Mchengerwa aagiza Mchakato wa uanzishwaji wa Mamlaka ya Uendelezaji wa Jjiji la Dar uanze

Mchengerwa aagiza Mchakato wa uanzishwaji wa Mamlaka ya Uendelezaji wa Jjiji la Dar uanze

Mtoa Taarifa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2024
Posts
213
Reaction score
671
IMG_20241024_153907_444.jpg

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Raia Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Mohamed Mchengerwa ameelekeza mchakato wa uanzishaji wa Mamlaka ya Uendelezaji wa Jiji la Dar es salaam uanze mara moja ili kurataibu maendeleo yote yanayofanyika kwenye halmashauri za mkoa wa Dar es salaam.

Mhe. Mchengerwa ameyasema hayo katika hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa barabara katika halmashauri tano za Mkoa wa Dar es salaam leo tarehe 24.10. 2024 kwenyz viwanja vya Mwengeyanga Manispaa ya Temeke.

Amesema Mkoa wa Dar es salaam unatakiwa kuwa Kioo cha nchi yetu na wageni wote wanapokuja hapa wanatakiwa kuona sura ya Tanzania hivyo mkoa huu unatakiwa na chombo kinachoratibu maendeleo ya mji huu na kuhakikisha kuwa mipango yote ya maendeleo inayofanyika hapa inakua na muunganiko ili kulete ile sura tunayoitegemea.

Ameongeza kuwa kupitia Mradi wa Uendelezaji wa Jiji ma Dar es salaa awamu ya Pili (DMDP II) kuna miradi mikubwa inayotekelezwa kama ya uboreshaji wa miundombinu ya barabara na uendelezaji wa bonde la mto msimbazi, miradi mikubwa kama hii ikiachwa kwenye halmashauri inaweza isiweze kujiendesha hivyo kuwe na chombo cha kusimamia miradi mikubwa kama hii na kuhakikisha inaungana na jitihada zingine za maendeleo zinazofanywa katika halmashauri za mkoa huu.

Hata majiji makubwa duniani yote yanakuwa na ‘Metropolitan City’ na sio halmashauri zinazojitemea kila moja inapangwa kivyake kunatakiwa kuwa na chombo ambacho kinaunganisha jitihada zinazofanywa kwenye halmashauri zote na kuzitaribu ili Jiji husika liweze kukua kwa viwango vya kimataifa.

Nataka hii Dar es salaam iwe ya viwango na ubora na ukuaji wake uratibiwe kwa taratibu maalumu na sio kukua kiholela tu hii itafanya hadhi ya Dar es salaam isikue haraka na kuwa na hadhi ya kimaraifa.

TAMISEMI
 
Pamoja na kurejesha Jiji la Dar, inafaa kuanzishwe Dar metropolitan Authority Ili kusimamia mambo ya Jiji la Dar.👇👇

======
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, ametoa agizo la haraka kwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo kuhakikisha mchakato wa uanzishwaji wa Jiji la Dar es Salaam unakamilika kabla ya mwaka 2025.Waziri Mchengerwa ametoa agizo hilo Oktoba 24, 2024, wakati wa hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa barabara katika halmashauri tano za Mkoa wa Dar es Salaam, hafla iliyofanyika katika Uwanja wa Mwembeyanga, Temeke, mkoani humo."

Ni lazima Dar es Salaam hii, hapa ndipo makao makuu na kitovu cha biashara... Dar es Salaam hii tukiijenga vyema maana yake taifa letu litaongeza mapato, kodi zitaongezeka, wageni mbalimbali watakuja hapa kuishi na kufanya biashara," amesema Waziri Mchengerwa.Aidha amesisitiza umuhimu wa kuboresha miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya kukuza uchumi na kuongeza mapato ya serikali.

Ameainisha kwamba ujenzi wa masoko, ukarabati wa barabara, na utekelezaji wa miradi mingine mikubwa ya maendeleo unaolenga kuboresha hali ya miundombinu ya Dar es Salaam unapaswa kwenda sambamba na uanzishwaji wa Jiji la Dar es Salaam."Tunajenga masoko, tunakarabati na kujenga barabara zote; karibu kilomita 250 zimezungumzwa hapa, na mikataba inakwenda kusainiwa leo," amesema Waziri Mchengerwa.

Ameeleza kuwa tayari mikataba ya ujenzi wa barabara hizo itasainiwa na kuanza kutekelezwa mara moja, akisisitiza kuwa mji wa Dar es Salaam una nafasi muhimu sana katika kuchangia uchumi wa nchi. Aidha, Waziri Mchengerwa amewataka watendaji wa wizara yake kufanya kazi kwa ufanisi na kuharakisha mchakato wa kuanzishwa kwa jiji hilo, akisisitiza kuwa agizo hilo ni sehemu ya maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan.

"Mchakato wa uanzishwaji wa jiji la Dar es Salaam usichelewe ufanyie mara moja...Wataalamu wapo, waharakishe wasinichokonoechokonoe," amesema Waziri huku akitoa angalizo kwa Katibu Mkuu wa TAMISEMI.Wakati wa hafla hiyo, Waziri Mchengerwa amebainisha kuwa maboresho ya miundombinu yanayofanyika jijini Dar es Salaam ni sehemu ya juhudi za serikali kuboresha huduma za kijamii na kuongeza tija katika sekta mbalimbali za kiuchumi.

Kwa mujibu wa Mchengerwa, utekelezaji wa mikataba ya ujenzi wa barabara zenye urefu wa karibu kilomita 250 katika mkoa wa Dar es Salaam ni hatua muhimu kuelekea katika kutengeneza jiji lenye miundombinu ya kisasa na ya kuvutia zaidi.
 
Back
Top Bottom