TANZIA Mch. Christopher Mtikila afariki baada ya kupata ajali, Msolwa - Chalinze mkoani Pwani

TANZIA Mch. Christopher Mtikila afariki baada ya kupata ajali, Msolwa - Chalinze mkoani Pwani

Nina wasiwasi na majeruhi wasije wakanunuliwa wakasema tuliwaona vijana wa chadema wakitushambulia ndipo ajal ikatokea
 
Uchunguzi wa nini hasa? Kwani mazingira ya hiyo ajali si ya kawaida kutokea?Kisichokuwa cha kawaida kwenye hiyo ajali ni nini mpaka uchunguzi ufanyike?
Poleni sana familia ya mchungaji mtikila!

Kuna watu hawajielewi kabisa, hii ajali imeshaanza kuzua maneno.
 
Vipi kuhusu Mwakyembe na sumu ya kunyoyoa nywele.
 
Dotworld

Heshima yako mkuu DotWorld, sina shaka umeziangalia hizo picha mbili kwa umakini sana, je zina tofauti na ajali ya Princess Diana huko Paris Ufaransa? Sio lazima unijibu mimi natoa angalizo tu.

R.I.P mpabanaji wa kweli ndugu Mtikila.
 
Last edited by a moderator:
Chinembe ni Mungu yupi huyo????? Mungu ni wa rehema na hataki hata mmoja apotee.

Kama huyo Mungu wa Lowasa anaua kila atakayemsema basi atauwa watu wengi sana. Lile kusudi la kazi ya msalaba litakuwa limefitinika.

Bwana wetu Yesu Kristo alifanyiwa kila namna ya uovu akasema Baba wasamehe hawajui wafanyalo. Huyo Mungu wa kulipiza papo kwa papo !!!!!!! Mh!!!!! Wapi kazi ya MSALABA???

Damu zilizomwagika hata sasa kama ni mapenzi ya Mungu zitaenda kwa AMANI. Kama ni umafya na ushirikina basi tegemeeni KISASI cha Bwana.

Queen Esther

Tatizo queen lipo pale binadamu anapochukua nafasi ya Mungu. Bila shaka umeshasikia ule msemo wa mdomo huumba. Unaposema mwenzio atakufa ujue kazi hiyo ni ya Mungu. Mungu atakuadhibu kwa kufanya kazi yake. Kwa kudhibitisha hilo hebu anza sasa hivi ukitabiria wenzio kifo usipoharakisha kifo chako.
 
Mtikila was never a threat to Lowasa..or Ukawa. Everywhat he said or did..was his right..we are in the world of democracy and liberty,remember that!
Let Lowasa rock..in Jesus name. R.I.P Pastor.
 
Kuumwa sio dhambi hata kidogo,na nafikiri historia ni mwalimu mzuri tu,naamini ulikuwepo au ulishuhudia uchaguzi wa mwaka 2005 yale yaliyotokea kwa nyakati mbalimbali za kampeni ya Mh Rais wetu Jakaya Kikwete,sitaki kuyasimulia hapa kwa sababu ya heshima ya Rais wetu,ninachotaka kuelezea hapa hakuna anaejua kesho yake wala mustakabali wa afya yake,mbona Rais wetu bado yupo na anafanya kazi vizuri tu?
Tujenge hoja nzuri kwa kumuuza Mh Magufuli na sio kukashifu afya ya mtu.

Kasome kwanza what is parkinsonism na ukasome alichougua mgombea wa 2005 kisha ufanye ulinganisho ndiyo sasa uje uniletee majibu
 
hapa napata picha fulani hiviiii, mwafulani ulipokuwa kule upande wapili mara watekwe, wauawe, wanyang'anywe laptop, wategeshewe ajali.

sasa umeenda kule umewageuka . eeeh kumbe weww ndo ulikuwa bingwa wa mizengwe yakufanyizia wenzio anayekugusa tu ananasa kama kagusa waya wa line kubwa ( joke)

Mkuu nawaza kwa sauti kubwaaaa nimekuelewa sana.
Ama kweli wewe ni great thinker.
 
Sikutegemea kama wakati huu ambao familia ya mwenzetu ipo katika kipind kigumu unaweza ukasema maneno hayo,after all yale ni maneno ya kisiasa nawe wajua siasa imejaa blah blah nying,si vizuri kumsema marehemu kwa mabaya yake sote ss ni wakosaji na Mungu pekee ndo anajua yupi mwema yupi mbaya, tuweke tofauti zetu pemben sote sisi ni mavumbi na tutarudi kuwa mavumbi,dunian tunapita ndugu yangu AMETANGULIA SI KWA SABABU YA UJINGA WAKE NASI TUMEBAKI SI SABABU YA WEREVU WETU.MUNGU NDO HUPANGA YOTE
 
Serikali ifanye uchunguzi mkubwa ili kubaini chanzo cha ajali iliyopoteza maisha ya Mwenyekiti wa chama cha dp mch Christopher mtikila hasa katika kipindi hiki kigumu cha uchaguzi. R.I.P MTIKILA
Kwanza unapaswa kujua Mungu hadhihakiwi,pili kumbuka unapomchimbia mtu aliye hai kaburi,unaweza kutumbukia mwenyewe,tatu watu wa Mungu wako kwenye maombi maalum kuliombea taifa lipone,na mwisho Mungu pekee ndiye mwamuzi wa hatma yangu mimi na wewe,mapenzi yake yatimizwe
 
Whaaaaat. rip mchungaji. Kuna jambo Mungu anataka watu wajifunze
 
mungu hapendi mzaha kwani yeye ndiye humpa mja wake afya na maradhi kwa hiyo basi kifo chake ni fundisho kwa wengine km akina mwigulu et el.
mungu ampunzishe mahala pema,ila kwa sisi tuliobaki kifo cha mtikila
kiwe funzo,watz tunakufulu
sana kumnyoshea mtu kidole eti
mgonjwa,
 
Acheni kuhusisha kifo chake na E.Lowasa hivi mkikamatwa mkaambiwa mthibitishe mtasema nini? Au mtabaki kujiuma uma km dem aliyekolezwa voko na mshkaj? Km kafa bas tumwachie tu Mungu
 
asmeandika contradiction tupu. Siamini kama Mungu karuhusu kifo cha Mtikila kwa ajili ya dhambi za Mtikila dhidi ya utakatifu wa lowasa na wafuasi wake. Nikionacho ni roho ya visasi na uuwaji ya kutaka kila anayekukosoa afe. "Heri Kijana maskini, kuliko mfalme mzee tajiri, asiyepokea maonyo." Ukimukosoa lazima ufee.
Vipi Celina combani na kauli yake? Vipi kuhusu Komba na kauli yake juu ya mzee warioba? Ni watu wangapi wamepata ajali kipindi hichi? Kwani mtikila Kupata ajali ni miujiza? Au ajali ni kwajili ya kundi fulani la watu? Wabunge wa chadema wawili wamepata ajali kipindi hichi cha uchaguzi, je nao tuseme kua Kuna watu wanahusika? Hembu tujaribu kua na fikra zenye mantiki kidogo..
 
RIP Mchungaji Mtikila...
Am speechless ila MUHIMU kila mtu ajue kuwa "sisi sote ni marehemu watarajiwa..."
 
Ukweli utaendelea kusemwa tu no matter wasemaji wataendelea kufa maana hakuna kitu muhimu kama kusema na kusimamia unachokiamini.

Heri kufa kwa kusema na kusimamia unachokiamini kuliko kuishi kinafiki,I believe wapo watakao okota silaha alizoanguka nazo Mtikila na mapambano yataendelea.

You played your part man!!

R.I.P Mtikila.

Vipi kaacha kesi ngapi zinazoendelea mahakamani?

Kitu ambacho hatujifunzi ni kuhusu falsafa ya kifo. Kuna mmoja tu ajuae kila mmoja wetu siku zake zitaisha lini. Mungu aliyetuumba huzihesabu siku zetu tulizoishi na kuzisitisha wakati wowote atakao, uwe mgonjwa au mzima when your time is ready you will go no matter what R.I.P Mchungaji
 
Kwa hali hii tunaitaji msaada wa mungu,kila anayeonekana kumpinga mgombea furani kifo ?,ushauri wa bure,

1,makongoro,
2,Nape
Kuwa makini,
 
Back
Top Bottom