Elections 2010 Mbunge wa Arusha apigwa hadi kuzirai na jeshi la polisi

Elections 2010 Mbunge wa Arusha apigwa hadi kuzirai na jeshi la polisi

Pamoja na kwamba sipendi wanajamvi wanaochochea wakiwa nje ya nchi, hii ya lema imeniuma kama kidole kilichobanwa na mlango. Nadhani binafsi niko tayari
 
Giza likizidi, .....
Hakuna marefu.....
Azimio la Arusha....
Mahakama ya kimataifa ipo....,


Mungu usiache mwaka huu upite....


Amina.
 
Hali inazidi kuwa tete nchini.. sidhani kama huko tunakoelekea ni salama!
 
Moshi mjini miaka ya nyuma CCM ilisumbua sana na madiwani wao kwani jimbo lilikuwa chini ya mbunge toka CHADEMA;
Mwaka huu tuliwafanyia kitu mbaya kwa kuwapa CHADEMA viti 17 na CCM viti 4, CCM wako baridi ile mbaya.

Arusha mwaka 2015 CCM ifutwe.
 
Jamani usanii mwingine ni mbaya sana. Mkurugenzi wa jiji aliwatangazia madiwani wote wakiwamo wa CCM kwamba kuna semina baada ya kutokubaliana kuhusu mamluki kutoka Tanga lakini baadae CCM wao wakaitana baadae Chadema wakshangaa kuwa wako peke yao ktk semina, wakakimbilia Manispaa wakakuta CCM wenzao na yule wa TLP wameshafanya uchaguzi na kujipa umeya na kumpa wa TLP Unaibu
 
Jamani usanii mwingine ni mbaya sana. Mkurugenzi wa jiji aliwatangazia madiwani wote wakiwamo wa CCM kwamba kuna semina baada ya kutokubaliana kuhusu mamluki kutoka Tanga lakini baadae CCM wao wakaitana baadae Chadema wakshangaa kuwa wako peke yao ktk semina, wakakimbilia Manispaa wakakuta CCM wenzao na yule wa TLP wameshafanya uchaguzi na kujipa umeya na kumpa wa TLP Unaibu
is this legal?
 
kabisa . ukijumlisha wajumbe wa ccm na huyo wa tlp tayari wanapata zaidi ya 50% kwahiyo huyo meya ni wa halali kabisa kisheria

Bucho huo uhalali unatoka wapi wakati hawajafanya kikao kilichotimia idadi?
 
Mbona mmezidi kulalamika sana na hakuna watu ambao wako tayari kuchukua hatua? Tumelala sana na kuona kwamba kama tukitoka kwenda kudai haki zetu TUTAONEKANA WAHAINI SIYO KWELI LAZIMA KUWE FREEDOM FIGHTER AMBAO TUTAWEKA HISTORIA tumezidi kujitetea na woga wetu na kuishia kulalamika na kuandika mambo marefu ya manung'uniko tu.

Hapa Arusha kuna watu wa marika mbalimbali watatuelewa tu na dunia nzima itakuwa nyuma yetu.

Kila mtu anaweza kupanga hata tukio moja kwa kusanya vijana kama 10 mpaka 20 ambao watakuwa wasiri na wakafanya matukio ya kuchoma moto na kuharibu mali za serikali pamoja na ofisi za chama tawala na atayeleta mdomo apewe hata kilema cha maisha.

Hii inatia uchungu na hasira za kutosha mtu yeyote mzalendo wa kweli unaibua mpaka magonjwa yaliyo lala kama vidonda vya vya tumbo na hata shinikizo la damu kwa nini tunanyanyasika nchini mwetu??????????
 
Mkuu Jasusi, tokea lini CCM wakazingatia uhalali na sheria? Rais wao kachakachua mchana kweupe na ameanikwa ktk magazeti lkn kauchuna. Hawana aibu!
 
I hope Anna Makinda atasema kitu in defence ya Lema juu ya hili! Naamini kabisa Sitta pamoja na UuCCM wake angefyatuka. Tukikubali wabunge wawe wanapigwa.....!
 
Hatimaye naona tanzania inaelekea kutufia mikononi. Hivi hivi wengine walianza hivi.
 
SOON TOTAINGIA VITANI

VISASI VYA HUYU JAMAA JK NDO UNATUPELEKA PABAYA

I HATE YOU ALL OF my LIFE

Huu ni unyama Mungu anakuona na mafisadi wako
 
Watanzania tumezidi kuwa soft mno, yaani hata wanaume wazima/watu wazima wananynganywa hivi hivi? Kama habari ndo hiyo na bado tunalia basi tunyamaze tu, soft soft haiwezi kuwafikisha popote.
 
Nimesikitishwa sana na taarifa hizi chafu. Serikali ya nchi yetu inaruhusu na kufagilia vitendo vya kikatili na vya kihuni vya Polisi kupiga watu. Mara zote Polisi wanapopiga watu hakuna kemeo na kuwajibika kokote kule kwa Polisi hawa. Mara ya mwisho kulipotokea uwajibikaji ilikuwa Mwaka 1976 ambapo Mwinyi na Marehemu Siyovelwa walipowajibika kutokana na kuuawa kwa mahabusu kule Shinyanga. Vilevile mwaka huo maofisa wengi wa Polisi walipoteza kazi zao. Baada ya hapo mambo ni mtindo mmoja. Ukitaka kupanda cheo fanya ukatili ndivyo ambavyo Mahita alipata cheo cha kuwa Mkuu wa Polisi kwani alimpiga Mrema mabomu mwaka 1995.

Raisi Kikwete wakati anapinga mgomo wa wafanyakazi alisema kuwa yeye ni mpole lakini sio polisi na kuwa Polisi imeundwa ili ifanye kazi ya kutumia nguvu. Hivyo akahalalisha matumizi ya nguvu. Wanafunzi wa vyuo vikuu wakigoma polisi wanatumia nguvu na kuwapiga. Mauaji ya Zanzibar polisi walitumia nguvu hakuna aliyewajibika wala kuadhibiwa. Vifo vya mahabusu kule Mbeya RPC alikuwa Said Mwema, akahamishwa kwenda Nairobi ili watu wasahau na baada ya hapo hivi sasa ni IGP. Huo ndio uwajibikaji wa Tanzania. Serikali inaamini kuwa Watanzania tuna kumbukumbu fupi kama kuku au hatuna kumbukumbu kabisa kama maji ya mto. Hivyo baada ya muda mfupi tutasema yaliyopita yamepita tugange yajayo.

Sasa huu uhuni na ukiukaji wa haki za binadamu ambao umefanywa Arusha nani anaweza kuuvumilia? Mtu ambaye ana dhamira hai na ambaye anamuogopa Mungu hawezi kuvumilia awe ni mfuasi wa CCM au wa ushindani. Kwani vitendo kama hivi ni vya kuiabisha nchi yetu na vinataka kutupeleka pabaya. Sasa kama hata mbunge anapingwa kama kibaka (sisemi kuwa vibaka wanatakiwa kupigwa wala kuuawa kama ambavyo bahati mbaya imekuwa ikitokea) je mwananchi wa kawaida si ndio hamna kitu. Hivyo ninawataka watu wote wale wenye dhamira hai na nia njema kwa majaliwa ya nchi yetu kukemea kwa nguvu zote vitendo hivi vya polisi wa Arusha na Jeshi zima la Polisi. Vitendo vyao ni ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu usioweza kuvumilika.

Kwa upande wa Chadema ni lazima wachukue hatua zote za kisheria na kisiasa kupambana na wale wote walioshiriki katika kuvuruga uchaguzi huo na kupigwa na kuumizwa kwa Mbunge Lema. Ni lazima wahakikishe kuwa madaktari wa kuaminika ndio wanamfanyia uchunguzi na kumpa matibabu. Kwani mara nyingi Polisi huwa kwanza hawatoi fomu ya P.F3 na vilevile ushinikiza madaktari wasiandike dawa zozote zile katika cheti cha mgonjwa anayetokana na kupigwa na kuumizwa na Polisi. Mwaka 1992 tukiwa Chuo Kikuu Dar es Salaam tulipogoma tukipinga kuchangia gharama za elimu mwenzetu mmoja alishikwa na kupigwa na polisi akalazwa Muhimbili. Tulipokwenda kumwangalia tulikuta cheti chake cha kwenye kitanda kina jina tu lakini hakuna hata dawa iliyoandikwa licha ya kuwekewa chupa za maji. Manesi walituita pembeni na kusema tumshauri mwenzetu huyo kuwa atoroke pale kwani kilichokuwa kinaandaiiwa si kizuri.

Cha mwisho Ndugu Lema ni lazima afungue kesi za madai na fidia dhidi ya wale wote waliompiga kuanzia kwa huyo Mkurugenzi wa Manispaa. Askari ikiwa ni pamoja na huyo RPC wa hapo Arusha. Anatakiwa awashtaki katika unafsi wao kwani kufanya vitendo vya kuvunja sheria hakulindwi na mamlaka yao. Hakuna cha suluhu katika hilo na kama msaada wa kisheria najua Wanasheria wengi watatoa nami ni tayari kutoa.
 
Jana tulionya kuhusu watu madiwani wa CHADEMA kutokujihusisha na kitendo chochote kitakachoruhusu uchaguzi ufanyike bila wao kuwepo. Uchaguzi sasa umefanyika na CCM wamechukua Halmashauri na hiyo imetoka.

Diwani wa TLP tayari sasa keshapata unaibu meya.

Narudia tena nilosema jana, CCM wanapotaka kitu na wewe ukaweka mizengwe, ama watakuhamisha, au watakuundia kesi ulale ndani wafanye wanavyotaka au watakutuma usafiri nje ya nchi au watakulaza hospitali kwa nguvu hata kama huumwi ila wapitishe wanachotaka. Nia ya CCM ilikuwa ni kuhakikisha walau madiwani wawili wa CHADEMA hawaingii kwa kikao na hilo wamefanikiwa.

CHADEMA mnapoona kuwa mnaelekea kushinda, mjitahidi sana kutokuwa na hasira. Muepuke kumshikia manati kuku wenu kwani wapita njia wanaweza wakapiga mayowe wakifikiri ni vibaka. Kila jambo lifanyiwe uchunguzi wa kina. Epukeni kumkimbiza kichaa alowanyanganya taulo. CCM inajifanya kichaa ili uikimbize watu wakushangae wakati yenyewe inakamilisha mambo yao. Ukirudi wameshamwaga maji yako na sabuni wamechukua.

Wameuchukuaje wakati takriban nusu ya madiwani ni wa chama pinzani? Ina maana kuwa huyo Naibu Meya atakuwa kila wakati anawapigia kura waliompa kula? Safari ndiyo imeanza.

Amandla......
 
Back
Top Bottom