Mchungaji Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama apewa likizo ya siku 60 na kutakiwa kuripoti Makao Makuu

Mchungaji Eliona Kimaro wa KKKT Kijitonyama apewa likizo ya siku 60 na kutakiwa kuripoti Makao Makuu

Niseme tu, hakuna marefu yasiyo na ncha.
Kilichokuwa kinatakiwa kufanyika ni kum demolish Kimaro tangu akiwa Usharika wa Kariakoo.

Kwa miaka mingi tumefanya mbinu na njama mbalimbali kumuondoa lakini hazikuwq na matokeo tuliyo yatarajia. Hivyo tukajaribu mbinu nyingine na nyingine tena, hatimaye leo mbuyu haujaanguka ila umemwagika.

Mara ya kwanza tulipofanya yetu akiwa pale Kariakoo alikimbia usharika na kwenda kujificha kwa Mapadre, na mapadre ndio waliofanya jitihada hadi akarudi tena usharikani, ila hii ya sasa harudi, na akirudi basi itakuwa zamu yetu kusalimu amri.

Kimaro alipokuwa Kariakoo, sio kwamba aliharibu taratibu za ibada hapana, hii ni cover tu, tunayoitumia.

Kimaro alipokuwa Kariakoo aliharibu biashara za wengi kwenye ulimwengu wa roho.

Watu walikuwa na madhabahu zao kubwa ambazo ziliprovide ulinzi wa pesa na mali, pia zikikuwa zikivuta mali kutoka kwa maboya wengine.

Alipofika Kimaro, wale ambao tulikuwa tukizivuta mali zao, wakaanza kumiminika kule kila alfajiri, ulinzi wa mali zao ukaanza kuongezeka, na zile biashara zao ambazo tulizifanya zisionekane na wateja zikaanza kuonekana, na taratibu taratibu wakaanza kukua na kutupora wateja wetu.

Kwa msio na ufahamu wa biashara, hamna biashara isiyo na madhabahu (iwe ya asili au hizo kama za Kimaro), hamna biashara isiye na kuhani, na wala hamna biashara isiyotolewa sadaka/kafara.

Watu wakaanza kufundishwa kutoa sadaka za maneneo na manuizi kwa ajili ya biashara zao, tukapata upinzani sana.

Kwa kushirikiana na wenzetu ndani ya kanisa, tukaanza figisu. Ibada hizo mpya zifutwe na ikiwezekana Kimaro ahamishwe Kariakoo.

Tukafanya Kimaro apitie magumu, tukakausha kabisa hali ya utoaji wa sadaka hadi kanisa likashindwa kulipia umeme na maji, tukahakikisha wanapitia kwenye hali ya ugumu kweli kweli.

Baadae Kimaro anajua alichokifanya, akapindua meza, hali ya uchumi wa kanisa ikaimarika sana, likawa pigo lingine kwetu.

Kipindi kile mkuu wa kanisa alikuwa yule jamaa wa Mbeya, tukafanya kila liwezekanalo ahamishwe. Ndipo akapelekwa Kijitonyama.

Zama zile Kijitonyama alikuwepo dogo mmoja anaitwa Kinyaha, hayo mambo ya ibada za asubuhi yalikuwa hayapo au yamekufa kabisa.

Ibada ilikuwa ikihudhuriwa na vizee vienne, wakizidi sana sita. Sasa alipokuja Kimaro sijajua alikuja na mguu upi, akaleta ibada za asubuhi na usiku.

Watu wakaanza kufurika, akaanza kununua nyumba za watu wetu na kuzifanya kuwa za kanisa. Kijitonyama yote ilikuwa ni ngome yetu.

Kata ya Kijitonyama ndio kata ina vijiji viwili mjini kati Dar es Salaam. Kijiji cha Mwenge na Kijiji cha Makumbusho. Jina na asili Kijitonyama sitaki kulielezea leo, lakini kaa ukijua kuwa ile ni ngome yetu na sehemu yetu ya kulia nyama na vitu vyetu vya kutuongezea nguvu. Kijitonyama ndiko kwenye madhabahu ya kuteketeza, ndio maana hata Wahindi miili yao huchomewa Kijitonyama.

Pale tulijaribu mbinu za kishushu, kuna kipindi tulitaka kumfitinisha na serikali kwa kupitia kijana aliyejinyonga kwa madeni aliyokuwa nayo, lakini alikwepa vihunzi kwa namna ya ajabu kabisa.

Kwetu sisi ni furaha, watu waharibifu aina ya KIMARO hawafai, wakakae huko vyuoni wafundishe. Na tutammaliza kwa njia hiyo.
Washirikina combine.
Yule apingaye roho wa Bwana ataangamia tu.
 
Eti ukifa hatukuziki. Sasa mimi hata mnizike msinizike inanisaidia nini? Si nimeshakufa? Dini zingine ni vituko tupu yaani [emoji706][emoji706][emoji706]

Kwanza hakunaga mfi anaekosa mzishi.

Waache kutumia kuzika kama fimbo ya kutishia watu kulazimisha kwenda kusali jumuia.

Watu wenyewe wako mwilini na matendo ya mwili yamewatawala na hawapo tayari kutahiriwa na Neno mioyo yao wapate kuwa viumbe vipya.
 
Umeandika Ukweli Mtupu na umeeleweka.

Eliona Kimaro ameshajiinua sana na hana UTII

Anajipa mamlaka makubwa na kudharau wengine
 
Kwenye hili nahisi pastor Kimaro ataenda kujitafakari.

Mimi ni muumini wa KKKT hapo Kijitonyama, shida iliyokuwepo kwa mchungaji Kimaro ni kwamba alikuwa anaenda kinyume na utaratibu wa kanisa na kibaya zaidi alishaonywa...
Ubarikiwe sana kwa kueleza ukweli.

Ukweli unauma lakini ukweli hutibu.

Kimaro kama ana masikio na asikie sasa.

Karama tupewazo na Mungu zilitolewa bure, na zitumike bure kwa utukufu wa Mungu
 
Tii mamlaka, tii mamlaka, fuata miongozo Kama unataka miongozo yako fungua kanisa lako sikio halizidi kichwa kamwe
Hapa Umemaliza kila kitu.

Mfumo ndio unaombadilisha Mtu, Mtu habadilishi Mfumo

Kimaro aliikuta KKKT na misingi pamoja na taratibu zake

Kama hawezi au hataki hizo tamaduni basi akaanzishe kanisa lake
 
Kiufupi huyu Kimaro ameamua ku Mordenize kanisa la KKKT kutoka kwenye old and boring formula ya liturujia tu. Watu sikuhizi wanafocus zaidi kwenye vibe. Vizazi vimebadilika sana vijana wengi wanaohudhuria hizo ibada ni uzao wa kuanzia mwaka 2000.
Mindset zipo tofauti na wazazi wao sio watu wa miaka ya 60 au 70 kama baba zetu.
Mordenize ❌
Modernize✅
 
Binafsi naona kama Kiburi kimemzamisha akiwa kati kati ya jahazi la utumishi. Alitumia madhabahu ya Mungu kujijenga yeye binasfi na sio MWILI WA KRISTO. Ndio maana yeye akawa maarufu kuliko utakatifu wa waumini wake. kumbuka kipimo cha kazi ya mwaadamu aliyeitwa na Mungu ni matunda aliyoweza kuzalisha.[emoji817][emoji818]
Umeongea jambo la msingi. Kimaro alianza kuwa na kiburi, ujivuni na kudhani yeye tayari ni mkuu na haambiliki. Shida ipo hapa.
 
Nadhani KKKT kuna shida kuanzia waumini wao tangu wakiwa watoto.
Hivi inakuaje mchungaji anayefanya mambo kinyume na miongozo ya taasisi yake iliyomuweka ndio anapendwa na kupata umaarufu? Kwanini waumini wenyewe wasimkatae?
Tatizo waumini siku hizi hawamfuati YESHUA wanamfuata mchungaji..... Si umeona mabango yameandikwa "daddy kimaro" [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom