Mbunge wa Geita Vijijini atunukiwa Udaktari wa heshima, sasa kuitwa Dkt. Joseph Kasheku

Mbunge wa Geita Vijijini atunukiwa Udaktari wa heshima, sasa kuitwa Dkt. Joseph Kasheku

hii mambo imesababishwa na wasomi wetu hasa walioko kwenye siasa na mifumo kushindwa kuonyesha maana ya elimu waliyosoma kwa vitendo matokeo yake jamii kufikia kudharau elimu na kuona sio kitu maana haina msaada zaidi ya kukufanya kuwa mwanasiasa na kubwabwaja tu pale mjengoni...

Msukuma kwa muda aliokaa bungeni kila akijipima ubavu na wasomi walioko mule anaona wako sawa tu kichwani hakuna namna kaamua kujitunuku tu hiyo heshima....
 
Sasahivi hakuna haja ya kusoma sana..tafuta hela tu udaktari waheshima unaupata hata ukiwa jinga.

Hata hivyo tanzania maprofesa au madaktari Phd wengi ni vilaza hawana tofuti na msukuma..

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rekebisha sio Phd bali ni udaktari wa heshima. Phd ni lazima uandike andiko la kiutafiti ulitete mbele ya maprofesa kulingana na vigezo vya nadharia ulizotumia lipite ndio upate PhD. Kifupi PhD lazima uisomee,udaktari wa heshima unatunukiwa na chuo kikuu kinachotambulika duniani kulingana na kazi fulani ulioifanya kwa jamii ikakupa heshima
Ila si anaitwa daktari ama..halafu kutunukiwa manake umefanya mkubwa.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanasiasa wanapenda sana shortcut katika elimu haswa katika level ya masters na Doctrate

Sasa uyo Msukuma kafanya jambo gani haswa mpaka katunukiwa huo ujinga
 
Mbunge wa Geita (CCM), Joseph Kasheku Msukuma leo jumapili jijini Dodoma, anatunukiwa Udaktari wa Heshima katika siasa na uongozi kutoka Chuo cha Academy of Universal Global Peace cha Marekani. “hiki ni chuo cha kimataifa na sasa naitwa Dkt. Msukuma.” https://t.co/Xq4n4BrSAl
View attachment 2033988
Hiko chuo kimejiharibia big time. Hivi kweli Msukuma ni wa kumpa digrii ya heshima? Kwa jambo lipi alilolifanya kwenye siasa? Vyuo vingine ni vya kipumbavu sana.
 
FF2oBTUXoAIM4lc.jpeg

angalieni hicho chuo kilichotoa hiyo degree
 
Hii nchi tutageuka kuwa kama Nigeria sasa. Kwani mtu lazima uwe na PhD au iutwe dokta ndiyo uhesimike? Au uonekane ni msomi? Why?

Kuanzia mwendazake, waziri wa fedha, madini, mazingira n.k.
Kuna nini huko kwenye udktari?
 
Back
Top Bottom