Mchezo umeisha! Msumbiji huru sasa

Rwanda hii hii ambayo Kikwete aliwavuruga wiki 2 tu mpaka Kagame na M23 yake wakaanza kulia ndo ya kuipiga Tanzania? Rwanda hii ambayo wanajeshi wake wanakuja kufundishwa hapa Monduli ndo waipige Tz? Utakuwa na matatizo wewe

Mbona kwny medani hayo ni mambo ya kawaida sana,nchi za E/Africa zina utaratibu wa kufundishiana wanajeshi wa nchi zao.Hicho chuo cha Gako Military academy huko Rwanda kina wabongo,wakenya,Wazambia,wazimbabwe etc wana graduate.

Vyuo vya kijeshi Kenya unakuta vinafundisha wabongo,Rwanda,Uganda etc
Na wala kufundishwa kwny chuo cha nchi nyingine hua haina u superior wowote kati ya nchi na nchi labda uende kusomea huko Sandhurst.
 
Tunahitaji siku mbili pekee kuitangaza Rwanda kuwa Wilaya
 
Unaongea ukiwa Burundi au Bangui? Yaani nchi ambayo ukiwa Tabora unapiga Popote unapotaka ukienda Karagwe itakuwaje si unalenga Ikulu na RPG
Sipo katika kutetea kuwa Rwanda wana jeshi lenye ubora kuliko Tanzania. Hili mimi silifahamu.
Lakini hoja yajo ya nchi kuwa ndogo haina mashiko. Japanese waliwasulubu China katika Sino-Japanese war, unaujua ukubwa wa China na Japan inaingia mara ngapi kwa China?
 
Kumbuka Mozambique kuna kundi la waasi la RENAMO ambalo japo kulikuwa na ceasefire agreement lakini baada ya uchaguzi wa kijinga walitaka kurejea msituni tena.

Mziki wa Renamo hua ni mnene kidogo hawawezi kupigwa kirahisi hivyo,kipindi kile cha frelimo vs renamo Serikali ya South Africa(makaburu) ya kipindi hicho ilikua inai support Renamo na hio imefanya mpk leo Mozambique(frelimo) anakua anasitasita kupata msaada wa kijeshi kutoka S/Africa inshort hua haiwataki basi tu mambo ya sadc yamebana.Iliacha deep scar kati yao.
 
Na sisi tunapaswa kuwa makini sana na Rwanda hasa ukizingatia hata viongozi wetu wa siku hizi hoya hoya tu.

Sijui wanaokotwa wapi?
 
Ingekuwa rahisi hivyo Israel wangekuwa wanaishinda hamas na kuwachapa kama watoto.
 
Je hivyo vikosi havitaanza kupata mafunzo kwa siri kutoka kwa hao vijana wa slim vianze kusumbua Tanzania hasa ukizingatiwa gas yetu Mtwara ?
Rwanda anaanzaje destabilize nchi kubwa ambayo hawezi kushindana nayo na iko stable. Rwanda iliweza kujiweka DRC kwa vile imegawanyika na ina maeneo very isolated, sasa Tanzania waasi wakae wapi ambako hawafikiki. Alafu Rwanda hiyo bajeti ya kufadhiri makundi atolee wapi au mnadhani ana hela sana.

Bila mkono wa nchi ya kigeni, Rwanda hawezi tengeneza adui mwingine tena so powerful. Technically Rwanda na Burundi ni maadui, DRC wamekaa wanachorana, Uganda ni allies. Sasa Rwanda yupi anafanya destabilization kwa nchi ambayo anategemea bandari yake kupitisha sehemu ya bidhaa zake
 
Aliwezaje kuwafadhili M23 ?

Je akipata msaada kutoka kwa mataifa ya Magharibi hasa Ufaransa ambao ni wachochezi wa migogoro mingi sana Africa ?

Sisemi kwamba wataweza kufadhili ila niko suspicious sana na uwepo wa Rwanda Kusini mwa Tanzania
 
Nashangaa wamewssumbua kwa miaka 4 lkn wameondolewa ndani ya mwezi 1.Watakua na jeshi dhaifu sana.
Ukiliweka jeshi la Msumbiji vs jeshi la Rwanda vita ya mataifa mawili, sio hii ya kukimbiza washika majambia mnayoita eti nayo ni vita. Unaweza kuta Rwanda inapigwa

Vita yeyote usiitazame mapigano yanapotokea, tazama chanzo na msukumo wake. Msumbiji wana sababu zao za kiwendawazimu zilizowafanya wasipigane, sio kwamba hawana uwezo huo. Msumbiji ni nchi yenye hasara ya kuwa na marais wabovu miaka yote. Hakuna nchi inayotuzunguka inayoshindwa kupigana na wavaa yeboyebo chini ya 2000 ambao hawajawahi kupitia mafunzo hata mgambo, bora hata waasi wa Congo wana mafunzo. Ni siasa mbovu zilizowafikisha hapa, sio kuwa wamepigana wakashindwa.
 
Gaddafi aliwekewa vikwazo kununua silaha tangu miaka ya 1990s uko. Hizo silaha ulizomuona nazo ni za miaka zaidi ya 30 alizokuwa amenunua. Alikuwa na project ya nuclear pia ila akaachana nayo, Saddam Hussein na Hafez al Assad baba yake Bashar wa sasa hivi pale Syria ndio wakakomaa nazo. Israel ilishambulia vinu vyao

Gaddafi hakununua silaha za maana baada ya vikwazo na vile hakuwa na mpango kuvamia nchi yoyote kama alivyowahi kushambulia Egypt. Madikteta wengi huwa hawana jeshi kubwa, huwa wanazingatia ulinzi wa ndani na kuzuia maandamano
 
Ka nchi kenye ukubwa wa kariakoo kutoka mashariki mwa Africa leo kameenda kuzima jaribio la kigaidi lililoitesa Mozambique na SADC nzima?

Afu tunataka kusema Tanzania tunaweza kuwahimili Rwanda kijeshi... Mnatania nyie.
We utakuwa ni mtusi Rwanda Tanzania tukiamua asubuhi Tu Tunakunywa chai asubuhi.watusi huwa mnajisifia Sana[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Huyo mkuu wa AFRICOM ameenda Kenya anawaambia hivyo hivyo wakenya hio inaitwa Military diplomacy.
Wabongo nakwambia waache tu, eti tumeambiwa. Yani unategemea mgeni aje kukutembelea kisha akwambie nyumba yako mbaya. Wangekuwa wazungu wangeambizana ukweli ila sisi wanajua tunapenda unafiki basi wanamwaga sifa kila wanakokwenda. Hata hivo Gen. Townsend hakusema sisi ni wa kwanza, alisema tunaongoza. Alisema leading sio first
 
Aliwezaje kuwafadhili M23 ?

Je akipata msaada kutoka kwa mataifa ya Magharibi hasa Ufaransa ambao ni wachochezi wa migogoro mingi sana Africa ?

Sisemi kwamba wataweza kufadhili ila niko suspicious sana na uwepo wa Rwanda Kusini mwa Tanzania
M23 wanachukua maliasili kutoka Congo na ile nchi haina hata miundombinu kuunganisha Western na Eastern parts. Uliwahi sikia waasi wako kule Kishasa au miji ya mbali, wanachezea uku ambako miaka zaidi ya 20 rais hajawahi fika. Congo inaweza ishi robo nzima ya eneo lake ikiwa haimilikiwi na serikali

M23 sio waasi pekee waliopo/waliokuwapo DRC. Wengine wanadhaminiwa na Rwanda? Hii M23 ya 2010s wakati DRC wanapigana since 1960s. Kule hata wewe unaweza ukaanzisha kikundi chako cha kigaidi, nani atakuzuia wakati serikali imelala. Kuna watu binafsi wana vikundi vya mgambo uko sembuse nchi. Ukitoa bilioni moja unapata AK-47 kama elfu moja, wapiganaji ni kama unaokota vibarua, kambi mapori yapo ya kutosha, kinachobaki mafunzo na supplies
 
Acha kupotosha watu wewe.hii ni nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…