Mbunge Tarimba apendekeza TANESCO kufumuliwa na kuwepo kampuni 3 kwa ajili ya Uzalishaji, Usafirishaji na Ugawaji umeme

Mbunge Tarimba apendekeza TANESCO kufumuliwa na kuwepo kampuni 3 kwa ajili ya Uzalishaji, Usafirishaji na Ugawaji umeme

Nini hoja yako mkuu, TANESCO isigawanywe kwa sababu tu ikigawanywa kutakua na CEO watatu ?
Kwaiyo wewe hofu yako ni kwenye "vyeo" tu !
Hii hoja kuna mtu aliileta humu akasema wanapanga kuligawa kisha waliuze
 
Dili lingine linapangwa, ukigawa maana yake menejimenti tatu, hapo tayari umemuongezea mlaji gharama. Pili mafisadi yatapewa ugawaji maana ndiko faida iliko uzalishaji itaachiwa umma.
Kuna faida gani upate huduma duni kwa gharama ndogo?
Heri mara 100 uhudumiwe kwa gharama upate huduma bora.
Ufike wakati tufunguke macho.
Kwasasa umeme unakatika nchi nzima, huma mbovu...huoni ni hasara kwa taifa?.ma ceos ndio wanakutesa?
Watu wapate ajira, uzalishaji uongezeke na huduma ziboreke
 
Saiv wanawaza Dili tu..Magufuli alikosea sana zoa zoa yake imeleta matatizo makubwa
 
Financing ya hayo mashirika matatu itakuwaje?
Ni lipi litapokea malipo ya luku? Mzalishaji, msafirishaji ama msambazaji?
Swali lako la kwanza:
Kwa sababu ni mashirika ya umma, anaye finance anapaswa kuwa anafahamika. Ni serikali.

Lengo hapa sio kubana matumizi, ni kuongeza tija na ufanisi. Unaongeza bajeti ili huduma iwe bora na pato liwe kubwa zaidi kutoka katika huduma ya umeme kwa ujumla wake.

Zamani tulikua na kitu inaitwa SUMATRA, ikagawanywa tukapata LATRA na TASAC, bila shaka hujawahi kuuliza nani ana finance LATRA na TASAC, hivyo ndivyo itakavyokua (kama TANESCO ikigawanywa).

Swali lako la pili:
Nani atapokea malipo ya luku.
Kwa akili tu ya kawaida, kati ya kuzalisha (production), kusafirisha (transmission) na kusambaza (supply) umeme, kitendo kinachoshabihiana zaidi na mauzo (sales) ni KUSAMBAZA.
Nadhani nimejibu swali hili.

NB: Tunaomba ieleweke wazi kwamba tunao support kwamba TANESCO igawanywe sio kwamba tunataka ikigawanywa isiongezewe chochote, hapana. Tunapendekeza ikishagawanywa ipewe uwezo (watu, fedha, teknolojia na miundombinu) ili tuone matokeo chanya kwa maana kila shirika litawajibika kwa umma katika angle yake.

Leo maji yakipungua Mtera, (TANESCO), Mpesa inashindwa kununua umeme (TANESCO), bibi kalipa elfu 27 yake hajaunganishiwa umeme TANESCO, miti imeota kwenye njia kuu ya umeme kwenye milima ya Kitonga TANESCO, Kigoma hawajauganishwa na gridi ya taifa TANESCO, Wamakonde wameiba koki ya kwenye kisima cha gesi kwenye mtambo wa kuzalisha umeme TANESCO,

Kazi kwelikweli.
 
Hii hoja kuna mtu aliileta humu akasema wanapanga kuligawa kisha waliuze
Kama sababu ni hiyo, unadhani "wanashindwa" kuliuza zima zima ?

Wanamuogopa nani?

Hivi, mbona kama tunataka kujifanya wageni, tunawajua tunawasikia ?
 
Kuwa makampuni 3 ni gharama kubwa gharama za uendeshaji zitakuwa Mara 3 ya hizi.
 
5DE16616-CA39-4B9E-961C-97E891EC4685.jpeg


Hawa watu waache kukariri ya kwamba makampuni yote ya kuzalisha nishati nchi ambazo zina ushindani wa soko yamegawanya kuna mengine yanayafanya shughuli zote tatu wenyewe.

Kikubwa kwenye soko huria ni regulator na strategies za mashirika kutokana na uwezo wao wa kifedha, available infrastructure which gives startup business options mainly kwenye usambazaji so wanatumia miundombinu ya wengine.

Kushindwa kwa TANESCO ni management issues solely.
 
2. Kuliboresha kwa structure ambayo linayo sasa hivi. Kuliongezea uwezo kwa aspects nilizozitaja hapo juu na zaidi ili liweze kuongeza ufanisi

I get it very well. Kwanini mnalilia hiyo option ya kuligawa shirika na sio hiyo option yako ya pili? Kwani hayo maboresho ya Kufanya shirika liwe na ufanisi na tija zaidi ni lazima liwe vipande vipande? Hiyo technology unayosema , haiwezi kuwa adopted mpaka shirika liwe vipande vipande? Duniani kuna mashirika makubwa mara mbili ya TANESCO na yana ufanisi na na tija hivyo hiyo argument yako ya size is moot!!

Kuna jambo nyuma ya pazia ambalo hawa wahuni wameona huu ndio wakati wao muafaka wa kutimiza azma yao . Kwanini hawakuja na mawazo hayo miaka miwili iliyopita wakati huo tulikwisha anza kusahau shida ya mgao? They had to wait until when they artificially created the load shedding as justification for their intended plans!!
 
View attachment 2115355

Hawa watu waache kukariri ya kwamba makampuni yote ya kuzalisha nishati nchi ambazo zina ushindani wa soko yamegawanya kuna mengine yanayafanya shughuli zote tatu wenyewe.

Kikubwa kwenye soko huria ni regulator na strategies za mashirika kutokana na uwezo wao wa kifedha, available infrastructure which gives startup business options mainly kwenye usambazaji so wanatumia miundombinu ya wengine.

Kushindwa kwa TANESCO ni management issues solely.

Nakubalina na wewe na hizo energy management issues haziwezi kutatuliwa kwa kupeana kazi kishikaji!! Maharage hana uwezo wa kuliendesha shirika , kuendesha DSTV sio sawa na kuendesha TANESCO; these guys are jokers!!
 
Tuiboreshe TANESCO kwa kweli, whatever the means, vinginevyo tutazidi kumlalamikia tu J. Makamba kila kunapokucha.

Kuboresha shirika lolote lile linahitaji management yenye weledi ambayo utaipata kwa kuwashindanisha wataalam ili kupata the best among them; huwezi kufanikiwa kama utaajiri watendaji kwa ushikaji / upendeleo!! Maharage Chande is not the best that could be found in the country to head Tanesco.
 
Nakubalina na wewe na hizo energy management issues haziwezi kutatuliwa kwa kupeana kazi kishikaji!! Maharage hana uwezo wa kuliendesha shirika , kuendesha DSTV sio sawa na kuendesha TANESCO; these guys are jokers!!
TANESCO wanademi la trillion saba waulize wana mpango gani wa ku neutralise hilo deni wakiligawa shirika. What is their privatisation plan kumlinda mlaji against price hike and how exactly would such measures improve efficiency.

Hao watakao nunua hilo deni costs zake watapeleka wapi? Kwa sasa hizo hela zinalipwa na serikali TANESCO wasipotengeneza faida ndio maana bei ya umeme Tanzania inabaki chini, vinginevyo bei ya umeme ingekuwa shida kwa watu wenye kipato cha chini.

Mengine atakuyaongelea shida based on their priorities lakini from day ulijua jamaa ungaunga na anakwenda tengeneza matatizo zaidi kadri siku zinavyoenda; hizo posts zimo humu.

Uwezi kuwa na mtazamo huu leo wa kufikia lengo, mwezi ujao ukabadili strategy kufikia lengo hilohilo Inaonesha hana skills za kuandaa strategic plan ya kutatua ata tatizo la muda mfupi let alone mipango ya muda mrefu.

Mfano strategy ya kufungia watu umeme kwa kasi kila siku inabadalika leo utaambiwa issue ni subcontractors ilikuwa wapelekwe bunge linaondelea wajibu hoja kwanini wanachelewesha kazi, kesho tatizo tofauti hela mjini wanachangia kidogo, keshokutwa na sababu nyingine wana option kadhaa kwenye table including issue of bonds ndio watu wanavyoanda strategic plan zao za kibiashara ivyo; hamna kitu hapo.
 
I get it very well. Kwanini mnalilia hiyo option ya kuligawa shirika na sio hiyo option yako ya pili? Kwani hayo maboresho ya Kufanya shirika liwe na ufanisi na tija zaidi ni lazima liwe vipande vipande? Hiyo technology unayosema , haiwezi kuwa adopted mpaka shirika liwe vipande vipande? Duniani kuna mashirika makubwa mara mbili ya TANESCO na yana ufanisi na na tija hivyo hiyo argument yako ya size is moot!!
Kuna jambo nyuma ya pazia ambalo hawa wahuni wameona huu ndio wakati wao muafaka wa kutimiza azma yao . Kwanini hawakuja na mawazo hayo miaka miwili iliyopita wakati huo tulikwisha anza kusahau shida ya mgao? They had to wait until when they artificially created the load shedding as justification for their intended plans!!
Uko negative sana, unawaza kupigwa tu 24/7.

Kama kuna options mbili to a solution, haiwezekani watu milioni 60 wote tuka chagua option moja kama unavyotaka kulazimisha.

Wapo ambao wanadhani option A ni sahihi zaidi, wapo pia wanaodhani option B ni sahihi zaidi.

Usiwape dhambi wenye maoni tofauti, hii ni nchi mkuu. Otherwise ungekua pekeyako sasa nchi nzima ili ukifanya maamuzi yanakua ni ya kufanana.

Sijui unapata wapi ujasiri wa kumuuliza mwingine kwanini ana maoni X na sio maoni Y.

Mimi nadhani unachopaswa kuonyesha ni kwanini unadhani njia unayoiamini wewe ndio chaguo bora zaidi kuliko machaguo mengine yaliyobaki. Hoja yenye mantiki zaidi ndio inapaswa kushinda.

Kama unaamini TANESCO ya sasa (bila maboresho yoyote) ndio inatufaa zaidi, weka hoja zako mezani, kama zina mashiko tuendelee nayo hivyo ilivyo.

Kama unaamini TANESCO inatakiwa kuboreshwa bila kuigawa, weka hoja zako mezani, kama zina mashiko tuendee nayo namna hiyo.

Anayetaka igawanywe, anaweka hoja zake mezani, kama zina mashiko tunaenda mwelekeo huo.
Simple.

Halafu kuhusu suala la upigaji, hivi nani kakwambia "kupiga" pale TANESCO ni hadi tu itakapogawanywa ?
Kwamba ikiwa moja watu hawawezi kupiga ?

Kuhusu swala la kugawa taasisi ili kuwatafutia ulaji "ndugu zao", hii hoja sijui hata inatoka wapi...

Kwahiyo pale LATRA kuna MD ambaye ni binamu yake Tarimba ? Abdul Mkeyenge wa TASAC ni last born wa kwa kina Tarimba ?
Katibu mkuu ya wizara ya kina Nape ni dada yake Tarimba ?
Naibu waziri wa wizara ya kina Gwajima ni shangazi yake Tarimba ?

Sio sawa.
 
Kuboresha shirika lolote lile linahitaji management yenye weledi ambayo utaipata kwa kuwashindanisha wataalam ili kupata the best among them; huwezi kufanikiwa kama utaajiri watendaji kwa ushikaji / upendeleo!! Maharage Chande is not the best that could be found in the country to head Tanesco.
Here you are, ndio maana nilieleza hapo awali kwamba miongoni mwa maeneo ambayo tunatakiwa kuiboresha TANESCO ni hapo kwenye rasilimali watu (mengine ni teknolojia, miundombinu, fedha, n.k).

Kwanza ni idadi ya hao watu, pili ni ubora wao (tunawezaje kupata the best among all we have).

Lakini, hatuwezi kukaa hapa na kuaminishana kwamba TANESCO haina shida yoyote, itatufaa kwa mahitaji ya umeme ya Tanzania ya kesho (yenye viwanda vingi, treni za umeme, umeme kila kijiji na yenye "kuuza umeme" nje ya nchi) ila tu tatizo ni Maharage Chande. Au tatizo ni January Makamba. Au tatizo ni Samia Suluhu. Hii sio sawa.

Matatizo ya TANESCO hayata tatuliwa pekee kwa:
Magufuli kuwa "ndiye" Rais au Kalemani kuwa "ndiye" waziri au Titus Mwinuka kuwa ndiye MD au Idris Rashid kuwa ndiye MD...

Shirika linahitaji maboresho makubwa zaidi kuliko hao "mtu mmoja mmoja" hapo juu.
 
Ushauri :

Serikali iruhusu sector binafsi kampuni nyingi nchini kuzalisha Umeme Kisha kuiuzia serikali.

Kwenye mikataba kuwe na sheria za kulinda masilahi ya taifa , mfano mzarishaji ahakikishe anazarisha Umeme mda wote ,na ikizidi kwa mda flani kuwe na fidia kwa serikali kukwamisha mahitaji ya Umeme.

Pili kuruhusu watu wenye mitaji na technology ya juu na gharama nafuu , kusiwe na limit ya makampuni ,maana Umeme ukizidi tutauza mpaka nje ya nchi , lakini itachochea wawekezaji na makampuni mengi kutoka nje ya nchi na ndani kujenga viwanda vizito na hatimaye kukuza uchumi na ajira teletele.

Ni Mambo yanayo wezekana yakisimamiwa vizuri
 
Hizi story hata zitto alishawahi kuzipiga bungeni miaka ya nyuma. Hii ni ajenda ya hawa mabepari ili wapate tenda zao. Siungi mkono hoja ya kulimega vipande Tanesco. Mashirika yote yaliyomegwa mfano TTCL na Posta yote yana underperform. Sanasana waliuza tu asset kwa bei rahisi basi.
 
Hizi story hata zitto alishawahi kuzipiga bungeni miaka ya nyuma. Hii ni ajenda ya hawa mabepari ili wapate tenda zao. Siungi mkono hoja ya kulimega vipande Tanesco. Mashirika yote yaliyomegwa mfano TTCL na Posta yote yana underperform. Sanasana waliuza tu asset kwa bei rahisi basi.
Tanesco ibaki Kama ilivyo na kujiendesha Bali makampuni mengine ya kuzalisha tu ya saini mikataba ili kuongeza nishatiya umeme nchini
 
Kuna faida gani upate huduma duni kwa gharama ndogo?
Heri mara 100 uhudumiwe kwa gharama upate huduma bora.
Ufike wakati tufunguke macho.
Kwasasa umeme unakatika nchi nzima, huma mbovu...huoni ni hasara kwa taifa?.ma ceos ndio wanakutesa?
Watu wapate ajira, uzalishaji uongezeke na huduma ziboreke
Ungekuwa uko makini ungejua sababu ya huduma duni.

Kukusaidia kidogo chanzo cha huduma duni ni ufisadi unaofanywa na wenye dhamana. Ufisadi huo uliasisiwa mwaka 1991 . Tangu wakati huo TANESCO haijawahi kuachwa ifanye majukumu yake kitaalam, manunuzi yote wanaagizwa wapi wanunue kipi na hata muda gani wanunue plus hiyo mikataba mibovu. TANESCO ilipumua kidogo wakati wa JPM .

Kwa hiyo hata ikikatwa vipande vitatu bado huduma zitazidi kuwa ghali na mbovu sababu kile kipande chenye hasara cha generation kitaachiwa umma, distribution ambacho kiko safe kwa faida hicho watapewa mafisadi na ndio wanachokitaka ndio maana hizi kelele zimeanza ni well calculated move. Kipande cha kati cha transmissiion nacho watakichukua mafisadi pia. Kila stage itanunua na kuuza kwa kuongeza bei ili ipate faida sasa fikiria hapo unit moja mpaka inakufikia wewe mlaji utainunua shilingi ngapi? Usisahau gesi inayotumika huko chini kuzalishia umeme ni ghali tayari sababu nayo iliuzwa kifisadi.
 
Mbunge wa Kinondoni, Tarimba Gulam Abbas amehoji ikiwa Serikali haioni ni muda mwafaka wa kulifumua Shirika la Umeme (TANESCO) ili kuwe na Kampuni tatu kwa ajili ya kufanya Generation Uzalishaji, Usafirishaji na Usambazaji kama ilivyo Nchi nyingine.

Akimjibu, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kukatwa na kutolewa kwa maeneo hayo kwa watu tofauti kunaweza kuleta athari kwenye Usalama wa Nchi pale Umeme unapohitajika wakati wote na mmoja ya waliopewa jukumu awe anaenda kinyume na mipango, hivyo malengo kushindwa kufikiwa.

Amesema kwa Hali iliyopo Nchini, maeneo yote ya Uzalishaji umeme yanaendelea kufanya hivyo lakini changamoto ni miundombinu ambayo hata sasa inapeleka baadhi ya maeneo kukatiwa Umeme.
Tarimba yupo very smart sn kwenye hoja zake
 
Back
Top Bottom