Mchungaji Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama apewa likizo ya siku 60 na kutakiwa kuripoti Makao Makuu

Ulipaswa uandike 'be courageous'
 
Labda ni ile kauli yake ya kuwa Wakristo wengi si waaminifu na ni wezi. Ile kauli wengi tulikubaliana nayo ila lazima ingemletea shida.

Kuhusu Upendo TV, mimi nilichangia katika uanzishwaji wa ile TV kupitia kampeni aliyokuwa anafanya kwenye kipindi chake cha asubuhi kwenye Upendo Radio kwa hiyo kama walikuja kumuondolea kipindi chake lazima imguse. Alitumia nguvu kubwa na ushawishi wake kukusanya michango.

Mchungaji Eliona Kimaro Yuko Vizuri
 
Huyo

Huyo mchungaji alizaliwa Kwa ajili ya kufanya Kazi hapo kimara pekee?? Anatolewa tu, na mikia yenu ya kichaga itakamata makalio tu
Du ukabila tena, mbona huajawazungumzia Mchungaji Kombo na wengine ambao sio wachaga? Mchungaji wa kimara sio mchaga sasa uchaga unatoka wapi. Askofu wao Malasusa Mnyakyusa wapi mzee unakoelekea??? Mbona unaleta tena chuki za kisiasa/kikabila kanisani?
 
Sijaona point yeyote ya maana iliyosababisha asimamishwe,kumbe alizuiwa kwa hila asihubiri upendo tv mkatukosesha huduma tuliyokuwa tunahubiriwa majumbani basi Mungu wetu halali atamlipia tu,sidhani kama ni kweli mchungaji anaweza kuacha kuhubiri kwa kufuata kalenda ibada zote,hii hutokea kwa ibada chache na ni kawaida kwa wachungaji wengi tu.
 
Maelezo mazuri sana,kama anakiuka viapo anapaswa kushughulikiwa na kama anaona ni mkubwa kuliko taasisi basi ni vema akaanzisha kanisa lake,ili achunge kondoo wake nje ya Mfumo wa KKKT.Kanisa linabebwa na Kristo sio mtu au kiongozi mmoja.
 
Huyo

Huyo mchungaji alizaliwa Kwa ajili ya kufanya Kazi hapo kimara pekee?? Anatolewa tu, na mikia yenu ya kichaga itakamata makalio tu
Hata huelewi Rev. Kimaro alikuwa mchungji wa Kijitonyama, wewe unazungumzia Kimara mbona unaongozwa na chuki za kikabila????
 
Naweza kuubaliana na wewe kwani mimi sisali kanisa hilo, ila amekubali amri ya kanisa na kukaa kando kwa siku 60, kusubiri hatua zaidi za askofu wake na wakuu wake. Angeongea kupinga hayo ningeona shida wazi wazi ya utovu wa nidhamu. Tuache tuone kwani lipo mikononi mwa vongozi wake.
 
Judgment is spiritual more than professional as you may see, let the leadership of the church take their spiritual role to resolve this.
 
KANISA NI MALI YA MUNGU, sio saccos za KKKT. Mungu huabudiwa kwa roho, na kanisa halisi la Mungu lazima litoe solutions za matatizo ya waumini wake through maombi, na mafundisho yenye uzima. Zama za kufuatisha liturugia mpaka watu wanasinzia zimekwisha. Nawaunga mkono hawa pastors Kimaro na mastai at least wameleta uhai kwenye ibada za KKKT.
Kama kweli wanafanya hayo kwa ajili ya Kristo, hata wakiwatimua halafu wakaamua kuwa na huduma zao still watapata followers wa kutosha.
 
Ila kkkt mmezidi. Mpunguze migogoro. Jifunzeni kutoleta mambo yenu mitandaoni.
Kwetu huwezi kusikia mambo yanaletwa hadharani kiasi hiki.
Sio kwamba hayapo yanakuwepo maana popote walipokusanyika watu lazima migogoro iwepo.
Huwezi kuzuia mambo kuletwa mitandaoni,hata serikali na vyombo vyake inapambana na hilo Ila imeshindwa,ukiangalia aliyeleta mitandaoni ni huyohuyo Kimaro,na hata asingeleta yeye,bado waumini aliowaeleza hayo wangeleta tu,hizi ni zama za uwazi kikubwa ni taratibu tu zifuatwe na haki itendeke.

Kama wanasema alikuwa na semina anaendesha unadhani angeondoka kimyakimya baada ya barua si ndio ingeleta taharuki zaidi?watu wangeanza kuulizana mbona hayupo.
 
Duuh kazi ipoo sema Ulimi ukiutumia vibayaa nao unashidaa sanaaa.

Huo huo unahubiri dini leo huo huo kesho unaponda dini yako na watu wake wanaoiamini na kufata mafundisho unayowafundisha sasa sijui kipi ni kipi...!!

Anyway kuusifu uislamu na Ukatoliki ni kuonesha kkkt inazingua na hufurahii kuwa hapoo.
 
Kuna kanisa lisilokataza dhambi?? Kama lipo hilo sio kanisa la Kristo bali wanajua wenyewe ni kitu gani. Hata Yesu alionya juu ya dhambi na kufa msalabani ili tutapoanguka turudi kwake kwa toba. Huyo asiyekataza hana ushirika na KRISTO.
Mavazi wanavaa uchi makanisani
 
Kwani si kaenda likizoo...!! Mchungaji kupewa likizo jambo la kawaida sema yeye ndo kayakuzaaa kuonesha kuwa kaonewaaa... aina ya wachungaji ambao usharika ukikuaa na wao ndo wameweka nguvu kuukuza huwa wana changamoto sana za kuongozaaa wao wako mbele sana kukemea ila ukweli na wao ni wachafu vile vile.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…