Mchungaji apigwa na wananchi wa Kigoma kwa kuzuia waganga wa kienyeji "Kamchape" wasiingie eneo la kanisa kutafuta uchawi

Mchungaji apigwa na wananchi wa Kigoma kwa kuzuia waganga wa kienyeji "Kamchape" wasiingie eneo la kanisa kutafuta uchawi

Funguka acha kukariri, Kila Jamii ina mungu wake, wachina Wana mungu wao, wahindi, waarabu, wazungu etc wana wa kwao pia, hata waafrica kabla ya ukoloni tulikuwa tuna mungu wetu, sasa Leo mmeletewa mungu na hao wazungu na waarabu mnaona hakuna mwingine, inabidi kutuma akili sana haya mambo ya Imani la sivyo utaonekana chizi tuu, Jamii nyingi sana zimeanza kushtukia huu usanii na hata hao wazungu waliowaletea huyo mungu wameanza kushtukia na kuachana na hayo mambo ya kufikirika na hadithi za watu wa kale
Ndio maana mambo yanazidi kwenda kombo.
 
Walikuja shuleni kutoa uchawi, wanakijiji waliwaleta, baadhi ya walimu tuliwagomea lakini wanakijiji wakashinikiza waingie wakatoe uchawi. Mara wakaingia ofisi ya mkuu wa shule na kudai wametoa uchawi wa mkuu wa shule na mwingine wakaufukua mbele ya shule. Walimu tusioamini uchawi tuliwaambia hatutaki ujinga wao na tutaripoti kwa mkurugenzi wa halmashauri kuwa tumevamiwa shuleni. Mchungaji hawezi kukubali upuuzi huo kwa mujibu wa imani ya kanisa lake. Huo ni uvamizi na hao wavamizi wanatakiwa washitakiwe kwa uchochezi

Hakuna kitu kinaumiza kama msomi uwe katikati ya wajinga.

Watakulazimisha ukubali imani zao za ushirikina kinguvu. Ukipinga unasingiziwa mchawi
 
Ingawaje uchawi upo

Lakini sasa hii njia wanayoitumia hao kamchape ,haifai

Kwanza waganga nao ni wachawi
 
Hakuna kitu kinaumiza kama msomi uwe katikati ya wajinga.

Watakulazimisha ukubali imani zao za ushirikina kinguvu. Ukipinga unasingiziwa mchawi
almanusura watusingizie ni wachawi tulivyowapinga. Kwanza hatukuchanga ili mganga huyo atoe uchawi shuleni. Tuliona anafanya udanganyifu kwa kujifanya anafukua uchawi ardhini huku akikimbizana na jini alikamate na kulifungia kwenye kitambaa huku hatulioni. Hawa watu wanapaswa kukamatwa na kufunguliwa mashitaka ya kuleta taharuki na uchonganishi katika jamii
 
almanusura watusingizie ni wachawi tulivyowapinga. Kwanza hatukuchanga ili mganga huyo atoe uchawi shuleni. Tuliona anafanya udanganyifu kwa kujifanya anafukua uchawi ardhini huku akikimbizana na jini alikamate na kulifungia kwenye kitambaa huku hatulioni. Hawa watu wanapaswa kukamatwa na kufunguliwa mashitaka ya kuleta taharuki na uchonganishi katika jamii

Ha ha ha. Mimi nazijua mbinu zao.

Kuna video nyingi youtube za waganga wa zamani zinaleza jinsi waganga wanavyotapeli watu.

Hicho wanachofunika wanajifanya wanakikimbiza nakijua ni nini. Kinakuwa kina hema hema
 
Hawa watu hawatoi uchawi wala majini, wanachofanya ni maigizo tu. Unakuta wanavamia nyumba ya mtu na kudai kuna uchawi. Waliwahi kumjeruhi titi bibi mmoja kwa kumchanja na kitu chenye ncha kali wakidai mwilini mwake kuna uchawi wanamtolea kwa nguvu bila ridhaa yake. Wale huenda nyumba ambazo wamedokezwa kuwa yumkini mkazi wa hapo anaamini ushirikina au kwenda kumdhalilisha tu kuwa ni mchawi. Ni washenzi afadhali ya wale wanaofanya mazingaombwe hawadhalilishi watu
 
Walikuja shuleni kutoa uchawi, wanakijiji waliwaleta, baadhi ya walimu tuliwagomea lakini wanakijiji wakashinikiza waingie wakatoe uchawi. Mara wakaingia ofisi ya mkuu wa shule na kudai wametoa uchawi wa mkuu wa shule na mwingine wakaufukua mbele ya shule. Walimu tusioamini uchawi tuliwaambia hatutaki ujinga wao na tutaripoti kwa mkurugenzi wa halmashauri kuwa tumevamiwa shuleni. Mchungaji hawezi kukubali upuuzi huo kwa mujibu wa imani ya kanisa lake. Huo ni uvamizi na hao wavamizi wanatakiwa washitakiwe kwa uchochezi
Pole Mkuu Kigoma napaelewa vyema
 
Acheni kuwa nyoronyoro, wapeni kipigo cha haja mpaka wajisaidie haja kubwa hadharani, hawatarudi tena, Kijiji na wananchi wake wake chini wapitishe azimio huo upuuzi ni marufuku atakayekaidi afanywe mfano, wataacha
 
mchungaji avamiwa na wananchi na kupigwa vikali baada ya kugoma kukubali watu wenye imani potofu kuingia kwenye viwanja vya kanisa kutoa uchawi.

waganga hao wa kienyeji wanakusanya 5,000/ kwa kila nyumba, kama malipo ya kuwatoa wachawi wote. Mchungaji aligoma kuwapa hela na aligoma kuwaruhusu kuingia kwenye maeneo ya kanisa.

Najiuliza kwanini watu Wa tanzania tunanaamini sana kwenye uchawi, Elimu itolewe ili Watanzania Tuache Imani za ushirikina. Imagine kwenye zama hizi za teknolojia bado kila nyumba inalipishwa 5000 na waganga wa kienyeji ili watoe wachawi

View attachment 2932691
"Nikapiga simu polisi ...polisi hawaji
Piga simu polisi hawaji
Nikampigia simu baba askofu alikuwa Dodoma
Ndipo naye akapiga simu polisi baadaye wakaja"

 
Back
Top Bottom