Mchango wa Chama cha Kikomunisti cha China kwa maendeleo, amani na utulivu wa dunia

Mchango wa Chama cha Kikomunisti cha China kwa maendeleo, amani na utulivu wa dunia

ldleo

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
1,116
Reaction score
1,121
Na Ronald Mutie

hgfjhgfjgfjgfhjh.jpg

jhgfjhgfjgfj.jpg

Chama cha Kikomunisti Cha China sio tu kimesaidia nchini hiyo kufikia muujiza wa maendeleo ya kiuchumi lakini pia China imekuwa mchangiaji mkubwa kwa maendeleo ya ulimwengu, amani na utulivu.

Mkuu wa Tume ya Uhusiano wa nje wa Chama cha Kikomunisti cha Kamati Kuu ya Vietnam Le Hoai Trung anasema China imeshiriki kikamilifu katika mifumo ya ushirikiano wa kikanda na kimataifa, na kutoa mchango mkubwa katika kukuza ushirikiano wa kimataifa katika mfumo wa Umoja wa Mataifa.

Mifano hai imeonekana katika nchi kama Sudan Kusini, Sudan na DR Congo ambako China imetuma walinda amani wake kushirikiana na serikali za huko na walinda amani wa nchi nyingine Chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa.

Mwezi Julai mwaka huu (2021) naibu balozi wa kudumu wa China katika Umoja wa Mataifa Dai Bing alisisitiza kuwa China inapenda kushirikiana na jamii ya kimataifa kuendelea kutoa mchango chanya kwenye mchakato wa ujenzi wa amani nchini Sudan, mkoani Darfur.

Anasema hivi sasa mkoa huo uko katika kipindi muhimu cha mpito kutoka kulinda amani hadi kujenga amani.

China ni moja ya nchi zilizopeleka askari wake kwenye Kikosi hicho mapema zaidi, ikionesha azma yake ya kutaka kuwepo kwa amani Darfur lakini pia na kote duniani.

Na Ili kukuza ubadilishanaji na ushirikiano kote ulimwenguni, Rais wa China Xi Jinping alitoa pendekezo la “Ukanda Mmoja, Njia Moja” (BRI) na ujenzi wa jamii yenye hatma ya pamoja kwa wanadamu wote.

Kupitia BRI ambalo ni wazo la Rais Xi la mwaka 2013, nchi nyingi kama vile Kenya, Ethiopia, Burundi na Tanzania tayari zina miradi kama reli, bandari, barabara na miundo mbinu mingine ya kukuza uchumi.

Lengo la BRI ni kuwezesha nchi nyingi zaidi kuunganishwa na mifumo ya uchukuzi na mawasiliano ili kukua haraka kiuchumi.

katibu mkuu wa chama tawala cha Uganda National Resistance Movement Richard Todwong anasema BRI ni maarufu ulimwenguni kwa sababu inaunganisha watu.

Anasema katika nchi nyingi za Afrika, haswa Kusini mwa Jangwa la Sahara, Wachina wamefanya miradi mingi ya miundombinu na nchini Uganda tayari wamejenga mabwawa kadhaa na vyote hivyo vinawezesha nchi husika kujitegemea zaidi kiuchumi

Mtazamo wa CPC na China ni kwamba suluhu za dunia kama vile mabadiliko ya tabia nchi, migogoro na kujitosheleza na chakula ni kuwa na mtazamo wa pande nyingi na kuwajumuisha wote.

Makamu wa rais wa chama cha New Left cha Poland Andrzej Szejna anasema wazo la kujenga jamii yenye mustakabali wa pamoja kwa wanadamu linaweza kutumika kama suluhisho kwa shida ambazo ulimwengu unakabiliwa nazo, kwani inategemea amani na ushirikiano.

Chini ya uongozi wa CPC, anasema Khuon Sodary, makamu wa pili wa rais wa Bunge la Kitaifa la Cambodia kwamba China imechangia sana maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wanadamu wote.

Anaona kuwa China itaendelea kubeba jukumu muhimu katika kujenga amani ya ulimwengu, kukuza maendeleo ya ulimwengu na kudumisha utulivu wa kimataifa.
 
Hawa jamaa ni laana kwa dunia.

wameuwa watu wasio na hatia, wameonea watu, wamepora watu mali, wanawahadaa viongozi wa nchi za ulimwengu wa tatu, na kupora mali, wanakandamiza haki za waislam na kuwalazimisha kwa kuwapeleka kwa labor concenraion camps, wanaminya uhuru wa wakristu kuabudu nk

maovu yao ni mengi kuliko hayo mema unayojaribu kueleza

Kwa maono yangu hawa watakuwa waaabaya mara mia kuliko wakoloni wakizungu
 
Hawa jamaa ni laana kwa dunia.

wameuwa watu wasio na hatia, wameonea watu, wamepora watu mali, wanawahadaa viongozi wa nchi za ulimwengu wa tatu, na kupora mali, wanakandamiza haki za waislam na kuwalazimisha kwa kuwapeleka kwa labor concenraion camps, wanaminya uhuru wa wakristu kuabudu nk

maovu yao ni mengi kuliko hayo mema unayojaribu kueleza

Kwa maono yangu hawa watakuwa waaabaya mara mia kuliko wakoloni wakizungu
Wazungu washenzi mara millions kama sio billions wameua watu JAPAN kwa atomic BOMB wanashirikiana na utawala wa Myanmar kuwakandamiza waislam wameua malaki kama sio mamilioni ya waafrika kipindi cha ukoloni
Wazungu hawana wema hata robo wameua watu IRAQ LIBYA YEMEN VIETNAM nk
Shenzi kabisaa[emoji35][emoji35][emoji35]

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Mpango Mzima ni Macho Kuvimba taka usitake
 
Back
Top Bottom