Ni kweli kabisa JPM alichukua behewa liitwalo.TANZANIA uelekeo ni ZIMBABWE wasukuma gang wanajitahidi kumnadi ila wapi JPM alikuwa na roho yenye kutu ka ruin maisha ya watu wengi mno hususani WAPINZANI ilifika pointi upinzani nchini ulionekana kama ugaidi ama uhaini huku kwenye katiba unatamburika.
JPM ni rais pekee aliekuwa anapelekea nchi yetu kutengwa na nchi jirani na mataifa mbalimbali kwa sababu ya kiburi binafsi na ubabe mavi huku akitumia nguvu nyingi kutuaminisha kuwa bifu lake liwe bifu la taifa.
Pia jamaa alikuwa muongo wa kiwango cha lami alituaminisha eti tupo kwenye vita vya kiuchumi na MABEBERU a.k.a MAREKANI uongo mwingine ni.ule wa kusema eti TANZANIA CORONA haipo utafikili TANZANIA ipo sayari ya PLUTO.
Kwangu mimi ni rais mbaya ambae hajawahi kutokea hapa nchini.
R.I.P JPM lakini ukweli ndo huo uliopo moyoni mwangu.