CHANANJA DYNASTY
JF-Expert Member
- Sep 14, 2024
- 772
- 1,121
Sio lazima ila wanatengeneza mazingira ya kufanya uone n lazima kutoa.Hata mimi nimehisi hivyo, imagine unapangiwa kiwango kabisa. Nimepiga hesabu hicho kwango ni mshahara wangu wa siku moja, hesabu zimekataa kabisa kama atakasirika poa tu.
Wale huwa desperate na suala lao tu. Wakishafanikisha huwaoni tenaNa ukitoa shughuli ikiisha mwendo ni ule ule, kuna dada nilisoma nae tulimchangia baada ya shughuli kupita yeye ndio wa kwanza kuleft group na hakuwahi kuchangia chochote kwenye grp la shule akijitetea yeye ni mke wa mtu.
Huo ni ubinafsi wa kiwango cha lami.Wale huwa desperate na suala lao tu. Wakishafanikisha huwaoni tena
Mkuu binadamu wengi ni wabinafsi haswa kwa umri wetu maana Kila mtu anakusogelea anapoona utampa wepesi kwenye jambo flani. Akifanikisha anaondokaHuo ni ubinafsi wa kiwango cha lami.
Kuna watu sio waelewa kabisa ila maisha lazima yaendelee hata asipokubaliana na uhalisia.ukiwa huna unaacha kwa lugha nzuri. Muelewa ataelewa, asiyeelewa hawezi kuelewa
Anzisha bar kabisa🤣🤣🤣Aisee halafu sijui kwanini zawadi nyingi kwenye harusi ni glass.
Kabisa mkuu, mwisho wa siku mwenye kutaka ku_judge hata umpe 50k or 100k bado atalalamika hujatoa wa kutosha. Mtu anaona kama ni yake kupata pesa kubwa hata kama hamna bondKuna watu sio waelewa kabisa ila maisha lazima yaendelee hata asipokubaliana na uhalisia.
Kweli kabisa aseh, Kuna jamaa yangu nae alikuwa kwenye kikao Kama hicho, Kwa kupenda sifa ndo akawa wa kwanza kunyoosha mkono na kutaja kiwango kikubwa zaidi kuliko wenzie,basi unadhani alitekeleza!!,wafuatiliaji aliwa block kabisa.Ni kweli..
Usilazimishe kuchangiwa.
Angalia hii...
Ilikuwa kikao cha kwanza cha Harusi...ndugu, jamaa na marafiki kila mmoja aliulizwa kiasi ambacho anaweza kuchangia bila kulazimishwa kuna aliyetaja laki 1, 2, 3,4, 5, na wengine elfu 50, 30, 20 hadi elfu 10 ( Kwa hiari), na wengine walisema hawana uhakika ila Mungu akipenda tuko pamoja.
Kwasababu hujalizimishwa na mtu, ila ni kiherere chako cha kujifanya mwamba na kuahidi Tsh laki 5..endapo utashindwa kutoa kama ulivyo ahidi hilo ni Deni na inakulazimu ulipe.
Kwanini utoe ahadi ikiwa hauna uhakika na bajeti zako na hujalazimishwa..?
Michango ya kijinga ni ile ya kulazimisha kwa kumpangia mtu kiasi cha kuchangia kwenye furaha yako.
Zitakua zinapasuka sana majumbaniAisee halafu sijui kwanini zawadi nyingi kwenye harusi ni glass.
Kila boksi ukifungua ni glass tu na wenyewe walivyoulamba sasa.Anzisha bar kabisa🤣🤣🤣
SitoiToa mchango huo kijana aoe ndio undugu huo
Kwani lazima? Acheni kusumbua watu. Jiandae mwenyewe kwa kadiri ya nguvu yako; michango ya ndugu, jamaa na marafiki iwe nyongeza tu. Mbona mimi nilijuandaa kwa kidogo nilichokuwa nacho, nikapanga sherehe kwa bajeti ndogo niliyokuwa nayo. Waliopewa kadi hawakufutiliwa kama vile wanadaiwa madeni.Bila kuwafatilia amtoi.
Kiuhalisia hiyo michango yenu yote inalipwa na mwanaume indirect.Heri wanaume mnapewa ya harusi tu.
jamani wadada kitchenparty, bridalshower, babyshower kajifungua kuna kibeseni ...akiolewa ana mimba basi mnachanga mpakaaa..... na Usipotoa mtu anakununia kheeee🙌🤣
Mwisho wa kunukuuMshikamano ni jambo la msingi sana lakini inakuwa kheri zaidi ukielekezewa kwenye mambo ya msingi kwenye jamii yetu kwa ujumla wake kama vile afya, elimu, misiba na majanga mengine ya kiasil
KInachoshangaza Mjomba akiumwa hachangiwi hata laki moja ya matibabu hadi anakufaSasa kwenye ufunguzi wa kamati ulipikiwa chakula Cha gharama ukala na kunywa, uliposhiba ukainuka na Kutoa ahadi,
Leo hii hutaki kukumbushwa ahadi uliyoitoa.
Kumbuka hata wazazi wako walisaidiwa walipooana.
Wacha kibri, this is Africa.