Mchanganuo tozo za LUKU kuanzia August 20-2021

Mchanganuo tozo za LUKU kuanzia August 20-2021

hapa kuna kitu iko imejificha, mfano nina nyumba ina wapangaji 3, na luku zinajitegemea....hao wapangaji wakilipa luku zote zinasoma jina la mwenye nyumba......ina maana wapangaji ndio watalipia jengo,,sawa...je itasomeka nina nyumba 3?.......kama sijaelewa....kuna kitu hapa italeta mgongano mkubwa sana....tusubiri tuone....je majengo yote yapo registered???? ..kuna kivuli cha dhuluma nyingine kinakuja....WATANZANIA zetu kelele tuu...tena kwa muda mfupi sana.....then we move on.........
Apo inatafutwa kodi ya mapato kutoka kwa wapangaji pesa mwenye nyumba anazo pokea kutoka kwa wapanaji!!
siku sio nyingi wenye majengo wata pandisha kodi maana wata lazimikana Ama wata julikana
 
ahsante sana.
najisikia fahari kuijenga nchi yangu.
watanzania tupo tayari, kazi na iendeleee.
Tupo tayari lakini vipi kwa wale watu wa hali ya chini? Umeshawafikiria hata kidogo?
 
Wanawake mtaambia nini watu??

"Manawake wanaweza????"
 
mtu wa hali ya chini hana uwezo wa kumiliki nyumba.
ukiweza kumiliki nyumba na ukavuta umeme wewe unajiweza, na uanao uwezo wa kulipa Sh.elfu moja kwa mwezi.
tulipe kodi kwa maendeleo yetu, hakuna nchi inayo weza kuleta maendeleo bila kutoza kodi.

Wakati wa kampeni za uchaguzi au hati ktk ziara za Viongozi wa Serikali ktk maeneo mbalimbali utawasikia wananchi wanailaumu/wanalalamikia Serikali kwa kushindwa kuletea maji, hospitali, dawa, shule,vyoo, barabara, umeme n.k.
sasa unadhani huduma hizo zitatatuliwaje bila sisi wenyewe kulipa kodi.
kumbuka wananchi wakizikosa huduma hizo lazima pia watailaumu Serikali kwa kushindwa kutatua kero zao.
tuache kuibabaisha Serikali, tulipe kodi.
 
Wamesema mwenye nyumba apeleke Luku hizo ziingizwe kwenye luku moja. Hakafu wapangaji hamtakiwi kulipa hii ni ya mwenye nyumba. Akigoma nendeni TRA(ila mnaweza kufukuzwa kwenye hio nyumba ha ha ha ha)
bado ni pagumu sana, sidhani kama wamejipanga vema......hapa kuna watu wasio na nyumba watalipia pango bila kupenda...tusubirie tuone...hii na TOZO NA MIAMALA haina tofauti....kila kona tutatachapwa.........fikiria unaishi nyumba uliyopangishiwa na serikali, ya kwako umempangisha HAJI MANARA.....wewe huku kila kitu serikali inamaliza..habari sijui umeme umeisha hunayo....kule kwa mpangaji ndie anaenunua LUKU.....atakaelipa kodi ya jengo ni nani......kuna kitu ndani ya kitu.....subiri tuone...na tulivyo na vilaza wengiii....endelea kusikilizia mdundo kwanza....
 
Magu alifanya uhuni na kutuletea Bunge lililojaa wapuuzi wasiojali matakwa ya wananchi, na matokeo yake ndio haya. Haya sasa.
Kodi ya majengo iliwepo toka kitambo, sema mmezoea kutolipa kodi mnataka watu wengine walipe huduma mpewe ninyi, now mmeona haikwepeki mmeanza vilio.
 
mtu wa hali ya chini hana uwezo wa kumiliki nyumba.
ukiweza kumiliki nyumba na ukavuta umeme wewe unajiweza, na uanao uwezo wa kulipa Sh.elfu moja kwa mwezi.
tulipe kodi kwa maendeleo yetu, hakuna nchi inayo weza kuleta maendeleo bila kutoza kodi.

Wakati wa kampeni za uchaguzi au hati ktk ziara za Viongozi wa Serikali ktk maeneo mbalimbali utawasikia wananchi wanailaumu/wanalalamikia Serikali kwa kushindwa kuletea maji, hospitali, dawa, shule,vyoo, barabara, umeme n.k.
sasa unadhani huduma hizo zitatatuliwaje bila sisi wenyewe kulipa kodi.
kumbuka wananchi wakizikosa huduma hizo lazima pia watailaumu Serikali kwa kushindwa kutatua kero zao.
tuache kuibabaisha Serikali, tulipe kodi.
kwani mkopo wa ma trillioni kutoka WB ni kwa ajili ya nini? au tunajiandaa kununua wapiga kura....
 
Amang'ana ghenu!

Naomba niende kwenye maada moja kwa moja,

Wakuu naomba kuelimishwa/kufafanuliwa kuhusu hili Tangazo la TRA na TANESCO kupitia maswali ninayotaka kuuliza hapa kwa sababu kuna vitu Tangazo halijaweka wazi pengine ndo ikapelekea mimi kutokuliewa vilivyo na kuibua mswali kichwani mwangu,

Maswali yangu ni kama ifutavyo

1) Swala la wapangaji kuhusu hii kodi ya majengo likoje? Na wao ni wahusika wa kulipa hii elf1 kila mwezi kama sivyo TANESCO na TRA wanaliweka vipi?

2) Nyumba moja inazo Luku zaidi ya mbili, hili nalo likoje? Jengo moja litakuwa linalipiwa kodi zaidi ya elf2?

3) Je kuna maelekezo yoyote tukilipa hiyo wenye nyumba wawarudishie hicho kiasi walicholipa? Kama yapo kuna utaratibu gani umeweka kwa hizo hela kurudi kwa wapangaji!

Nb, Nimepita kwenye moja ya page zao kwenye mitandao hakuna majibu ya maswali yangu.

Hata kama sio wao watajibu naomba mwanaJF alieliewa Tangazo majibu yako tafadhali.

Mkuu Wgr30 salamu kwako.
Nashukuru kwa maswali mazuri. Kama sijakosea inaonekana kwamba TRA wame-Assume kila mtumiaji wa umeme atakuwa ananunua Umeme mara moja kila mwezi ambapo uhalisia unaweza usiwe huo. Kimkakati wa kukusanya kodi ya majengo hili zoezi litaiwezesha Serikali kupata mapato zaidi kutokana na majengo tofauti na ilivyokuwa awali. Najaribu kuwaza kama akitokea mtu akanunua Umeme mwingi (Mfano Unamnunulia Mzazi Kijijini) mara moja kwa mwaka utekelezaji wa haya makato utakuwaje.

Anyway, naipongeza Serikali kwa huu ubunifu
 
Ndiyo. Kwa mujibu wa TRA ni kwamba mtu mwenye jengo la kawaida anapaswa lipa kodi ya jengo ya shilingi 12,000/= kwa mwaka, na wale wenye maghorofa watalipa 60,000/= kwa mwaka bila kujali idadi ya sakafu/floors iwapo jengo litakuwa kwenye miji midogo.

Sasa hii 1000/= kwa kila mwezi ndiyo italeta 12,000/= kwa mwaka na hii 5,000/= kwa mwezi ndiyo italeta 60,000/= kwa mwaka.
Tafadhali, Mimi sijaelewa. Ni kwamba kila anayenunua LUKU wana-asume ana jengo?
 
Ndio maana watu wakapendekeza iitwe kodi ya luku/ umeme/ meter kwa sababu inatozwa kwa meter sio jengo.

Jengo lenye meter 2 litatozwa 2,000 kwa mwezi wakati kimsingi kodi ya jengo inatakiwa iwe 1,000/- kwa jengo.
Au iitwe kodi ya watumia umeme kabisa😀😀
 
Au iitwe kodi ya watumia umeme kabisa😀😀

Kabisa, ni kosa kuiita kodi ya jengo wakati unawatoza wapangaji kila wanaponunua umeme na inatozwa kwa kila meter na sio kila jengo.
 
Hyo Kodi ni inakatwa mara Moja ndani ya mwezi sio Kila ukinunua
 
bado ni pagumu sana, sidhani kama wamejipanga vema......hapa kuna watu wasio na nyumba watalipia pango bila kupenda...tusubirie tuone...hii na TOZO NA MIAMALA haina tofauti....kila kona tutatachapwa.........fikiria unaishi nyumba uliyopangishiwa na serikali, ya kwako umempangisha HAJI MANARA.....wewe huku kila kitu serikali inamaliza..habari sijui umeme umeisha hunayo....kule kwa mpangaji ndie anaenunua LUKU.....atakaelipa kodi ya jengo ni nani......kuna kitu ndani ya kitu.....subiri tuone...na tulivyo na vilaza wengiii....endelea kusikilizia mdundo kwanza....
Apa wasipokuwa makini hii kodi watalipa wapangaji tena wengine bila kujua,watanzania wengi hata wakungalia yale makato ni shida.
 
Back
Top Bottom