TANZIA Mch. Christopher Mtikila afariki baada ya kupata ajali, Msolwa - Chalinze mkoani Pwani

TANZIA Mch. Christopher Mtikila afariki baada ya kupata ajali, Msolwa - Chalinze mkoani Pwani

Alimkashifu lowasa kuhusu ugonjwa,mpaka akatishia kumshitaki mahakamani kwamba kwa nini anagombea wakati ni mgonjwa
Na akatishia pia kumpeleka mahakamani Mbowe kwa kifo cha Wangwe. Basi Eddo na Freeman wakamatwe kwa uchunguzi
 
Mungu alitoa na Mungu ametwaa jina lake lihimidiwe.

Pia ni vyema kusema kuwa, Mungu ninayeamuamini si Mungu wa visasi si Mungu wa gadhabu wa kutoa hukumu kama wengi wanavyotaka tuamini. Ni Mungu anayetusubiri kutupa adhabu siku ya hukumu na si hapa duniani. Mtoa adhabu hapa duniani naamini ni shetani.

Kama Mungu angelikuwa anatoa adhabu hivihivi kweli hao wanaopiga mabomu na kuua ma milioni ya watu Iraq, Libya, Afghan, syria, Ukraine nk wangepata adhabu papo kwa papo.

Marehemu mtikila aliwahi kushangilia kifo cha Mwl hadi akafungwa. Hivyo kifo kilichomkuta mwezetu, ni jinsi Mungu alivyokuwa amepanga na kama sio basi ni mafia walivyopanga kupata kutisha watu.

Na pia naamini magonjwa yote yatoka kwa shetani, na ndio maana kuna hospital ya kuyatibia. Wakati ule Yesu alipita kuwatibu magonjwa yaliyokuwa yanatesa wananchi kutoka kwa shetani -matendo 10:38. Na pia kuna vifo vinavyosababishwa na shetani/watu. Mfano hebu watu waache kwenda hospitali uone vifo vitakavyoongezeka.
 
Akawekwe anapostahiki.

Namsikitikia kuwa alikuwa hajajisalimisha kwa Muumba wake mpaka umauti unamfika.

Wewe Jee?

unasikitika what?ulikuwa naye? kujisalimisha kwa mola/Mungu nimaneno machache sana so huwezi jua, au ulimaanisha nini?
 
Mungu mkubwa,hadhihakiwi akakaa kimya.
Wenye kuona na waone utukufu wake.

Nashangaa dada, hawaachi kucheza na mungu wa lowasa. Mwakyembe aliponea chupuchupu, Kubenea kidogo apofuliwe macho (nafuu yake sasa ameamua "kuokoka" - HALELUYA!!)
 
Tukio hili ni kumbusho kwa wale wote wanaopagia uzima binadamu wezao. Mimi nimekuwa naangalia tu hizi kampeni na watu waliojivika u mungu mtu kusemea afya na vifo vya watu. Mimi Ng'wanapagi pamoja na kuandika posti hii lkn sijui afya yangu hususani yale mgojwa ya moyo na mengine ya kustukiza yamekaa aje kwenye hili cover (mwili). Ndiyo sababu zamani Redio Tanzania ilikuwa na kipindi cha salamu kwa wagojwa jumapili na kulikuwa na wimbo unasema.............ajuae bwana mungu kwa mzima kuwa mfu mgojwa kuwa salaaaaam leo tunawapa pole....,...... CC Nepi
.
 
katika Vitabu vitakatifu Mungu amekuwa akitoa ishara nyingi nyingi sana. Na hii leo anasema na Watanzania kwa namna tofauti kabisa ya kuondokewa na mwanasiasa mwenye chachu kabisa katika Siasa za Vyama vingi. Hebu kaa dakika moja mkumbuke Mch.Mtikila, Kumbuka siasa za Mtanganyika, Kumbuka siasa za --------- na mengine mengi.

Mungu anasema kwa ishara mabalimbali kipindi hiki cha uchaguzi, matukio mengi sana yametokea hapa Tanzania na duniani yakitukumbusha sisi ni mavumbi tu. Nikipindi ambacho Tunakumbushwa kurudi Miskitini na makanisani kusiliza sauti ya Mungu na kuzitambua ishara hizi kwa unyeyekevu mkubwa. Mungu anatukumbusha kujali maskini,Watu wenye njaa, na wagonjwa mbalimbali. Mungu anatukumbusha si kwa akili zetu tumepata dhamana kuliongoza taifa hili bali yeye mwenyewe ndio kafanya yote haya.

Mungu anatukumbusha Gas Mafuta na madini ni mali yake na vitumie kwa utukufu wake kwa kuhudumia watu wenye mahitaji zaidi. Mungu anatukumbusha Mikataba ya madini/Gas iwekwe wazi ili iwafikie walengwa wake. Mungu anatukumbushaTuache rushwa na ufisadi,Tutubu zambi zetu na Tujenge taifa kwa kizazi kijacho.

Mungu ameota ishara hizi ila kila mwanadamu apate kumjua yeye ndie Mungu Muumba wa Taifa hli.
1.Lowassa Kuhama CCM
2.Magufuri kuwa Mgombea Urais
3.Lipumba Kuacha siasa
4.Dr Slaa kuacha Siasa
5.Halima mdee na Mbatia kwenye Jukwaa moja.
6.Tanzania kuwa giza wakati wa uchaguzi
7.Vyama vinne kusimamisha mgombea
8.Rais kupiga campaign
9.Hotuba za Nyerere kutamba katika jukwaa la upinzani.
10.Kwa mara ya kwanza Watanzania hawajui nani atashinda uchaguzi.
11.Campaign bila kept.Komba.
ukiangalia kwa mbali utaona ni vitu vidogo sana lakini ukirudi utakuta mabadiliko makubwa sana katika radha ya siasa za Tanzania. kwa ujumla kifo cha mtikila ni pigo zito sana katika radha ya siasa ya vyama vingi. R.I.P
 
Pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa Mchungaji Mtikila. Tangulia Mtanganyika. Ukionana na Edward Sokoine na JK Nyerere waambie Uchaguzi wa Tanzania ni Oktoba 25.
 
Hawa wanasiasa wasikuhizi nimithili ya wehu.

Badala ya kuhubiri sera, aman upendo na umoja wao wanafanya mambo ya ajabu.

1. Matusi
2. Masimango
3. Uzushi wa mambo yakufikirika
4. Kutabiria watu wengine maradhi na vifo
nk.

Akina Polepole, Bulembo, Nape,Mwigulu, J makamba nawengine waache upumbavu wakujadili afya za wengine na private matters.

Wajadili issues sio mtu na waache ujinga wa propaganda nasiasa za maji taka.

Isitoshe raia tunahitaji kusikiliza matatizo yetu yamsingi yatatatuliwa vipi

Elimu

Afya

Miundombinu

Uchumi.

Waache ujinga.


wote wanaomtukana lowasa kuwa mgonjwa hawatadumu,wote wanaotukana wengine hawatadumu,wataangamia wote mmoja baada ya mwingine,komba,kombani,mtikila sasa bado kikwete na ridhiwani.hawa nawaombea wafe mapema.
 
Mtu asije akakudanganya neno wasamehe na kuwaombea Baraka ndio laana yenyewe,unapo muombea adui yako Baraka,Mungu hugeuza baraka kuwa laana ndiyo maana hata Yuda mwenyewe alichukua kitanzi akajitundika pamoja na kuombewa msamaha na Yesu.

Kabisaaa....ukitukanwa ukidhihakiwa piga goti muombe Mungu..atakupigania..akupigae shavu moja mgeuzie na jingine...yanini kurumbana wakt hakimu wa yote yupo hai...
 
Siamini kama na wewe umeamua kuwa mtu wa siasa nyepesi kiasi hiki.Angalia wale unaowaona ni watu sahihi kwako,ambao walifika bei na kusaliti safari ya ukombozi mbele ya watanzania wanavyoanza kutenda kinyume na kile walichotuaminisha.Dk.alisema ameachana na siasa za majukwaani,alisahau kuwa yeyeni mpiga zumari tu ambaye hawezi kujichagulia apige wimbo upi.sasa wanaomtumia wamemtaka arudi jukwaani akafanye kile wanachopenda kukiona na kukisikia.Subiri kuanzia 7/10/2015,utabaki kinywa wazi kwa kutoamini utayoyasikia kutoka ktk kinywa kilekile cha mtu unayemuamini ambaye alifika bei na sasa analipa ghalama alizopewa.

Nimeanza kumuogopa mungu wa akina lowasa na Rostam.
 
katika Vitabu vitakatifu Mungu amekuwa akitoa ishara nyingi nyingi sana. Na hii leo anasema na Watanzania kwa namna tofauti kabisa ya kuondokewa na mwanasiasa mwenye chachu kabisa katika Siasa za Vyama vingi. Hebu kaa dakika moja mkumbuke Mch.Mtikila, Kumbuka siasa za Mtanganyika, Kumbuka siasa za --------- na mengine mengi.

Mungu anasema kwa ishara mabalimbali kipindi hiki cha uchaguzi, matukio mengi sana yametokea hapa Tanzania na duniani yakitukumbusha sisi ni mavumbi tu. Nikipindi ambacho Tunakumbushwa kurudi Miskitini na makanisani kusiliza sauti ya Mungu na kuzitambua ishara hizi kwa unyeyekevu mkubwa. Mungu anatukumbusha kujali maskini,Watu wenye njaa, na wagonjwa mbalimbali. Mungu anatukumbusha si kwa akili zetu tumepata dhamana kuliongoza taifa hili bali yeye mwenyewe ndio kafanya yote haya.

Mungu anatukumbusha Gas Mafuta na madini ni mali yake na vitumie kwa utukufu wake kwa kuhudumia watu wenye mahitaji zaidi. Mungu anatukumbusha Mikataba ya madini/Gas iwekwe wazi ili iwafikie walengwa wake. Mungu anatukumbushaTuache rushwa na ufisadi,Tutubu zambi zetu na Tujenge taifa kwa kizazi kijacho.

Mungu ameota ishara hizi ila kila mwanadamu apate kumjua yeye ndie Mungu Muumba wa Taifa hli.
1.Lowassa Kuhama CCM
2.Magufuri kuwa Mgombea Urais
3.Lipumba Kuacha siasa
4.Dr Slaa kuacha Siasa
5.Halima mdee na Mbatia kwenye Jukwaa moja.
6.Tanzania kuwa giza wakati wa uchaguzi
7.Vyama vinne kusimamisha mgombea
8.Rais kupiga campaign
9.Hotuba za Nyerere kutamba katika jukwaa la upinzani.
10.Kwa mara ya kwanza Watanzania hawajui nani atashinda uchaguzi.
11.Campaign bila kept.Komba.
ukiangalia kwa mbali utaona ni vitu vidogo sana lakini ukirudi utakuta mabadiliko makubwa sana katika radha ya siasa za Tanzania. kwa ujumla kifo cha mtikila ni pigo zito sana katika radha ya siasa ya vyama vingi. R.I.P


karibu tuchangie
 
huyu mamvi atatumaliza hadi 25/10 tutakuwa tumeisha Dr magufuri ukiingia madarakani futa uchaguzi kama China na Russia hii dhahama inatupunguzia Maendeleo badala ya kujadili kufanya Kazi tunajadili Vigo vya kutengeneza.

Mungu hapangi Vigo Bali aliumba kifo na sio kila Kifo eti ni mapezi ya Mungu hapana kunalijamaa linatengeneza basi its shame
 
Queen Esther naomba usisumbuke kubishana na wajinga.

Watu wanataa kututisha mtu asisemwe kile alicho nacho. Lowasa ni mgonjwa kama wagonjwa wengne. Fidel castro baada ya kuandamwa na magonjwa aliamua kukabidhi madaraka kwa mdogo wake. Sasa kama urais unatakiwa mtu mgonjwa kwann aliamua kuacha madaraka?

Kila mtu ana uhuru wa kuongea anachotaka kuongea. Semeni Lowasa mgonjwa semeni chochote mtakacho. Lakini mimi na nyumba yangu na jirani zangu wote tunampa kura zetu Lowasa pamoja na ugonjwa wake akafie ikulu.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom