Mchawi kazi yake ni kuroga urudi nyuma, jilinde

Mchawi kazi yake ni kuroga urudi nyuma, jilinde

Sikupi connection Ila nakupa Siri ....
Dar es salaam Hakuna mganga kuna Wafanyabiashara..

Dar es salaam Hakuna miti...

Utajiri nenda iringa
mapeNzi nenda mbeya/Tabora
Kinga ya mwili kigoma/ sumbawanga...

Iyo ndio connection yangu kwako.
Alafu Tiba ya laki moja kigoma vijijini Ni Tiba ya 1m dar es salaam!
Kutokana na ugumu wa maisha vijijini pesa Ina Thamani...

So ukitengeneza kwa laki sita mkoani kwa dar es salaam Ni zaidi ya 7m.
Trust me.
 
Uchawi ni imani na nguvu inayo fanya kazi kwa siri kubwa miongon mwa jamii nyingi za kiafrika na kwengineko Ulimwenguni ,matumizi yake halisi yapo kwa muhusika mwenyewe yaliyo mengi ni simulizi za kusadikika ,Unayo nafasi ya kuuishi Uchawi ikiwa utaona yafaa zaidi kwa mambo yako(Mafanikio) ,Yote katika yote maamuzi ni ya kila mtu
(MWENYEZI MUNGU YUPO) (UCHAWI UPO)
 
Uchawi ni imani na nguvu inayo fanya kazi kwa siri kubwa miongon mwa jamii nyingi za kiafrika na kwengineko Ulimwenguni ,matumizi yake halisi yapo kwa muhusika mwenyewe yaliyo mengi ni simulizi za kusadikika ,Unayo nafasi ya kuuishi Uchawi ikiwa utaona yafaa zaidi kwa mambo yako(Mafanikio) ,Yote katika yote maamuzi ni ya kila mtu
(MWENYEZI MUNGU YUPO) (UCHAWI UPO)
Fact kiongozi [emoji120]
 
Nimeishi ulaya na bado nakwenda ulaya, uchawi upo ulaya tena mkubwa sana ila matumizi ndio tofauti.

Hawatumii uchawi kumtia mtu nuksi.

Mfano leo ni mwaka mpya sehemu nyingi ulaya usiku watawasha moto mkubwa sana wa kuni ikiwa ni matambiko ya imani zao lakini ni za kishirikina pia.
Mzungu siku hizi harogi kukurudisha nyuma anatumia tu policies na sheria alizoweka. Na wewe kumshinda tumia hizo hizo sheria
 
Mungu alimuumba mwanadamu akiwa kakamilika kwa kumpatia akili Ili avitawale vyote vilivyomo.
Shetani kupitia majini ndio waliomfunza mwanadamu uchawi kwa lengo kuu moja ni kuupunguza uwezo wa kufikiri wa mwanadamu aache kutumia akili zake alizopewa na Mwenyezi Mungu bali ategemee ushirikina ktk kutatua changamoto zake.Washirikina na wachawi wameharibu mindset za waafrika wengi kwa kuwaamisha huwezi fanya jambo iwe biashara,kilimo, elimu, mahusiano, kuchimba madini nk bila ndumba huu ni uwongo mkubwa kabisa lengo lake ni kufifisha uwezo wa kufikiri, wenzetu wazungu baada ya kuijua Siri hii ya kwamba ushirikina unapunguza uwezo wa kufikiri kwa kuleta utegemezi wa fikra wakaamua kuachana na fikra za kuamini ushirikina ikiwemo hata kuwaua na kuharibu kabisa Kazi za wachawi lengo kuu lilikuwa ni kupata Jamii inayotumia akili ilizopewa na Mwenyezi Mungu Ili kutatua changamoto mbalimbali.
Unapokuja mtazamo wa maendeleo waliotumia akili zao wenyewe Wana maendeleo makubwa Sana sababu wanatumia akili zao wenyewe tofauti na sisi waafrika tunaotumia akili na mawazo ya kishirikina.
Mtu yeyeto au Jamii yeyeto inayohusudu ushirikina uwezo wake wa kufikiri upo chini sana.
 
Back
Top Bottom