TANZIA Mbunge wa Jimbo la Konde Zanzibar, Khatib Haji afariki Dunia

TANZIA Mbunge wa Jimbo la Konde Zanzibar, Khatib Haji afariki Dunia

Alikuwa mchangiaji mzuri sana bungeni,poleni wabunge,poleni Watanzania wote,poleni ndugu wa marehemu.
 
Msimtwishe Zitto zigo la kujifia kwa chadrama
Chadema imekufa???toka lini mkuu??nijuavyo aliedhamilia kuiuwa Chadema yeye ndio katangulia,wewe uko wapi??chama kiko mioyoni mwa watu.
 
Kuna dalili zote Second Wave imeshaanza, uzuri Rais Samia kasema tupambane na huu Ugonjwa Kitaalamu na sio Kisiasa.
Hiyo wave ya tatu sasa, tena mbaya zaidi ni hii ya India inaondoa watu vibaya sana.
 
TheMbunge wa Jimbo la Konde Ndugu, Khatib Haji wa Chama cha ACT Wazalendo, amefariki Dunia. Umauti umemfika katika Hospitali ya Rufaa ya Muhimbili akipatiwa matibabu Alfajiri ya leo.

Khatibu aliwahi kuwa Mbunge wa Konde kupitia Chama cha Wananchi CUF mwaka 2010 hadi 2020. Alishawahi kushika nafasi ya Waziri wa Kilimo Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mwaka 1984 hadi 1987

Katika Bunge hili la 12, Khatib amekuwa Mbunge wa tatu kufariki tangu Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020. January 21 2021 Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Mkoa wa Manyara, Martha Umbulla alifariki dunia na Feb 12, 2021 Mbunge wa Jimbo la Muhambwe, Mkoa wa Kigoma Atashasta Nditiye alifariki Dunia baada ya kupata ajali ya gari.

View attachment 1791420
Mbunge wa Jimbo la Konde Ndugu, Khatib Haji

View attachment 1791491

Screenshot_20210520-110503~3.png


Taarifa za tarehe ya leo kuhusu covid-19​
 
Apumzike kwa amani.

Wenye lao jambo watasema wanakufa ili kuchagiza iletwe chanjo.

Yaani kwao mwendazake huyu ni halali wa chanjo.

Hiiiiii bagosha!
 
Pumzika kwa amani mbunge, kama kuna kuonana huko salamu nyingi kwa Maalim Seif.
 
Kwani Ndungai amepata chanjo mbona Corona inampitia pembeni badala ya kumnyookea moja kwa moja?
 
Zipo wapi hizi takwimu?kwenye tovuti ya wizara au?

Sent from my TECNO K8 using JamiiForums mobile app
Hizi ni takwimu ambazo zinatoka moja kwa moja kutoka Shirika la Afya duniani, yaani WHO.

Kuna Website Link Home ambayo unaweza kujiunga na kupata taarifa hizi kupitia namba yako ya simu ya WhatsApp.

Sijafahamu vizuri kwa upande wa TANZANIA, hali ni ikoje! Jinsi ya kujikinga na kupata taarifa mpya dhidi ya maambukizi ya COVID-19.

Lakini mimi binafsi nilipata hii huduma nikiwa Uwanja wa Ndege wa Entebbe nikijaribu kwenda Johannesburg [☺️☺️☺️]. Ilinibidi nisitishe safari yangu kwa sababu ya COVID-19.

Jaribu tena hii Website Link ya WHO Avaa WhatsApp ambayo ni mfumo wa kiotomatiki. Unaweza kujiunga na kupata taarifa mpya dhidi ya maambukizi ya COVID-19 kupitia namba yako ya simu ya WhatsApp.
 
Hizi ni takwimu ambazo zinatoka moja kwa moja kutoka Shirika la Afya duniani, yaani WHO.

Kuna Website Link Home ambayo unaweza kujiunga na kupata taarifa hizi kupitia namba yako ya simu ya WhatsApp.

Sijafahamu vizuri kwa upande wa TANZANIA, hali ni ikoje! Jinsi ya kujikinga na kupata taarifa mpya dhidi ya maambukizi ya COVID-19.

Lakini mimi binafsi nilipata hii huduma nikiwa Uwanja wa Ndege wa Entebbe nikijaribu kwenda Johannesburg [[emoji3526][emoji3526][emoji3526]]. Ilinibidi nisitishe safari yangu kwa sababu ya COVID-19.

Jaribu tena hii Website Link ya WHO Avaa WhatsApp ambayo ni mfumo wa kiotomatiki. Unaweza kujiunga na kupata taarifa mpya dhidi ya maambukizi ya COVID-19 kupitia namba yako ya simu ya WhatsApp.
OK,asante kwa maelezo

Sent from my TECNO K8 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom