Mbunge Garisa: Tanzania Walituchomea kuku,wakapiga mnada ng'ombe wetu

Tanzania Inafuata Utawala Wa Sheria
Kuku Hawakuingia Kwa Utaratibu
Huyo Aliyetaka Kuja Vodacom Hivyo Hivyo
Huyo mama wa Vodacom ilikuwa dharau kubwa kwa Tanzania .Mtu kasomea mambo ya vyakula halafu unampa kuwa Managing director wa kampuni ya Simu.Alichosomea haki match na role aliyotaka kupewa.Ndio Maana serikali ilimkataa.Kuku walichomwa Moto wasilete magonjwa yao Tanzania walikuwa hawakuwa na vibali vya Hali za afya zao.Huwezi safirisha kiumbe hai bila vyeti vya madaktari wa mifugo.Kwa hiyo huyo mbunge alitaka walete migonjwa yao ya midondo ya kuku Tanzania?
 
Kwa nini hasemi chanzo cha kuchomewa na kupigwa mnada vifaranga na ng'ombe ....!?
 
Tatizo kubwa kuhusu Kenya ni kwamba, they are ahead of us kwa kutumia akili zao. Sasa sisi tunataka kuwazidi kwa kuwavuta shati badala ya kutumia akili zetu
 
Dawa Alichoma Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
Imewaingia Sasa Hivi Wanahaha Tu
 
Inatakiwa tuwapige leo kule Egypt halafu ndo mjadala uendelee
 
Hata kama walichomewa kuku zao na hzo ng'ombe kupigwa mnada tz ilishawahi kuhamasisha kuwapiga wakenya??

Wekeaneni vikwazo vya kibiashara na si mambo ya kupigana,huo sio ustaarabu,ni ujinga
 
Hata tukisema kwa kejeli, haitaondoa ukweli kwamba kwa mujibu wa kanuni bora ya ujirani mwema, hata sisi hatukufanya vizuri sana katika mambo aliyotaja Mbunge. Tulisema sana kuhusu vifaranga vya kuku vilivyovhomwa moto, hata kama kulikuwa na ukiukaji wa sheria busara ingetuongoza kuwarudishia vifaranga vyao na siyo kuviteketeza. Kama tunaweza kuwarudishia wananchi wetu wanaokiuka kanuni za ufugaji tulishindwa nini kuwa waungwana na kuwapiga faini (kwa faida ya mahusiano) badala ya kupiga mnada?
Hata sisi tuna shida, tujisahihishe.
 
Huyo Slyvia Mulinge aliyekataliwa kibali kuwa Managing director wa Vodacom Tanzania ana digriii ya food science.Eti ndio walimleta awe mkurugenzi mkuu wa kampuni ya simu!!! Food sience na Telecommunication wapi na wapi.? Serikali iliona hawa Wakenya wanafanya Tanzania wajinga Fulani Tungempa tungeonekana kituko
 
Now if you say soo what is the role of EAC then? Do you mean we break it also?
 
Kumbe imeleta chuki
 
JK alishawahi kusema number one investor in Tz ni Kenya tusichezee uhusiano huu Kenya anatuhitaji kama sisi tunavyo wahitaji. Suala hilo la Voda ni kuwa tulimnyima Mkenya kibali lakini tukakubali Mmisri haileti maana vitu vingine, hutaki mgeni unataka Mtanzania sawa lakini mkenya NO ila mwingine wa mbali sawa inaleta shida hii kitu. EA ni lazima wafanye regulations ziwe clear kwa wote na ushindani uwepo kwa manufaa hatuwezi kufanikiwa dunia ya sasa bila kutegemeana kiuchumi sisi ni majirani na tutabaki kuwa majirani milele ni suala la kutafuta formula nzuri ya kuishi pamoja na hizi sheria zisiwe zinategemea nani raisi ziwe ni sheria umekuja umezipenda au hapana ishi nazo kama mbaya process ya kuchange iweshirikishi. kuwa watani sio jambo baya ni zuri kimaendeleo tushindane kwa kujenga lakini sio chuki lakini mimi sitaki kushangaa sana maana hata Tanzania bara tu tunachukiana na Zanzibar hatutaki kusema lakini huo ndio ukweli, sisi kama UK England wakicheza na team yoyote Scotland wanafurahi England afungwe japo wote ni UK sababu yako mambo hayatatuliwi yanabaki katika mioyo mwisho yanajenga chuki.
 
Mbunge anayo haki ya kutoa maoni.Wabongo wacha kelele Fika Nairobi city angalia pale sokoni owners wa biashara za pale mitaani wengi kutoka tz kama wale watu tunaita Juakali(machinga) nadhani utaelewa maana ya yule MP .Wakati wao wanamiliki biashara za magumashi bongo Watz wanamiliki biashara za halali pale Mombasa(wasambaa) Nairobi(Wachaga+ waarusha) sasa kumbukeni tu kuwa Wakenya wanaamini zaidi kwenye ajira na usomi kwa kifupi wanakawaida ya kujifungia kwenye msitu wa vitabu lah maskini kumbe maisha ya wanainch yanastawi kwenye biashara .Wakati wakija bongo wanataka ajira sisi tukienda Kenya tunatafuta wateja wa bidhaa zetu au zao wenyewe tunamake profit .Wao wako bize na vyuo vikuu kutafuta madigirii wabongo wapo bize na simple biznes .Si unajua tena kinachowauma zaidi shule zao bora kabisa ndiyo wanasoma watoto wetu kwa ada kubwa kabisa matokeo yakitika wanaonekana watoto wa tz wapo kwenye peak. Msijali wapendwa Rudini nyumbani kumenoga.
 
We kweli pimbi! Hata huelewi nini kinasemwa unakimbilia Chadema inaunga mkono mateso!
Hivi hivyo vichwa vyenu kweli vina ubongo au matope?
Tulisema mapema hapa hapa JF kuwa vitendo kama vile vya kuchoma vifaranga na kutaifisha mifugo vinasababisha utengano mkajifanya wabwiga, sasa matokeo ya chuki ndio yalianzia pale.
Wewe unakuja na nywi nywi nywi!
 
Kwani hayo yote yalifanyika kisheria? Je kwasababu ya hayo mambo ambayo unahisi serikali ya tz ilikosea ndo ushadie watanzania wenzako wasio wanasiasa wapigwe nchini Kenya ambao wengi ni wachaga wenzenu?
Eti wengi ni wachaga wenzenu!
Tukisema akili matope mnaona mnaonewa!
 
Kama wakenya wanabaguana wao kwa wao itakuwaje sisi ambao siyo RAIA wa Kenya? Huko Kenya kuna wanajamii walimkataa Headmaster wa shule Fulani kisa tu si mzawa wa eneo hilo.
 
Mshkaji wangu wewe bado hujatembea.
CRDB iko pale Nairobi wewe tu na hela zako.
Bidhaa Bora za Bakhresa ziko Kenya za kumwaga.
Kifupi. No research no right to speak.
 
Wangeleta fye ningeanza na huyu wa Tanzania oxygen anatelipwa 25m kwa mwezi.
He should have come to Tz n see how his fellow Kenyans are living lavishly. Kenyans in Tz are enjoying top jobs with big salaries and other fringe benefits. Most of these Kenyans have vowed not to go back home. They deem Tz to be their USA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…