Mchawi kazi yake ni kuroga urudi nyuma, jilinde

Kuna mambo mengine ni ya kushughulikia ili uepukane nayo,pindi mimba za mke wangu zinatoka bila sababu ya msingi nilidharau akiniambia nimeota tu mimba imeharibika hasubuhi anakuta kweli imeharibika nikaona kawaida,muda ulivyozidi kwenda muhusima wa mchezo ule mwenyewe akaanza kunipa vitisho na mikwala mingi na alifanya mengi sanaa kwa kutaka kumdondosha mke wangu ikawa sifanyi lolote bali kumkinga na hila zile maana ilikua anaweza inuka akaenda ukutani atajibamiza sana kichwa kama haupo karibu anaweza poteza maisha au akiwa karibu na kisu anachukua na kutaka kujidhuru nilisumbuka sanaa huku nikipokea simu za vitisho na sms za vitisho maana alikua mmoja wa ndugu wa mke wangu,nilipochoka kuvumilia haya mateso na kupoteza kipato kidogo nilicho nacho kwa kumuangaikia mke wangu ndipo mateso yote yalipokwisha hadi sasa yupo salama kabisa na mtoto tulipata baada ya mwaka tu..unapokutana na changamoto yoyote ni wewe tu kuamua kuilea au kuimaliza.
 
Uchawi upo na unafanya mengi ila sitaki kuutilia maanani na kuuamini

Hivyo huwa naupuuza sana na kuupinga sana ingawa huwa naona wanaoathirika nayo

Ukiamini uchawi utaamua kuutafuta ili upate kinga au utafute utajiri au mapenzi yaani mradi ujihusishe tu
Ila kwa mimi na familia yetu hatutaki kuingia kwenye haya mambo ya kishetani

Kurogwa kupo ila bado naamini Mungu ndio mwenye nguvu zaidi na ninamuomba sana
Biashara zetu riziki tunayoipata ndio hiyo hiyo tunaipokea na kushukuru Mungu

Na kama jirani wateja wanajaa kwake ni sawa tu huwa hainipi ushawishi wowote wa kutaka kutafuta mganga ingawa wanakuja watu na kutuambia
Ooh mimi naweza kukupelekea mjuzi anaeweza kufanya wateja wafurike

Huwa nawaambia nendeni nyie mkachukue
Na wote wanaoshawishi wamechoka mbaya, na hapo inazidi kutuongezea imani kwa Mungu na kushukuru kuwa huyu ninamzidi kipato kwa mbali anataka kunipeleka kwa mganga au yeye mwenyewe mganga na hana hata ya panadol

Anyway ni kuchagua kuomba Dua sana au kwenda kwa waganga uamuzi ni wa mtu na mtu ila sidhani kama eti kila mwenye biashara ana ndagu sio kweli

Tangu babu zangu walikuwa wanafanya biashara miaka ya 40 na leo ni 2022 bado tunarithishana biashara zile zile na hata siku moja sijawahi kuambiwa na mzee wetu eti mkikwama nendeni kwa fulani never

Bali huwa ni sala na kumcha Mungu tu
L
 
Mimi na hisi nimerogwa kabisa tena aliye turoga sio mtu mzuri

Sisi tupo watu 7
Wanaume wa 5 na wanawake 2
Tuna ishi uku kwenye inch za wenzetu uku
Ndugu yangu tulivyo fika tu uku mama na baba wakagombanishwa na watu wakachana
Mpaka sasa ivi mimi na familia yangu akuna chochote ambacho tunaweza kufanya pesa tunapata kwa mwezi mimi na familia yangu tuna kusanya dollars 14000 lakini cha ajabu atun hata nyumba ya miti afrika tuna fanya kila tukipokea pesa kwenye familia kuna kuwa vurugo kubwa kila mtu anachukuwa pesa zake hata kama tulikuwa tunapanga kufanya kitu cha maana afrika

Kwa style hii nimehanza kuwa na wasiwasi kabisa mimi si amini uchawi ila kwa style hii naona tumerogwa kabisa
 
kateni mawasiliano huku bongo kwa kipindi cha mwaka mzima 2022.
 

Hama mji na acha kwenda kwa unaowaona ni wazuri

Wakati mwingine sio uchawi bali ni jicho la hasidi linakupata
Ndugu anaumia unavyopata akikuangilia tu ile husda inakupata

Kaa nao mbali kwa mda na utamjua mbaya wako

Huenda ni huyo unaeishi nae pia maana hata wake/waume huwa wanakurudisha pia labda kisa huwasaidii kwao
 
Aise wapi huko? Niende na mimi.
 
Dah pole sana mkuu, ila mama mzazi si bado yupo hai?
 
Uwa namshangaa sana mtu ambae ahamini uchawi, nna jamaa angu uyu bwana aliacha shule tukiwa fomu two.
Eeh beana we baada ya miaka mitatu mbele nakuja kuonana na jamaa nilishangaa sana, jamaa anapesa za kutosha, anamiliki na hotel mjini[emoji2] kuja kuuliza jamaa anatumia mitishamba, na safari zake nyingi ni tanga.
Yapo mengi sana aya mambo
 
Uchawi lkn siwezi kuamini kwamba eti una nguvu kiasi kinachosimuliwa na wengi.
 
Hakika wewe ndg yangu Mungu akulinde sana imebidi nikuombeee tuuuu!! una jambo jema mnooooo jf hoyeee!
 
Naona umejaribu kupromote uchawi na ushirikina. Hivyo vitu vina nguvu kwenye maisha yako kama ukiamua kuvipa nguvu.
Uchawi still bado ni teknolojia duni Sana ungekuwa na nguvu kihivyo kama watu wanavyoupa nguvu, dunia Ingekuwa na watu wachache Sana wengi wangeuliwa na wachawi, pili mwafrika asingechukulika utumwani au kutawaliwa na mkoloni kwa kupitia kinga ya uchawi.
Bado uchawi ni kitu duni Sana na ufanya Kazi kwa watu duni.
 
Sikupi connection Ila nakupa Siri ....
Dar es salaam Hakuna mganga kuna Wafanyabiashara..

Dar es salaam Hakuna miti...

Utajiri nenda iringa
mapeNzi nenda mbeya/Tabora
Kinga ya mwili kigoma/ sumbawanga...

Iyo ndio connection yangu kwako.
Mbona still wengi hata huko kwenye hao waganga bado ni masikini Sana.
Kama ni utajiri kwann mganga asiwape ndugu zake wawe matajiri.
 
Lengo kuu la shetani kuwafunza uchawi wanadamu ni kuupunguza uwezo wao wa kufikiri. Maana ndumba, uchawi, ushirikina unapunguza uwezo wa kufikiri. Mtu akiacha kufikiri kwa akili zake alizopewa na Mwenyezi Mungu utumia akili bandia alizopewa na mganga kupitia dawa hapa lengo la shetani huwa limetimia.
Still uchawi ni kitu dhaifu sana na duni na hakika nguvu kubwa Sana kama Jamii inavyoaminishwa. Uchawi Ili utende Kazi ni lazima wapenyeze hofu kwako. Kupitia Hofu utadhurika.
 
Umesahau wengine wako humu JF,
makanisani kifupi nyumba za ibada!
mashuleni huko!
lengo ni wewe ukae ivoivo!! sababu ukifanikiwa roho zinawaumaga sana, tena mnooo km kidonda!! inafika kipindi hawaoni mbele!...kibiashara wale watu wanao kuja mwishoni hatari sana!! ukifunga Duka lako jioni, funga kabisa usikubali kufungua bishara tena! eti mtu amekufuata mwishoni!
 
Sikupi connection Ila nakupa Siri ....
Dar es salaam Hakuna mganga kuna Wafanyabiashara..

Dar es salaam Hakuna miti...

Utajiri nenda iringa
mapeNzi nenda mbeya/Tabora
Kinga ya mwili kigoma/ sumbawanga...

Iyo ndio connection yangu kwako.
Tanga vip? Sikuizi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…