Mchawi wa mwanamke ni mwanamke mwenyewe, tuache kulaumu wanaume

Mchawi wa mwanamke ni mwanamke mwenyewe, tuache kulaumu wanaume

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Mwanamke anataka jamii imtambue kama mtu dhaifu anaehitaji kulishwa, kutunzwa na kutunduliwa na mwanaume, anaona ni sawa lazima atolewe mahari na kuhurumiwa sana na kupewa upendeleo na wanaume.

Mwenyezimungu amewaumba viumbe wake wote sawa bila upendeleo wowote ila tofauti unazoziona baina ya viumbe ni kwasababu ya kazi zao kwenye uso wa dunia na kuepusha kugombania vyakula na makazi. Ndio maana ndege anaruka na binadamu anatembea, mchwa anaozesha vitu viwe mbolea majani yamee binadamu hawezi.

Lakini pamoja na tofauti hizi zote viumbe vuote vinapumua, vinazaa, vinajisaidia haja kubwa na ndogo, vinahisi, vinakula, vinasogea. Mke na mume wako sawa kwa viumbe vyite isipokuwa mifumo yao ya uzazi tu basi.

Majike yoote ya viumbe vingine yanajilisha, yanajitunza na kujitafutia na kupambana isipokuwa majike ya binadamu tu ambayo yanataka huruma za kusaidiwa vitu vyote la sivyo unapelekwa mahakamani kwanini humpi chakula. Majike ya simba, mbuzi, fisi, kuku, mbweha, nguchilo na mengine yote yanazaa, kutuza watoto wao na kujilisha, majike ya binadamu yanatafuta huruma za wanaume kwenye mambo yao? HII itawachelewesha sana. Jike la simba halisubiri dume likamate nyumbu ili yeye na watoto wake wale, kuku hivyohivyo, nyoka hivyohivyo.

Wanawake msisubiri huruma za wanaume fanyeni yote kama wanaume isipokuwa kwenye taratibu za kuzaa tu na uzazi baaaaasi. Jikomeesheni wenyewe vitu vyote vya kuwafanya muwe tegemezi kwa:

1. Kuamua bila kujali mwanaume atasema nini
2 fanya kazi zote sawa na wanaume isipokuwa kwwnye uzazi tu
3 Nendeni shuleni kama wanaume
4. Gombeeni kama wanaume
5. Pigeni vita sheria na kanuni za kupendelewa nanaume, zinazidi kuwadidimiza.
6. Pingeni kuolewa kwa mahari, kunakowageuza kuwa bidhaa. Hata utumie kugha gani mahari ni bei ya kununua mwanamke kutoka kwa wazazi wake.
 
Ishini nao kwa akili. Mwanamke sio mnyonge na wala sio dhaifu.. wanaweza wakiwa na wanaume wenye akili
 
Ujumbe umepokelewa kwa ukamilifu, Asante kwa niaba.
 
Kwahiyo unataka kusema kupitia uzi wako wanaume tunatakiwa kujaza mimba na kupita na hamsini zetu kama dume la simba
Hewaaa, yaaani wanawake hawa wana akili na nguvu sana na wamejaliwa vitu vingi kuliko wanaume. Akiwa na mimba anaweza kufanyakazi za ofisini, shambani, kuchota maji na kukata kuni mbali, kupika na kazi zote za mwanamke. Kosa la mwanamke ni kudhani kuwa wanatakiwa kuwapikia, kuwafulia, kuwatii wanaume kwakuwa wametoa mahari. Uhusiano wa mwanamke na mwanaume ni kwenye kusex tu baaasi, baada ya hapo hahitajiki tena aende zake kama wanavyokwenda madume ya kuku, mbuzi, tumbili na mijumsi.

Watoto wanaolelewa na baba hawana vipaji, baba anaua vipaji vyote vya watoto kwa vipigo, kukemea na achaacha nyingi kwa watoto wao. Ndio maana watoto wa mitaani na watoto wanaolelewa na mama pekee wana talents nyingi kuliko watoto wenye baba nyumbani
 
Mwanamke anataka jamii imtambue kama mtu dhaifu anaehitaji kulishwa, kutunzwa na kutunduliwa na mwanaume, anaona ni sawa lazima atolewe mahari na kuhurumiwa sana na kupewa upendeleo na wanaume.

Mwenyezimungu amewaumba viumbe wake wote sawa bila upendeleo wowote ila tofauti unazoziona baina ya viumbe ni kwasababu ya kazi zao kwenye uso wa dunia na kuepusha kugombania vyakula na makazi. Ndio maana ndege anaruka na binadamu anatembea, mchwa anaozesha vitu viwe mbolea majani yamee binadamu hawezi.

Lakini pamoja na tofauti hizi zote viumbe vuote vinapumua, vinazaa, vinajisaidia haja kubwa na ndogo, vinahisi, vinakula, vinasogea. Mke na mume wako sawa kwa viumbe vyite isipokuwa mifumo yao ya uzazi tu basi.

Majike yoote ya viumbe vingine yanajilisha, yanajitunza na kujitafutia na kupambana isipokuwa majike ya binadamu tu ambayo yanataka huruma za kusaidiwa vitu vyote la sivyo unapelekwa mahakamani kwanini humpi chakula. Majike ya simba, mbuzi, fisi, kuku, mbweha, nguchilo na mengine yote yanazaa, kutuza watoto wao na kujilisha, majike ya binadamu yanatafuta huruma za wanaume kwenye mambo yao? HII itawachelewesha sana. Jike la simba halisubiri dume likamate nyumbu ili yeye na watoto wake wale, kuku hivyohivyo, nyoka hivyohivyo.

Wanawake msisubiri huruma za wanaume fanyeni yote kama wanaume isipokuwa kwenye taratibu za kuzaa tu na uzazi baaaaasi. Jikomeesheni wenyewe vitu vyote vya kuwafanya muwe tegemezi kwa:
1. Kuamua bila kujali mwanaume atasema nini
2 fanya kazi zote sawa na wanaume isipokuwa kwwnye uzazi tu
3 Nendeni shuleni kama wanaume
4. Gombeeni kama wanaume
5. Pigeni vita sheria na kanuni za kupendelewa nanaume, zinazidi kuwadidimiza.
6. Pingeni kuolewa kwa mahari, kunakowageuza kuwa bidhaa. Hata utumie kugha gani mahari ni bei ya kununua mwanamke kutoka kwa wazazi wake.
Hii mada ya hovyo sana,
Mtu,jamii ya watu waliteswa na mifumo,siku zote na wao watatesa wengine,ukisema mchawi wa mwanamke ni mwanamke,basi hata mchawi wa Mtu mweusi ni mweusi mwenzie!
Haivi umeishawahi kuona watu wanapoishi uswahili wanavyochukiana Richa ya kwamba wote ni mafukara?!!
Mchawi wa mwanamke ni mfumo uliomfsnya hivyo,maana hata mwanamke mwenzie ni muhanga wa mfumo,
Kibaka akiiba kuku,anapigwa mpaka afe,fisadi akiiba bilioni 5!hakuna maskini wa kwenda hata masaki arushe jiwe kwenye nyumba yake,
Wanawake ni victim wa mfumo,
 
Ni kweli na ingependeza mahariwatoe wanawake pia...

Asili hazipotei....ukilazimisha kugeuza matokeo ndio hayo..hakuna maisha ya kijamii na maadili... kupotea..

Mwanamme ni kichwa na mwanamke ni.mwili...

Hapo ndio akili kumkichwa...
 
Yaan ukiwa huna hela unawaza vitu ambavyo ni kinyume na wenzio toka dunia iumbwe
Critical thinking haimaanishi ufikirie sawa na wengine bro. Wanawake wanadai uhuru kutoka kwa watu wasiostahili, Mungu wao tayari ameshawapa uhuru siku moja pamoja na viumbe wengine. Hawahitaji huruma, msaada wala ruhusa za wanaume ili wawe wanachotaka kuwa kama vile wanaume wasivyohitaji ruhusa za wanawake ili wawe wanavyotaka kuwa. Makutano muhimu ya pekee ya mume n mke ni wakati wa kutafuta mimba baaasi. Mwanamke anaweza kuwa bondia, askari, rubani, msukuma mkokoteni, mwashi, mwindaji. nk kama mwanaume, ni yeye tu. Mim nikiwasikia wanalala majukwaani wanadai pedi za kike nacheka sana, viti maalumu, madawati ya kijisia, ukeketaji. Nk
 
Hii mada ya hovyo sana,
Mtu,jamii ya watu waliteswa na mifumo,siku zote na wao watatesa wengine,ukisema mchawi wa mwanamke ni mwanamke,basi hata mchawi wa Mtu mweusi ni mweusi mwenzie!
Haivi umeishawahi kuona watu wanapoishi uswahili wanavyochukiana Richa ya kwamba wote ni mafukara?!!
Mchawi wa mwanamke ni mfumo uliomfsnya hivyo,maana hata mwanamke mwenzie ni muhanga wa mfumo,
Kibaka akiiba kuku,anapigwa mpaka afe,fisadi akiiba bilioni 5!hakuna maskini wa kwenda hata masaki arushe jiwe kwenye nyumba yake,
Wanawake ni victim wa mfumo,
Hakuna mfumo uliotesa watu, kama majike ya viumbe wengine kama nyumbu yaliweza kuepuka mfumo dume kwanini majike yetu yameshindwa? Kwaasili madume ya viumbe vyote yana wivu wa kutaka kumiliki wanawake wengi , lakini wivu wao unaishia kupigana yenyewe kwa yenyewe hadi ajulikane Nani ana nguvu zaidi kushinda wengine lakini hiyo haiwahusu wanawake.

Wanawake wakiungana hakuna mwanaume anayeweza kuingilia mifuko Yao kwakuwa wanawake Wana akili, Wana nguvu na wako wengi ndani ya jamii. Shida Yao wanawake hawapendani kabisaaaaaa. Hawezi kumchagua mwanamke mwenzao kuwa kinara kwenye jamii. Vitabu vya dini vilivyoandikwa na wanaume vikazidi kumdidimiza mwanamke hadi basi.

Women workup hakuna kuomba uhuru wenu chukueni. Uhuru wenu unaporwa na utegemezi wenu kwa wanaume, eti mlishwe, mvalishwe, mnunuliwe heleni na wanaume. Endesheni maguta barabarani
 
Kama unataka kuwa na hali nzuri ya kifedha mruhusu mkeo afanyekazi, mpe uhuru na acha wivu, hutalala na njaa hata siku moja
Ila vumilia maneno yao,maana wakitoa hana mia kusapoti maneno mtaa mzima hali sisi tunawapa hadi milioni na wala ukumbi.
Mentality za kupewa ni shida
 
Ila vumilia maneno yao,maana wakitoa hana mia kusapoti maneno mtaa mzima hali sisi tunawapa hadi milioni na wala ukumbi.
Mentality za kupewa ni shida
Tabia hii ya kupenda kupewa ndiyo inayowapiga mweleka wanawake, maana yule aliyelipa ndio anachagua wimbo. Ukienda baa ukamkuta dada mzuri kakaa peke yake mezani na kachafua meza kwa bia za kujilipia mwenyewe kwa hela yake, wewe mwanaume utambabaisha na nini? Simtapatana kwa kupenda mwenyewe?
 
NILIWAHI KUSIKIA KUWA WANAWAKE KUWA HAWAPENDANI(SIO WOTE) BADO NAFANYA TAFITI
 
HAMPENDANI HASA KWENYE ISHU ZA MAENDELEO, ANNA AKIMUONA BERTHA KAFANIKIWA ATAMNUNIA KISA TU KAPIGWA GEPU
Baadhi sio wote.

Mimi hiyo roho ya ajabu siwezi kuruhusu ktk maisha yangu.
Huwa nikimuona mwanamke mpambanaji nafurahi sana
 
Eh we jamaa mbona unataka ku'destabilize misimamo ya Mwenyezi Mungu?
 
Back
Top Bottom