Mbunge Shabiby: Wapigaji wameongezeka serikalini, sitasifia kila kitu

Mbunge Shabiby: Wapigaji wameongezeka serikalini, sitasifia kila kitu

Etwege

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2018
Posts
7,207
Reaction score
17,674
Mbunge wa jimbo la Gairo mh Shabiby, wakati akichangia hotuba ya bajeti kuu amemshukia kama mwewe waziri wa fedha Mwigulu Nchemba kuwa tabia yake ya kutaka kuwa mzuri kwa kila mtu na kila taasisi imesababisha awe na mipango mingi isiyo na tija kwa taifa ikiwemo hela kutopelekwa kwa wakati kwenye miradi na kulea mafisadi serikalini!

Mh Shabiby ameonya kuwa hayuko tayari kusifia kila kitu kwani kwenye serikali ya awamu ya 6 wapigaji wamekuwa wengi na wakitoka kuiba hela wanaenda kujisafisha kwa kumsifia mama anaupiga mwingi!!

Mh Shabiby amemuonya waziri Nchemba kuwa hatakuwa tayari kuona mafisadi wanalelewa kama mayai na atasema ukweli kwa wananchi.


Mbunge wa Shabiby akitoa mchango wake bungeni amedokeza namna wizi ulivyoenea kwa sasa nchini huku akimtaka Waziri wa Fedha kukaa pembeni kumpisha ikiwa kama kazi imemshinda. Akifafanua hoja hiyo Shabiby anasema:

Ukiwa waziri wa Fedha unatakiwa uwe ngangari kama umeshindwa niachie mimi nafasi nije nikae hapo, unafanya kazi nzuri lakini inabidi uwe ngagari kwenye hizi vitu. Mtu akitaka kuchukua pes, na kama ukitaka kuwa mzuri kwa kila taasisi hiyo kazi haiwezekani.
Nchi imefikia mahali ambapo sasa hivi lazima tuseme ukweli, wapigaji wamekuwa wengi. Wengine utasikia tu mama anaupiga mwingi, sio anaupiga mwingi kana kwamba anamsifia kwenye moyo, anaupiga mwingi yeye anaiba hela. Anatandika pesa halafu akija huku anasifia.
Mbunge wa Jimbo la Gairo Ahmed Shabiby akichangia hoja ya Bajeti Kuu ya Serikali Bungeni Jijini Dodoma amesema hayuko tayari kusifia Serikali kama vitu haviendi sawa na amesema atakuwa Mbunge wa kwanza kupinga bajeti hiyo endapo bajeti haitoongezwa Wizara ya Ujenzi na TARURA.

Shabiby amehoji pia kuhusu minada ya magari ya Serikali kutotangazwa hadharani akidai kuwa magari hayo yanauzwa kwa Watumishi kwa bei ya hasara.

“Mwaka jana ulisema Serikali inatumia zaidi ya bilioni 500 kuagiza magari lakini najiuliza hii Serikali ni tajiri sana au kuna shida gani umekuja ukalalamika na ukaleta mpango kwa kuondoa gharama hizo na kila Mtumishi atanunua gari lake ili alie na uchungu lakini najiuliza twende Halmashauri zote haya magari mabovu yanaoza mengine hayauzwi na yakiuzwa wanajiuzia wenyewe hii Nchi ina utajiri kiasi gani hadi haipigi mnada yale magari?, umewahi kusikia magari ya Serikali yanauzwa kwenye mnada?”
 
Hamna kitu kigumu maishani kama kuficha ukweli ulioko ndani yako ili kutetea ugali, roho itakusuta mwishowe utaongea tu ukweli.

Mpina anaanza kupata wafuasi taratibu..

Simply serikali ya mama Abdul ni ya hovyo, ilifanya mambo ya hovyo, na inaendelea kufanya mambo ya hovyo kila siku, huku mawaziri kama kina Mwigulu wakiwa ndio viongozi wa mambo hayo ya hovyo.

Kwa mtu mwenye akili timamu kutetea huu ujinga ni ngumu sana, unaweza kushangilia pale bungeni kwa kugonga meza lakini ndani ya nafsi yako unalia machozi, hauwezi kushangilia ufisadi unaofanywa na kina Bashe kwa watanganyika kisha unimbie una akili timamu, never.
 
Mbunge wa jimbo la Gairo mh Shabiby, wakati akichangia hotuba ya bajeti kuu amemshukia kama mwewe waziri wa fedha Mwigulu Nchemba kuwa tabia yake ya kutaka kuwa mzuri kwa kila mtu na kila taasisi imesababisha...
Kuna namna inabidi Mama aanze kuwapoteza watu katika mazingira ya kutatanisha kama mtangulizi wake la sivyo mambo yatakuwa magumu kabla na baada ya 2025.
 
Mwanangi unasemaje hapo Tlaatlaah

Ova
dosari, kasoro na changamoto za kimaadili kwa watumishi wa umma, mashirika ya kiraia, mashirika ya kidini kitaifa na kimataifa yapo, na kila uchao Serikali sikivu ya chama cha Mapinduzi itaendelea kung'ag'ana nao na wengine ambao wameshabainika wapo mahakamani,

na siku zote wito wa Serikali ni kwamba, kwenye mambo kama haya ya unadhifu kwenye rasilimali za umma, haitoshi kupiga kelele tu kwamba kuna upigaji mahali fulani ili upihiwe makofi na huku ukiunyamazia upigaji huuo bila kuripoti katika mamlaka zinazo husika, hiyo itakua ni kazi bure,

ni lazima pawe na jitihada binafsi na ushirikiano wa dhati, wa maneno na matendo kuanzia kwenye majimbo yetu, kuwasilisha vielelezo vya uthibitisho wa malalamiko yako ya upigaji kwenye taasisi na vyombo vya ulinzi na usalama vinavyohusika kushughulika na changamoto hiyo...

hata hivyo,
nampongeza sana Mh.Shabby ushauri mzuri kwa Serikali na kwa mchango wake, kwa kuchukizwa na baadhi ya watumishi wa umma, wasio waaminifu na wapiganaji mali ya umma kwa manufaa yao,
na kwa jinsi ambavyo, anawatumikia wananchi wa Jimbo la Gairo kwa uaminifu na bidii kubwa...

zaidi sana, nampongeza sana Mh.Shabiby,
kwa kuunga mkono, jitihada na hatua za makusudi, za chama na Serikali sikivu ya CCM, katika kuchochea, na kuwaletea maendeleo endelevu wanainchi wa Gairo kwenye maji, afya, elimu, kilimo, ufugaji, barabara, biashara na masoko n.k.🐒

kwako mrangi
 
Mbunge wa jimbo la Gairo mh Shabiby, wakati akichangia hotuba ya bajeti kuu amemshukia kama mwewe waziri wa fedha Mwigulu Nchemba kuwa tabia yake...
Shabiby Huwa hakopeshi,aliibua Ufisadi wa Kalemani Kupitia kuweka pgment Mafuta ,wizi wa Ewura nk.

Ingawa this time amekuwa too general ,alitakiwa awataje directly
 
Shabiby Huwa hakopeshi,aliibua Ufisadi wa Kalemani Kupitia kuweka pgment Mafuta ,wizi wa Ewura nk.

Ingawa this time amekuwa too general ,alitakiwa awataje directly
Hawezi kuwataja kwa majina muda hautoshi maana selikali nzima ni wezi
 
Hawezi kuwataja kwa majina muda hautoshi maana selikali nzima yawezi
Mbona Hawa aliwataja? 👇👇
Screenshot_20221119-094007.png
Screenshot_20221119-093841.png
 
Mbunge wa jimbo la Gairo mh Shabiby, wakati akichangia hotuba ya bajeti kuu amemshukia kama mwewe waziri wa fedha Mwigulu Nchemba kuwa tabia yake ya kutaka kuwa mzuri kwa kila,,,
Mwambieni HAMSIKILZI..
 
Back
Top Bottom