Mchawi kazi yake ni kuroga urudi nyuma, jilinde

Mchawi kazi yake ni kuroga urudi nyuma, jilinde

Kuna mambo mengine ni ya kushughulikia ili uepukane nayo,pindi mimba za mke wangu zinatoka bila sababu ya msingi nilidharau akiniambia nimeota tu mimba imeharibika hasubuhi anakuta kweli imeharibika nikaona kawaida,muda ulivyozidi kwenda muhusima wa mchezo ule mwenyewe akaanza kunipa vitisho na mikwala mingi na alifanya mengi sanaa kwa kutaka kumdondosha mke wangu ikawa sifanyi lolote bali kumkinga na hila zile maana ilikua anaweza inuka akaenda ukutani atajibamiza sana kichwa kama haupo karibu anaweza poteza maisha au akiwa karibu na kisu anachukua na kutaka kujidhuru nilisumbuka sanaa huku nikipokea simu za vitisho na sms za vitisho maana alikua mmoja wa ndugu wa mke wangu,nilipochoka kuvumilia haya mateso na kupoteza kipato kidogo nilicho nacho kwa kumuangaikia mke wangu ndipo mateso yote yalipokwisha hadi sasa yupo salama kabisa na mtoto tulipata baada ya mwaka tu..unapokutana na changamoto yoyote ni wewe tu kuamua kuilea au kuimaliza.
 
Uchawi upo na unafanya mengi ila sitaki kuutilia maanani na kuuamini

Hivyo huwa naupuuza sana na kuupinga sana ingawa huwa naona wanaoathirika nayo

Ukiamini uchawi utaamua kuutafuta ili upate kinga au utafute utajiri au mapenzi yaani mradi ujihusishe tu
Ila kwa mimi na familia yetu hatutaki kuingia kwenye haya mambo ya kishetani

Kurogwa kupo ila bado naamini Mungu ndio mwenye nguvu zaidi na ninamuomba sana
Biashara zetu riziki tunayoipata ndio hiyo hiyo tunaipokea na kushukuru Mungu

Na kama jirani wateja wanajaa kwake ni sawa tu huwa hainipi ushawishi wowote wa kutaka kutafuta mganga ingawa wanakuja watu na kutuambia
Ooh mimi naweza kukupelekea mjuzi anaeweza kufanya wateja wafurike

Huwa nawaambia nendeni nyie mkachukue
Na wote wanaoshawishi wamechoka mbaya, na hapo inazidi kutuongezea imani kwa Mungu na kushukuru kuwa huyu ninamzidi kipato kwa mbali anataka kunipeleka kwa mganga au yeye mwenyewe mganga na hana hata ya panadol

Anyway ni kuchagua kuomba Dua sana au kwenda kwa waganga uamuzi ni wa mtu na mtu ila sidhani kama eti kila mwenye biashara ana ndagu sio kweli

Tangu babu zangu walikuwa wanafanya biashara miaka ya 40 na leo ni 2022 bado tunarithishana biashara zile zile na hata siku moja sijawahi kuambiwa na mzee wetu eti mkikwama nendeni kwa fulani never

Bali huwa ni sala na kumcha Mungu tu
L
 
Mimi na hisi nimerogwa kabisa tena aliye turoga sio mtu mzuri

Sisi tupo watu 7
Wanaume wa 5 na wanawake 2
Tuna ishi uku kwenye inch za wenzetu uku
Ndugu yangu tulivyo fika tu uku mama na baba wakagombanishwa na watu wakachana
Mpaka sasa ivi mimi na familia yangu akuna chochote ambacho tunaweza kufanya pesa tunapata kwa mwezi mimi na familia yangu tuna kusanya dollars 14000 lakini cha ajabu atun hata nyumba ya miti afrika tuna fanya kila tukipokea pesa kwenye familia kuna kuwa vurugo kubwa kila mtu anachukuwa pesa zake hata kama tulikuwa tunapanga kufanya kitu cha maana afrika

Kwa style hii nimehanza kuwa na wasiwasi kabisa mimi si amini uchawi ila kwa style hii naona tumerogwa kabisa
 
Mimi na hisi nimerogwa kabisa tena aliye turoga sio mtu mzuri

Sisi tupo watu 7
Wanaume wa 5 na wanawake 2
Tuna ishi uku kwenye inch za wenzetu uku
Ndugu yangu tulivyo fika tu uku mama na baba wakagombanishwa na watu wakachana
Mpaka sasa ivi mimi na familia yangu akuna chochote ambacho tunaweza kufanya pesa tunapata kwa mwezi mimi na familia yangu tuna kusanya dollars 14000 lakini cha ajabu atun hata nyumba ya miti afrika tuna fanya kila tukipokea pesa kwenye familia kuna kuwa vurugo kubwa kila mtu anachukuwa pesa zake hata kama tulikuwa tunapanga kufanya kitu cha maana afrika

Kwa style hii nimehanza kuwa na wasiwasi kabisa mimi si amini uchawi ila kwa style hii naona tumerogwa kabisa
kateni mawasiliano huku bongo kwa kipindi cha mwaka mzima 2022.
 
Mimi na hisi nimerogwa kabisa tena aliye turoga sio mtu mzuri

Sisi tupo watu 7
Wanaume wa 5 na wanawake 2
Tuna ishi uku kwenye inch za wenzetu uku
Ndugu yangu tulivyo fika tu uku mama na baba wakagombanishwa na watu wakachana
Mpaka sasa ivi mimi na familia yangu akuna chochote ambacho tunaweza kufanya pesa tunapata kwa mwezi mimi na familia yangu tuna kusanya dollars 14000 lakini cha ajabu atun hata nyumba ya miti afrika tuna fanya kila tukipokea pesa kwenye familia kuna kuwa vurugo kubwa kila mtu anachukuwa pesa zake hata kama tulikuwa tunapanga kufanya kitu cha maana afrika

Kwa style hii nimehanza kuwa na wasiwasi kabisa mimi si amini uchawi ila kwa style hii naona tumerogwa kabisa

Hama mji na acha kwenda kwa unaowaona ni wazuri

Wakati mwingine sio uchawi bali ni jicho la hasidi linakupata
Ndugu anaumia unavyopata akikuangilia tu ile husda inakupata

Kaa nao mbali kwa mda na utamjua mbaya wako

Huenda ni huyo unaeishi nae pia maana hata wake/waume huwa wanakurudisha pia labda kisa huwasaidii kwao
 
Sawa usijari!
Unaweza kuwa na biashara Fulani sawa sawa na mtu X...

Wewe ukawa mchapakazi Sana Tena mwenye Hofu ya Mungu ..

Lakini mfanyabiashara X akawa na mtaji wa kawaida Sana Tena Sana.. rakini baada ya muda unashangaa anakupiga gape. Hapo huwa Kuna Siri! Ila Wengi hawataki kusema na wanaficha, Hakuna motivation speaker anaezungumzia kuhusu chuma ulete wao wanaamini katika pay yourself first ya the richest man in the Babylon....

Usione utajiri wa Mo ukajua Ni kurithi tu, ukiacha Mali Kuna vitu vingi sana amerithi...

So wewe Kama mfanyabiashara au mfanyakazi lazima uwe na akili ya kuchangamka...


Nina ndugu yangu Ana hardware zaidi za 10 dar es salaam.
Na migodi shinyanga, Ana mashamba mengi sana...

Ila kila mwaka lazima aende kwa wataalamu kujitapishwa dawa za limbwata anazopewa na wake zake guess what???

Wewe na ukapuku wako bado unamwamini mwanamke!!!!

Uchawi upo hasa wa kurudishana nyuma...

Nakupa my experience!
Nilikuwa na tabia ya kutumi fedha hovyo na pesa yangu huwa inapotea bila kuacha impact yoyote...

Nilijitahidi kusoma Sana vitabu na kubadilisha tabia lakini wapi kitabu Kama... The richest man in the Babylon... Poor Dad rich dad... The mirrioner in the next door na The money formula!!!

Bila manufaaa... Ila baada ya kwenda kwa mtaalamu kujisafisha nilibaini kuwa... Kuna ndugu zangu wanaamini Mimi nitakuja kuwa faraja kwa mzazi wangu

Kwaiyo wkaamua kuweka mazingira kuwa hela yangu isiwe na mchango wowote kwangu na kwa mama Yangu....

Nilikuwa sivai vizuri, sinywi pombe Sina makundi na makundi na hela sina...

Nakupa Siri, huwa Kuna mashetani wao kuja wakati una pesa kukushawishi kwa matumizi yasio na mbele Wala nyuma...

Hii Siri huwezi kusikika kwa mfanyabiashara Au motivation speaker yoyote..

Mwisho#
Miti imeubwa na Mungu Kama Tiba... Tumieni mitishamba...

Mfano baada ya kuweka au kulaza gari lako car parking kwa Malipo Kuna dawa ya mti Shamba unaweka kwenye gari. Au pikipiki

Mwizi akija wewe una amua afe baada ya siku moja .. au akute jiwe kubwa.....

Huoni Nina reduce cost ya kulaza gari kwa kununua mti Shamba????

Mwisho [emoji2]
Aise wapi huko? Niende na mimi.
 
Mwanamke Ni mtu hatari sana, Mimi ni mfano Hai wa Matendo ya ukatili wa Mwanamke:

Hii naongea kutoka Moyoni mwangu wanao Bisha tabia za wanawake hawazijui.

Sikia hii story ya kweli katika Familia yangu,

Mama mkubwa mke wa Baba yangu walio oana na Baba yangu bonge la Harusi ujanani wali Dumu katika ndoa yao kwa miaka 5tu na wakazaa watoto wa3. Ila ugomvi ulikuwa daily tatizo mwanamke Alikuwa hafanyi majukumu yake ya nyumbani bali alipenda sana starehe na waganga kumchezea mume, Mume akapewa taarifa na majirani akafuatilia aka kuta kweli mkewe na vitu vya ajabu kwenye kabati la nguo na kitandani kwenye mto wa Baba na uvunguni kaweka dawa za mitishamba..

Mume kufuatilia vizuri aka gundua Mwanamke pia alikuwa anaiba hela ndani na kujenge kwao.. Wakaachana ndai ya miaka mi5 ya ndoa.

Mzee akachiwa watoto wa3 wadogo sana, akaishi bila mke kwa miaka4 , wazazi wake wakamshauri Aowe mke mwingine baada ya taarifa za yule mke wake kusambaa kuwa anaishi na mawanaume Mwingine Arusha na nimja mzito, wakati kamuachia watoto tena kwenye Nyumba ya kupanga uja nani akiwa na hali ya kawaida sana kimaisha kwa maana ya kipato cha kawaida.

Mzee kweli akajiongeza aka chukua mke mwingin ambaye ndio mama Yangu, tukazaliwa sisi, baada ya miaka kama 25 kupita tukiwa tusha zaliwa watoto6, Baba alisha pandishwa cheo na kusoma zaidi maisha yakawa makubwa na akawa msaidizi wa mkurugenzi wa Bank kuu ya tanzania na baadaye mkuu wa Azina, akawa kesha wekeza sana kila kona ya jiji la Dar na kwao Mkoani..

Ghafl mauza uza ya ugomvi ndani yakaibuka mzee kawa kama anachanganyikiwa haishi kumpiga mama kila mara yaani akawa kama siyo yeye tena.. Mara afukuze watoto mara hili mara lile, Baadaye Mama yangu akaugua ugonjwa wa ajabu sana akabaki mifupa tupu mm nikiwa ndio nimezaliwa nina mwaka 1 , mzee akawa hajali huduma wala hataki kuangali watoto,

Mama akaja kuchukuliwa apelekwe matibabuni, walizunguka mahospitali yote tanzania na ukumbuke hadi kenya na South africa alipelekwa lakini haponi wala ugonjwa hauonekani, Mwishoe akawa anakaribia kukata roho kabaki mifupa tu waka mrudisha Kijijini kwao asubirie kufa tu. Lakini kule kijijini wazee wa upande wa Mama wakajiongeza wakampeleka kwa mtaalamu wa Jadi aka aguliwa na ukweli ukajulikana alitupiwa jini na mke mkubwa na mambo mengine mengi tu.. bahati nzuri akatibiwa akapona akarudi kwenye hali yake baadaye Wakati anarudishwa nyumbani kwa wazazi wake maana alitokea kwa Matibabu ya jadi.. aka kuta watoto wote wame teletwa na kutelekezwa kwa wazazi wote. . wamekonda nusu ya kufa yule mkubwa kuliko wote aliye kuwa ana mika15 ndio kachangnyikiwa wengine wote wameacha shule na hawataki kabisa kusikia shule wala hawajielewi. Wazee wakoo waka jiongeza kuwapokea na kuwalea.

Mama alipo fuatilia aka ambiwa alivyo ondoka tu kwenda matibabuni, Week ile ile Mke mkubwa aliyekuwa ame achana na baba kwa miaka 25 alirudi na kugina ndani kwenye nyumba aliyejenga Mama yetu na Baba, na wakati huo Mzee hajitambui tena kawa kama mjinga wala hakumbuki watoto ana itwa ustawi wa jamii anaulizwa matumizi ya watoto ana sema mbona yeye hana watoto zaidi ya watatu aliyo nao nyumbani,?? watu wakadhani ni utani, kuja kumbana sana wakaagundua kweli hana kumbukumbu .. ila kesi ikaenda mahakamani ika amuliwa ahudumie watoto na aangaliwe kama akili ziko sawa. baadaye Ikaisha kienyeji Majaji wakapewa hongo na yule mke kubwa maana sasa yeye ndio alishikilia account zote za baba na mzee alifukuzwa kazi maana alikuwa haeleweki tena..

Baada ya Muda Baba kaja kufa kiajabu ajabu tu.. tuka mzika, mama mkubwa kaendelea kuishi ndani na wanawe, Ukoo ukasema kuwa kila kitu kwenye nyumba aliyokimbilia kuishi Mke mkubwa nicha watoto wa mke mdogo kwa kuwa Marehemu alisha Andika na kuwambia Wazazi wake kuwa Nyumba ya ujanani aliyo jenga kabla ya mama yangu kuishi naye na kuzaa naye ni ya watoto wake watatu aliye zaa n mke wake wandoa, ila hii mpya aliyojenga akiwa na mke mdogo yaan maa yang ni ya watoto 6 aliyo zaa na mama yangu.. Una ambiwa kile kikao cha ukoo kilivurugika kwa ugomvi mke mkubwa akawa moto na yule aliye kuwa kiongozi wa ukoo alikufa ndani ya week iliyofuata, Kukawa na viongozi wengine wanao chaguliwa Kushika nafasi ya Ukoo ila wakigusia haki za watoto wa mama yangu tu wanakufa, mpaka sasa Ninavyo ongea Baba wakubwa wa5 wote wamekufa kimaajabu. . na haki yetu hatuja ipata .. ndugu zangu karibia wote ni vichaa . nime baki mm tu ndio angalao nina jitambua..ingawa vita ya maisha yangu ni kubwa kama siyo kujificha katika maombi wangesha ni maliza..

Lakin kikubwa kinacho ni shangaza ni kuwa Baba anaonekana kule kijijin watu kazaa wana muona akiwa mchafu na manywele ila waki msogelea anapotea, mwanzoni tulidhani ni utani tukasema labda watu wanongea tu kwa kuwa yaliyotokea kweye familia yangu yameumiza watu wengi hadi majirani wa kule kijiji hivyo wanazusha tu kwa hasira walizo nazo juu ya mateso wanayo yaona kwa ndugu zangu.. Lakin sasa Hivi ni navyo ongea juzi tu mwezi wa kumi na moja mwaka huu uliyoisha. Kaka yangu mkubwa akiwa ndani kwake Katokewa na baba, kaamka zake aka kojoe ghafla akamuona mzee kakaa kwenye kochi ila haongei kitu alipo piga kelele mzee kapotea.


Jamani Uchawi Upo.. Ila naku hakikishia siku nikiingia kwenye Uchawi.. Nita angamizaa kizazi cha huyu Mwanamke mpaka kitukuu cha mwisho.. Naupima tu Uvumilivu wangu katika maombi.. Mungu aniongoze maana naijua nafsi yangu ilivyochoka na siku nikihamia kwa Shetani nitakuwa Shetani Halisi wala sita Igiza kabisa.
Dah pole sana mkuu, ila mama mzazi si bado yupo hai?
 
Sipo hapa kumshawishi mtu aingie kwenye ushirikina, sipo hapa kudharau Imani ya dini ya mtu yoyote... Ila Nipo hapa kusema ukweli...

Watu wanatupa moyo kuhusu mafanikio, wengi wao husema kufanya kazi kwa bidii ndio njia ya mafanikio! Wao huita hiyo ndio Siri!

Lakini Ndugu zangu nipo hapa kuwapa Siri ingine ya mafanikio! Sio kuua mzazi wa kutoa kafara Ila Ni kukulinda...Katina mafanikio au katika biashara yoyote.

Mtu asikuambie mtaji wa laki Tano ndio ulionifanya niwe na nyumba na magari! Tena wanasema nilifanya kazi Sana kwa bidii, na siri ya mafanikio yangu Ni kufanya kazi kwa bidiii! Huo Ni uongo mtupu...

Siri za mafanikio zipo kwenye Siri ya ushirikina moja, Ni wewe kujikinga kupitia ushirikina! Au kukinga biashara yako kwa ushirikina, usipozingatia Ayo maisha yako yatakuwa chini miaka nenda miaka rudi huku ukiona wengine wanashaini

Mchawi kazi yake sio kuroga tu kazi yake ingine Ni kurudisha nyuma maisha yako....

Karibuni 2022.
Uwa namshangaa sana mtu ambae ahamini uchawi, nna jamaa angu uyu bwana aliacha shule tukiwa fomu two.
Eeh beana we baada ya miaka mitatu mbele nakuja kuonana na jamaa nilishangaa sana, jamaa anapesa za kutosha, anamiliki na hotel mjini[emoji2] kuja kuuliza jamaa anatumia mitishamba, na safari zake nyingi ni tanga.
Yapo mengi sana aya mambo
 
Uwa namshangaa sana mtu ambae ahamini uchawi, nna jamaa angu uyu bwana aliacha shule tukiwa fomu two.
Eeh beana we baada ya miaka mitatu mbele nakuja kuonana na jamaa nilishangaa sana, jamaa anapesa za kutosha, anamiliki na hotel mjini[emoji2] kuja kuuliza jamaa anatumia mitishamba, na safari zake nyingi ni tanga.
Yapo mengi sana aya mambo
Uchawi lkn siwezi kuamini kwamba eti una nguvu kiasi kinachosimuliwa na wengi.
 
Sipo hapa kumshawishi mtu aingie kwenye ushirikina, sipo hapa kudharau Imani ya dini ya mtu yoyote... Ila Nipo hapa kusema ukweli...

Watu wanatupa moyo kuhusu mafanikio, wengi wao husema kufanya kazi kwa bidii ndio njia ya mafanikio! Wao huita hiyo ndio Siri!

Lakini Ndugu zangu nipo hapa kuwapa Siri ingine ya mafanikio! Sio kuua mzazi wa kutoa kafara Ila Ni kukulinda...Katina mafanikio au katika biashara yoyote.

Mtu asikuambie mtaji wa laki Tano ndio ulionifanya niwe na nyumba na magari! Tena wanasema nilifanya kazi Sana kwa bidii, na siri ya mafanikio yangu Ni kufanya kazi kwa bidiii! Huo Ni uongo mtupu...

Siri za mafanikio zipo kwenye Siri ya ushirikina moja, Ni wewe kujikinga kupitia ushirikina! Au kukinga biashara yako kwa ushirikina, usipozingatia Ayo maisha yako yatakuwa chini miaka nenda miaka rudi huku ukiona wengine wanashaini

Mchawi kazi yake sio kuroga tu kazi yake ingine Ni kurudisha nyuma maisha yako....

Karibuni 2022.
Hakika wewe ndg yangu Mungu akulinde sana imebidi nikuombeee tuuuu!! una jambo jema mnooooo jf hoyeee!
 
Naona umejaribu kupromote uchawi na ushirikina. Hivyo vitu vina nguvu kwenye maisha yako kama ukiamua kuvipa nguvu.
Uchawi still bado ni teknolojia duni Sana ungekuwa na nguvu kihivyo kama watu wanavyoupa nguvu, dunia Ingekuwa na watu wachache Sana wengi wangeuliwa na wachawi, pili mwafrika asingechukulika utumwani au kutawaliwa na mkoloni kwa kupitia kinga ya uchawi.
Bado uchawi ni kitu duni Sana na ufanya Kazi kwa watu duni.
 
Sikupi connection Ila nakupa Siri ....
Dar es salaam Hakuna mganga kuna Wafanyabiashara..

Dar es salaam Hakuna miti...

Utajiri nenda iringa
mapeNzi nenda mbeya/Tabora
Kinga ya mwili kigoma/ sumbawanga...

Iyo ndio connection yangu kwako.
Mbona still wengi hata huko kwenye hao waganga bado ni masikini Sana.
Kama ni utajiri kwann mganga asiwape ndugu zake wawe matajiri.
 
Lengo kuu la shetani kuwafunza uchawi wanadamu ni kuupunguza uwezo wao wa kufikiri. Maana ndumba, uchawi, ushirikina unapunguza uwezo wa kufikiri. Mtu akiacha kufikiri kwa akili zake alizopewa na Mwenyezi Mungu utumia akili bandia alizopewa na mganga kupitia dawa hapa lengo la shetani huwa limetimia.
Still uchawi ni kitu dhaifu sana na duni na hakika nguvu kubwa Sana kama Jamii inavyoaminishwa. Uchawi Ili utende Kazi ni lazima wapenyeze hofu kwako. Kupitia Hofu utadhurika.
 
watu wanaojifanya wakali pale unapogusia ukweli kuhusu kuwa uchawi hupo na kujifanya kama hawafahamu wakati wapo nyuma ya pazia!.

*sokoni
*mitaani
*kazini
*kwenye biashara zetu.
*biashara zinazo fanana
*ndugu,jirani,jamaa na marafiki.

uchawi hupo ndugu.kama una muamini mungu alafu utaki kumjua shetani !.si ujinga hapo

Dunia hii ni mbaya sana tena kwa nchi zetu hizi tulizopo.

ukiona watu wanamafanikio hata siku moja uwezi sikia anakwambia jikinge wala nenda kwa mtu fulani bali yeye atakwambia fanya kazi kwa bidii !?
Umesahau wengine wako humu JF,
makanisani kifupi nyumba za ibada!
mashuleni huko!
lengo ni wewe ukae ivoivo!! sababu ukifanikiwa roho zinawaumaga sana, tena mnooo km kidonda!! inafika kipindi hawaoni mbele!...kibiashara wale watu wanao kuja mwishoni hatari sana!! ukifunga Duka lako jioni, funga kabisa usikubali kufungua bishara tena! eti mtu amekufuata mwishoni!
 
Sikupi connection Ila nakupa Siri ....
Dar es salaam Hakuna mganga kuna Wafanyabiashara..

Dar es salaam Hakuna miti...

Utajiri nenda iringa
mapeNzi nenda mbeya/Tabora
Kinga ya mwili kigoma/ sumbawanga...

Iyo ndio connection yangu kwako.
Tanga vip? Sikuizi
 
Back
Top Bottom