Mbowe: Wabunge wamejiongezea Mishahara Kutoka Tsh milioni 13 za awali na sasa wanalipwa Tsh milioni 18 kwa mwezi mbali na posho

Mbowe: Wabunge wamejiongezea Mishahara Kutoka Tsh milioni 13 za awali na sasa wanalipwa Tsh milioni 18 kwa mwezi mbali na posho

Wakati ule akiwa bungeni alikuwa anapokea hiyo milioni 13 na yeye????? au hakukubali kupokea? Maana hakuna mkutano wowote aliwahi kusimama wakati ule na yeye ni mbunge akalalamika kuwa analipwa hela nyingi mno zipunguzwe.

Porojo za wanasiasa baaana![emoji38]

Swali la kijinga.

Hivi hata ukiwa ni wewe umeingia bungeni, ukakuta mshahara ni huo, utaacha kuupokea? Na ukiuacha itasaidia nini?

Lakini ukiingia huko, ukakuta mshahara ni huo, na ukaona kwa kuzingatia uhalisia wa nchi, siyo halali. Ukautangazia umma kwa uwazi, tayari umetimiza wajibu wako. Wanaotakiwa kuchukua hatua ni wenye pesa yao, ambao ni wananchi. Kama wao wanaona ni halali mbunge achukue 26m kwa mwezi na Rais 50m kwa mwezi, basi hakuna wakubadilisha.
 
Swali la kijinga.

Hivi hata ukiwa ni wewe umeingia bungeni, ukakuta mshahara ni huo, utaacha kuupokea? Na ukiuacha itasaidia nini?

Lakini ukiingia huko, ukakuta mshahara ni huo, na ukaona kwa kuzingatia uhalisia wa nchi, siyo halali. Ukautangazia umma kwa uwazi, tayari umetimiza wajibu wako. Wanaotakiwa kuchukua hatua ni wenye pesa yao, ambao ni wananchi. Kama wao wanaona ni halali mbunge achukue 26m kwa mwezi na Rais 50m kwa mwezi, basi hakuna wakubadilisha.
Acha mpigwe tu,subiri foleni uchafue kidole na wino uwachague tena

Ova
 
Mwenyekiti wa Chadema mh Freeman Mbowe amesema Wabunge wa Bunge la JMT wamejiongezea Mishahara kutoka TSH 13 million walizokuwa wanalipwa awali hadi TSH 18 million

Mbowe amesema mshahara huo ni mbali na Posho mbalimbali wanazolipwa kila Siku

Jumaa Mubarak 😀🔥

----
Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa Freeman Mbowe amedai kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamejiongezea mishahara yao kutoka milioni 13 waliyokuwa wanapata hapo awali hadi kufikia milioni 18 kwa mwezi, hiyo ikiwa ni nje ya posho ya vikao anayopatiwa Mbunge kila anapohudhuria kikao kimoja cha Bunge

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Machi 21.2024 Babati mjini, mkoani Manyara Mbowe amesema kuwa mara nyingi viongozi wa serikali wamekuwa wakijitokeza hadharani na kueleza kuwa uchumi umekua hapa nchini, jambo ambalo anakubaliananalo kwa kutumia kipimo cha pato la Taifa (GDP) lakini ameeleza kuwa uchumi huo umekua kwa watu wachache walioko serikalini na sio kwa mtu mmoja mmoja au jamii kwa ujumla wake

Amesema viongozi walioko serikalini wamekuwa wakiendekeza maisha ya anasa ambayo kwa kiasi kikubwa hayaangalii maslahi ya nchi na wananchi wake ndio maana inawawia vigumu kukubali kufanya marekebisho ya msingi ya sheria za nchi kutokana na msingi wa uwepo wa Katiba mpya

Ametolea mfano kupitishwa kwa sheria ya mafao ya wenza wa viongozi kama sehemu ya anasa hizo kwa kuwa sasa mwenza wa Rais mstaafu analazimika kupokea asilimia 60 ya mshahara wa Rais aliyeko madarakani, wakati Rais mstaafu akipokea asilimia 80 ya mshahara huo, hiyo ikienda sambamba na kupatiwa magari yanayobadilishwa kila baada ya muda, walinzi, nyumba na watumishi wengine binafsi.

Chanzo: Jambo Tv
wasaKj8I_400x400.jpg

Kweli PESA ni fitna asee jamaa angu.

huyu jamaa kipindi ni mbunge alikuwa sio wenge Sana.

CCM mrudisheni huyu jamaa bungeni
 
Mwenyekiti wa Chadema mh Freeman Mbowe amesema Wabunge wa Bunge la JMT wamejiongezea Mishahara kutoka TSH 13 million walizokuwa wanalipwa awali hadi TSH 18 million

Mbowe amesema mshahara huo ni mbali na Posho mbalimbali wanazolipwa kila Siku

Jumaa Mubarak [emoji3][emoji91]

----
Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa Freeman Mbowe amedai kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamejiongezea mishahara yao kutoka milioni 13 waliyokuwa wanapata hapo awali hadi kufikia milioni 18 kwa mwezi, hiyo ikiwa ni nje ya posho ya vikao anayopatiwa Mbunge kila anapohudhuria kikao kimoja cha Bunge

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Machi 21.2024 Babati mjini, mkoani Manyara Mbowe amesema kuwa mara nyingi viongozi wa serikali wamekuwa wakijitokeza hadharani na kueleza kuwa uchumi umekua hapa nchini, jambo ambalo anakubaliananalo kwa kutumia kipimo cha pato la Taifa (GDP) lakini ameeleza kuwa uchumi huo umekua kwa watu wachache walioko serikalini na sio kwa mtu mmoja mmoja au jamii kwa ujumla wake

Amesema viongozi walioko serikalini wamekuwa wakiendekeza maisha ya anasa ambayo kwa kiasi kikubwa hayaangalii maslahi ya nchi na wananchi wake ndio maana inawawia vigumu kukubali kufanya marekebisho ya msingi ya sheria za nchi kutokana na msingi wa uwepo wa Katiba mpya

Ametolea mfano kupitishwa kwa sheria ya mafao ya wenza wa viongozi kama sehemu ya anasa hizo kwa kuwa sasa mwenza wa Rais mstaafu analazimika kupokea asilimia 60 ya mshahara wa Rais aliyeko madarakani, wakati Rais mstaafu akipokea asilimia 80 ya mshahara huo, hiyo ikienda sambamba na kupatiwa magari yanayobadilishwa kila baada ya muda, walinzi, nyumba na watumishi wengine binafsi.

Chanzo: Jambo Tv
Na katika hali hii kima cha chini cha pensheni kwa wastaafu imebaki kuwa Tshs. 100,000/= kwa mwezi tangu utawala ya Kikwete 2015 - miaka 9 iliyopita. Tunaambiwa eti wataalam wanaangalia hesabu za mifuko ya pensheni kuona kama kuna uwezekano wa kufanya mabadiriko, ambayo kiutaratibu yanatakiwa kutekelezwa kila baada ya miaka mitatu. Mungu ibariki Tanzania.
 
Back
Top Bottom