Mchezo gani wa utoto ulikuwa unaupenda sana?

Wang Shu

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2014
Posts
2,562
Reaction score
3,715
Kila mtu katika makuzi yake kuna michezo ilikuwa ni ngumu kuacha ata baadhi imeweka alama katika miili yetu,
Mfano, mpira, karata, katagoli, rede, mdako n.k

Kombolela ni mchezo wakujificha alafu unatafutwa,nilikuwa napenda kujificha na kasichana flani sehemu moja tulivu sana.
Watatafuta mpaka wachoke wenyewe tumetulia tunafanya yetu.

Unakumbuka michezo gani ambayo ulikuwa tayari unyimwe chakula lakini sio kuacha kucheza?

 
Kuingia kwenye Tairi kubwa unajikunja humo halafu Mwenzako analiachia kwenye mlima..
Sitaki kukumbuka kilichonikutaga mara ya mwisho mpka nikaacha huu mchezo..

Nikahamia kwenye ndege, Nikikosa Natafuta njiwa kwenye mabanda ya watu, Nikimkuta anakula manati, naenda kulingishia nimeua.

Nako sikua na bahati, hio siku navuta manati kwenye mlango wa banda la watu, kabla sijaachia nilikutana na Banzi, Manati niliacha pale palee, nakimbia sikio moja lime mute...
Siku nyingine nikalazimishwa kula mtama mbichi.
 
Aaaaaaaaah πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚pole sana kwa kilichokutokea Kweny ajari ya tairi
 
Sema nilichokuwa napenda hii michezo ilikuwa inakuja kama trend kwa kipindi fulani, mfano kuna wakati mtaa mzima ni malingi tuu, mara mtaa utaamia kwenye golori, kipindi cha kombolela, kitakuja kipindi cha manati sana

Sema tumeenjoy udogo wetu sana, juzi napiga story na vitoto fulani pale mbweni havijuo ata kutengeneza manati ahahah

Mchezo nilikuwa napenda ni uwindaji ndege, kuwinda paka na mbwa, na mpira.
 
siku izi wapo bize wanachezea remote wanachek movie
 
Hawa watoto wetu yani hawana hata amsha amsha ukipita mitaani saa 1 jioni tu kimyaaaaaaaaa hakuna kombolela wala kukimbizana, muda huo wanacheza magemu tu
 
Nilikua napenda one touch (football) alafu kuna ule mnatumia vifuniko vya soda(wachezaji) na ndulele(mpira) then mnachora chini kama play station ya soccer!!
 
Nilikuwa sipendi kucheza ile michezo ya baba na mama kila wakati nilikuwa nikichaguliwa mimi kuwa baba sasa sijui kutokana na umbile langu
ha ha ha sasa ulikuw unataka uchaguliwe nani nani mkuu πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Mi nilikuwa sipendi wanifanya mtoto alafu unakuta baba mwenyewe mnafanana umri anafaidi tu wanakuta mbaliii ili uchelewe wao wanafanya yao
 
Mdako,rede na mpira wa miguu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…