TANZIA Mch. Christopher Mtikila afariki baada ya kupata ajali, Msolwa - Chalinze mkoani Pwani

Wajuzi wa sheria hebu tufahamisheni kuhusu hili, baada ya kifo cha Mchungaji mtikila ambae alikuwa mgombea urais wa chama cha DP je sheria inasemaje kuhusu uchaguzi? Utaakhirishwa au inakuwaje?

Nakumbuka miaka ya nyumba alipofariki Marehemu Dr Omar Ally Juma aliekuwa mgombea mwenza wa ccm uchaguzi uliakhirishwa vipi kuhusu la mtikila?
 
Alijaza fomu lakini hakurejesha fomu au alirejesha lakini vigezo vikapwaya.
Hata hivyo jana nilitahadharisha kuwa wagombea wenza walindwe sana wakati huu.
Kuna wanaotamani uchaguzi uhairishwe.
 

Mtukila hakuwa mgombea wa Urais, kila siku tanawambieni muwe mnatunza kumbukumbu vizuri!
 
Kweli JF siku hizi inashuka hadhi, marehemu Mtikila alikuwa mgombea kweli? Kwani kuchukua form na usirudishe unabaki kuwa mgombea? Kasome ndugundugu aibu hii umeitafuta ili kutwist situation ya Kingunge? Mmezoea akili mgando za Mwl. JK kujifanya kaota ili aendelee kujaza Watanganyika ujinga. Sio karne hii. Eti Mr. Hero. Utakuw Mr. Ebo wewe
 
Na watu wapo jf kila siku. Ila taarifa ya nini kinachoendelea hawana. Tanzania kuna shida mahali. Kuna mahali tulikosea bigtime
 

Mleta mada umekurupuka.....na sidhan kama unafatilia siasa za nchi hii.........kwanza Mtikila hakuwa mgombea wa urais maana hakukidh vigezo vya kuidhinishwa na tume ya uchaguzi............
Lakin pia Dr Omary Ali Juma alipofarik hakuwa mgombea mwenza alikuwa tayari yupo mamlakan......bila shaka umechanganya mafail aliyefariki mpaka uchaguz ukaahirishwa alikuwa ni mgombea mwenza wa Mbowe mwaka 2005 kupitia chadema...
 
Kesi yake ilikuwa bado mahakamani baada ya Tume kutoridhika na vigezo vyake ikiwami kukosa mgombea mwenza alikimbilia mahakamani na ilikuwa bado haijaamliwa.

So hakuwa mgombea kisheria.
 


Sijui ni kutokuelewa au huna kumbukumbu!
1.Mchungaji Mtikila hakuwa mgombea Urais mara hii kwani hakupitishwa na NEC.
2. Dr. Omar Ali Juma alifariki tarehe za mwanzo wa July 2001. TZ hatukuwahi kuwa na uchaguzi tarehe hizo. Na wala sio kweli kwamba kuna Uchaguzi ulioahirishwa kwa ajili ya kifo chake.

Sasa kwa ufupi ni kwamba HAKUNA suala la kuahirisha uchaguzi wa mwaka huu. Hapa tunasema 25 Oktoba 2015 basi Mkono kwa mkono Lowasa hadi ikulu
 

Lowassa alisema elimu ni bure bado hajachelewa
 

Mtikila hakuwa mgombea urais kwa sababu alienguliwa na Tume.
 

Sio kila mtu anakuwa na kila taarifa.

Mueleweshe tu kama hafahamu.
 

Soma biblia uje tujadili kwa vifungu tuone Mungu anayemuua mwanasiasa ili chama kimoja kisikosolewe. UKAWA na mashabiki wao wana upeo finyu sana. Kwanza kitendo cha kufurahia kifo cha nafsi moja ni kuchuma laana kutoka kwa Mwenyezi Mungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…