nina audio ya mdahalo lakini nashindwa kuuweka
Nimependa assumption yako mkuuKiukweli kazi bado tunayo tena kubwa sana, nilikuwa njiani kurudi nyumbani nilipo chungulia JF mara moja nika kutana na hii topic, ilinibidi nisitishe safari ya kwenda nyumbani na nika pita bar ilitu niweze kutizama huo mdahalo. Wakati mdahalo unaendelea muudumu wa bar akasikikia akisema "hamna lolote nyie wezi tu na kura hampati" wakati huo alikuwa anazungumza Zitto, baada ya mda nilimuita na kumuuliza
M: kwa nini umesama hawana lolote, ni akina nani wenye lolote?
Muudumu: Chadema/CUF wote wezi tu na kura hawapati mwaka ,CCM ndio wenyewe bana
Mganyizi: Ok, Kwa hiyo mwaka huu utapigia chama gani kura na ni sababu gani zitakufanya ukipigie kura?
Muudumu: CCM kwa sababu na kipenda isitoshe viongozi wake wanapesa
Mganyizi: dah! utakipigia kura kwa sababu unakipenda na siyo kwamba kimefanya mengi ya kwa taifa hili
huoni jinsi wanavyo tumia madaraka tuliyowapa vibaya?
Muudumu: ndiyo ni kwa sababu na kipenda na Mbunge fllani (akamtaja jina ) ni bwana angu
Mganyizi: Dah hiyo kali kwa kweli, na kushauri ufikirie uhamuzi wako juu ya kura yako usiitumie vibaya kwa kuwapa watu wasiyoweza kubadilisha maisha yako kwa miaka 49 sasa...
Muudumu: sawa nitafikiria kuhusu hilo, naomba ninunulie bia Kaka...
Kwa kweli huyu muudumu amenishagaza sana kwa majibu yake, ukweli ni kwamba watanzania wengi wenye helimu ya chini na wasiyo na kipato cha kutosha wako nyuma sana kifikra na ndio type ya huyu muudumu wa bar"ni mdada mzuri kweli kweli sema hana elimu ndio maana yuko bar sehemu ambayo hakustahili kuwepo pale the way alivyo jaliwa.
.
una bahati sikufahamu n ingekulengesha kwa TAKOKURU. next time tumia nguvu ya hoja kumkabili asiyeelewa ili achukue uamuzi sahihi usitumie njia wanazotumia CCM kuwahadaa watuNimempa Tsh 10,000/= ya bia a,efurahi sana na alamia,bia atakipigia Chadema kura. nika mwambia awashawishi na waudumu wenzie wakipigie chama ambacho kinaonyesha nia ya kuleta mabadiliko kwenye chi hii.
Duh! Hii kali. Yaani ccm siku hizi naiona kama mifisi fulani hivi, au mimbweha inayohangaika kujiokoa na mitego ya waadilifu. Wana kazi kweli kweli. Mpaka wanakimbia midahalo na ubabe wao wote?!
Kiukweli kazi bado tunayo tena kubwa sana, nilikuwa njiani kurudi nyumbani nilipo chungulia JF mara moja nika kutana na hii topic, ilinibidi nisitishe safari ya kwenda nyumbani na nika pita bar ilitu niweze kutizama huo mdahalo. Wakati mdahalo unaendelea muudumu wa bar akasikikia akisema "hamna lolote nyie wezi tu na kura hampati" wakati huo alikuwa anazungumza Zitto, baada ya mda nilimuita na kumuuliza
M: kwa nini umesama hawana lolote, ni akina nani wenye lolote?
Muudumu: Chadema/CUF wote wezi tu na kura hawapati mwaka ,CCM ndio wenyewe bana
Mganyizi: Ok, Kwa hiyo mwaka huu utapigia chama gani kura na ni sababu gani zitakufanya ukipigie kura?
Muudumu: CCM kwa sababu na kipenda isitoshe viongozi wake wanapesa
Mganyizi: dah! utakipigia kura kwa sababu unakipenda na siyo kwamba kimefanya mengi ya kwa taifa hili
huoni jinsi wanavyo tumia madaraka tuliyowapa vibaya?
Muudumu: ndiyo ni kwa sababu na kipenda na Mbunge fllani (akamtaja jina ) ni bwana angu
Mganyizi: Dah hiyo kali kwa kweli, na kushauri ufikirie uhamuzi wako juu ya kura yako usiitumie vibaya kwa kuwapa watu wasiyoweza kubadilisha maisha yako kwa miaka 49 sasa...
Muudumu: sawa nitafikiria kuhusu hilo, naomba ninunulie bia Kaka...
Kwa kweli huyu muudumu amenishagaza sana kwa majibu yake, ukweli ni kwamba watanzania wengi wenye helimu ya chini na wasiyo na kipato cha kutosha wako nyuma sana kifikra na ndio type ya huyu muudumu wa bar"ni mdada mzuri kweli kweli sema hana elimu ndio maana yuko bar sehemu ambayo hakustahili kuwepo pale the way alivyo jaliwa.
Nimempa Tsh 10,000/= ya bia a,efurahi sana na alamia,bia atakipigia Chadema kura. nika mwambia awashawishi na waudumu wenzie wakipigie chama ambacho kinaonyesha nia ya kuleta mabadiliko kwenye chi hii..
Ukiona chadema wanapata kigugumizi cha kubandika mkanda ktk jf ujue wamezidiwa!!!!!
Wadau mtatiro julius amefumika mdahalo wa wagombea vijana leo movenpick,kwa kweli jamaa anatisha na ndugu mnyika ana kazi ngumu sana ubungo
Mtatiro anajulikana Manzese tu ukienda Kimara mpaka Mbezi huko hawamjui huko ni Mnyika tu mpaka Mabibo ni Mnyika tu
Punguza uongo. Mkapa alikubali kuingia mdahalo kwenye uchaguzi wa 1995 lakini ule wa 2000 aliukacha. Sasa mwaka 2000 katibu mkuu wa CCM alikuwa nani kama siyo Mangula? Hizo agenda zenu za kuwa CCM ilikuwa nzuri kabla ya kuingia Kikwete na Makamba ndiyo tunazozipiga vita hapa.
Na mie Bibi Ntilie nimekuja mjini toka kijijini (ambako hakuna umeme kwa hiyo hakuna TV) na nimeweza kuuona mdahalo wa vijana wanaowania kuchaguliwa kuwa Wabunge kutoka vyama vya CUF na CHADEMA. Naweza kudiriki kusema kwamba vijana wote (pamoja na wale walioonekana kama wazee!) wamejieleza vizuri lakini wa CHADEMA wameonekana kujieleza vizuri zaidi wakielewa nini chama chao kinasimamia na wakaeleza na kujibu kiufundi na kisomi zaidi kuliko wagombea wa CUF. Hata hivyo, waliokuwa wakipigiwa makofi zaidi ni CUF, hususan Mtatiro ambaye baadhi ya mambo aliyokuwa akieleza yalikuwa ni yaleyale ya CHADEMA lakini akayaeleza kwa namna tofauti na akapigiwa makofi hayo.
Pengine swali la kujiuliza ni kwa nini vijana wa CHADEMA - Halima Mdee, Zitto Kabwe, John Mnyika, Regina na Mrema hawakupigiwa makofi ya kutosha ingawa ndio walioeleza sera zao vizuri zaidi? Kwa nini hawakuweza kupata makofi ya nguvu hata pale walipojaribu kuwaeleza wasikilizaji jinsi wabunge wa CHADEMA wa bunge lililopita walivyofanya kazi kubwa ya kuichachafya serikali ya CCM bungeni? Yawezekana pia huenda wapiga makofi wale walikuwa ni wana CCM wenzangu ambao kwa kuwa hakuna mgombea wetu aliyejitokeza basi wakaamua ama walipangwa kuingia kwenye mdahalo kuwadhoofisha CHADEMA kwa kutowapigia makofi waliyostahili. Naambiwa eti Chama chetu CCM siku hizi hakiaminiki tena!
Lakini, upo upande mwingine wa shilingi kwamba huenda katika wakati huu tulionao wa joto la uchaguzi kupanda, kwenye kampeni ama midahalo ya aina hii wananchi wanapenda kusikia maneno ya kishabiki zaidi kuliko yale ambayo yanaweza yakawa na uzito mkubwa lakini hayagusi hisia za kishabiki!
Nawashauri vijana mnaowania kuchaguliwa mkiwa kwenye majukwaa mbalimbali muangalie aina ya wasikilizaji wenu, muwe makini mgundue haraka wasikilizaji wale wanataka kusikia nini kutoka kwenu na kwa lugha ya aina gani. Muwe tayari kubadilisha mbinu haraka pale mnapoona makofi hayawi mengi ipasavyo! Mnyika amchunge Mtatiro asijempoka tonge mdomoni.
Mtatiro anajulikana Manzese tu ukienda Kimara mpaka Mbezi huko hawamjui huko ni Mnyika tu mpaka Mabibo ni Mnyika tu
Ha ha ha hata manzese nina shaka mkuu, nilikuwa Pale tip Top kwa jamaa wauza Magodoro, yaani wao Mnyika ni kama ilivyokuwa kwa Watanzania na Jeikei wao 2005! Mtatiro ni Kijana Mpiganaji Ameogombea Ubunge akijua kabisa Hatashinda but Mnyika asishinde vile vile, ila Kwa Dar Mkuu this time wabunge wengi watashinda kwa <50%