuu
 
Mbowe sijui amepatwa na nini?!!!! Amebadilika sana kwani huko nyuma hakuwa hivyo kabisaaaa.

Hata hivyo mleta mada hayo maneno kayasema lini?!!!
 
Huoni kwamba magufuli alipenda watanzania wote? Ni ukweli zusiopingika kwamba kaskazini imeendelea Sana, Yani mkoa wa Kilimanjaro vijijini uko mbali kuliko manispaa nyingi Sana za mikoa mingine. Yamkini aliteleza lakini tumeshuhudia uboreshaji wa miundombini kaskanizi licha ya kwamba alisema msubiri kwanza. Hakuwahi kufika Nyasa lakini alipeleka meli na wala hakuahidi, Yule Mzee mumuache tu apumzike, amefanya makubwa Sana.
Hakuna cha kuteleza, alichokisema kilikuwa rohoni mwake na chuki hiyo aliendelea nayo muda

Rais wa nchi hapaswi kutoa maneno ya kuchochea chuki na ubaguzi , Magufuli alifanya kwasababu aliamini katika ubaguzi. Kiongozi wa nchi hawatambui Raia kwa ukanda, chuki ilimuongoza

Barua ya kujenga kiwanja cha Chato ilitamka wazi mkandarasi lazima we mtu wa kanda ya Ziwa

Rekodi ya Magufuli katika ubaguzi ni mbaya sana!

JokaKuu
 
Hii kauli ya Kiongozi huyu amekuwa akiirudia rudia sana naona kama haina afya kwa taifa!
Inabidi asamehe asonge mbele maisha ndo yalivyo! Yeye anaona utawala wa Magufuli uliwatesa lakini kuna watu hawaoni hivo!
Inabidi aondokane na hizi chembechembe za ubaguzi yeye kwanza!
Hata kama unasamehe, uovu lazima ujulikane, usemwe.

Ni vema maovu ya kupindukia yaliyofanywa na Magufuli yawekwe kwenye kumbukumbu kwaajili ya vizazi vijavyo ili mtu mwovu wa kiwango cha Magufuli, asitokee tena kwenye uongozi.

Uovu kama ule wa kuasisi magenge ya kuteka watu, kuua, kutesa na kuwabambikia kesi watu wanaomkosoa, ulikuwa ni unyama na ushetani wa hali ya juu ambao hauwezi kuwepo kwenye iliyostaarabika.

Magufuli amekwishapata msamaha wa asili kwa maana marehemu hashtakiwi. Wanaotaja maovu yake ni kwaajili ya kumbukumbu tu.

Kila mtu ana mapungufu yake, lakiniuuaji, utesaji, na kubambikia watu kesi siyo mapungufu bali ni uovu uliofuta mazuri machache aliyoyafanya.
 
Back
Top Bottom