Mc Pilipili utanisamehee kwa ukweli huu "huna kipaji cha kuchekesha"

Umenifurahisha sana, ushasema MC, au nikupe kirefu chake ni Master of Ceremony. Na kazi yake kuu ni kuwa mshehereshaji sio mchekesheji, unajua mchekeshaji yeye uandaa igizo liwe lefu au fupi litakalo wachekesha watu, na mc hupewa ratiba ya matukio linaanza hili, litafuata hili na la mwisho ni hili. Sasa kile kipindi cha kusubili tukio lianze, au ule muda watu wametulia kimya yeye kazi yake ni kufanya watu wasiboleke na tukio zima. Sasa basi mc hutoa vitu kichwani hapo hapo, vingine atabicopy yaani ni kazi ngumu kuliko unavyofikili. Nonachokuona hukuwa na nia mbaya, ila ulikuwa hautofautishi mc na comedy. Nikutakie jumamosi njema.
 
NAUNGA MKONO HOJA ..SIO WOTE WAMEBARIKIWA KATIKA FANI FULANI
 
Huyo jamaa hata akialikwa studi, huwa anateka show kwa kupiga makelele utadhan mic ipo mail moja.
 
Kiujumla stand up comedy wa bongo hawachekeshi ila wanaelezea matukio afu wanakufosi ucheke, kwa sababu wanaanza kucheka wao kabla ya wanaochekeshwa, kenya, nigeria na uganda kidogo wametupiga bao ukiwachek omondi, pablo, kansiime, basket mouth.

Bora utafute cd ya majuto kuliko hao kina pilipili
 
Nakubaliana na wewe mkuu,naona kundi la haters wanavomuunga mkono mwenzao
Hata mimi mkuu naamini kwenye mafanikio maadui wengi... Ukiwa unapambana watakwambia kila la heri..Mungu akubariki lakini ukifanikiwa sasa wanaanza kuchukia mafanikio yako!! Ndio binadamu tulivyo
 
Expensive mc,we songa mbele tu boresha kazi kuza brand basi,Haters tubaki tunaumia tu
 
Siku ya kwanza kumfahamu huyu jamaa ilikuwa kwenye clip moja ambapo alikuwa MC kwenye harusi. Kichekesho chake kilikuwa kizuri sana na kilinivutia sana. Kilihusu wadada kunata kuolewa hasa wanapokuwa na umri mdogo, lakini wanalegeza masharti kadri umri unavyokwenda. Mwisho wa kichekesho anamalizia kwa kusema 'Mungu nipe yeyote hata akiwa mfupi kama Joti sintojali'.

Sadly kichekesho hicho ni copy na paste ya mchekeshaji mmoja wa ki-Nigeria, tofauti ni lugha na badala ya jina Joti, anatajwa mtu mwingine huko Nigeria.

Nadhan kuna mapungufu makubwa ya ubunifu na usanii. Kwangu mimi mchekeshaji mzuri wa stand up commedy lazima awe na sifa zifuatazo:
  1. Awe mbunifu
  2. Awe mwigizaji (mfano: mwigizaji wa sauti au hali halisi, aweze kuvaa uhusika wa kile anachochekesha)
  3. Awe anafuatilia masuala yanayotokea ktk jamii
  4. Awe relaxed. Kuna watu wanataka kukuchekesha lakini wenyewe hawako comfortable kabisa. Unamuona kabisa anatumia nguvu kubwa sana. Sauti yake sio relaxed kabisa.
Naamini mtu anaweza kujifunza kuchekesha, hata kama hana kipaji. Cha msingi ni kujitambua na kukubali kujifunza.
 
Kabsa binafsi wanaoshobokea sijui hata wanafurahishwa na nin yaan ni anaforce balaaa
 
Huyo mc pilipili au sijui kachumbali hana lolote ni kama steve nyenyere wote ni watu wa kuforce-force tu watu kucheka....
kuwa mc au comedian mzuri mara nyingi ni kipaji au ( is an art ), na kipaji ni kitu kinakuja automatic yani mtu anatiririka tu na watu wenyewe wanachanganyikiwa kwa vicheko sasa hawa wanaonekana wazi ni watu wa kulazimisha lazimisha tu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…