Mchengerwa aagiza Mchakato wa uanzishwaji wa Mamlaka ya Uendelezaji wa Jjiji la Dar uanze

Mchengerwa aagiza Mchakato wa uanzishwaji wa Mamlaka ya Uendelezaji wa Jjiji la Dar uanze

Dar es salaam ianzishwe mara ngapi, Dar imebanana mno, hayo ilibidi yakafanyike Dodoma, ingesaidia kupunguza msongamano wa watu na changamoto zisizo za lazima. Watu wakienda kujenga mabondeni watasema serikali haihusiki...đź’€
 
Jiwe alikuwa mwehu yule.

Alikuwa anatafuta gia ya kutaka kukipatia hadhi ya jiji kile kile Kijiji bjs cha Chato.

Alikuwa mshamba na mjinga sana yule jamaa.
Sijaelewa ilikuwaje Dar ikawa jiji ilihali haikuwa kuwa Wilaya wala Manispaa?
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, ametoa agizo la haraka kwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo kuhakikisha mchakato wa uanzishwaji wa Jiji la Dar es Salaam unakamilika kabla ya mwaka 2025.

Hivi wadau mnambuka kuwa Rais Magufuli alivunja rasmi halmshauri ya jiji la Dar es salaam na kuipandisha hadhi halmashauri ya Ilala kuwa Jiji, Februari 24, 2021?

==========

Waziri Mchengerwa ametoa agizo hilo Oktoba 24, 2024, wakati wa hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi wa barabara katika halmashauri tano za Mkoa wa Dar es Salaam, hafla iliyofanyika katika Uwanja wa Mwembeyanga, Temeke, mkoani humo.

"Ni lazima Dar es Salaam hii, hapa ndipo makao makuu na kitovu cha biashara... Dar es Salaam hii tukiijenga vyema maana yake taifa letu litaongeza mapato, kodi zitaongezeka, wageni mbalimbali watakuja hapa kuishi na kufanya biashara," amesema Waziri Mchengerwa.

Aidha amesisitiza umuhimu wa kuboresha miundombinu katika Jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya kukuza uchumi na kuongeza mapato ya serikali. Ameainisha kwamba ujenzi wa masoko, ukarabati wa barabara, na utekelezaji wa miradi mingine mikubwa ya maendeleo unaolenga kuboresha hali ya miundombinu ya Dar es Salaam unapaswa kwenda sambamba na uanzishwaji wa Jiji la Dar es Salaam.

"Tunajenga masoko, tunakarabati na kujenga barabara zote; karibu kilomita 250 zimezungumzwa hapa, na mikataba inakwenda kusainiwa leo," amesema Waziri Mchengerwa.

Pia soma:
Rais Magufuli aivunja Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na kuipandisha hadhi Halmashauri ya Manispaa ya Ilala

Ameeleza kuwa tayari mikataba ya ujenzi wa barabara hizo itasainiwa na kuanza kutekelezwa mara moja, akisisitiza kuwa mji wa Dar es Salaam una nafasi muhimu sana katika kuchangia uchumi wa nchi.

Aidha, Waziri Mchengerwa amewataka watendaji wa wizara yake kufanya kazi kwa ufanisi na kuharakisha mchakato wa kuanzishwa kwa jiji hilo, akisisitiza kuwa agizo hilo ni sehemu ya maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan.

"Mchakato wa uanzishwaji wa jiji la Dar es Salaam usichelewe ufanyie mara moja...Wataalamu wapo, waharakishe wasinichokonoechokonoe," amesema Waziri huku akitoa angalizo kwa Katibu Mkuu wa TAMISEMI.

Wakati wa hafla hiyo, Waziri Mchengerwa amebainisha kuwa maboresho ya miundombinu yanayofanyika jijini Dar es Salaam ni sehemu ya juhudi za serikali kuboresha huduma za kijamii na kuongeza tija katika sekta mbalimbali za kiuchumi.

Kwa mujibu wa Mchengerwa, utekelezaji wa mikataba ya ujenzi wa barabara zenye urefu wa karibu kilomita 250 katika mkoa wa Dar es Salaam ni hatua muhimu kuelekea katika kutengeneza jiji lenye miundombinu ya kisasa na ya kuvutia zaidi.

TAMISEMI
Hayo ndiyo maamuzi sahihi CCM acheni kukurupuka katika maamuzi nchi si mali ya kiongozi bali ni mali ya Raia.
 
Kwenye hili nakubaliana na Mchengerwa,jiji la Dar es Salaam lipo tofauti na majiji mengine. Majiji mengine wamechukua lile eneo la mjini ndiyo imepewa hadhi ya jiji na kuziacha zile halmashauri za pembezoni kuwa manispaa na halmashauri za miji lakini Dar es Salaam yote ni mjini hivyo huwezi kuifanya wilaya ya Ilala tu ndiye iwe jiji halafu uiache Kinondoni, Oysterbay,Masaki n.k eti ziwe katika manispaa hii siyo kweli.

Tena napendekeza liundwe jiji kama ilivyokuwa awamu ya kwanza na ya pili kwamba halmashauri ya jiji iwe moja na iwe na kanda za Ilala,Kinondoni, Temeke,Ubungo na Kigamboni lakini Mkurugenzi ni mmoja tu hao wa kanda waitwe vyovyote lakini bosi wao ni mmoja tu isiwe kama jiji lilovunjwa na Magufuli ambapo wilaya zote zilikuwa manispaa na jiji likawa lipo kisanii tu lisilo na jukumu wala nguvu yoyote kwa sababu kila halmashauri ilikuwa ndiyo wenye ardhi,shule,vituo vya afya n.k.
 
Dar ilishapitia hatua zote hizo kabla wengi wenu hamjazaliwa.

Wakati nchi unapata uhuru Mkoa wa pwani kwenye eneo la Mzizima ndio kilikuwa na watu wengi 30,000.
 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, ametoa agizo la haraka kwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo kuhakikisha mchakato wa uanzishwaji wa Jiji la Dar es Salaam unakamilika kabla ya mwaka 2025.



TAMISEMI
Hizo Wilaya za Dar ziwe majijini, halafu kuwe na Greater Dar es Salaam halafu hizo nyingine ziwe miji ndogondogo.
 
Kumbe wakati inaamuliwa Jiji la DSM kuvunja, Makamo wake hakupendezwa au yeye hakuwa sehemu ya Serikali?

Kuanzisha tena Jiji la DSM pamoja na uwepo wa Faida zake, lakini ni gharama Kwa Serikali.

Ni mzigo Kwa Wananchi
 
Kwenye hili nakubaliana na Mchengerwa,jiji la Dar es Salaam lipo tofauti na majiji mengine.
Majiji mengine wamechukua lile eneo la mjini ndiyo imepewa hadhi ya jiji na kuziacha zile halmashauri za pembezoni kuwa manispaa na halmashauri za miji lakini Dar es Salaam yote ni mjini hivyo huwezi kuifanya wilaya ya Ilala tu ndiye iwe jiji halafu uiache Kinondoni, Oysterbay,Masaki n.k eti ziwe katika manispaa hii siyo kweli.
Tena napendekeza liundwe jiji kama ilivyokuwa awamu ya kwanza na ya pili kwamba halmashauri ya jiji iwe moja na iwe na kanda za Ilala,Kinondoni, Temeke,Ubungo na Kigamboni lakini Mkurugenzi ni mmoja tu hao wa kanda waitwe vyovyote lakini bosi wao ni mmoja tu isiwe kama jiji lilovunjwa na Magufuli ambapo wilaya zote zilikuwa manispaa na jiji likawa lipo kisanii tu lisilo na jukumu wala nguvu yoyote kwa sababu kila halmashauri ilikuwa ndiyo wenye ardhi,shule,vituo vya afya n.k.
Jiji wakati wa awamu ya tano lilivunjwa kwakuwa lilikuwa linahang tu halina vyanzo vyake binafisi wala eneo la kiutawala na lilikuwa linategemea manispaa kuingiza kipato.

Lilikuwa mzigo tu. Hawa wanasiasa wanatuchanganya na Dana Dana zao kila siku.

Kwa staili hii ya kupiga hatua moja na kurudi nyuma maendeleo tuyasikie kwa wengine tu.

Huyo mchengerwa apambane na mwendokasi kwanza wateja wapo ila mabasi hakuna.
 
Back
Top Bottom