Mchungaji Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama apewa likizo ya siku 60 na kutakiwa kuripoti Makao Makuu

Mchungaji Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama apewa likizo ya siku 60 na kutakiwa kuripoti Makao Makuu

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1674101456763.png

Picha: Mchungaji Eliona Kimaro

Semina iliyokuwa imeanza katika usharika wa KKKT Kijitonyama ikiongozwa na Rev Dr. Eliona Kimaro imelazimika kusimama kufuatia barua aliyopewa ya likizo ya siku 60 na kupelekea kushindwa kuendelea na semina hiyo.

Mchungaji Kimaro amesema anatumia fursa hiyo kuwaaga Washarika wake na kuanzia Januari 17 Mchungaji Anna ataendelea kuwa kiongozi wa Kanisa hilo.

Kwa mujibu wa barua, Mchungaji Kimaro atamaliza likizo yake ya lazima 17/03/2023 na barua inamuelekeza kuripoti makao makuu na sio usharika wa KKKT Kijitonyama ambapo atapangiwa sehemu nyingine.



Video: Mchungaji Kimaro akiwaaga waumini
Amesema:
"Mimi ni Mchungaji wa Lutheran ninayeheshimu kiapo changu cha kichungaji na kuishi katika kiapo changu cha kichungaji na maadili pia ya kichungaji kwa neema ya Mungu. Kwa sababu hiyo imenilazimu kutii amri na kwenda kwenye hiyo likizo ya siku 60 na baadae kuripoti kwenye ofisi ya Askofu kama nilivyoelekezwa" Asante.


Video: Mchungaji Kimaro akiombea Waumini baada ya kuaga

UPDATES
Baadhi ya Waumini wa KKKT wajitokeza kupinga uamuzi wa Mchungaji Kimaro kupewa likizo
Waumini Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kijitonyama wamekubaliana kutoingia ndani ya Kanisa hilo hadi watakwporudishiwa Mchungaji wao Dk Eliona Kimaro aliyepewa likizo ya siku 60.

Uamuzi huo umefikiwa na waumini hao baada ya kukubaliana kufanya maandamano ya amani katika viwanja vya kanisa hilo hadi pale mchungaji wao atakaporudishwa au kupewa sababu za kupewa likizo hiyo.

Tazama baadhi ya video hapa chini:







Video hizo hapo juu zinawaonesha Waumini wa KKKT Usharika wa Kijitonyama wakipinga mchungaji wa usharika huo Dkt. Eliona Kimaro kupewa likizo ya siku 60.


PIA SOMA:
1. KKKT ni kubwa kuliko Mch. Kimaro, msihuzunike kuna jambo hamlijui, viongozi wake hawajakurupuka

2. Projects za Mchungaji Kimaro akiwa KKKT Kijitonyama

3. Kwenye sakata la Mchungaji Kimaro, nasimama na Kiongozi wangu Askofu Malasusa
 
Nilijua ipo siku KKKT watamfyatua out aidha kwa figisufigisu ili akimbie mwenyewe.

KKKT haipendagi mtu alinyooka ktk ukweli, sasa jamaa huwa yupo straight forward huwa hapindipindi hata kidogo, so kwa Lutheran hiyo ni kasoro, pia kuna ngoma nyingine Askofu Bagonza huyu nae ni kisiki hawana cha kumfanya make huyu nae ni kichwa kingine ambacho kimenyooka na hakuna mtu mwenye uwezo nacho ndani ya KKKT.
 
Nilijua ipo siku KKKT watamfyatua out aidha kwa figisufigisu ili akimbie mwenyewe.KKKT haipendagi mtu alinyooka ktk ukweli,sasa jamaa uwa yupo straight forward uwa hapindipindi hata kidogo,so kwa Lutheran hiyo ni kasoro,pia kuna ngoma nyingine Askofu Bagonza huyu nae ni kisiki hawana cha kumfanya make huyu nae ni kichwa kingine ambacho kimenyooka na hakuna mtu mwenye uwezo nacho ndani ya KKKT
Huyu watachemka ni fitina za askofu tu anaona jamaa anakubalika zaidi.
 
Mimi Nimezaliwa katika familia ya kiluteri na kupata hadi kipaimara ila mambo haya ya migogoro upande wa viongozi yalinikera ukifuatilia chanzo pesa halafu michango karibia mitano lol niliamua niwe tu nasali kwa ukawaida kwa mashahidi wa yehova watu walio na upendo wa hali ya juu wakiyaishi maisha ya viwango ya kikristo kwa matendo.

Kwanza KKKT inashangaza eti mtu anaweza akaacha kanisa lake la KKKT mtaani ila akawa anaenda kusali usharika wa Kimara eti kisa mchungaji wa Kimara ni maarufu anamvutia swali Je, akifa huyo mchungaji utaendelea kwenda huo usharika wa Kimara?
 
Makanisa na migogoro ni sawa na samaki na maji.

Makanisa yote yemejaa changamoto, wakatoliki na ushoga na ulawiti watoto, waangillikano ushoga, walutheri sadaka na ukabila na uzinzi, kumbukumbu kesi ya Malasusa ambae aliondolewa madarakani polisi wakamlinda. wasabato ukabila, unafiki, walokole sadaka, ni balaa tupu.

Anyway, kama anaona hatendewi haki ajutenge na kanisa lake aendelee kufunisha watu wake kama kina kamobe, mwingira, Mama Rwakatale, yule mwingine alikua anafudisha wanawake tu na mapenzi, mxee wa upako nk.
 
Huo usharika una mapato makubwa, pesa ndio tatizo, Huyu mchungaji, umaarufu umezidi kuzidi wakubwa wake, ameng'aa sana kuliko viongozi wa kanisa, Tatizo la Lutheran, ukiwa kwenye usharika wenye pesa ndefu, na wewe unanufaika zaidi, Gari, nyumba, miradi, kandarasi.

Mchungaji kwenye usharika mdogo, aina ya gari na nyumba itategemea mapato ya usharika, kama ni madogo, atanunuliwa hata bodaboda, ukiwa kwenye usharika wenye pesa, hapo V8, Prado, nk.

Kingine KKKT kuna ukabila sana, mchungaji akiwa mchaga, kandarasi zote zitaenda kwa wachaga, wahaya nk.
 
Nilijua ipo siku KKKT watamfyatua out aidha kwa figisufigisu ili akimbie mwenyewe.KKKT haipendagi mtu alinyooka ktk ukweli,sasa jamaa uwa yupo straight forward uwa hapindipindi hata kidogo,so kwa Lutheran hiyo ni kasoro,pia kuna ngoma nyingine Askofu Bagonza huyu nae ni kisiki hawana cha kumfanya make huyu nae ni kichwa kingine ambacho kimenyooka na hakuna mtu mwenye uwezo nacho ndani ya KKKT
Amefanya nini?
 
Kwenye hili nahisi pastor Kimaro ataenda kujitafakari.

Mimi ni muumini wa KKKT hapo Kijitonyama, shida iliyokuwepo kwa mchungaji Kimaro ni kwamba alikuwa anaenda kinyume na utaratibu wa kanisa na kibaya zaidi alishaonywa zaidi ya mara 3 ila shida yake akiitwa akaonywa anakuja kanisani anaanza kuongea kwa waamini na kurusha vijembe kwa viongozi wake.

Tarehe 8 ukiweza fatilia alichokifanya kwa pastor mwenzake ANNA maneno aliyoongea kumuhusu huyo mchungaji kuna jambo utaelewa.

Kimaro ana kiburi cha umaarufu. Mchungaji hafati kalenda ya kanisa, yeye anafanya mambo yake, aliitwa akaonywa ila akaja kanisani hadharani na kusema hawezi kupangiwa cha kufanya ila Mungu tu, sasa hapo kweli kuna utii?

Kimaro toka amekuja usharikani anazo nyimbo 6 tu anazoimba kutoka kitabu cha tumwabudu Mungu wetu, aliitwa akaambiwa hiki kitu ila akawa mkaidi, ni mchungaji anayependa yeye aongee zaidi, hapendi kuwapa wachungaji wengine nafasi ya kuhubiri, ikitokea mchungaji mwingine akahubiri basi na yeye baada ya mahubiri atasimama na kuanza kujazilishia kuonekana kwamba mwenzake hajafanya kama inavyopaswa.

Ni kimaro na masai wa kimara ambao ukifatilia utaratibu wanao ufanya kanisani siyo wa KKKT ila najua wachache sana wataelewa hili.

Kama mtaweza kumbuka pia aliondolewa kwenye vipindi vya upendo Tv kisa mambo yake hayo ya kufanya kinyume na utaratibu wa kanisa ikabidi wamuonye ila akakaidi, baada ya kuondolewa alikuja kanisani hadharani na kuanza kusimanga na kuongea mbovu na tokea hapo hajawahi kutangaza kitu chochote kinacho husu upendo kama magazeti.

Alitamba sana kwamba kwa jinsi alivyo barikiwa na Mungu hakuna mwanadamu wa kumshusha hapo alipo, na haya alikua anaongea kanisani mbele ya waamini na kujitapa kabisa.

Kwa sisi waamini wachache ambao tulikua tunamuona kanisani na kutambua madhaifu yake tulijua hana mda mrefu atapigwa chini na kweli leo kaondoka.

Wengi mnaongea hamjui kilicho nyuma ya huyu kimaro ila nakuhakikishia KKKT KIJITONYAMA haiwezi kutetereka kisa kimaro kuondolewa na alishasema akitolewa Kjitonyama basi ataanzisha kanisa lake, ngoja nione atakachofanya baada ya hili.

Namuombea hekima na maarifa atambue kosa lake arudi kundini na awe mnyenyekevu kwa Mungu na Viongozi na Kanisa kwa ujumla.

ANAYEFATA NI MASAI WA KIMARA MWISHO.
 
Nimezaliwa katika familia ya kiluteri na kupata hadi kipaimara ila mambo hata ya migogoro upande wa viongozi yalinikera ukifuatilia chanzo pesa afu michango karibia...
Waafrika mmelaaniwa unajisifu kwa ujinga na kukosoa kwa ujinga,huyo yehova unayemtolea ushahidi anavinasaba gani vya UAFRIKA hadi umshuhudie?

Mjinga na shetani ni anayeamini ktk mafundisho ya kupandikizwa na kuacha asili yao.

Waafrika wenye DINI za kuja wote wachomwe moto ni mashetani WEUSI
 
Back
Top Bottom