Mchengerwa awashukia maofisa ‘wanaobania’ watumishi kupanda madaraja

Mchengerwa awashukia maofisa ‘wanaobania’ watumishi kupanda madaraja

Ze Bulldozer

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2020
Posts
1,070
Reaction score
568
mchengerwa pic

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa amewaagiza waajiri wote nchini kuchukua hatua kuwaondoa katika nafasi zao baadhi ya maofisa utumishi walioshiriki kuficha sifa za watumishi wenzao hali iliyosababisha kutopandishwa madaraja.

===
Arusha. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa amewaagiza waajiri wote nchini kuchukua hatua kuwaondoa katika nafasi zao baadhi ya maofisa utumishi walioshiriki kuficha sifa za watumishi wenzao hali iliyosababisha kutopandishwa madaraja.

Akizungumza katika mafunzo ya viongozi wa matawi ya Chama cha wafanyakazi wa Serikali na Afya (Tughe) na waajiri yaliyofanyikia jijini Arusha, Mchengerwa amesema waajiri waende kuwashusha vyeo maofisa utumishi hao na nafasi hizo wawekwe watu wenye uwezo ambao watakuwa tayari kusikiliza kero za watumishi wenzio.

Amesema si watumishi ambao wapo katika ofisi kwa ajili ya matumbo yao hiyo haikubaliki hivyo ni lazima kila mmoja akabadilisha mitazamo yake kwa sababu Serikali ya sasa haitaki uonevu.

"Kila kiongozi lazima atengeneze ushawishi wa kuleta mapinduzi ya kifkra kama tunakuwa na watendaji ambao hawapendi kuona wenzao wanafanikiwa na wakipewa nafasi wanadhani miji yote ya kwao, hawafahamu kuwa vyeo hivi ni vya kupita tu pia wanasahau kwamba utumishi wa umma una muda," amesema waziri huyo.

Waziri huyo amehimiza waajiri kujenga utamaduni wa kuwajengea uwezo watumishi wao ili kuweza kupata weledi na kuleta uelewa ambao utakwenda kutoa kasoro ambazo zitakwenda kuleta ajali kazini.

Naye Katibu Mkuu wa Tughe, Hery Mkunda amesema mafunzo hayo yanalenga kuleta uelewa wa pamoja katika masuala ya waajiri na watumishi lakini pamoja na ushirikiano huo bado wanakabiliwa na changamoto ya uwepo wa baadhi ya vifungu vya sheria na kanuni ambazo zinaweza kuleta mgongano katika utendaji kazi.

Source: Mwanachi
 
Huyu Waziri hakika atarudisha amani na ari kwa watumishi walio kuwa wamevunjika mioyo kutokana na matendo ya viongozi wao wa juu kuwavuruga na kuwaonea.

lkn bado anakazi ngumu sana ya kuwabaini viongozi wenye roho mbaya na wanao waumiza watumishi wa chini, anatakiwa aingie ndani zaidi ndipo atabaini uonevu mkubwa unao fanywa na watendaji dhidi ya watumishi wa chini na haswa wasio na godfather wana umizwa sana makazini.

Mungu amlinde na ambarizi zidi kwa nia yake ya kuondoa dhuluma na unyanyasaji unaoendwlea ndani ya watumishi wenyewe kwa wenyewe.
 
Huyu Waziri hakika atarudisha amani na ari kwa watumishi walio kuwa wamevunjika mioyo kutokana na matendo ya viongozi wao wa juu kuwavuruga na kuwaonea.

lkn bado anakazi ngumu sana ya kuwabaini viongozi wenye roho mbaya na wanao waumiza watumishi wa chini, anatakiwa aingie ndani zaidi ndipo atabaini uonevu mkubwa unao fanywa na watendaji dhidi ya watumishi wa chini na haswa wasio na godfather wana umizwa sana makazini.

Mungu amlinde na ambarizi zidi kwa nia yake ya kuondoa dhuluma na unyanyasaji unaoendwlea ndani ya watumishi wenyewe kwa wenyewe.
Naungana na hoja yako 100%
 
Huyu Waziri hakika atarudisha amani na ari kwa watumishi walio kuwa wavunjika moyo kutokana na matendo ya viongozi wao wa juu.
lkn bado anakazi ngumu sana ya kuwabaini viongozi wenye roho mbaya na wanao waumiza watumishi wa chini, anatakiwa aingie ndani zaidi ndipo atabaini uonevu mkubwa unao fanywa na watendaji dhidi ya watumishi wa chini.
Mungu amlinde na ambarizi zidi kwa nia yake ya kuondoa dhuluma na unyanyasaji unaoendwlea ndani ya watumishi wenyewe kwa wenyewe.
Nakubaliana na wewe
 
Mchengerwa !Unapaswa kuwapandisha madaraja mara mbili watumishi waliotumika muda mrefu kazini bila kupanda daraja!mf.walioajiriwa miaka 2013, 2014 wote wametumika kwa miaka 7 hadi 8 na wamepanda mara moja tu! Nashauri wapandishe marambili zaidi ili kufidia miaka yao ya utumishi walioitumikia.
 
Maajabu,

1. Mshahara hutoi pesa yako,

2. Akipanda cheo haina maana chako kitashuka,

3. Hizi roho mbaya zinawafanya watumishi wasifurahie taaluma zao,

#Mchengelwa Chapa Kazi
shida hata waajiri wenyewe ni sehemu ya matatizo.matamko yanatolewa mengi lkn hakuna utekelezaji.waajiri wametengeneza scheme za kuwabana watumishi ili wasipande madaraja na kuwasomesha pia hawataki.Tanzania black country.
 
CHADEMA leo naona umeunga mkono hoja ya Serikali, Safi sana, huo ndio Uzalendo
Mtu akifanya vizuri mpe haki yake na akikosea mkosoe, awamu ya 5 watumishi wa umma walidharauliwa sn na kuonekana ni takataka, ukitaka kupata matokeo mazuri anza na watumishi wako kuwajali ili wawe na ari ya kufanya kazi
 
mchengerwa pic

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa amewaagiza waajiri wote nchini kuchukua hatua kuwaondoa katika nafasi zao baadhi ya maofisa utumishi walioshiriki kuficha sifa za watumishi wenzao hali iliyosababisha kutopandishwa madaraja.

===
Arusha. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa amewaagiza waajiri wote nchini kuchukua hatua kuwaondoa katika nafasi zao baadhi ya maofisa utumishi walioshiriki kuficha sifa za watumishi wenzao hali iliyosababisha kutopandishwa madaraja.

Akizungumza katika mafunzo ya viongozi wa matawi ya Chama cha wafanyakazi wa Serikali na Afya (Tughe) na waajiri yaliyofanyikia jijini Arusha, Mchengerwa amesema waajiri waende kuwashusha vyeo maofisa utumishi hao na nafasi hizo wawekwe watu wenye uwezo ambao watakuwa tayari kusikiliza kero za watumishi wenzio.

Amesema si watumishi ambao wapo katika ofisi kwa ajili ya matumbo yao hiyo haikubaliki hivyo ni lazima kila mmoja akabadilisha mitazamo yake kwa sababu Serikali ya sasa haitaki uonevu.

"Kila kiongozi lazima atengeneze ushawishi wa kuleta mapinduzi ya kifkra kama tunakuwa na watendaji ambao hawapendi kuona wenzao wanafanikiwa na wakipewa nafasi wanadhani miji yote ya kwao, hawafahamu kuwa vyeo hivi ni vya kupita tu pia wanasahau kwamba utumishi wa umma una muda," amesema waziri huyo.

Waziri huyo amehimiza waajiri kujenga utamaduni wa kuwajengea uwezo watumishi wao ili kuweza kupata weledi na kuleta uelewa ambao utakwenda kutoa kasoro ambazo zitakwenda kuleta ajali kazini.

Naye Katibu Mkuu wa Tughe, Hery Mkunda amesema mafunzo hayo yanalenga kuleta uelewa wa pamoja katika masuala ya waajiri na watumishi lakini pamoja na ushirikiano huo bado wanakabiliwa na changamoto ya uwepo wa baadhi ya vifungu vya sheria na kanuni ambazo zinaweza kuleta mgongano katika utendaji kazi.

Source: Mwanachi
Huyu waziri anachapa kazi na anafahamu vizuri matatizo sugu ya wizara yake na jinsi ya kuyatatua. Wafanya kazi tujitokeze popote pale ( Mitandaoni, magazetini, maofisini, bararani, katika sherehe tofauti........) kumpongeza Waziri huyu.

Mohamed Mchengerwa ni moja kati ya viongozi 40% aliowasema Prof Assad kuwa ndio wana uweledi katika nafasi zao. Hongera.
 
Back
Top Bottom