Mda wa mtoto kuwa shule upunguzwe

Mda wa mtoto kuwa shule upunguzwe

Uwesutanzania

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2019
Posts
1,380
Reaction score
1,686
Mda ambao mtoto anautumia kuwa shule ni mda mwingi mno.

Namaanisha ni ile anaenda shule saa 11 asubuhi alafu anarudi saa 11 jioni, kuanzia Jumatatu mpaka ijumaa,.

Hii inapelekea mtoto kukosa malezi bora ya mzazi na kutengeneza jamii isio na maadili mema.

Au kama ni ngumu kupunguza mda wa mtoto kuwa shule basi msogeze mda wa kuwapokea hawa watoto.

Yaani muanze kupokea watoto wenye umri wa miaka 12 na zaidi au hata 14. Hii itasaidia kupokea watoto ambao tayari wana malezi bora kutoka kwa wazazi wao familia na jamii kwa ujumla.

Nimesema haya yote ni baada ya kuwa na mitaala mibovu katika shule zetu za msingi na kuwa na waalimu wasio na weredi katika kumjengea mtoto kesho yake iliyo njema katika jamii na maisha yake kiujumla.


Siku izi kumekuwa na vijana wenye maadili mabovu na wasio na matendo mema bila ya kujua nini mzizi wa haya yote,.

Ndugu yangu msomaji mwaribifu mkubwa wa kizazi chako ni shule na waalimu.

Hivyo ili kuokoa kizazi chako jitahidi sana uwe unatumia mda mwingi kuwa kalibu na watoto wako ni si kuipa majukumu shule.

Cha kushangaza zaidi wazazi wengi mmekuwa mnaanza kupeleka watoto katika shule za awali wakiwa wadogo sana miaka 3,4,5 nk hii sio sawa.

Huku ni kumuaribu mtoto kizungu wanachojifunza na masomo wanayofundishwa hayana maana yeyote katika maisha yao na familia zao za baadae.

Ni mimi wako UWESUTANZANIA.

Daaaah, mwanangu umefikili kimjini sana. Alafu mimi nipo zangu kijijini huku. Tunaamka asubuhi mimi na mke wangu tunaenda shamba kila siku bila ya watoto wetu kwa kigezo cha shule,. Afu inakuwa wakija hawajui jembe, afu wanarudi mtaani elimu imeshawatupa.

Mazazi menyewe matakataka haya yana malezi gani?

Nchi zilizofanikiwa ktk elimu,muda wa masomo ni mdogo sana.Kwa mfano Finland watoto wanaanza shule kuanzia umri wa miaka 7 na masomo yanakuwa masaa machache kwa siku.Walimu wa kwanza ni wazazi au walezi nyumbani na watoto lazima wapitie utoto wao wakiwa nyumbani.Tunaomba Mhe Rais alione hili na afanye mabadiliko ktk elimu na historia itamkumbuka kwa hili.
 
Shule Gani inapokea watoto saa 11 alfajiri?

Kama muda huo ndo muda anaotoka nyumbani kwako hizo ni chanagamoto zako wewe tafuta shule karibu na maeneo unayoishi

Cha kushangaza zaidi wazazi wengi mmekuwa mnaanza kupeleka watoto katika shule za awali wakiwa wadogo sana miaka 3,4,5 nk hii sio sawa
Haya ni matatizo ya nani wazazi au shule ?
Huku ni kumuaribu mtoto kizungu wanachojifunza na masomo wanayofundishwa hayana maana yeyote katika maisha yao na familia zao za baadae.
Sasa unawapeleka kufanya nini kama hakuna faida
 
Nchi zilizofanikiwa ktk elimu,muda wa masomo ni mdogo sana.Kwa mfano Finland watoto wanaanza shule kuanzia umri wa miaka 7 na masomo yanakuwa masaa machache kwa siku.Walimu wa kwanza ni wazazi au walezi nyumbani na watoto lazima wapitie utoto wao wakiwa nyumbani.Tunaomba Mhe Rais alione hili na afanye mabadiliko ktk elimu na historia itamkumbuka kwa hili.
 
Mda ambao mtoto anautumia kuwa shule ni mda mwingi mno.

Namaanisha ni ile anaenda shule saa 11 asubuhi alafu anarudi saa 11 jioni, kuanzia Jumatatu mpaka ijumaa,.

Hii inapelekea mtoto kukosa malezi bora ya mzazi na kutengeneza jamii isio na maadili mema.

Au kama ni ngumu kupunguza mda wa mtoto kuwa shule basi msogeze mda wa kuwapokea hawa watoto.

Yaani muanze kupokea watoto wenye umri wa miaka 12 na zaidi au hata 14. Hii itasaidia kupokea watoto ambao tayari wana malezi bora kutoka kwa wazazi wao familia na jamii kwa ujumla.

Nimesema haya yote ni baada ya kuwa na mitaala mibovu katika shule zetu za msingi na kuwa na waalimu wasio na weredi katika kumjengea mtoto kesho yake iliyo njema katika jamii na maisha yake kiujumla.


Siku izi kumekuwa na vijana wenye maadili mabovu na wasio na matendo mema bila ya kujua nini mzizi wa haya yote,.

Ndugu yangu msomaji mwaribifu mkubwa wa kizazi chako ni shule na waalimu.

Hivyo ili kuokoa kizazi chako jitahidi sana uwe unatumia mda mwingi kuwa kalibu na watoto wako ni si kuipa majukumu shule.

Cha kushangaza zaidi wazazi wengi mmekuwa mnaanza kupeleka watoto katika shule za awali wakiwa wadogo sana miaka 3,4,5 nk hii sio sawa.

Huku ni kumuaribu mtoto kizungu wanachojifunza na masomo wanayofundishwa hayana maana yeyote katika maisha yao na familia zao za baadae.

Ni mimi wako UWESUTANZANIA.
Tatizo ni sisi wazazi. Mtoto unampeleka shule ya mbali so school bus inamptia saa 11 na inamrudisha saa 12 maana wa kwanza kupitiwa wa mwisho kurudishwa.
Mimi wanangu school hus inapita saa moja na nusu na saa tisa na robo wako nyumbani maana shuleni ni karibu sana kiasi kwamba kwenda au kurudi kwa gari ni mwendo usiozidi dakika 15
 
wazazi wenyewe wanaokaa nyumbani wako wako wapi, au umeongea tu bila utafiti?
Na wengine hadi kwakuwa hawakai home wanawapeleka shule wakashinde huko watoto wa miaka miwili watawapitia wakiwa wanarejea.
Hata watoto wakirejea home wanakuta dada wa kazi si wazazi.
 
Na wengine hadi kwakuwa hawakai home wanawapeleka shule wakashinde huko watoto wa miaka miwili watawapitia wakiwa wanarejea.
Hata watoto wakirejea home wanakuta dada wa kazi si wazazi.
ndio maana nimemuuliza mtoa mada hao wazazi wa kuleta malezi kwa watoto wanarudi majumbani saa mbili mpaka saa nne usiku
 
Uvivu wa kufikiri tunakuja na thread haina mashiko
 
Tatizo ni sisi wazazi. Mtoto unampeleka shule ya mbali so school bus inamptia saa 11 na inamrudisha saa 12 maana wa kwanza kupitiwa wa mwisho kurudishwa.
Mimi wanangu school hus inapita saa moja na nusu na saa tisa na robo wako nyumbani maana shuleni ni karibu sana kiasi kwamba kwenda au kurudi kwa gari ni mwendo usiozidi dakika 15
Jamani olympio na diamond hv kuanza kufundisha saa moja kamili ni SERA ya wizara u wao Peke yao maana mostly wanafunz wa hz shule wanatoka suburban mfano mbagala kimara kigamboni nk huwez kukuta wakaz wa upanga na kariba yao wanapeleka watt hapo lakn mda wa kuanza ni exactly saa moja jaman kwa nn isiwe saa mbl halafu watt wanakaa mpk saa 10 hv jamn darasa la 7 kwa mtihan gan mnakomaza watt mpk mda huo na mpk jpl excluding sikukuu za dini baas
 
Tatizo ni kutojua mzizi wa tatizo. Mnaoambana na maua badala ya kutibu mizizi ya mti.

Chimbuko ni mfumo wa majukumu ya Mzazi. Zamani kulikuwa na mgawanyo wa majukumu katika familia ambapo baba alikuwa Mtafuta hela na mama mtunza familia.

Kwa sasa baba na mama ni watafuta hela. Hili halina tatizo. Tatizo ni kuwa mabadiliko haya hayajaendana na mfumo wa kazi.

Kama tungekuwa tunajielewa saa za kuingia ofisini ingekuwa saa 3 asubuhi, badala ya saa 1 na nusu asubuhi. Hili tatizo la Watoto kuondoka nyumbani saa 11 asubuhi lingeisha. Wazungu si wajinga walioweka utaratibu wa kuanza kazi saa 3.

Mimi katika taasisi yangu kazi zinaanza saa mbili na nusu asubuhi.
 
Tatizo ni wewe wala siyo shule. Serikali imejenga shule kila kata Ina maana wewe huishi kwenye kata? Shule za serikali watoto wanatoka saa 5-6 mchana.
 
Nchi zilizofanikiwa ktk elimu,muda wa masomo ni mdogo sana.Kwa mfano Finland watoto wanaanza shule kuanzia umri wa miaka 7 na masomo yanakuwa masaa machache kwa siku.Walimu wa kwanza ni wazazi au walezi nyumbani na watoto lazima wapitie utoto wao wakiwa nyumbani.Tunaomba Mhe Rais alione hili na afanye mabadiliko ktk elimu na historia itamkumbuka kwa hili.
Sawa kabisa
 
Tatizo ni wewe wala siyo shule. Serikali imejenga shule kila kata Ina maana wewe huishi kwenye kata? Shule za serikali watoto wanatoka saa 5-6 mchana.
Oya mwanangu tusivunjiane heshma,

Shule ipi ya msingi mtoto anatoka saa 5…
 
Tatizo ni kutojua mzizi wa tatizo. Mnaoambana na maua badala ya kutibu mizizi ya mti.

Chimbuko ni mfumo wa majukumu ya Mzazi. Zamani kulikuwa na mgawanyo wa majukumu katika familia ambapo baba alikuwa Mtafuta hela na mama mtunza familia.

Kwa sasa baba na mama ni watafuta hela. Hili halina tatizo. Tatizo ni kuwa mabadiliko haya hayajaendana na mfumo wa kazi.

Kama tungekuwa tunajielewa saa za kuingia ofisini ingekuwa saa 3 asubuhi, badala ya saa 1 na nusu asubuhi. Hili tatizo la Watoto kuondoka nyumbani saa 11 asubuhi lingeisha. Wazungu si wajinga walioweka utaratibu wa kuanza kazi saa 3.

Mimi katika taasisi yangu kazi zinaanza saa mbili na nusu asubuhi.
Bado hayo masaa mawili ni machache mno kwa kombinesheni ya mzazi na mtoto
 
Jamani olympio na diamond hv kuanza kufundisha saa moja kamili ni SERA ya wizara u wao Peke yao maana mostly wanafunz wa hz shule wanatoka suburban mfano mbagala kimara kigamboni nk huwez kukuta wakaz wa upanga na kariba yao wanapeleka watt hapo lakn mda wa kuanza ni exactly saa moja jaman kwa nn isiwe saa mbl halafu watt wanakaa mpk saa 10 hv jamn darasa la 7 kwa mtihan gan mnakomaza watt mpk mda huo na mpk jpl excluding sikukuu za dini baas
Tupo pamoja, wanaosema shule saa moja waulize kengele ya kwanza inagongwa saa ngapi
 
wazazi wenyewe wanaokaa nyumbani wako wako wapi, au umeongea tu bila utafiti?
Daaaah, mwanangu umefikili kimjini sana. Alafu mimi nipo zangu kijijini huku. Tunaamka asubuhi mimi na mke wangu tunaenda shamba kila siku bila ya watoto wetu kwa kigezo cha shule,. Afu inakuwa wakija hawajui jembe, afu wanarudi mtaani elimu imeshawatupa.
 
Back
Top Bottom