Elections 2015 Mbunge wa Jimbo la Monduli, Julius Kalanga (CHADEMA), ajiuzulu na kuhamia CCM

Elections 2015 Mbunge wa Jimbo la Monduli, Julius Kalanga (CHADEMA), ajiuzulu na kuhamia CCM

NISAIDIE NAMBA ZAKE MZEEE NIJIKWAMUE

Nakuuliza; Una cheo chochote hata cha kufagia chooni pale ufipa?? Kupata namba zake kama una cheo itisha tu Press useme, Mimi flan bin/bint flan kiongozi wa kaya moja tu huku cdm nataka kurudi nyumbani ccm pamoja na familia yangu ya watu 2. Kabla ya saa moja tu kuisha, bwana pole atakuwa mlangoni mwako. Siku hizi ana mpaka dream liner achilia mbali tuk tuk
 
Aondoke na ubunge wake, hawa wanasiasa ifike muda wawe na huruma kwa wapiga kura. Waache kuchezea pesa za walipa kodi. Huu ni unaa wa hali ya juu.
 
2015 Kalanga hakuona serikali ya CHADEMA ikiundwa; halikadhalika 2016 na 2017. 2018 nusu imeshakatika ndio anagundua hawataunda serikali tena. Anatimkia kuliko na serikali. Hivi mnatufananishaje WATANZANIA...., mazuzu flani hivi au?
Unahamia CCM kwa madai kwamba ulidhani 2015 CHADEMA wangechukua nchi na ungekuwa serikalini...

Hii ina maana kwamba siku CCM ikiwa upinzani utahama CCM utahamia tena kweny chama ambacho kitakuwa kimeshika dola..

Waitara juzi pamoja na mambo mengi alisema atarudi Ukonga akiwa Waziri kamili..

Haka kajamaa Karanga nako kanasema kalitegemea 2015 wataunda Serikali..

Two MPigs speaking the same thing halafu unashindwa kuelewa hii premeditated narrative?

#UchuWaMadaraka

Naheshimu Haki yake ya Kikatiba.
 

Attachments

  • IMG_1186.JPG
    IMG_1186.JPG
    36.2 KB · Views: 24
Last edited:
Mwenzio Waitara kahama leo kesho yupo kwenye timu ya campaign
Na wewe tunakusubiri kwenye jukwaa la campaign za CCM maana umeandaliwa.
 
Tumeshawaambia chadema siku nyingi, hizo siasa za kupinga kila kitu siyo za kistaarabu na haziwezi kuwasaidia chochote. Matokeo yake ndo haya wabunge wanajiondoa ili kuepuka kuonekana ni wasaliti kwa chama kwa kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali ili kuleta mabadiliko nchini. Usingizi wa siasa za chuki za #lissumsaliti zitawamaliza.
 
When imbeciles are pretending to be idiots...kama nchi tumefikia astronomical levels za upumbavu. Kutumia fedha za walipa kodi kununua wanasiasa uchwara halafu unazoa fedha nyingine unaitisha chaguzi mshenzi za marudio. maisha yanazidi kuwa magumu kwa watu masikini, hii mijitu haijali kabisa.
 
Huyu mbunge sijaona alichofanya monduli. Nimekaa monduli 3 years hamna kitu alichofanya.kila kitu hovyo. Watu wamejaa majungu tu hamna kipya.hata asingehama chadema 2020 asingepata ubunge.bure kabisa.
Kamanda, una mifano ya wabunge waliofanya cha maana kwenye maji mbona yao?
 
Kuna haja ya wanazuoni wa kimataifa si hawa wa bongo kuja kuitafiti aina mpya ya siasa tunayoiendesha hapa tz ni kwa faida ya vizazi vijavyo..lakini tanzania ni ya pili kwa vivutio vya utalii duniani si mbaya kuongeza utalii wa siasa pia
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Viongozi wa upinzani hasa Chadema wanajisahau kuwa wao sio sawa na mwenyekiti wa CCM.
Mwenyekiti wa CCM na wale wa vyama vya upinzani ni kama mbingu na ardhi.
Mwenyekiti wa CCM akiwalazimisha wanachama wake kupigia kura bajeti analenga kutimiza malengo ya serikali yake.
Lakini wale wapinzani kila mwaka wanalazimishwa kupinga bajeti bila kutuambia wanataka ipitishwe ipi ?
Yani wanataka nchi isiwe na bajeti au wanataka nini na uchache wao?

Mwenyekiti wa Chadema akimbana Mwanachama wake wakati mwingine mtu anaona isiwe tabu naweka maisha yangu rehani halafu bado nabughudhiwa na kutishwa tishwa na mtu asiye na teuzi zaidi ya viti maalum.
Mwenyekiti wa CCM akimtishia mtu ujue kweli mtu anapata tabu sana mana fursa zote za nchi hii zipo mikoni mwake. Sasa mwenyekiti wa Chadama ana nini cha kumtishia mtu mpaka mtu aufyate?

Mbowe ajaribu sasa kusikiliza watu wa maeneo mengine nje ya wale wa waliomzunguka ambao wanaangalia maslahi yao kwanza.
Vinginevyo chama kitapukutika kabisa.
Watanzania hawana uelewa huo wanaoufikiria wapinzani.
Wengi wanaamini kuwa juhudi za Mh. Rais zinavunja nguvu ya vyama vya upinzani. Watapinzani wamejisaha kabisa.
Ngoja wabunge wao waishe ili wajipange upya.
Zipi?
 
Hatua gani..!?
Wananchi wenyewe wameridhika tena wanashangilia kama ushabiki wa simba na Yanga. Wewe mwenye akili zako ndiyo unafikiria kuchukua hatua ipi?
Wenzako kwanza wanafikiri budjet yote ni pesa ya Magufuli anatoa mfukoni kwake ndiyo maana kila mtu akiwa ma shida anaomba muheshimiwa raisi amsaidie.
Ahante ndege wenzio wanajua ni pesa ya Magufuli kutoka mfukoni kwake. Sasa watu kama hao kuwashauri inawezekana kweli?
 
Wananchi wenyewe wameridhika tena wanashangilia kama ushabiki wa simba na Yanga. Wewe mwenye akili zako ndiyo unafikiria kuchukua hatua ipi?
Wenzako kwanza wanafikiri budjet yote ni pesa ya Magufuli anatoa mfukoni kwake ndiyo maana kila mtu akiwa ma shida anaomba muheshimiwa raisi amsaidie.
Ahante ndege wenzio wanajua ni pesa ya Magufuli kutoka mfukoni kwake. Sasa watu kama hao kuwashauri inawezekana kweli?
Elimu ndo tatizo hapa Tanzania..wengi hawajielewi..!
 
Back
Top Bottom