MDAHALO: M4C, Hatima ni Mageuzi au Mapinduzi?

MDAHALO: M4C, Hatima ni Mageuzi au Mapinduzi?

is this the same as saying Poverty is Injustice therefore fighting Poverty is Fighting Injustice?
Fighting injustice is fighting poverty.

Kwanza tuanze na definition hii ya injustice...
in·jus·tice

   /ɪnˈdʒʌstɪs/ Show Spelled[in-juhs-tis] Show IPA
noun 1. the quality or fact of being unjust; inequity.

2. violation of the rights of others; unjust or unfair action or treatment.

3. an unjust or unfair act; wrong.
Rushwa ni injustice,ufisadi ni injustice.(vinasababisha umasikini)

Utawala unaotumia nguvu ni injustice,polisi kuuwa wananchi wasio na hatia ni injustice(vina violate haki za kimsingi za wananchi)

Chochote kinachofanywa na watawala wetu ambacho kina negative impact kwenye maisha ya wananchi wake ni injustice.

So yes poverty is injustice,and therefore fighting injustice is fighting poverty amongst others.

m4c is for educating the mass on their rights,and the state of their economic and political affairs,that equals to fighting injustice.

Kuhusu wether lengo la m4c ni reforms au revolution,nadhani swali lako hilo ni la kimtego zaidi.Kwasababu umezungumzia economic ferorms peke yake na ndiyo maana ukazungumzia issue za world bank etc.Je unataka kusema hata hizo reforms ambazo zimefanyiwa kazi na ccm zilifanikiwa?Jibu ni hapana!Sababu zake,bado ni injustices inayotokana na poor implementations.Ni kweli sera nyingi za world bank na imf siyo very helpfull kwa mataifa masikini,lakini bado tungeweza kufanya vyema kuliko sasa.

Same thing kuhusiana na rasilimali zetu,yes makampuni makubwa yanatubana kuhusiana na wanacholipa,lakini corruptions na 10 percent ndiyo injustices kwa wananchi.Hayo yangekuwa fixed kwanza,ndiyo tuangalie whats next kuhusiana na kuifanya mikataba itunufaishe.Hatuwezi kuzungumzia kuhusu mikataba kutunufaisha na wakati kuna viongozi wanaopendwa na hayo makampuni kwasababu in reality wanawakilisha matumbo yao badala ya maslahi ya taifa.

Wala hakuna haja ya kujiumiza kichwa kuuliza kama ni revolution ama reforms,kwasababu hayo ni matokeo ya maamuzi ya wananchi na wala si chama cha siasa.Chama cha siasa kinaweza kujikita kutoa elimu hiyo(m4c),lakini ni juu ya wananchi kufanya maamuzi.Na ndiyo maana tunatabiri kuwa maamuzi hayo watayafanya 2015.

Ila ikitokea kuwa watawala wanawanyima wananchi wake haki zao za kimsingi(unyanyasaji na mauwaji kwenye m4c),basi ujuwe kuwa watawala ndiyo wanaweza kusababisha mapinduzi kutokana na injustice.Hayo mambo hayapangwi,bali hutokea kwenye proccess ya wananchi kudai haki na wao kubinywa,hapo ndipo wana revolt kutokana na udhalimu wa watawala.

Nafahamu kwamba umetoa definitions kadhaa za mapinduzi ie umezungumzia mapinduzi ya kiuchumi,hayo hayahusiana na injustice,kwa mfano industrial revolution,hayo ni mapinduzi ya viwanda,kilichofanyika si sawa na tunachozungumzia hapa na wala hakina relation yoyote na yatakayoweza kutokea kutokana na m4c.Hilo haliwezekani kwasababu chadema siyo chama cha kisoshalisti wala kikomunisti.Hivyo hakutaweza kuwa na rapid change of the economic system(characteristic ya economic revolution).

However tunaweza kuwa na economic revolution kama tukiwekeza pesa nyingi kwenye ukuwaji wa viwanda badala ya mafisadi kuziweka uswisi na kwingineko.

Pia hata ubepari wenyewe,umepitia reforms na bado unaendelea kupitia reforms.Na ndiyo maana hata mimi nimekuwa nikisema kuwa tunayapokea ya ubepari bila kujitathimini,haina maana kwamba tukiyafanyia teforms basi ni kwamba hatuupendi ubepari,la hasha!La msingi kuelewa hapa,ni kwamba hata ubepari bado unahitaji reforms na ndicho kinachoendelea hata kwenye mataifa ya wenzetu.Kila mara kuna reforms zinazofanyika ili kuweza kuwanufaisha wananchi na ku eliminate injustices as much as possible.

Njia ya kujaribu kubadili ubepari, au 'mageuzi', ni mojawapo ya njia ambazo zimewahi kuchukuliwa na wenzetu ambapo walitaka kuboresha jamii. Baadhi ya mageuzi yamesaidia kuboresha maisha yao kwa ujumla na mazingira yao ya kazi.

Kiukweli,hakuna ubaya kuona kampeni(m4c) kwa ajili ya mageuzi ya kuleta maboresho muhimu na kuongeza ubora wa maisha ya wananchi.Kuna mifano ya hili katika nyanja kama vile elimu, makazi(mipango mji nk),na usalama wa kijamii.Tumeona kuna matatizo kwenye idara ya afya(migomo ya madaktari,wagonjwa kulala chini,ukosefu wa vifaa na madwa etc etc),tumeona pia kuhusiana na elimu(malipo ya walimu,na hali halisi ya shule zetu pamoja na vifaa,madarasa nk).

Mageuzi hayo ambayo hata wenzetu waliyafanya chini ya mfumo wa kibepari,yamesaidia sana.Ni kweli hayajamaliza matatizo yote,lakini yamesaidia.Kujaribu kutaka kuyamaliza matatizo yote ya ubepari,ni kujaribu mfumo mwingine tofauti na ubepari(REVOLUTION),jambo ambalo sidhani kama linaendana na sera na itikadi za chadema,ambao wameshasema kuwa wao ni a "right wing party"

Ni kweli kwamba kumekuwepo na reforms ama shinikizo la reforms kutoka kwa world bank na IMF kuhusiana na mikopo wanayotupa,mingine ina masharti ya kupeleka pesa hizo kwenye nyanja ambazo binafsi huwa naona kama sizo ambazo tungezichaguwa sisi endapo tungepewa uhuru huo.Kwa maana ya kwamba there are strings attached that tends to be unbeneficial to us,however bado unaweza kuona kwamba hata hiyo mikopo bado tunai missuse.Hili linahitaji reforms in terms of how we manage the funds and how we implement the projects.Hilo linahitaji serikali mbadala.

WB na IMF kiukweli,zilianzishwa ili kukabiliana na usoshalisti pamoja na ukomunisti,(my take)haswa baada ya serikali zenye mirengo hiyo kutengwa,na baada ya chumi zake kuyumba,ndipo zikaja hizo institutions.

Kama unakumbuka,hayo ni baadhi ya mambo ambayo mwalimu Nyerere alikubaliana nayo kwa shingo upande,na masharti yao yalikuwa ni reforms ambazo hata yeye mwalimu aliona ni kinyume kabisa na maono yake kwa taifa hili.(ujamaa na kujitegemea)

Pamoja na hayo,bado serikali zetu zimekuwa kama zinacheza upatu kwa kuyaweka maisha ya wananchi wake rehani.

Niishie hapo kwasasa...Na kama ikiwezekana,ama kama umenielewa,basi tuyazungumzie hayo ya reforms tulizozifanya(chini ya ccm), ili kuweza kuendana na mapendekezo ya WB na IMF.Hilo litatusaidia kuona kuwa ni wapi tumeshindwa na kama sababu hizo za kushindwa huko ni za kwetu sisi ama kama ni za hizo instituiton.Au pengine labda ni a combination of both factors.

The bottomline ni kwamba m4c haina nia mbaya na taifa letu,unless kama unaamini kwamba tuko on the right track.

Undo edits
 
Wembe Wenge,

Nashukuru sana kwa mchango wako mzuri na wenye kutia moyo; Nimekuwa Napata mashambulizi makali sana humu kwamba nia yangu sio njema kwa Chadema na Demokrasia kwa ujumla,lakini pia kuna nyakati huwa natumiwa Private Messages za mashambulizi na vitisho kila ninapowasilisha mada zinazoonekana kuishika CCM pabaya, na pia mara kutoka kwa wapenzi wa Chadema; Pamoja na haya yote, haijalishi kwani TO GOD, ONE IS MAJORITY.

Kwa jinsi navyokusoma, wewe ni Reformer kama mimi, lakini muhimu zaidi, ninaheshimi matakwa, ndoto na maamuzi ya UMMA kuliko imani yangu binafsi katika suala zima la Mabadiliko, na katika hili, naunga mkono hoja yako kwamba UMMA ndio Watendaji Wakuu.

Lakini unaposema tunahitaji mabadiliko ya kimfumo, huoni kama kuna a very thin line baina ya mageuzi na mapinduzi iwapo suala ni mabadiliko ya mfumo? Kwa mfano, Tanzania imejikita katika MAGEUZI ya Kisiasa - kutoka demokrasia ya Chama Kimoja kwenda Vyama Vingi, lakini je, ni kweli kuna mabadiliko ya Kimfumo katika hili? Hoja yangu hapa ni kwamba we may believe in Reforms but it may take more than reforms kufanikisha tunachokitaka; Ndio maana CCM ikaitwa Chama Cha Mapinduzi kwani yalihitajika mapinduzi kuliko mageuzi kufanikisha mabadiliko mbalimbali ya kimfumo, hasa katika utekelezaji wa Sera ya Ujamaa na Kujitegemea; Lakini Suala hili la Mapinduzi kwa CCM limeshapitwa na wakati, na katika siasa za Leo, CCM kutumia neno mapinduzi is more of a political liability kuliko a political asset, hasa kwa sababu CCM has betrayed its own history;

Ningependa pia kukuuliza swali lingine – Je, binafsi unapendelea Mageuzi kuliko Mapinduzi kwa sababu zipi hasa? Je ni kwa sababu Mapinduzi huambatana na ghasia na umwagaji wa damu? Au ni kwa sababu una amini kwamba Mageuzi yanayoongozwa na World Bank na IMF carry so much potentials kutufikisha tunapotaka kwenda, tatizo ni ufanisi katika utekelezaji wa Sera hizi? Iwapo sababu yako ni hii, basi tuzidi kuamini kwamba Chadema wakienda ikulu wataenda kufanya kazi ile ile chini ya World Bank na IMF ambayo kwa sasa inafanywa na CCM;

Tofauti itakayojitokeza pengine tukiwa na Chadema ikulu ni ya KIUFANISI ZAIDI katika kutekeleza mageuzi ya kisiasa, kiuchumi, sekta ya utumishi wa umma na sekta ya usimamizi wa fedha za umma, hivyo kuongeza uwazi, uwajibikaji, kuthibiti rushwa, kuongeza mapato ya serikali, kuandaa bajeti zinazoendana na mahitaji ya watanzania, kuboresha huduma za kijamii, hivyo kupunguza umaskini/kuboresha hali za wananchi walio wengi; This in itself ni swa kabisa, kama lengo kuu la chadema ni hilo, ni kwamba tu liwekwe wazi;

Pia umezungumzia suala la Utawala wa Kibabe, dhuluma n.k, kama kichocheo cha Mapinduzi; hii ni sahihi kwani Mapinduzi yanatokea iwapo tu Mabadiliko Kupitia Mageuzi become futile/unproductive; Syria, kama ulivyoelezea, awali UMMA ule haukuwa na tatizo na utawala wa Assad, walipendelea uendelee kuwepo lakini on condition kwamba Assad alete mageuzi ya kisiasa hasa; lakini kwa sababu tusizozijua kwa undani sana, reaction ya Assda ndio imepelekea UMMA kujikita katika mapinduzi; Ni matumaini yetu sisi reformers wote kwamba CCM itafanikisha mabadiliko kuboresha equality and equity kwa wananchi – kisiasa, kiuchumi, na kijamii kwa kupitia mageuzi na haita fanya makosa kama ya Assad;

Na mwisho ningependa kuzungumzia hoja yako juu ya utayari wa mabadiliko miongoni mwa UMMA, bila ya kujali whether M4C ipo au haipo; hii ni hoja nzito na kama wanaopingana na wewe katika hili watajitokeza, jiandae kujikinga KI-HOJA; Vinginevyo I find your view interesting; Kuna hoja za wadau kadhaa humu zilizojadili kwamba – Watanzania hawapo tayari kwa mabadiliko, na badala yake, mikusanyiko mikubwa tunayoona kwenye harakati za M4C, ni hulka tu ya watanzania kupenda kukusanyika na ku-share their griefs, na muda mfupi baadae, wanarudi katika hali zao za maisha ya kila siku na kusahau kinachoendelea; Una mtazamo gani katika hili?
 
Kwa maana hii, UMMA wa watanzania (sehemu kubwa) unaotikia M4C kwa mwamko mkubwa, je ni kwamba:

*Umma huu Hauna ufahamu juu ya Mageuzi yanayoendelea kutekelezwa na serikali ya CCM na kusimamiwa na World Bank na IMF kwa miaka 26 sasa, Mageuzi ambayo yanalenga kuboresha hali zao za maisha? AU

*Wana ufahamu lakini kasi na matunda ya mageuzi haya imeshindwa kukidhi matarajio, matumaini, matakwa na ndoto za watanzania walio wengi, hivyo they are increasingly becoming open to more/other options including Radical ones?
Hakuna nchi ambayo imeendelea/inaendelea kupitia misaada ya IMF na World Bank tuachane na hii dhana,Tunahitajika kufikiria zaidi/.mbali ya hawa wakoloni.wanachokifanya ni kutufanya survivors.
 
Mkuu Mchambuzi,

Wamekuwa wakiichagua CCM kwa
(1) mazoea tuu,
(2) ignorance na
(3) no credible option hivyo bora "zimwi likujualo"!.


Kwa mliongalia mjadala wa jana US, sisi pia tutatamani kuwapima vagombea wetu kwa utaratibu huu, na tuweke mecchanisim lazima wagombea washiriki debate, sio options bali a compulsory ili kuwapima, tupate kiongozi bora na sio bora kiongozi!.

Thanks.

Pasco.

NB: Kwa msisitizo!, Pasco wa JF sio mwanachama, mfuasi, au mshabiki wa chama chochote cha siasa, bali ni muumini wa kutanguliza mbele maslahi ya taifa ili 2015 tupate ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania.

Mkuu Pasco,

Hilo la kushinikiza mediahouse kusponsor mijadala ya kitaifa ni la muhimu sana kama tunataka viongozi wa kweli,tuachane na tabia hii ya kujadili watu na kuwajenga. Kama ni kujijenga basi wajijenge wenyewe kwa kujitokeza kwenye mijadala ya kitaifa ili tuwapime sawasawa uwezo na matarajio yao kwa maendeleo ya nchi.

Mjadala au mdahalo wa wagombea wa Marekani iwe ni fundisho kwetu kushinikiza wagombea kushiriki midahalo.Yule ambaye ataonekana ana ogopa midahalo vyombo vya habari vipaishe sauti kumuonyesha kuwa uwezo wake ni wa kutia shaka na ana ajenda ya siri dhidi ya umma wa watanzania.

Sioni sababu nzuri ya mtu anayetafuta uongozi wa umma aogope kujitokeza kusailiwa makusudi yake ya kutaka uongozi.Hali itatengeneza mwelekeo kuwa anasukumwa na masilahi binafsi ya wale walio nyuma yake.Utaratibu tuujengee wigo wa wagombea kutotoa visingizio visivyo na mashiko na uwe ni utamaduni wa kupima dhamira ya wanaotaka uongozi.

Ndugu Mchambuzi mungu akupe nguvu zaidi ili uwafungue fikra watanzania kujenga mustakabali mwema wa nchi yetu.
 
Mkuu Pasco,

Hilo la kushinikiza mediahouse kusponsor mijadala ya kitaifa ni la muhimu sana kama tunataka viongozi wa kweli,tuachane na tabia hii ya kujadili watu na kuwajenga.Kama ni kujijenga basi wajijenge wenyewe kwa kujitokeza kwenye mijadala ya kitaifa ili tuwapime sawasawa uwezo na matarajio yao kwa maendeleo ya nchi.Mjadala au mdahalo wa wagombea wa Marekani iwe ni fundisho kwetu kushinikiza wagombea kushiriki midahalo.Yule ambaye ataonekana ana ogopa midahalo vyombo vya habari vipaishe sauti kumuonyesha kuwa uwezo wake ni wa kutia shaka na ana ajenda ya siri dhidi ya umma wa watanzania.

Sioni sababu nzuri ya mtu anayetafuta uongozi wa umma aogope kujitokeza kusailiwa makusudi yake ya kutaka uongozi.Hali itatengeneza mwelekeo kuwa anasukumwa na masilahi binafsi ya wale walio nyuma yake.Utaratibu tuujengee wigo wa wagombea kutotoa visingizio visivyo na mashiko na uwe ni utamaduni wa kupima dhamira ya wanaotaka uongozi. Ndugu Mchambuzi mungu akupe nguvu zaidi ili uwafungue fikra watanzania kujenga mustakabali mwema wa nchi yetu.

Nsaji Mpoki,

Asante sana kwa mchango wako na vile vile kunitia moyo; Kuhusu suala la Wanasiasa kujijenga wenyewe, nadhani moja ya njia ya kufanikisha hilo ni kupitia midahalo, lakini cha ajabu, wanasiasa wa CCM wanaogopa midahalo kama ukoma; Unakuta hata kwenye kampeni za ndani ya chama kuchagua wagombea ubunge na udiwani, masuala ya majadiliano, au wagombea kuhoji juu ya utendaji wa madiwani na wabunge waliopo hayaruhusiwi kwa sababu eti kufanya hivyo ni kukivuruga chama kwani wapinzani wakisikia hoja husika, watazibeba na kuzitumia kwenye majukwaa wakati wa uchaguzi mkuu; Unakuta wagombea hawana wanachoshindania zaidi ya uwezo wa fedha, na kwa hilo tusiwalaumu sana wapiga kura katika michakato hii kwani hawapewi uwanja wa kutosha kupima wagombea;
 
Mchambuzi, desperation brings actions.. watu wetu wanaweza kuwa katika umaskini lakini bado hawajawa "desperate". Bado hatujafikia kwenye hiyo desperation ambayo in reality ndiyo inasababisha watu waamue kutenda. Sasa hivi tuko kwenye level ya chini sana ambayo ni contemplation.. tunatafakari tunachokiona na tunajaribu ku rationalize. We are trying to make sense of the insensible.

Wanasiasa na wana harakati wetu hawajaweza kuonesha kuwa tuko kwenye 'desperate situation'. Ni kwa sababu hii basi mapinduzi hayawezi kuja au kuletwa kwa sababu we are not in dire situation. Mageuzi yanaweza kuletwa lakini nayo yanakuwa precipitated na kutambua kuwa the 'status quo' CAN NOT and MUST NOT be maintained. So far tunaambiwa the status quo "CAN NOT" be maintained lakini haijajengwa hoja ya uthabiti (a firm argument) ya kwanini 'IT MUST NOT BE MAINTAINED'.

Na wapo watu watakaoshtushwa! Not me of course.

Hapo nilipohighlight ndilo lilikuwa kosa kubwa la Movement ya Egypt dhidi ya Mubarak na kuwapa mwanya Muslim Brotherhood kufill haraka hiyo vacuum ya kutojipanga.
 
Jmushi1,
Kwanza naomba nianze na hili:

The bottomline ni kwamba m4c haina nia mbaya na taifa letu,unless kama unaamini kwamba tuko on the right track.
Kama umenisoma vyema, naona mengi mazuri kuliko mabaya juu ya ujio wa M4C.

Fighting injustice is fighting poverty.
Rushwa ni injustice,ufisadi ni injustice.(vinasababisha umasikini)
Utawala unaotumia nguvu ni injustice,polisi kuuwa wananchi wasio na hatia ni injustice(vina violate haki za kimsingi za wananchi)
Chochote kinachofanywa na watawala wetu ambacho kina negative impact kwenye maisha ya wananchi wake ni injustice.
So yes poverty is injustice,and therefore fighting injustice is fighting poverty amongst others.

Baada ya kutafakari kwa muda, nakubaliana na wewe kwamba HAKI ni key denominator. FIGHTING INJUSTICE IS FIGHTING POVERTY badala ya mtazamo wangu wa awali kwamba Fighting POVERTY is Fighting INJUSTICE. Hii ni kwa sababu moja kubwa: Structural injustice ndio chanzo cha Umaskini, na moja ya njia za uhakika za kutatua the ‘injustice of poverty' ni kubadilisha muundo uliopo/structural change; Kwa maana nyingine, injustice ni tatizo la kimuundo zaidi, kuliko kimfumo. Iwapo unakubaliana na mimi katika hili, yafuatayo ni maeneo yanayozaa structutal injustice, na kupelekea Umaskini ndani ya jamii husika:


  • Unequal Access to Key Assets – Kwa Financial Assets (access to credit), Physical Assets (nyumba na vifaa mbalimbali vya kurahisisha shughuli za uchumi), Natural Assets (kama vile Ardhi) n.k


  • Unequal Participation in the Market Place – tunajua jinsi gani soko huria umewaacha watanzania walio wengi, hasa wa vijijini wamebakia wameduwaa kwa miaka zaidi ya 25 sasa – tangia ujio wa soko huria; Maskini Tanzania hawakupewa maandalizi ya kuingia katika mfumo wa soko huria, walishtukizwa tu, na mbaya zaidi ni kwamba mageuzi ya kiuchumi yaliingizwa na utawala wa Mwinyi kwa siri kubwa sana katika hatua za awali, pengine kuogopa Revolts;


  • Unequal Access to Human Development – Hapa masuala muhimu to determine human capital ni Afya Bora na Elimu Bora, sio Bora Elimu (kama shule zetu za kata) au Bora Afya (kama huduma za ovyo ovyo zinazotolewa kwa wananchi wetu, hasa wa vijijini);


  • Unjust Government – Utawala wetu largely disenfranchises the poor, na hili linatokana zaidi na ukosefu wa elimu ya uraia ambapo wananchi wengi hawajua wajibu wao kama raia ni nini na na hawajui wajibu wa serikali kwa raia ni nini;

Iwapo tunakubaliana katika haya, hasa kwamba injustice ni suala la kimuundo kuliko kimfumo, swali, linalofuata ni je: Kwanini inachukua muda mrefu sana kwa Mageuzi kuleta ufumbuzi wa tatizo hili? Nini kifanyike?
M4C is for educating the mass on their rights, and the state of their economic and political affairs, that equals to fighting injustice.

Mbowe alinukuliwa akielezea haya kuhusu M4C:

"Under the initiative, too, the party intended to make deeper inroads into the countryside, by opening several new branches, consolidating exiting ones, and recruiting many members. Through M4C, furthermore, Mr Mbowe told the audience, Tanzanians would be enlightened on their democratic rights, socialize into electing patriotism-driven national leaders, and advocate earnest protection of national resources." Source; The Citizen.

Hapa tupo pamoja...

Kuhusu whether lengo la M4C ni reforms au revolution, nadhani swali lako hilo ni la kimtego zaidi. Kwasababu umezungumzia economic ferorms peke yake na ndiyo maana ukazungumzia issue za world bank etc.Je unataka kusema hata hizo reforms ambazo zimefanyiwa kazi na ccm zilifanikiwa?Jibu ni hapana!Sababu zake,bado ni injustices inayotokana na poor implementations.Ni kweli sera nyingi za world bank na imf siyo very helpfull kwa mataifa masikini,lakini bado tungeweza kufanya vyema kuliko sasa.

In my original post, niliuliza hivi:

"Je: Viongozi wanaoendesha "Mass Movements" wana lengo gani – kuboresha Mageuzi (Reforms) ambazo Serikali ya CCM imekuwa inazitekeleza kwa miaka 26 sasa chini ya usimamizi wa IMF na World Bank au Viongozi wanaoendesha hizi "Mass Movements" wanalenga mbali zaidi ya Mageuzi?"

Hili halikuwa swali la mtego, na mdau mwenzetu miwatamu alikuja na majibu mazuri juu ya hili ambapo alitamka hivi:
"Ili kuonesha kuwa CCM sasa hivi inafanya kazi kama chama cha upinzani; kwanza ni hali yake ya kufanya kazi zake kwa kutekeleza matakwa ya Chadema, mpaka hapo utaona kuwa tayari chadema ipo madarakani hivyo kilichobaki ni kuthibitishwa kwa wananchi tu."

Tafsiri yangu juu ya hili ni kwamba Mageuzi bado ni njia sahihi kuletea mabadiliko watanzania lakini chini ya CCM, utekelezaji wake ni duni sana, na ndio maana baada ya amsha amsha za Chadema, CCM imeanza kukaza buti na angalau mambo yameanza kwenda, na iwapo Chadema itaingia ikulu 2015, itaenda kutekeleza Mageuzi haya kwa ARI ZAIDI, NGUVU ZAIDI, na KASI ZAIDI. Hii ni kauli mbiu ya CCM ambayo ni ya maneno tu, vinginevyo inahitajika kivitendo katika utekelezaji wa Mageuzi na pengine Chadema wataweza kutekeleza mageuzi haya kwa ufanisi zaidi ya CCM iwapo watashinda uchaguzi 2015;

Wala hakuna haja ya kujiumiza kichwa kuuliza kama ni revolution ama reforms,kwasababu hayo ni matokeo ya maamuzi ya wananchi na wala si chama cha siasa.Chama cha siasa kinaweza kujikita kutoa elimu hiyo(m4c),lakini ni juu ya wananchi kufanya maamuzi.Na ndiyo maana tunatabiri kuwa maamuzi hayo watayafanya 2015.

Hili nilishalijadili kwa mtazamo unaofanania na wako, ingawa nilihoji kwamba iwapo Chadema hawatapita 2015, wamejipanga vipi, hasa ikizingatiwa kwamba Mbowe alitoa kauli tata kidogo kwamba CCM ikishinda atajiuzulu Siasa? Sijapata jibu kutoka kwa mdau wowote hadi sasa.

However tunaweza kuwa na economic revolution kama tukiwekeza pesa nyingi kwenye ukuwaji wa viwanda badala ya mafisadi kuziweka uswisi na kwingineko.

Hapa umenichanganya kidogo - unaposema ECONOMIC REVOLUTION, una maana gani, Mapinduzi ya Kiuchumi? Na kwa Tanzania chini ya Chadema yatachukua mkondo gani?

Pia hata ubepari wenyewe,umepitia reforms na bado unaendelea kupitia reforms.Na ndiyo maana hata mimi nimekuwa nikisema kuwa tunayapokea ya ubepari bila kujitathimini,haina maana kwamba tukiyafanyia teforms basi ni kwamba hatuupendi ubepari,la hasha!La msingi kuelewa hapa,ni kwamba hata ubepari bado unahitaji reforms na ndicho kinachoendelea hata kwenye mataifa ya wenzetu.Kila mara kuna reforms zinazofanyika ili kuweza kuwanufaisha wananchi na ku eliminate injustices as much as possible.

Ni kweli, ubepari umekuwa unapitia reforms constantly, lakini ukumbuke kwamba ndani ya global capitalist system, kuna nchi participating from the centre (nchi tajiri) na nchi participating from the periphery/pembezoni (nchi maskini kama Tanzania), na ni zile in the centre calling all the shots; Ni hili ndio limepelekea Lenin-Marxist views kushika kasi kubwa katika dunia ya tatu, starting with the liberation movements and independence struggles in the 1950s-60s, and to an extent throughout the cold war period;

Vile vile ukumbuke kwamba hata mataifa makubwa, kabla ya kuachia ubepari utawaliwe na soko huria, kila nchi ilikuwa busy sana kujipanga ili kuweka the fundamentals right kwanza, kwa mfano kupitia slave trade, imperialism, colonialism, na uhalifu wa kila aina, kitu ambacho kilipelekea mataifa haya makubwa kupigana katika vita nyingi sana; ni baada ya vita kuu vya pili vya dunia kuisha ndipo mambo yakatulia huku wakiwa wameshajiwekea the world order kwa matakwa yao; so unaposema kwamba ubepari undergo reforms kila wakati, upo sahihi, lakini uelewe kwamba ubepari wa nchi tajiri ni tofauti na ubepari wa nchi maskini kama Tanzania ambapo hatuna real capitalists bali mafisadi ambao technically ni agents wa mabepari waliokamilika huko nje; Ndio maana many reforms kwa miaka 26 sasa zinaleta faida kwa foreign capital and its owners kuliko watanzania;

Kujaribu kutaka kuyamaliza matatizo yote ya ubepari,ni kujaribu mfumo mwingine tofauti na ubepari(REVOLUTION),jambo ambalo sidhani kama linaendana na sera na itikadi za chadema,ambao wameshasema kuwa wao ni a "right wing party"

Hili ni kweli, na sio tu Chadema haiwezi kufuata njia hii, bali chama chochote cha siasa including CCM; lakini hii aina maana kwamba hakuna alternative to the current system, mimi nina amini mbadala upo, na ni kwa kupitia democratic socialism ambayo inahimiza a welfare state, kama ilivyokuwa kwa nchi kadhaa za Scandnavia, Sweden in particular; Ndio maana Sweden walikuwa ni marafiki wa Ujamaa katika kipindi chote kuliko taifa lingine lolote, ni bahati mbaya tu kuna maeneo kadhaa Mwalimu aliyakoseka katika utekelezaji wa sera ya Ujamaa;

Ni kweli kwamba kumekuwepo na reforms ama shinikizo la reforms kutoka kwa world bank na IMF kuhusiana na mikopo wanayotupa,mingine ina masharti ya kupeleka pesa hizo kwenye nyanja ambazo binafsi huwa naona kama sizo ambazo tungezichaguwa sisi endapo tungepewa uhuru huo.Kwa maana ya kwamba there are strings attached that tends to be unbeneficial to us,however bado unaweza kuona kwamba hata hiyo mikopo bado tunai missuse.Hili linahitaji reforms in terms of how we manage the funds and how we implement the projects.Hilo linahitaji serikali mbadala.
WB na IMF kiukweli,zilianzishwa ili kukabiliana na usoshalisti pamoja na ukomunisti,(my take)haswa baada ya serikali zenye mirengo hiyo kutengwa,na baada ya chumi zake kuyumba,ndipo zikaja hizo institutions.
Kama unakumbuka,hayo ni baadhi ya mambo ambayo mwalimu Nyerere alikubaliana nayo kwa shingo upande,na masharti yao yalikuwa ni reforms ambazo hata yeye mwalimu aliona ni kinyume kabisa na maono yake kwa taifa hili.(ujamaa na kujitegemea)
Pamoja na hayo,bado serikali zetu zimekuwa kama zinacheza upatu kwa kuyaweka maisha ya wananchi wake rehani.
Niishie hapo kwasasa...Na kama ikiwezekana,ama kama umenielewa,basi tuyazungumzie hayo ya reforms tulizozifanya(chini ya ccm), ili kuweza kuendana na mapendekezo ya WB na IMF.Hilo litatusaidia kuona kuwa ni wapi tumeshindwa na kama sababu hizo za kushindwa huko ni za kwetu sisi ama kama ni za hizo instituiton.Au pengine labda ni a combination of both factors.

Ndio maana huwa nahimiza kwamba ili tuendeleaa we need a new and radical orientation – not necessarily Mapinduzi bali mfumo ambao utatufanya tuondokane na madudu haya ya IMF na World Bank, hasa mfumo ambao utakuwa na uwezo wa kulikemea soko huria na ubepari pale masuala haya yatakapokuwa yana act contrary to the welfare of Wananchi walio wengi; Tunahitaji mfumo ambao Utavumiliwa na Ubepari na Soko Huria huku vile vile na wenyewe utavumilia Ubepari na Soko Huria; Hili linawezekana na linawezekana kupitia A New Democratic Socialism System.
 
Wanasiasa na wana harakati wetu hawajaweza kuonesha kuwa tuko kwenye 'desperate situation'. Ni kwa sababu hii basi mapinduzi hayawezi kuja au kuletwa kwa sababu we are not in dire situation. Mageuzi yanaweza kuletwa lakini nayo yanakuwa precipitated na kutambua kuwa the 'status quo' CAN NOT and MUST NOT be maintained. So far tunaambiwa the status quo "CAN NOT" be maintained lakini haijajengwa hoja ya uthabiti (a firm argument) ya kwanini 'IT MUST NOT BE MAINTAINED'.

Mzee Mwanakijiji, nimekuwa najitahidi kuelewa hoja yako kuhusu the Status Quo Can not...Must Not be maintained.., lakini natoka kapa; Hii ni kwa sababu kwa uelewa wangu, Mageuzi Maintains the Status Quo, this is almost a principle that comes handy with the reforms hizi za Washington Consensus kwani nia ya mageuzi under the auspices of the World Bank & IMF ni kuzuia mianya ya mapinduzi to overthrow the current relations of production ambazo foreign capital enjoys by a larger margin kuliko maskini, lakini pia tunajua kwamba mapinduzi ni matoeo ya kushindwa kwa mageuzi; na katika mapinduzi, suala la Status Quo mara nyingi hutupwa kule. In other words mara nyingi than not, Mapinduzi isnt about the sustenance of the status quo but rather, kuitupilia mbali;
 
Kwa maana hii, UMMA wa watanzania (sehemu kubwa) unaotikia M4C kwa mwamko mkubwa, je ni kwamba:

*Umma huu Hauna ufahamu juu ya Mageuzi yanayoendelea kutekelezwa na serikali ya CCM na kusimamiwa na World Bank na IMF kwa miaka 26 sasa, Mageuzi ambayo yanalenga kuboresha hali zao za maisha? AU

*Wana ufahamu lakini kasi na matunda ya mageuzi haya imeshindwa kukidhi matarajio, matumaini, matakwa na ndoto za watanzania walio wengi, hivyo they are increasingly becoming open to more/other options including Radical ones?

una maana kwa miaka 26 tuendelee kusubiri??nilifikiri miaka mitano tunaweza kuona mabadiliko makubwa.jana nilisikia kwenye news Zambia imebadilika kwa mwaka mmoja na inaongoza kwa kukua kwa kasi kutokana na uongozi bora,ina maana uongozi bora unabadili hali halisi ya maisha ya mwananchi,tusidanganyane mabadiliko yanayolengwa na watanzania kwa sasa hayana macho,ni kama vita yatakayomkumba yatamsomba kama tsunami
 
Unaanza kutukana? You have to think hard au una interest zako.
 
Ili hoja yako hii ieleweke, ni muhimu ukatuzungusha japo kidogo KWA HOJA, vinginevyo ulichokisema hakijitoshelezi kwani CCM imekuwa inatekeleza mageuzi makubwa kwa miaka 26 sasa, na moja ya mageuzi hayo kwa mfano ni ya kisiasa ambayo yalipelekea kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi hence ujio wa Chadema 1995, mageuzi ya uchumi ambayo yameruhusu vyama vya upinzani mfano Chadema kuweza uza itikadi zao nje ya ile ya Ujamaa na Kujitegemea, n.k; nadhani you get my point- ili ueleweke, kuna umuhimu wa kuzunguka KIHOJA, vinginevyo ulichozungumza hapa hakina maana, na ni rahisi sana kika potoshwa na kikawekwa completely out of Context; Ni kwa sababu ya kuzunguka zunguka, ndio maana ni wachangiaji wachache sana humu ambao wananiuliza maswali, vinginevyo niliyosema kupitia mzunguko wa Hoja, kwa wengi yanajitosheleza na ndio maana tunaendesha Mdahalo tukiwa ukurasa Mmoja;mfano rejea post No.35 ya uzi huu by karug;

Ushauri wangu ni - jaribu kuzunguka zunguka kidogo, KWA HOJA, ili ueleweke vyema;

Mkuu makala yako ni nzuri na umechambua mambo mengi vizuri na kutoa dondoo za mdahalo. Isipokuwa kwa baadhi ya watu itakuwa ni vigumuni kuelewa hoja Kama hatataweza kufanya proper interpretation , na ukumbuke interpretation itategemea sana uelewa au mtu alivyo-perceive hoja.

Kwa mfano heading ya topic yako 'M4C, Hatima ni Mageuzi au Mapinduzi?' Ni kweli unaweza kuwa na hatima ya mageuzi AU Mapinduzi. Lakini Kama nilivyoeleza kwa ufupi, unaweza kuwa na hatima ya vyote kwa pamoja yaani mageuzi NA Mapinduzi.

CCM haijawahi kufanya Mapinduzi yoyote mbali na kumpindua mkoloni ikiwa kama TANU. CCM haijawahi kuleta Mapinduzi ya kisiasa, kiuchumi hata ya kijamii. CCM imekuwa ikifanya mabadiliko-yaani kuweka viraka na hasa kwa maslahi a watawala.
Mfano kwa miaka hamsini serikali imekuwa ikitumia katiba na sheria zilezile zilizoachwa na mkoloni ambazo kusudi lake ilikuwa ni kumlinda mkoloni. Mabadiliko yaliyofanyika ni yale yasiyoingilia maslahi ya watawala. Hakuna vipengele vya katiba au sheria vilivyofanyiwa marekebisho ili kufanya watawala wawajibike kwa wananchi. Watawala wameendelea kuwa wakoloni.

Ujio wa vyama vingi haikuwa maamuzi ya CCM. Ilikuwa ni matokeo ya international pressure iliyotaka hivi vi-nchi vyetu vya ki-dictator vi-adopt mfumo wa ki demokrasia ili viendelee kupata misaada. Na hata baada ya hapo chama tawala hakijajiandaa kukubali mfumo huu kwamba kuna siku chama tawala kitakuwa chama pinzani. Vile vile hata ukiangalia mfumo wa utawala/uongozi nchini si wa ki demokrasia au ki-multiparty. Mfano rais amekuwa na madaraka makubwa mno, anateua majaji, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa wilaya, wakurugenzi wa mashirika, Mkuu wa majeshi, polisi, usalama wa taifa nk, nk.

Whether CCM Kama itapoteza kuwa chama tawala itaendelea ku-exist na labda kuwa chama kikuu cha upinzani, kwa maoni yangu, itategemea sana itaondoka madarakani kwa njia gani. Kama wananchi wakiamua kuiondoa CCM kwa kura, na CCM ikakubali kuachia madaraka bila vurugu au vita, CCM itaendelea ku-exist. Kosa ni pale CCM ikikosa kura za kuendelea Kuongoza lakini ikang'ang'ania madarakani. Wananchi wakipambana na kuiondoa kwa njia nyingine, ndipo CCM itafutika.

Kama mshauri, CCM inabidi ilione hili, Badala ya kujenga mbinu za kuhakikisha kwamba inabaki madarakani kwa njia yoyote, ianze kujenga uelewano na vyama vikuu vya upinzani hasa chadema ili kuwe na muafaka wa maridhiano ili kuepuka vita ambavyo si CCM, chadema wala wananchi watanufaika nayo: wote tutakuwa losers!

Ukija kwa upande wa uchumi na huduma za jamii ndio hata usiongee. Bora hata enzi za mwalimu alijaribu kuweka misingi ya ujenzi wa uchumi wa umma. Mfano, vyama vya ushirika, viwanda karibu Kila mkoa, SIDO, akaanzisha hata machismo na maka, chuma ili baadaye kujenga uchumi imara wa nchi. Mwl. Alithamini na kujenga elimu. Alizuia ufisadi kwa kiasi kikubwa. Sitaki kueleza mengi, nittachosha wasomaji. Lakini angalia Leo Hii, viongozi wetu wamegawa rasilimali za nchi yetu kwa kisingizio cha uwekezaji na ubinafsishaji! Malipo yake ni wananchi kuendelea kuwa masikini na wao kujilimbikizia mabilioni nje ya nchi. Au hayo ndiyo Mapinduzi?

Leo hii Kila sector ya uma kuna malalamiko mengi na watu kukata tamaa, angalia mfano walimu, madaktari, wanafunzi, wafugaji na wakulima kufukuzwa kutoka kwenye ardhi zao etc, etc: Au hayo ndiyo Mapinduzi?

Sector kubwa zote za uchumi zimeshikwa na wageni. Mwananchi hathaminiki ndani ya nchi yake. Leo hii kukiwa na dispute kati yako na mwekezaji, hebu niambie, mbele ya serikali nani atalindwa? We're au mwekezaji? Raia wa Tanzania kwenye nchi yake amekuwa second class citizen! Au ndiyo Mapinduzi unayoongelewa yaliyoletwa na chama tawala? Mapinduzi ya kisiasa, kiuchumi au kijamii si maneno yanatakiwa Kama yapo yaonekane kwenye maisha ya raia. Na wala usifikiri ni magorofa yanayoonekana dar es salaam.

Anyway, Mkuu nitachosha watu ngoja niishie hapa
 
Katika maisha ya kila siku kwa bahati mbaya sioni watu wanaotaka mabadiliko, ninachoona ni kukua kwa kundi la watu ambao siasa kwao ni kama kiburudisho.

Watu wanaotaka mabadiliko hukemea uovu katika ngazi zote sio ngazi ya taifa tu na sio kwa yanayoandikwa kwenye magazeti tu. Unakuta mtu ni kinara wa kutoa na kuchukua rushwa lakini kutwa yuko kwenye mitandao akilalamikia mikataba mibovu iliyotokana na rushwa. Kwa vijana wa leo mtu anayefanya kazi sehemu yenye mwenya wa rushwa anaonekana amepata "shavu au deal". Hawa siwezi kuwaita wapenda mabadiliko.

Kama tunataka mabadiliko inatakiwa tuwe wakweli katika maisha yetu ya kila siku.
 
Mkuu makala yako ni nzuri na umechambua mambo mengi vizuri na kutoa dondoo za mdahalo. Isipokuwa kwa baadhi ya watu itakuwa ni vigumuni kuelewa hoja Kama hatataweza kufanya proper interpretation , na ukumbuke interpretation itategemea sana uelewa au mtu alivyo-perceive hoja.

Kwa mfano heading ya topic yako 'M4C, Hatima ni Mageuzi au Mapinduzi?' Ni kweli unaweza kuwa na hatima ya mageuzi AU Mapinduzi. Lakini Kama nilivyoeleza kwa ufupi, unaweza kuwa na hatima ya vyote kwa pamoja yaani mageuzi NA Mapinduzi.

CCM haijawahi kufanya Mapinduzi yoyote mbali na kumpindua mkoloni ikiwa kama TANU. CCM haijawahi kuleta Mapinduzi ya kisiasa, kiuchumi hata ya kijamii. CCM imekuwa ikifanya mabadiliko-yaani kuweka viraka na hasa kwa maslahi a watawala.
Mfano kwa miaka hamsini serikali imekuwa ikitumia katiba na sheria zilezile zilizoachwa na mkoloni ambazo kusudi lake ilikuwa ni kumlinda mkoloni. Mabadiliko yaliyofanyika ni yale yasiyoingilia maslahi ya watawala. Hakuna vipengele vya katiba au sheria vilivyofanyiwa marekebisho ili kufanya watawala wawajibike kwa wananchi. Watawala wameendelea kuwa wakoloni.

Ujio wa vyama vingi haikuwa maamuzi ya CCM. Ilikuwa ni matokeo ya international pressure iliyotaka hivi vi-nchi vyetu vya ki-dictator vi-adopt mfumo wa ki demokrasia ili viendelee kupata misaada. Na hata baada ya hapo chama tawala hakijajiandaa kukubali mfumo huu kwamba kuna siku chama tawala kitakuwa chama pinzani. Vile vile hata ukiangalia mfumo wa utawala/uongozi nchini si wa ki demokrasia au ki-multiparty. Mfano rais amekuwa na madaraka makubwa mno, anateua majaji, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa wilaya, wakurugenzi wa mashirika, Mkuu wa majeshi, polisi, usalama wa taifa nk, nk.

Whether CCM Kama itapoteza kuwa chama tawala itaendelea ku-exist na labda kuwa chama kikuu cha upinzani, kwa maoni yangu, itategemea sana itaondoka madarakani kwa njia gani. Kama wananchi wakiamua kuiondoa CCM kwa kura, na CCM ikakubali kuachia madaraka bila vurugu au vita, CCM itaendelea ku-exist. Kosa ni pale CCM ikikosa kura za kuendelea Kuongoza lakini ikang'ang'ania madarakani. Wananchi wakipambana na kuiondoa kwa njia nyingine, ndipo CCM itafutika.

Kama mshauri, CCM inabidi ilione hili, Badala ya kujenga mbinu za kuhakikisha kwamba inabaki madarakani kwa njia yoyote, ianze kujenga uelewano na vyama vikuu vya upinzani hasa chadema ili kuwe na muafaka wa maridhiano ili kuepuka vita ambavyo si CCM, chadema wala wananchi watanufaika nayo: wote tutakuwa losers!

Ukija kwa upande wa uchumi na huduma za jamii ndio hata usiongee. Bora hata enzi za mwalimu alijaribu kuweka misingi ya ujenzi wa uchumi wa umma. Mfano, vyama vya ushirika, viwanda karibu Kila mkoa, SIDO, akaanzisha hata machismo na maka, chuma ili baadaye kujenga uchumi imara wa nchi. Mwl. Alithamini na kujenga elimu. Alizuia ufisadi kwa kiasi kikubwa. Sitaki kueleza mengi, nittachosha wasomaji. Lakini angalia Leo Hii, viongozi wetu wamegawa rasilimali za nchi yetu kwa kisingizio cha uwekezaji na ubinafsishaji! Malipo yake ni wananchi kuendelea kuwa masikini na wao kujilimbikizia mabilioni nje ya nchi. Au hayo ndiyo Mapinduzi?

Leo hii Kila sector ya uma kuna malalamiko mengi na watu kukata tamaa, angalia mfano walimu, madaktari, wanafunzi, wafugaji na wakulima kufukuzwa kutoka kwenye ardhi zao etc, etc: Au hayo ndiyo Mapinduzi?

Sector kubwa zote za uchumi zimeshikwa na wageni. Mwananchi hathaminiki ndani ya nchi yake. Leo hii kukiwa na dispute kati yako na mwekezaji, hebu niambie, mbele ya serikali nani atalindwa? We're au mwekezaji? Raia wa Tanzania kwenye nchi yake amekuwa second class citizen! Au ndiyo Mapinduzi unayoongelewa yaliyoletwa na chama tawala? Mapinduzi ya kisiasa, kiuchumi au kijamii si maneno yanatakiwa Kama yapo yaonekane kwenye maisha ya raia. Na wala usifikiri ni magorofa yanayoonekana dar es salaam.

Anyway, Mkuu nitachosha watu ngoja niishie hapa

Blue Ray,

Umetoa mchango mzuri sana, na ungeendelea tu kwani kinacho chosha ni hoja zisizo na mashiko, lakini hoja zako zimekamatia pazuri sana; Ushauri unaoutoa kwa CCM ni mzito na muhimu sana, kuna makala moja ninaandaa na umegusia vitu ambavyo vilikuwa akilini mwangu - hasa suala la umuhimu wa CCM kuondoka kwa roho safi and in a non-violent way, iwapo itaanguka katika uchaguzi mku ujao; kinyume na hapo, yatatokea mawili: kwanza, as you rightly put it, iwapo kitashindwa lakini kung'ang'ania madaraka, kitaondolewa kwa nguvu na UMMA, na kupoteza sifa zote za kuwa chama cha upinzani; Pili, bila ya uangalifu, baadhi ya viongozi watafunguliwa kesi za mauaji ya alaiki, iwapo mtutu wa bunduki na mabomu yatatumika kuzima maandamano ya kukitoa CCM madarakani kwa nguvu;

Mimi nadhani yote haya hayapo at the best interest sio ya CCM tu, bali watanzania wote kwani pamoja na kwamba UMMA ndio mwamuzi juu ya hatima ya CCM 2015, bado chama hiki kinahitajika kiwepo kwani kimekuwa ni sehemu ya utamaduni wa mtanzania; kama kitakufa, ni bora kife taratibu huko kwenye benchi la upinzani, sio ghafla tu;

Kuhusu CCM na Uchumi, naunga mkono hoja yako; ukiondoa sekta ya madini ambayo ndiyo inayochangia sana kitakwimu kwa uchumi kukua kwa karibia 7% kwa wastani, miaka kumi mfululizo, sekta nyingine zenye impact kwa wananchi walio wengi zaidi, aidha zipo katika hali ile ile kwa miaka zaidi ya ishirini, au zimezorota kabisa; Wananchi wengi wanazidi kukihama Kilimo - ushahidi ni labour force in Kilimo inashuka kukaribia 70% if not less; lakini ukiangalia jeshi hili linaenda wapi, ni vigumu kubaini kwani walio wengi katika taifa hili ni vijana, na tatizo lao la kwanza ni ajira, la pili ajira, na la tatu pia ajira; Vijana wengi wameishia kuwa tu wabangaizaji;

Yet CCM bila aibu inashindana na Chadema kwenye suala la Umati kwenye mikutano ya hadhara wakati wingi wa watu kwenye mikutano hii ni a political asset kwa chadema and a major political liability kwa CCM; Why? Kwa sababu wingi wa vijana katika mikutano ya namna hii, tena nyakati za mchana maana yake ni kwamba hawana AJIRA;
 
Mkuu Shayu
Kama huelewi "Dhana ya M4C" ungeomba kueleweshwa ndo ujadili. Sasa umejijadilisha nini kama huielewi!!!!!
Au ndo ulikuwa unaonyesha jinshi usivyoielewa?
 
Jmushi1,
Kwanza naomba nianze na hili:


Kama umenisoma vyema, naona mengi mazuri kuliko mabaya juu ya ujio wa M4C.



Baada ya kutafakari kwa muda, nakubaliana na wewe kwamba HAKI ni key denominator. FIGHTING INJUSTICE IS FIGHTING POVERTY badala ya mtazamo wangu wa awali kwamba Fighting POVERTY is Fighting INJUSTICE. Hii ni kwa sababu moja kubwa: Structural injustice ndio chanzo cha Umaskini, na moja ya njia za uhakika za kutatua the ‘injustice of poverty' ni kubadilisha muundo uliopo/structural change; Kwa maana nyingine, injustice ni tatizo la kimuundo zaidi, kuliko kimfumo. Iwapo unakubaliana na mimi katika hili, yafuatayo ni maeneo yanayozaa structutal injustice, na kupelekea Umaskini ndani ya jamii husika:


  • Unequal Access to Key Assets – Kwa Financial Assets (access to credit), Physical Assets (nyumba na vifaa mbalimbali vya kurahisisha shughuli za uchumi), Natural Assets (kama vile Ardhi) n.k


  • Unequal Participation in the Market Place – tunajua jinsi gani soko huria umewaacha watanzania walio wengi, hasa wa vijijini wamebakia wameduwaa kwa miaka zaidi ya 25 sasa – tangia ujio wa soko huria; Maskini Tanzania hawakupewa maandalizi ya kuingia katika mfumo wa soko huria, walishtukizwa tu, na mbaya zaidi ni kwamba mageuzi ya kiuchumi yaliingizwa na utawala wa Mwinyi kwa siri kubwa sana katika hatua za awali, pengine kuogopa Revolts;


  • Unequal Access to Human Development – Hapa masuala muhimu to determine human capital ni Afya Bora na Elimu Bora, sio Bora Elimu (kama shule zetu za kata) au Bora Afya (kama huduma za ovyo ovyo zinazotolewa kwa wananchi wetu, hasa wa vijijini);


  • Unjust Government – Utawala wetu largely disenfranchises the poor, na hili linatokana zaidi na ukosefu wa elimu ya uraia ambapo wananchi wengi hawajua wajibu wao kama raia ni nini na na hawajui wajibu wa serikali kwa raia ni nini;

Iwapo tunakubaliana katika haya, hasa kwamba injustice ni suala la kimuundo kuliko kimfumo, swali, linalofuata ni je: Kwanini inachukua muda mrefu sana kwa Mageuzi kuleta ufumbuzi wa tatizo hili? Nini kifanyike?


Mbowe alinukuliwa akielezea haya kuhusu M4C:

"Under the initiative, too, the party intended to make deeper inroads into the countryside, by opening several new branches, consolidating exiting ones, and recruiting many members. Through M4C, furthermore, Mr Mbowe told the audience, Tanzanians would be enlightened on their democratic rights, socialize into electing patriotism-driven national leaders, and advocate earnest protection of national resources." Source; The Citizen.

Hapa tupo pamoja...



In my original post, niliuliza hivi:

"Je: Viongozi wanaoendesha "Mass Movements" wana lengo gani – kuboresha Mageuzi (Reforms) ambazo Serikali ya CCM imekuwa inazitekeleza kwa miaka 26 sasa chini ya usimamizi wa IMF na World Bank au Viongozi wanaoendesha hizi "Mass Movements" wanalenga mbali zaidi ya Mageuzi?"

Hili halikuwa swali la mtego, na mdau mwenzetu miwatamu alikuja na majibu mazuri juu ya hili ambapo alitamka hivi:
"Ili kuonesha kuwa CCM sasa hivi inafanya kazi kama chama cha upinzani; kwanza ni hali yake ya kufanya kazi zake kwa kutekeleza matakwa ya Chadema, mpaka hapo utaona kuwa tayari chadema ipo madarakani hivyo kilichobaki ni kuthibitishwa kwa wananchi tu."

Tafsiri yangu juu ya hili ni kwamba Mageuzi bado ni njia sahihi kuletea mabadiliko watanzania lakini chini ya CCM, utekelezaji wake ni duni sana, na ndio maana baada ya amsha amsha za Chadema, CCM imeanza kukaza buti na angalau mambo yameanza kwenda, na iwapo Chadema itaingia ikulu 2015, itaenda kutekeleza Mageuzi haya kwa ARI ZAIDI, NGUVU ZAIDI, na KASI ZAIDI. Hii ni kauli mbiu ya CCM ambayo ni ya maneno tu, vinginevyo inahitajika kivitendo katika utekelezaji wa Mageuzi na pengine Chadema wataweza kutekeleza mageuzi haya kwa ufanisi zaidi ya CCM iwapo watashinda uchaguzi 2015;



Hili nilishalijadili kwa mtazamo unaofanania na wako, ingawa nilihoji kwamba iwapo Chadema hawatapita 2015, wamejipanga vipi, hasa ikizingatiwa kwamba Mbowe alitoa kauli tata kidogo kwamba CCM ikishinda atajiuzulu Siasa? Sijapata jibu kutoka kwa mdau wowote hadi sasa.



Hapa umenichanganya kidogo - unaposema ECONOMIC REVOLUTION, una maana gani, Mapinduzi ya Kiuchumi? Na kwa Tanzania chini ya Chadema yatachukua mkondo gani?



Ni kweli, ubepari umekuwa unapitia reforms constantly, lakini ukumbuke kwamba ndani ya global capitalist system, kuna nchi participating from the centre (nchi tajiri) na nchi participating from the periphery/pembezoni (nchi maskini kama Tanzania), na ni zile in the centre calling all the shots; Ni hili ndio limepelekea Lenin-Marxist views kushika kasi kubwa katika dunia ya tatu, starting with the liberation movements and independence struggles in the 1950s-60s, and to an extent throughout the cold war period;

Vile vile ukumbuke kwamba hata mataifa makubwa, kabla ya kuachia ubepari utawaliwe na soko huria, kila nchi ilikuwa busy sana kujipanga ili kuweka the fundamentals right kwanza, kwa mfano kupitia slave trade, imperialism, colonialism, na uhalifu wa kila aina, kitu ambacho kilipelekea mataifa haya makubwa kupigana katika vita nyingi sana; ni baada ya vita kuu vya pili vya dunia kuisha ndipo mambo yakatulia huku wakiwa wameshajiwekea the world order kwa matakwa yao; so unaposema kwamba ubepari undergo reforms kila wakati, upo sahihi, lakini uelewe kwamba ubepari wa nchi tajiri ni tofauti na ubepari wa nchi maskini kama Tanzania ambapo hatuna real capitalists bali mafisadi ambao technically ni agents wa mabepari waliokamilika huko nje; Ndio maana many reforms kwa miaka 26 sasa zinaleta faida kwa foreign capital and its owners kuliko watanzania;



Hili ni kweli, na sio tu Chadema haiwezi kufuata njia hii, bali chama chochote cha siasa including CCM; lakini hii aina maana kwamba hakuna alternative to the current system, mimi nina amini mbadala upo, na ni kwa kupitia democratic socialism ambayo inahimiza a welfare state, kama ilivyokuwa kwa nchi kadhaa za Scandnavia, Sweden in particular; Ndio maana Sweden walikuwa ni marafiki wa Ujamaa katika kipindi chote kuliko taifa lingine lolote, ni bahati mbaya tu kuna maeneo kadhaa Mwalimu aliyakoseka katika utekelezaji wa sera ya Ujamaa;



Ndio maana huwa nahimiza kwamba ili tuendeleaa we need a new and radical orientation – not necessarily Mapinduzi bali mfumo ambao utatufanya tuondokane na madudu haya ya IMF na World Bank, hasa mfumo ambao utakuwa na uwezo wa kulikemea soko huria na ubepari pale masuala haya yatakapokuwa yana act contrary to the welfare of Wananchi walio wengi; Tunahitaji mfumo ambao Utavumiliwa na Ubepari na Soko Huria huku vile vile na wenyewe utavumilia Ubepari na Soko Huria; Hili linawezekana na linawezekana kupitia A New Democratic Socialism System.
Mkuu,mengi ambayo ningetaka kuyasema,ameyasema ndugu blueray hapo juu.Especially hayo niliyoya quote hapo chini...
blueray said:
Kwa mfano heading ya topic yako 'M4C, Hatima ni Mageuzi au Mapinduzi?' Ni kweli unaweza kuwa na hatima ya mageuzi AU Mapinduzi. Lakini Kama nilivyoeleza kwa ufupi, unaweza kuwa na hatima ya vyote kwa pamoja yaani mageuzi NA Mapinduzi.

CCM haijawahi kufanya Mapinduzi yoyote mbali na kumpindua mkoloni ikiwa kama TANU. CCM haijawahi kuleta Mapinduzi ya kisiasa, kiuchumi hata ya kijamii. CCM imekuwa ikifanya mabadiliko-yaani kuweka viraka na hasa kwa maslahi a watawala.

Mfano kwa miaka hamsini serikali imekuwa ikitumia katiba na sheria zilezile zilizoachwa na mkoloni ambazo kusudi lake ilikuwa ni kumlinda mkoloni. Mabadiliko yaliyofanyika ni yale yasiyoingilia maslahi ya watawala. Hakuna vipengele vya katiba au sheria vilivyofanyiwa marekebisho ili kufanya watawala wawajibike kwa wananchi. Watawala wameendelea kuwa wakoloni.

Ujio wa vyama vingi haikuwa maamuzi ya CCM. Ilikuwa ni matokeo ya international pressure iliyotaka hivi vi-nchi vyetu vya ki-dictator vi-adopt mfumo wa ki demokrasia ili viendelee kupata misaada. Na hata baada ya hapo chama tawala hakijajiandaa kukubali mfumo huu kwamba kuna siku chama tawala kitakuwa chama pinzani. Vile vile hata ukiangalia mfumo wa utawala/uongozi nchini si wa ki demokrasia au ki-multiparty. Mfano rais amekuwa na madaraka makubwa mno, anateua majaji, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa wilaya, wakurugenzi wa mashirika, Mkuu wa majeshi, polisi, usalama wa taifa nk, nk.

Whether CCM Kama itapoteza kuwa chama tawala itaendelea ku-exist na labda kuwa chama kikuu cha upinzani, kwa maoni yangu, itategemea sana itaondoka madarakani kwa njia gani. Kama wananchi wakiamua kuiondoa CCM kwa kura, na CCM ikakubali kuachia madaraka bila vurugu au vita, CCM itaendelea ku-exist. Kosa ni pale CCM ikikosa kura za kuendelea Kuongoza lakini ikang'ang'ania madarakani. Wananchi wakipambana na kuiondoa kwa njia nyingine, ndipo CCM itafutika
Neno mapinduzi lisikupe shida,kwasababu hata ccm si ni chama cha mapinduzi?Je mapinduzi ambayo chama hicho kinajinasibisha nayo ni yapi hayo?Yale ya Zanzibar?

Kuhusu mapinduzi ya kiuchumi kwamba yatachukuwa mkondo gani,nilikupa mfano wa industrial revolution,nikasema hata sisi tukiwekeza zaidi kwenye viwanda,basi tunaweza kuyapata mapinduzi ya kiuchumi.Economic revolution is simply a rapid change in economic system.It can be a significant change in the ways goods and services are produced and marketed.

Kuhusu democratic socialism,nakubaliana na wewe kabisa.Hayo ya ubepari niliyazungumzia kwasababu kama unazitaja WB na IMF,basi ujuwe kuwa ni institutions zinazoshikiliwa ama kumilikiwa na mabepari.Niliyazungumza hayo ya ubepari pia kwasababu ulizungumzia reforms ambazo zilishinikizwa ama zinashinikizwa na institution hizo to the third world countries kama mojawapo ya masharti ya mikopo.

So tusubiri tuone kama chadema wana msimamo gani kuhusiana na hilo la Democratic socialism,tatizo tulilonalo ni kwamba tumeshajiingiza sana kwenye matatizo ya mfumo wa ubepari na madeni tuliyonayo ni makubwa,na pia utaratibu wa kutembeza bakuli ambao ni wa ccm umetulemaza.

Pia structural injustice kama ulivyosema,ninaamini vinaenda hand to hand na system(mfumo) injustice.Kwa mfano mimi ninaamini kabisa kuwa structure ya mfumo wa kibepari ni injustice by itself.

Ninaamini kabisa kuwa nchi masikini haiwezi kuwa nchi ya kibepari hata siku moja,kwasababu kwanza hatuna nguvu zinazohitajika za kibepari za kujitanuwa(sifa kuu ya ubepari).

Mabepari na mataifa yao wanasema wanaamini in free market,lakini hapo hapo wanakwambia wazi kabisa freedom is not free.

Na kwa kutaka wapate hizo market,mara nyingine wanatumia nguvu ama hata njia mbalimbali za coerscion.Kwahiyo ndiyo maana nikasema mfumo wa ubepari bado unaendelea kufanyiwa mageuzi.Mfano civil rights movement ya USA,hizo ni movements ambazo zinapingana na structure iliyotokana na mfumo wa kibepari.

Kuanzia walipochukuliwa utumwani chini ya mwavuli wa ubepari,hadi kupigania uhuru wao,na bado kupigania haki zao.Kumbuka kwamba maneno yenye kutokana na structure ya kibepari na mfumo huo bado yalikuwa yakisisitizia personal freedom,na kwamba all men are created equal,lakini bado inreality ilikuwa sivyo.So mara nyingi yanayoandikwa kuhusu mfumo flani,siyo neccessarily kwamba ndiyo yanayokuwa practiced.
 
Agenda za mapinduzi ni lazima ziwe hidden kwa adui?
 
Mkuu,mengi ambayo ningetaka kuyasema,ameyasema ndugu
blueray hapo juu.Especially hayo niliyoya quote hapo chini...

Neno mapinduzi lisikupe shida,kwasababu hata ccm si ni chama cha mapinduzi?Je mapinduzi ambayo chama hicho kinajinasibisha nayo ni yapi hayo?Yale ya Zanzibar?

Dhana ya Mapinduzi kwa CCM kuitumia leo hii ni more of a political liability than an asset, na nilijadili hili kwa kina sana wakati wa majibu ya hojaa yangu kwa mdau mwenzetu Joka Kuu ambae na yeye aliuliza swali kama lako in relation to CCM na Mapinduzi; ukipata muda, tembelea ukurasa wa tatu wa mjadala huu, post number 45, utakuta majibu yangu ya kina, hasa kwanini CCM haina tena credibility, legitimacy na authority over the term MAPINDUZI katika zama hizi; Vinginevyo suala hapa sio kupata shida juu ya dhana ya mapinduzi, bali kuelewa tu kwamba mabadiliko katika jamii huja kwa njia mbili kuu, mageuzi au mapinduzi, hivyo sisi kama jamii, hasa kwa njia ya UMMA, ni muhimu tukaelewa kwa undani juu ya dhana hizi, kwani hata kama hazitatumika in practice, ni sehemu ya Elimu ya Uraia;

Kuhusu mapinduzi ya kiuchumi kwamba yatachukuwa mkondo gani,nilikupa mfano wa industrial revolution,nikasema hata sisi tukiwekeza zaidi kwenye viwanda,basi tunaweza kuyapata mapinduzi ya kiuchumi.Economic revolution is simply a rapid change in economic system.It can be a significant change in the ways goods and services are produced and marketed.

Nilijadili mapinduzi haya kwenye hoja yangu ya msingi kwa ku categorize kama mapinduzi ya aina nyingine nje ya yale makuu ambayo ni ya kisiasa na kijamii, lakini pengine yenye madhara makubwa zaidi kwenye jamii 'KIMFUMO' kuliko mapinduzi mengine yote; naongelea mapinduzi ya kilimo na mapinduzi ya viwanda; Baada ya kusema haya, naomba niseme kwa uwazi kabisa kwamba Tanzania haitaweza kufikia hatua ya mapinduzi ya viwanda kama ile iliyotokea East Asia bila kwanza kupitia mapinduzi ya Kilimo; Na mpaka tufikie hatua ya mapinduzi ya kilimo, ingawa safari huanza kwa hatua moja, tuna safari ndefu sana kufikia mapinduzi ya kilimo na ili kufanikiwa, itahitaji mabadiliko makubwa sana katika jamii yetu ambayo bila kuwa waangalifu, yanaweza kuwa counter productive kwa sababu ya suala la Ardhi na historia ya nchi yetu kiuchumi, kisiasa na kijamii;

The bottom line hapa ni kwamba, pamoja na ndoto hizi za kufikia hatua ya mapinduzi ya viwanda, tunapoteza tu muda kuzungumzia mapinduzi ya viwanda kama kwanza hatukamilishi mapinduzi ya kilimo; Isitoshe, nje ya Mauritius, hakuna nchi nyingine yoyote in Sub Saharan Africa ambayo imeweza to undergo Industrial Revolution kwa hadhi ya South East Asia;

Kuhusu democratic socialism,nakubaliana na wewe kabisa.Hayo ya ubepari niliyazungumzia kwasababu kama unazitaja WB na IMF,basi ujuwe kuwa ni institutions zinazoshikiliwa ama kumilikiwa na mabepari.Niliyazungumza hayo ya ubepari pia kwasababu ulizungumzia reforms ambazo zilishinikizwa ama zinashinikizwa na institution hizo to the third world countries kama mojawapo ya masharti ya mikopo.
Kwa mtazamo wako, kwanini hakuna chama cha siasa chenye kufuata itikadi hii ya Democratic Socialism na kuiza vizuri kwenye UMMA ambao hakika utainunua kwa urahisi? Itikadi na sera zitakazo zaliwa na mfumo huu zitaua ndege wawili kwa jiwe moja: Kwanza, wananchi walio wengi wapo vijijini, na ni maskini, lakini pia waliopo mijini wengi ni maskini kuliko wenye uwezo, na itikadi ya namna hii itajibu matatizo mengi sana ya kada hii, lakini muhimu zaidi itakuwa na elements za kijamaa ambazo bado zipo vijijini, huku pia zikiwa na elements muhimu za kushibana na Ubepari; Pili, nchi wahisani pia hawatakuwa na tatizo na mfumo huu as long as mfumo unategemea zaidi domestic resources to finance the welfare state, na hilo linawezekana given the abundant resources mungu alizotujalia;

So tusubiri tuone kama chadema wana msimamo gani kuhusiana na hilo la Democratic socialism,tatizo tulilonalo ni kwamba tumeshajiingiza sana kwenye matatizo ya mfumo wa ubepari na madeni tuliyonayo ni makubwa,na pia utaratibu wa kutembeza bakuli ambao ni wa ccm umetulemaza.
Chadema wameshajipambanua kama chama cha kiliberali kinachofuata itikadi ya mrengo wa kati; democratic socialism is more towards the left; vile vile itikadi mbili hizi ni tofauti sana in terms of kutoa huduma kwa wananchi; ingawa hivi karibuni chadema wamekuja na mawazo ya elimu bure, hiki bure, kile bure, hii sio asili ya itikadi yao ya mrengo wa kulia wa kiliberali, ni kwamba tu UMMA hauna uelewa wa kutosha kuhusu umuhimu wa viongozi to stick and die in the ideological boots;

Pia structural injustice kama ulivyosema,ninaamini vinaenda hand to hand na system(mfumo) injustice.Kwa mfano mimi ninaamini kabisa kuwa structure ya mfumo wa kibepari ni injustice by itself.

Ingawa wapo wanaosema kwamba nia ya ubepari sio kuzalisha injustice and poverty, wakati ukweli ni kwamba haya mawili yapo inherent to capitalism; ndio maana mataifa makubwa kupitia madalali wao ambao ni World Bank na IMF wapo very keen kuja na mageuzi ya kiuchumi, kisiasa n.k kama nilivyojadili - ili kuaminisha nchi maskini kwamba ubepari ni mzuri, unahitaji kufanyiwa marekebisho tu ya hapa na pale ili na nyie nchi maskini mfaidike nao, wakati ukweli ni kwamba, as long as nchi maskini kama Tanzania zinaendelea kushiriki kwenye global capitalist system from the periphery huku wakubwa wakishiriki from the centre and call of the shots on Trade, FDI, etc, hakuna cha maana kitakachotokea Tanzania chini ya mfumo wa sasa; hadithi za East Asian Tigers kama vile South Korea ni kiini macho; ubepari wao hawa ulikuwa wa kupakatwa ili wasitumbukie kwenye kambi ya ukomunisti;

Ninaamini kabisa kuwa nchi masikini haiwezi kuwa nchi ya kibepari hata siku moja,kwasababu kwanza hatuna nguvu zinazohitajika za kibepari za kujitanuwa(sifa kuu ya ubepari).
Nakubaliana na wewe katika hiki kama nilivyokwisha jadili awali;
Mabepari na mataifa yao wanasema wanaamini in free market,lakini hapo hapo wanakwambia wazi kabisa freedom is not free.
Mfano, why not give us access to their markets i.e. Free Trade? Does Tanzania need more AID or more TRADE to develop? Definitely more TRADE. Lakini wanajua kwamba AID comes with conditionalities, mfano kutulazimisha sisi tu facilitate investment climate ili foreign capital ije kuchota chota rasilimali zetu kwa urahisi; pia AID inawasaidia wao kuuza vipuri vyao, kutoa ajira kwa wataalam wao via miradi ya maendeleo, kukuza sekta muhimu kwa mitaji ya nje, sio muhimu kwa watanzania hasa sekta zinazochangia pato la taifa kukua ili tuweze kulipa interests za mikopo yao, the list goes on and on....
Na kwa kutaka wapate hizo market,mara nyingine wanatumia nguvu ama hata njia mbalimbali za coerscion.Kwahiyo ndiyo maana nikasema mfumo wa ubepari bado unaendelea kufanyiwa mageuzi.Mfano civil rights movement ya USA,hizo ni movements ambazo zinapingana na structure iliyotokana na mfumo wa kibepari.
Ni kweli, na wanajaribu sana kuzuia mapinduzi kwa kuhimiza umuhimu wa mageuzi; kwa mfano, suala la Libya, waliwahi sana kuingia pale ili mabadiliko yake yasiharibu relations of productions ambazo zipo at the US advantages; vinginevyo kama walikuwa wanakubali mapinduzi, kwanini walikuwa wazito kuunga mkono mapinduzi ya Misri? Yote ni kutokana na ukweli kwamba pamoja na udikteta wa Mubarak, he delivered to the US and major western powers economically;

...Kumbuka kwamba maneno yenye kutokana na structure ya kibepari na mfumo huo bado yalikuwa yakisisitizia personal freedom,na kwamba all men are created equal,lakini bado inreality ilikuwa sivyo.So mara nyingi yanayoandikwa kuhusu mfumo flani,siyo neccessarily kwamba ndiyo yanayokuwa practiced.

Ni kweli - kwa mfano watumwa walianza revolts kuanzia ndani ya meli lakini haikusaidia; religious leaders and philanthropists walipinga sana utumwa kwa muda mrefu sana, lakini haikusaidia; ni hadi pale economic value ya watumwa iliposhuka kutokana na mechanization ndio vilio dhidi ya utumwa vikaanza kusikilizwa and eventually the abolition of slave trade;

Kuna kitabu kimoja by Zinn: A People's History of the United States…, kinaelezea unachozungumza kwa undani sana; Kwa mfano, mwandishi huyu anaelezea jinsi gani Rais Lincoln (ambae anasifiwa kama kiongozi aliyeua utumwa Marekani), alivyokuwa na malengo tofauti kabisa – not on moral grounds, bali kwa sababu za kisiasa, lakini hasa kiuchumi ; Zinn anaeleza kwamba "Lincoln was against slavery but still did not believe blacks were equals." Pia anamnukuu Lincoln akitamka kwamba: "What I do about Slavery and the colored race, I do because it helps to save this Union.

Kwa kifupi, the elites are in control of this world, they only act on Economic Grounds, na ni watekelezaji wazuri sana wa LIWALO LIWE, ili mradi matakwa yao ya kiuchumi yanaenda wanavyotaka; ndio maana hata kwa suala hili la utumwa, it was the clashes of the elites wa North and South iliyopelekea abolition of slave trade, vinginevyo for so many years, watumwa walikuwa in revolts, viongozi wa kidini walikuwa wanapinga, philanthropists wanafanya kila aina ya lobbying kumaliza dhambi hii, lakini IT TOOK ECONOMICS TO GET THESE ELITES TO LISTEN, NOT MORALITY;
 
Mabadiliko ya kweli ni lazima ili kulukomboa Taifa letu. Huwezi kubadilika bila kubadili mfumo. Kuwa mwoga wa mabadiliko tayari ni failure na hutachaingia chochote ktk mabdiliko tunayoyatamani.
Kusema CDM waweza wasilete mabadiliko ni mtizamo wako ambao unaonesha woga wa mabadiliko.

Hivi kweli CDM wanaeneza sera zilezile za CCM au wapo na sera mbadala??????????jiulize.

Hivi kweli CDM hawazungumzii kuhusu kubadili mfumo wetu wa uongozi na utendaji..(mgawanyo wa madaraka, uteuzi wa viongozi, utendaji serekalini,...elimu..afya..miundo mbinu.etc)..jiulize?

Sasa hebu tupatie hayo mapungufu unayoyaona ndio tuchangie kaka otherwise.........ungamkono mabadiliko...b strong...
Ifanyie kitu tZ.
 
RENOVATION ya MFUMO uliopo ni MAGEUZI na tumekuwa katika hili kwa miaka 26 sasa, tukianza na renovation ya uchumi mwaka 1986 baada ya Nyerere kung'atuka; Hoja yako haiweki wazi iwapo suluhisho ni Renovation ya Mfumo au Ujio wa mfumo mpya;
Siku zote nasimama kwenye kuuondoa mfumo mzima kwanza na kuuweka Pembeni na kuamua ni nini tutachukua kutoka kwenye mfumo huo na kuingiza kwenye mfumo mpya. Ndiyo maana mimi nilikuwa ni mshabiki mkubwa sana wa Ibarahim Msabaha aliyesema kilichotokea kwenye suala la Richmond ni tatizo la kimfumo na wala si tatizo la dhamira mbaya. Bangusilo alikuwa sahihi.

Pitia Ansard ya maelezo yake hayo jinsi alivyotaka mfumo ubadilishwe. Tatizo kwenye kubadili mfumo si jambo linalopiganiwa na wengi kwani wengi wetu tunafaidika na mfumo huu uliooza na ndiyo maana mimi naamini iwe ni mageuzi au mapinduzi ya kweli yataanzia vijijini na wala si mijini.
 
Siku zote nasimama kwenye kuuondoa mfumo mzima kwanza na kuuweka Pembeni na kuamua ni nini tutachukua kutoka kwenye mfumo huo na kuingiza kwenye mfumo mpya. Ndiyo maana mimi nilikuwa ni mshabiki mkubwa sana wa Ibarahim Msabaha aliyesema kilichotokea kwenye suala la Richmond ni tatizo la kimfumo na wala si tatizo la dhamira mbaya. Bangusilo alikuwa sahihi.

Pitia Ansard ya maelezo yake hayo jinsi alivyotaka mfumo ubadilishwe. Tatizo kwenye kubadili mfumo si jambo linalopiganiwa na wengi kwani wengi wetu tunafaidika na mfumo huu uliooza na ndiyo maana mimi naamini iwe ni mageuzi au mapinduzi ya kweli yataanzia vijijini na wala si mijini.

Kigarama,

Asante sana kwa mchango wako mzuri; Una hoja nzuri sana - matatizo mengi yanayoikabili nchi yanatokana na ubovu uliopo kwenye mfumo; Lakini nia ya Mageuzi niliyojadili ambayo ni ya aina nne, yakianzia na mageuzi ya kiuchumi mwaka 1986 inalenga kurekebisha madhaifu haya ya kimfumo, sasa ni kwanini kwa miaka 26 bado mageuzi ynayayoendelea na kugharimu fedha nyingi sana katika utekelezaji wake bado hayana tija kwa wananchi walio wengi?

Tatizo kwenye kubadili mfumo si jambo linalopiganiwa na wengi kwani wengi wetu tunafaidika na mfumo huu uliooza na ndiyo maana mimi naamini iwe ni mageuzi au mapinduzi ya kweli yataanzia vijijini na wala si mijini.

Hapa kidogo sijakuelewa; Maana yako ni kwamba sio watanzania wengi wenye mwamko wa kupigania mabadiliko ya mfumo? Au maana yako ni kwamba kwa kawaida mabadiliko ya mfumo huwa hayapiganiwi na walio wengi?

Mapinduzi ni kweli yataanzia vijijini, lakini hili la mapinduzi kuanzia vijijini sijakuelewa vizuri; wananchi wa vijijini watajiletea vipi mabadiliko kupitia mageuzi? Au maana yako ni kwamba ili mageuzi yawe na tija kwa walio wengi, basi ni muhimu yalenge kuboresha hali za wananchi walio vijijini?
 
Back
Top Bottom