Pre GE2025 Mchungaji Msigwa: Tuungeni mkono CHADEMA ili tukatae mfumo wa ukandamizaji wa kikoloni uliopo

Pre GE2025 Mchungaji Msigwa: Tuungeni mkono CHADEMA ili tukatae mfumo wa ukandamizaji wa kikoloni uliopo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Mchungaji Peter Msigwa akizungumza Jumatano kwenye mkutano wa hadhara wa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA bara Tundu Lissu uliofanyika Jumatano Juni 05, 2024 katika Kijiji Ughandi -Singida Kaskazini amesema kuwa "Ikitokea Mkurugenzi hamridhiki naye mkitaka kumtoa, hamna uwezo wa kumtoa mpaka Rais aamue, hata madiwani kama mnataka kumtoa uwezo hamna wa kumtimua mpaka Rais aamue”

Mnalazimishwa kulipa kodi, mnapeleka Halmashauri. Mbunge mliyemchagua awatetee hana uwezo kwasababu mkurugenzi anapata amri kutoka kwa Rais, hii ni akili au Matope?

Huu ni mfumo kandamizi na wa kikoloni ndiyo maana huwa mnasikia maelekezo kutoka juu kwa sababu Rais amamteua Jaji Mkuu, ukiwa na kesi Rais anaweza kumwagiza Jaji Mkuu peleka taarifa mpaka mahakama ya Wilaya hawa walioshtakiwa wafungwe, hakimu anaweza kumbishia Jaji Mkuu?
 
Baada ya kukandamizwa kwenye uchaguzi wa kanda sio, ameanza kubwekabweka :pedroP:

Viongozi wasimamizi wa uchaguzi wa kanda yake si walimwambia wamwpewa malekezo kutoka juu au alisemaje ndungu zango, tena yeye mwenyewe kwa kinywa chake:pedroP:

Kwani yeye Msigwa na wenzie alikua ana uwezo wa kumkataa au kimtoa msimamizi wa uchaguzi kule nyasa?, si mpaka mwenyekiti aamue:pedroP:

Kama mwenyekiti Taifa hajaamua yule yule atasimamia uchaguzi na ikawa hivyo pamoja na mabarua kibao aloandika ya kulalamikia rafu za uchaguzi:pedroP:
 
Naona baadhi wanapata shida sana kumuelewa Msigwa, binafsi namuona kapevuka sana kwenye ulingo wa siasa za kiushandani sio ndani ya Chadema alipo, bali kwenye siasa za Tanzania kiujumla.

Mara kadhaa Msigwa amekuwa akihusishwa na kutaka kwenda CCM, ukitazama wanaomhusisha na hizo tuhuma wengi ni walaini kwenye siasa za kiushandani, wanaoogopa malumbano ndani ya taasisi hata kama mwisho wa siku ndio yanazidi kuijenga taasisi husika.

Mfano, Msigwa kusema hakuridhishwa na namna mshindi alivyopatikana kwenye uchaguzi wa kanda ya Nyasa hivi karibuni hivyo kuamua kukata rufaa, ajabu wengi wanaona hiyo ni njia yake ya kuelekea CCM, hawaoni kama hiyo ni njia yake ya kudai haki yake anayoona amedhulumiwa kwenye ule uchaguzi!.

Ajabu zaidi wengine akiwemo MMM kuonekana kushangazwa na namna baadhi ya viongozi/wafuasi wa CCM wanavyoshangilia na kuonekana wapo upande wa Msigwa kwenye hiyo issue, kwao wanamuona Msigwa kama ana wafuasi ndani ya CCM.

Hawakumbuki CCM ni mshindani wao na lazima wakiona kuna dalili ya mgogoro ndani ya Chadema, waitumie nafasi kuukuza kwa kuchukua upande mmoja wa aliye kwenye huo mgogoro, hawa wanadhani kuna siku CCM itasema mazuri ya Chadema, hawajiulizi mbona CCM hawaripoti anayosema Msigwa akiwa na Lissu kwenye mkutano wao huko Singida?

Kwa akili zao mbovu wao ndio wanaamua kuukuza zaidi mgogoro na kuipa ushindi CCM kwa kuanza kumpiga kwa mawe mwanachama mwenzao ndani ya Chadema, hawa simply hawajioni kama wameshaingia kwenye mtego wa CCM.

Licha ya kuwa kwao kwenye siasa za upinzani kwa muda mrefu, bado ni wachanga kwenye siasa za ushindani, siasa za nguvu ya hoja, wao wanataka mkiwa chama kimoja basi mfanane kila msimamo na kila jambo, tena kila wakati, kama maembe juu ya mti, Msigwa is above them all.

Wanataka kama Msigwa anaona amedhulumiwa haki yake anyamaze kimya, huo kwao ndio utii kwa chama na sio ujinga, hawa hawataki aitishe press conference, hiyo kwao ni dalili ya kuondoka Chadema kwa Msigwa na wala sio haki yake ya uhuru wa kutoa maoni yake kikatiba, wako negative tu ajabu wanajiita wana demokrasia!.

Iko siku watamuelewa Msigwa tu.
 
Mchungaji Peter Msigwa akizungumza Jumatano kwenye mkutano wa hadhara wa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA bara Tundu Lissu uliofanyika Jumatano Juni 05, 2024 katika...
Chadema miaka yote mwenye maaamuzi ya mwisho ni Mbowe na HAKUNA mwenye kuleta fyoko akiishaamua Mbowe. Mfano, Mbowe alitaka ashinde Sugu na sio Mch. Msigwa na ikawa. Ondoa mfumo kandamizi Chadema kabla hujakemea wengine Dogo!
 
Huyu alifaa kabisa kuwa Katibu Mkuu wa Chama. Mnyika amepoa sana. Siyo yule wa zamani.
John Pambalu Kijana Machachari sana anafaa Ukatibu Mkuu wa CHADEMA.
images.jpeg-1.jpg
 
Never and I repeat never will this happen.
It is just a pipe dream or a wishful thinking.
Yaani shemeji zangu wawaachie chiasaka uongozi wa Chadema?
Endelea kuota.
Hii safu labda ianzishe chama chao sio Chadema.
Utakuwa huna akili wewe tui la nazi
 
Never and I repeat never will this happen.
It is just a pipe dream or a wishful thinking.
Yaani shemeji zangu wawaachie chiasaka uongozi wa Chadema?
Endelea kuota.
Hii safu labda ianzishe chama chao sio Chadema.
Imefika zamu ya dikteta uchwara kunyofolewa kwenye uongozi.
 
Back
Top Bottom