DOKEZO Mchengerwa! Usiishie kutoa maelekezo tu kagua barabara zinazojengwa na TARURA hapo Dar ujionee vituko

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Waziri Mchengerwa nimesikia maagizo yako kwa TARURA kuhusu ubora na viwango vya barabara wanazozijenga.

Ombi langu usiishie kutoa maagizo ingia site ujionee vituko mwenyewe.

Anzia na barabara za hapo Dar. Barabara zinajengwa kwa design za karne ya 18 kwenye karne ya 21. Kuna barabara mpya kabisa hapo Dar zimejengwa bila njia za watembea kwa miguu, bila njia za waendesha baiskeli mfano njia ya mbezi msakuzi.

Barabara zinajengwa bila kufungwa taa kuwezesha watu kutembea na kufanya shughuli mbalimbali hata usiku.

Kuna uhuni mkubwa sana unafanywa kwenye ujenzi wa barabara nchi hii. Tena sio kwa TARURA tu hadi TANROADS.

Kama Dodoma Mtumba waliweza kudesign barabara wakaweka njia za watembea kwa miguu, njia za kupita baiskeli na wakafunga taa swali ni je kwa nini hawafanyi sehemu zingine?

Mulikeni hili eneo na wananchi waone umuhimu wa kulipa kodi kwa ubora wa miradi inayojengwa.
 
Uko sahihi na angalizo lako lakini shida inaanzia pale kwenye mafungu je wako nayo kuweza kutosha kwa hizo designs zenye miundombinu yote unayoisema ?
 
Mambo ya.ujenzi.watu.wanamkumbuka sana magufuli. Hivi ni kwanini.service.road hazijengwi kusaidia upitaji.wakati.njiazinajengwa.mwendokasi
Mwendokasi ni uhuni mwingine unaofanywa na kudhalilisha akili zetu. Njia ya Gongo la Mboto- Posta badala ya kujenga line 3 za magari kila upande huku wakiweka mwendokasi katikati wanasiliba na masimenti njia mbili kila upande. Sasaivi unaweza kuta foleni hadi daraja za Tazara kutokana na uvivu wa kufikiri na kuamua kwa Watanzania.
 
Kama barabara ya posta gongolamboto isee pale wamechemka na haitapita miaka 5 watakuja kuitanua tena..
Hawa watu wanashida gani sijui.
 
Napinga kabisa mwendokasi bila.lujenga.njia 3 kila upande.ili.wanaosafiri na magari. Malori ya mizigo. Bajaj wote.waweze.kuwahi.

Naona kuna.utapeli.fulani.wa ujenzi hauna.tija na miaka inayokuja itakuja.kuonekana ni kero zaidi
 
Ume-mention barabara ya Msakuzi nadhani utakuwa unaijua hii barabara ya kupitia Madukani inayosimamiwa na municipal.

Hiki kituko walichoongeza kutoka ilipoishia mwanzo pale darajani mpaka karibu na shule ya Saint Ann aisee hii nchi inapigwa vibaya sana.
 
Tena vituko kweli kweli,mashimo yaliyochimbwa barabara nyingi kama miezi miwili iliyopita yanageuka kuwa mahandaki,wito wangu ziandaliwe breakdown zenye winch ili kuja kuyatoa magari yatakayotumbukiamo.Bahati tuliyo nayo mvua za vuli zimetuhurumia turekebishe tudosari twetuu.Ila badotumelalaa.
 
Hii nchi kama viongozi hawatafunguka akili na kuzuia huu upigaji kuna siku wanajeshi watakuja kupata akili ndo ktutafahamiana vizuri
 
Kuna njia imejengwa pale makabe kama mita mia nane kwa mabilioni lakini haijafikisha hata miezi mitano imeanza kuwa na mashimo.awamu ya mama wakandarasi wanajilia fedha za umma Kwa miradi ya chini ya kiwango maana wanajua maza hajui kitu.
 
Ile barabara kwenye nchi serious kuanzia msimamizi wa mradi, engineer na aliye design wangekuwa washanyongwa saivi
 
Kuna njia imejengwa pale makabe kama mita mia nane kwa mabilioni lakini haijafikisha hata miezi mitano imeanza kuwa na mashimo.awamu ya mama wakandarasi wanajilia fedha za umma Kwa miradi ya chini ya kiwango maana wanajua maza hajui kitu.
Ile barabara kwenye nchi serious kuanzia msimamizi wa mradi, engineer na aliye design wangekuwa washanyongwa saivi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…