Pre GE2025 Mchungaji Msigwa: Ningependa Tundu Lissu ashinde Uenyekiti CHADEMA kwa faida ya demokrasia ya Tanzania na hata kwa CCM yenyewe

Pre GE2025 Mchungaji Msigwa: Ningependa Tundu Lissu ashinde Uenyekiti CHADEMA kwa faida ya demokrasia ya Tanzania na hata kwa CCM yenyewe

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mchungaji Msigwa ameeleza wazi kuwa anamuunga mkono Tundu Lissu katika kinyang’anyiro cha Uenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Akizungumza kuhusu mwelekeo wa uchaguzi huo, amesema:

"Mimi nam-support Tundu Lissu, ningependa ashinde, lakini ni matatizo yao hayo. Mimi, yeyote atakayeshinda yaani sisi (CCM) tunataka chama kile tukishinde. Yeyote atakayeshinda bado tutakabiliana naye, awe Lissu, awe Mbowe, au mtu mwingine kutoka Burundi, Rwanda. Lakini kwa kuwa mimi ni kada wa Chama cha Mapinduzi, nitakabiliana na yeyote. Hata hivyo, kwa faida ya demokrasia ya Tanzania na hata kwa faida ya CCM yenyewe, anayepaswa kuwa Mwenyekiti pale ni Lissu."
Soma, Pia: Tundu Lissu: Mchungaji Peter Msigwa ni rafiki yangu, lakini nitamkabili Kisiasa
huyu ccm haitakiwi kumwamini.labda wampe ubalozi
 
Shida yenu mnapenda majibu mepesi kwa maswali magumu.Tangu lini mfuasi wa dhati wa Chadema atakubali ushauri wa hao wawili kuhusu nani anastahili kupigiwa kura?

Wao kwa kumpigia debe Mbowe wanajenga hisia kuwa Mbowe ni kibaraka wa CCM hivyo kuwafanya watu wampigie kura Lissu.

Msigwa hawezi kufanya hivyo kwa sababu kila mtu anajua anavyomchukia Mbowe.

Bahati mbaya wako watakaoingia mkenge na kumpigia kura Lissu ambae CCM wanamtaka. Lengo lao ni Lissu ashinde halafu Mbowe asuse. Ikitokea hivyo CDM itakuwa ICU by the time Uchaguzi Mkuu unafanyika.

Amandla...
MamaSamiah,Tlahtlah ni CHADEMA?
 
Angalia hii nguruwe ya kijani nayo
Katika Mambo ya Walawi 11:7-8 na Kumbukumbu la Torati 14:8, Mungu aliwaambia Waisraeli kuwa nguruwe ni najisi kwa sababu hula nyama lakini hawatafuni cud (chakula mara ya pili). Hivyo, Waisraeli walikatazwa kula nyama ya nguruwe au kugusa mizoga yake. Hili lilikuwa sehemu ya sheria ya Musa, ambayo iliwaongoza Waisraeli jinsi ya kuishi kwa usafi wa mwili na kiroho.
 
Mchungaji Msigwa ameeleza wazi kuwa anamuunga mkono Tundu Lissu katika kinyang’anyiro cha Uenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Akizungumza kuhusu mwelekeo wa uchaguzi huo, amesema:

"Mimi nam-support Tundu Lissu, ningependa ashinde, lakini ni matatizo yao hayo. Mimi, yeyote atakayeshinda yaani sisi (CCM) tunataka chama kile tukishinde. Yeyote atakayeshinda bado tutakabiliana naye, awe Lissu, awe Mbowe, au mtu mwingine kutoka Burundi, Rwanda. Lakini kwa kuwa mimi ni kada wa Chama cha Mapinduzi, nitakabiliana na yeyote. Hata hivyo, kwa faida ya demokrasia ya Tanzania na hata kwa faida ya CCM yenyewe, anayepaswa kuwa Mwenyekiti pale ni Lissu."
Soma, Pia: Tundu Lissu: Mchungaji Peter Msigwa ni rafiki yangu, lakini nitamkabili Kisiasa
Hajasema kwa upande wa CCM anapenda nani awe makamu mwenyekiti?
 
MamaSamiah,Tlahtlah ni CHADEMA?
Ndio maana nasema mnapenda majibu mepesi kwa maswali magumu. Unadhani watu watampigia kura Mbowe katika uchaguzi wa CHADEMA kwa sababu hao wanampigia debe? Au ndio wataona ni uthibitisho kuwa Mbowe ni mamluki wa CCM na hivyo watampigia kura Lissu?

Chadema wanaamini kuwa CCM wanamuogopa sana Lissu kwa sababu atawasemea ovyo jukwaani! Ukweli ni kuwa CCM hawamtaki Mbowe kwa sababu ya resilience kubwa aliyonayo. Pamoja na kutupiwa kila kitu (yeye na viongozi kufungwa, viongozi waandamizi kuunga mkono juhudi, biashara zake za Tanzania kuhujumiwa, account zake kufungwa) ameweza kuifikisha CDM hapa ilipo pamoja na kukataa kupokea ruzuku za masharti. Wakati huo baadhi ya hao mnaowaona kama mashujaa wakiwa ughaibuni wakichangia mapambano kwa remote. CDM wakimchagua Lissu wataipa CCM ushindi.

Amandla...
 
Sio Mbowe tena ?...
Hata siku moja Mkuu. Lissu akiwa Mwenyekiti CCM watakuwa na kazi rahisi. Kama atatekeleza anayosema, atasusa chaguzi na hivyo kuwapa CCM na vyama vingine ushindi wa kirahisi. Atakataa majadiliano wakati vyama vingine vitaendelea nayo na hivyo kuifanya CHADEMA ionekane un reasonable hasa kwa taasisi na nchi za nje zenye interest na utulivu nchini. Aidha, Lissu ataitisha maandamano kitu ambacho serikali ina uzoefu mkubwa wa kuyanyima pumzi. Wazuie wakubwa kutoka nyumbani kwao, tangaza kuwa jeshi linafanya usafi siku hiyo, Tanpol itangaze kuwa ni haramu na wasilaumiwe kwa yatakayowapata watakaoandama. Maandamano yasipofanikiwa mara kadhaa CDM watabaki kulaumiana tu na kutafuta wachawi.

Mbowe akishindwa anaweza kufunga waleti yake na hivyo kuifanya ijiendeshe kwa shida sana. Kuna uwezekano utawala wa Lissu utawashughulikia kambi ya Mbowe na hivyo kujipunguzia pool ya watu wenye uzoefu wa administration na uhamasishaji. Aidha, itaongeza mpasuko ndani ya CHADEMA.
Ushindi wa Lissu utakuwa zawadi kwa CCM.

Amandla...
 
Katika Mambo ya Walawi 11:7-8 na Kumbukumbu la Torati 14:8, Mungu aliwaambia Waisraeli kuwa nguruwe ni najisi kwa sababu hula nyama lakini hawatafuni cud (chakula mara ya pili). Hivyo, Waisraeli walikatazwa kula nyama ya nguruwe au kugusa mizoga yake. Hili lilikuwa sehemu ya sheria ya Musa, ambayo iliwaongoza Waisraeli jinsi ya kuishi kwa usafi wa mwili na kiroho.
Tuondolee upuuzi wako wa kiccm hapa
 

Attachments

  • images (13) (1)~2.jpeg
    images (13) (1)~2.jpeg
    16.3 KB · Views: 2
Back
Top Bottom