Mbunge wa Kahama Mjini ashauri Vyuo Vikuu kuwajibika kutafuta ajira kabla ya kusajili Wanafunzi

Kwani kutafuta degree ni lazima? Hiyo ni hiyari ya mtu. Kwa nini iwe tukose wote? Tutazifuata nje ya nchi!
Kwa hiki kiburi wewe huwezi kuwa wanaoongelewa na kishimba! You are free mzee! Sababu nyie ndio mnaosisitiza tutafte namna ya kuishi in informal ways!
 
watu wanapewa uanajeshi miezi 9 tu.

hii elimu yetu ina shida somewhere.
 
Sure ana hoja sn, elimu yetu haina maana yoyote, afisa utumishi anasoma miaka 3 kuja kupandisha watu madaraja, ruhusa, likozo na barua za kustaafu kazi ambayo hata mlinzi ukimuelekeza ataifanya kwa ufanisi sn. Over
Yani utendaji unachukua 1% ya mafunzo yote hapo ndipo inaposhangaza! Kimsingi yanayofanywa na wengi huko makazini yanaweza kufanyika na mtu yeyote yule ambaye ana akili timamu tu ambayo inaweza pokea training! Unakuta mtu ana cheo kazi yake kupiga muhuri na sign tu na kumuamuru secretary amchapie barua 😂😂😂! Zaidi na zaidi atakaa kwenye vikao na semina za kulipana posho! Sasa hili nalo linahitaji degree? Kuna mtu wa la 7 hawezi haya? Na ndio maana wana jeuri ya kutuona wenye degree ma hayawani tu!

Ndio maana std 7 wengi walijazana na kufoji vyeti vya form 4 ila still wameweza kuwa productive tu kwa miaka mingi sana kabla ya kufurushwa! Na yote hio kutokea ni sababu ya ufinyu wa ajira kwa vijana.
 
Sasa huu ulioandika wewe sindio ushuzi wa dengu kabisa!

Wewe toa suggestion kama hoja unayosimamia mbadala ya Kishimba maana degree za uchumi zipo tunaziona zinauza juisi za miwa tu wakati tulitarajia ziende BOT zikashauri mambo ya kiuchumi! Nafasi hizo hamna.

Je, mtu anahitaji degree kukamua juisi ya miwa? Amepoteza miaka takribani 17 kuja kukamua juisi ya miwa ambapo angeweza kuanza hio kazi miaka 10 nyuma! Ni muda kiasi gani amepoteza katika maisha yake kwa miaka 10 nzima!
 
Hatarin na nusu, ukweli ukitoa field ya madaktari, computer programmers na wengine wachache, elimu yetu haina faida yoyote zaidi ya makaratasi.
 
Hizi ndio suggestion ambazo zinatakiwa ziendane na hoja ya kishimba sio ulalamishi na povu la jamaa wanaodai sijui mwamba ni tajiri kwa njia ovu! Hayo hayahusiani we want suggestions
 
Hatarin na nusu, ukweli ukitoa field ya madaktari, computer programmers na wengine wachache, elimu yetu haina faida yoyote zaidi ya makaratasi.
Kweli kabisa halafu kuna mbuzi mbuzi wanakuja kushupaza shingo eti ooh elimu ni muhimu! Elimu ilio muhimu ni ile ya kujitambua ama UPE (Universal Primary Education)! Elimu ya utawala hizi za degree hazina mashiko kama huna pa kuipeleka ukatawale! Kazi ikiwa hamna na degree haina mantiki yeyote utauza ubuyu tu na kukaanga bisi kama la 7!

Na kwa asilimia kubwa mie ndio naona UPE ina apply katika maisha ya kila siku kuliko hata zile nyinginezo za degree!
 
Huyo Kishimba hoja zake za kudharau elimu ziko na msukumo wa kwamba yeye hakusoma lakini ana hela. But I tell you historia yake ya kupata hela hizo inahusisha umwagaji damu.

Angekaa kimya tu Ila mawazo yake hayana maana
Acha wivu!

Kishimba kakupa mtihani wewe kama msomi, Umjibu kisomi, anauliza....!

Ni nani aliyesema Kwamba, ubongo wa Mwanadamu bila kufundishwa mwaka mmoja Kwa somo moja hauwezi kushika na kuelewa?

Je, kusomea manunuzi ni lazima iwe miaka mitatu?

Je, kuna aliyefanya liseach ya hayo akafahamu uwezo wa ubongo wa Mwanadamu kuwa masomo ya kusomea manunuzi, ili mtu aelewe inahitajika asomee miaka mitatu ni Nani huyo?

Acheni kubisha kila kitu, fanyieni kazi hayo wasomi wetu muone kama hatukingizwa chaka na mkoloni
 
Huyu mbunge hayuko serious kabisa
 
Kiongozi inashangaza sn mtu anaitwa Engineer hawezi hata kupaka rangi jiko lake, mpaka unajiuliza miaka 4 yote chuo alikuwa anafanya nini? anachojua ni BOQ pekee
 
Hahahaha ndio maana nikasema awali wanaoponda hoja za mzee kishimba watakuwa on the advantaged side! Mtu yuko UDSM ana lecutre anapokea 2M au zaidi kwa mwezi lazma amuone kishimba mwehu flani! Degree inakuwa na maana kama unaifanyia kazi mahali na kulipwa pesa ya kuridhisha.

Ila wanaozunguka juani na bahasha for 4 years in a row na kazi hakuna! Wazazi wameuza asset wakijua wanakukomboa ni msiba kwa kweli. Hamna mzazi mwenye nia njema asiyependa mwanae aendeshwe kwenye STK. Hawa ndio wanamuelewa vizuri kishimba!
 
Anajadili kitu cha msingi kwa hisia binafsi badala ya utafiti kwanza.

Anaichukulia taaluma kwa 1+1=2 kitu ambacho siyo sawa.
Unataka utafiti, amesema na akakutaka wewe kama msomi, useme, ni kivipi ubongo wako pasipo kukaa chuo miaka mitatu ukisomea manunuzi huwezi kuelewa? Fanyia utafiti Hilo wewe kama msomi
 
Hata Veta itafikia mahali itakuwa inatapika watu hawana michongo maana mafundi wakizidi kitaani unafikiri kitachotokea ni nini?
At least sasa tunaongea lugha moja. Mpaka wakati wa JK Madaktari wote walikuwa wanaajiriwa na Seikali na Hospitali binafsi. Lakini Mwendazake miaka 5 hakuajiri, amaekazana na kununua bombardier na kununua wabunge! Still demand ya Madaktari nchini bado ni kubwa, Serikali haikuona kuwa ni priority

Leo tunasahau chanzo cha tatizo na tunaanza kuponda elimu yetu nzuri. Na tunamshangilia Msukuma wa Darasa la 7, eti ana point?? CRAZY
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…