Mdahalo wa ndoa, Idadi kubwa ya Waafrika wanaamini kuoa au kuolewa ni kufanikiwa maisha, hoja zangu ni za upande wa hasara, weka zako

Mdahalo wa ndoa, Idadi kubwa ya Waafrika wanaamini kuoa au kuolewa ni kufanikiwa maisha, hoja zangu ni za upande wa hasara, weka zako

Je, kuoa au kuolewa ni kufanikiwa maisha?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Sijui


Results are only viewable after voting.

Mr Why

JF-Expert Member
Joined
Nov 27, 2019
Posts
2,235
Reaction score
4,252
Idadi kubwa ya Waafrika wanaamini kuoa au kuolewa ni kufanikiwa maisha ndiyo maana neno ndoa limekuwa likipigiwa kelele kila kona huku maswali ya kuoa au kuolewa yakizidi kusumbua akili za watu wanaoulizwa au kuwakera ikitegemea na namna mtu anavyochukuliwa

Ukweli ni kuwa Kuoa au Kuolewa sio kufanikiwa maisha bali ni kitendo cha kutafutia watu wengine maisha ambao watakuwa watoto wako
Kuoa au kuolewa sio kufanikiwa maisha kwasababu hakuna faida unayoingiza zaidi ya kutoa matumizi maanake ni kuwa unafanya jambo la hasara au kwa maana nyingine kutoa sadaka
Ingelikuwa ni biashara ndipo ungesema unaingiza faida

Unapopata watoto maana yake ni kuwa kazi yako uliyofanya ni kuwaleta duniani watu wapya na uhakikishe unawatafutia maisha tangu wakiwa vijusi mpaka wanapobalehe na uhakikishe baada ya hapo wanaanza maisha yao

Kazi hii hupaswi kutegemea malipo unatakiwa kufanya kama kutoa sadaka sasa ni wewe utaamua
Hao watu ambao unasema ni watoto wako wao wataamua wakulipe fadhila ama waache

Ndiyo maana wapo watu wanaosaidiwa na watoto wao na wengine wakiwa wamegeuziwa mgongo ilihali waliwaleta wao

Mtoto akishazaliwa sio wako bali ni wa muumba na Serikali ndiyo maana mtoto uliyemzaa ana uwezo wa kukupeleka gerezani na ukafungwa kama wafungwa wengine na wapo wazazi wengi sana ambao wameshalala gerezani

Unapoingia katika familia kama wewe ni mwanaume usimnyanyase mke wako na wala mke asikunyanyase kwasababu wote mmeungana pasipo kulipwa na mtu yeyote ili mtoe sadaka ya kuwaleta watu wengine duniani pasipo kutegemea malipo kwahiyo hampaswi kunyanyasana bali unganeni ili mgawane hasara au faida mtakayopata

Kama watoto watawasaidia baadaye basi mtagawana faida na kama watawatelekeza au kushindwa basi mtagawana hasara vivyo hivyo

Kwahiyo ndoa ni kazi ya kujitoa sadaka na wala sio kufanikiwa maisha

Huu ni mdahalo wa ndoa hoja zangu ndizo hizo ukiwa na zako weka hapa watu wachangie
 
nimekurupuka kupiga kura hapana😅 naona kura hairudi

jibu ni ndio kwasababau ndoa inaleta hisia za ukamilifu(fulfilment)

unachukua nafasi ya kujenga familia, ambayo ndo msingi wa ustawi wa jamii

hata kama ukifeli, ni jambo jema umejaribu
 
Nakumbuka miaka ya nyuma kulikuwa na falsafa moja ya kuamini kwenye kuoa ili kuzaa watoto wengi waje wawasaidie.

Baada ya wazazi kushindwa kutumia nyakati zao kujijenga kiuchumi wakaona ni muda wa kuzaa watoto wengi ili waje wawanusuru.

Siku zikapita matakwa ya ndoa yakabadilika.

Mabinti waliamini kuwa ili waweze kuepuka kikombe cha shulba za utafutaji njia pekee ni kuolewa ili hilo jukumu liwe juu ya mwanaume.

Tukaenda na mfumo huo mpaka pale hali ilipobadilika.

Maisha yalipozidi kuwa magumu nao wanaume wakaanza kuona mzigo kama umewaelemea na hivyo kuona umuhimu wa kufanyika mabadiliko madogo kuendana na mfumo.

Wanaume wasaizi wanaamini kuwa kama maisha yamekupiga basi njia sahihi ni kuoa ili mje msaidiane.

Hapa ndio conflict of interest inapoingia.

Mwanaume ambaye alikuwa anategemewa na mwanamke kuwa sehemu ya msaada naye anamuona mwanamke kwa jicho hilo hilo.
 
Nakumbuka miaka ya nyuma kulikuwa na falsafa moja ya kuamini kwenye kuoa ili kuzaa watoto wengi waje wawasaidie.

Baada ya wazazi kushindwa kutumia nyakati zao kujijenga kiuchumi wakaona ni muda wa kuzaa watoto wengi ili waje wawanusuru.

Siku zikapita matakwa ya ndoa yakabadilika.

Mabinti waliamini kuwa ili waweze kuepuka kikombe cha shulba za utafutaji njia pekee ni kuolewa ili hilo jukumu liwe juu ya mwanaume.

Tukaenda na mfumo huo mpaka pale hali ilipobadilika.

Maisha yalipozidi kuwa magumu nao wanaume wakaanza kuona mzigo kama umewaelemea na hivyo kuona umuhimu wa kufanyika mabadiliko madogo kuendana na mfumo.

Wanaume wasaizi wanaamini kuwa kama maisha yamekupiga basi njia sahihi ni kuoa ili mje msaidiane.

Hapa ndio conflict of interest inapoingia.

Mwanaume ambaye alikuwa anategemewa na mwanamke kuwa sehemu ya msaada naye anamuona mwanamke kwa jicho hilo hilo.
💯
 
Nakumbuka miaka ya nyuma kulikuwa na falsafa moja ya kuamini kwenye kuoa ili kuzaa watoto wengi waje wawasaidie.

Baada ya wazazi kushindwa kutumia nyakati zao kujijenga kiuchumi wakaona ni muda wa kuzaa watoto wengi ili waje wawanusuru.

Siku zikapita matakwa ya ndoa yakabadilika.

Mabinti waliamini kuwa ili waweze kuepuka kikombe cha shulba za utafutaji njia pekee ni kuolewa ili hilo jukumu liwe juu ya mwanaume.

Tukaenda na mfumo huo mpaka pale hali ilipobadilika.

Maisha yalipozidi kuwa magumu nao wanaume wakaanza kuona mzigo kama umewaelemea na hivyo kuona umuhimu wa kufanyika mabadiliko madogo kuendana na mfumo.

Wanaume wasaizi wanaamini kuwa kama maisha yamekupiga basi njia sahihi ni kuoa ili mje msaidiane.

Hapa ndio conflict of interest inapoingia.

Mwanaume ambaye alikuwa anategemewa na mwanamke kuwa sehemu ya msaada naye anamuona mwanamke kwa jicho hilo hilo.
Una kitu
 
Hasara ni viungo vya uzazi kutumika vibayaaa

Hakuna mwanamke asiyependa nyonyesha mtoto ziwa lake.

Shukuru Mungu ka umemudu kujamiiana na jinsia ingine na kuanzisha maisha yasiyo na bughudha Wala khadhiaaa
 
Nakumbuka miaka ya nyuma kulikuwa na falsafa moja ya kuamini kwenye kuoa ili kuzaa watoto wengi waje wawasaidie.

Baada ya wazazi kushindwa kutumia nyakati zao kujijenga kiuchumi wakaona ni muda wa kuzaa watoto wengi ili waje wawanusuru.

Siku zikapita matakwa ya ndoa yakabadilika.

Mabinti waliamini kuwa ili waweze kuepuka kikombe cha shulba za utafutaji njia pekee ni kuolewa ili hilo jukumu liwe juu ya mwanaume.

Tukaenda na mfumo huo mpaka pale hali ilipobadilika.

Maisha yalipozidi kuwa magumu nao wanaume wakaanza kuona mzigo kama umewaelemea na hivyo kuona umuhimu wa kufanyika mabadiliko madogo kuendana na mfumo.

Wanaume wasaizi wanaamini kuwa kama maisha yamekupiga basi njia sahihi ni kuoa ili mje msaidiane.

Hapa ndio conflict of interest inapoingia.

Mwanaume ambaye alikuwa anategemewa na mwanamke kuwa sehemu ya msaada naye anamuona mwanamke kwa jicho hilo hilo.
we fala unaandika wewe😂
 
Idadi kubwa ya Waafrika wanaamini kuoa au kuolewa ni kufanikiwa maisha ndiyo maana neno ndoa limekuwa likipigiwa kelele kila kona huku maswali ya kuoa au kuolewa yakizidi kusumbua akili za watu wanaoulizwa au kuwakera ikitegemea na namna mtu anavyochukuliwa

Ukweli ni kuwa Kuoa au Kuolewa sio kufanikiwa maisha bali ni kitendo cha kutafutia watu wengine maisha ambao watakuwa watoto wako
Kuoa au kuolewa sio kufanikiwa maisha kwasababu hakuna faida unayoingiza zaidi ya kutoa matumizi maanake ni kuwa unafanya jambo la hasara au kwa maana nyingine kutoa sadaka
Ingelikuwa ni biashara ndipo ungesema unaingiza faida

Unapopata watoto maana yake ni kuwa kazi yako uliyofanya ni kuwaleta duniani watu wapya na uhakikishe unawatafutia maisha tangu wakiwa vijusi mpaka wanapobalehe na uhakikishe baada ya hapo wanaanza maisha yao

Kazi hii hupaswi kutegemea malipo unatakiwa kufanya kama kutoa sadaka sasa ni wewe utaamua
Hao watu ambao unasema ni watoto wako wao wataamua wakulipe fadhila ama waache

Ndiyo maana wapo watu wanaosaidiwa na watoto wao na wengine wakiwa wamegeuziwa mgongo ilihali waliwaleta wao

Mtoto akishazaliwa sio wako bali ni wa muumba na Serikali ndiyo maana mtoto uliyemzaa ana uwezo wa kukupeleka gerezani na ukafungwa kama wafungwa wengine na wapo wazazi wengi sana ambao wameshalala gerezani

Unapoingia katika familia kama wewe ni mwanaume usimnyanyase mke wako na wala mke asikunyanyase kwasababu wote mmeungana pasipo kulipwa na mtu yeyote ili mtoe sadaka ya kuwaleta watu wengine duniani pasipo kutegemea malipo kwahiyo hampaswi kunyanyasana bali unganeni ili mgawane hasara au faida mtakayopata

Kama watoto watawasaidia baadaye basi mtagawana faida na kama watawatelekeza au kushindwa basi mtagawana hasara vivyo hivyo

Kwahiyo ndoa ni kazi ya kujitoa sadaka na wala sio kufanikiwa maisha

Huu ni mdahalo wa ndoa hoja zangu ndizo hizo ukiwa na zako weka hapa watu wachangie
Ndoa ni faida Tupu mwanzo mwisho
 
Wanaume wasaizi wanaamini kuwa kama maisha yamekupiga basi njia sahihi ni kuoa ili mje msaidiane.

Hapa ndio conflict of interest inapoingia.
Hii kitu imewapa watu wengine msononeko wa moyo maana kamwe haiko hivyo.

Mwanaume ukiona maisha yamekupiga pambana hivyo hivyo. Ila sio kuweka matumaini kwa mwanamke
 
Faida ni nyingi ukifanya upembuzi yakinifu kabla kukurupuka kuoa. Ukioa msaidizi utapata msaidizi ila ukioa kwa kuangalia mat×ko utapata pia unachostahili.
Yote kwa yote mungu ndie mjuzi zaidi akimua kukufanya ujute utajuta na kama kufurahi utafurahi
 
Back
Top Bottom