Mdee, Gekul, Silinde, Nassari, Butiku, Bulaya, Katambi, ndio wamenifanya niamini kwamba siasa Tanzania ni kuchumia tumbo tu sio kuwatumikia wananchi

Kilichomtoa Dr Slaa pale Ufipa ni msimo wake.

Hizo habari za kusema alinunuliwa sijui mkewe alimfungia ndani ni propaganda tu.
 
Umechokoza kutaka kutuletea habari za Makonda ukapigwa spana za kutosha sasa unatafuta kupunguza maumivu
 
Huwa natamani Mdee aombe msamaha na aachane na ubunge angalau asamehewe.

Amepitia misukosuko mingi hakustahili kujikosesha heshima kwa kitu kidogo kiasi hiki
Hata akiomba msamaha hawezi kupewa heshima ambayo alikuwa anapewa.
 
Ilikuwa hujui mpaka leo hii!
 
pole kwankichelewa kulifaham hilo. wenzio tulishajua mapema before jpm.. before jk
 
Kwa hiyo, nini maoni yako
 
Kufa,umia au nenda jela kama Mdude kwaajili ya siasa za Bongo alafu mwisho wa siku mnaemfia anakuwa naibu waziri Bwana Morel au Waitara[emoji16]
 
Kilichomtoa Dr Slaa pale Ufipa ni msimo wake.

Hizo habari za kusema alinunuliwa sijui mkewe alimfungia ndani ni propaganda tu.
Kweli kabisa,msimamo wake wa kumkataa Lowasa ambae miaka yote yeye Slaa alimtanabaisha kama mmoja wa mafisadi. alafu anakaribishwa eti kwasababu kaweza kumnunua Mbowe mmiliki wa chama!,mzee wa watu akajiondokea chama kikafa kimikakati na weredi.
 
Sio hao tu,hata ingekuwa wewe ungafanya hivyihivyo
 
Tafadhali Siku zingine uache kabisa Kumfafanisha Mzee Joseph Butiku ( Jicho Kuu Kiakili la Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere katika Utawala wake wote ) na hawa 'Majuha' wengine uliowataja hapa sawa?
 
Huwa natamani Mdee aombe msamaha na aachane na ubunge angalau asamehewe.

Amepitia misukosuko mingi hakustahili kujikosesha heshima kwa kitu kidogo kiasi hiki
Yaani hata hajishtukii

Ndio kwanza anakunja 4 bungeni
 
Bora hao wana timu.

Hawa wabunge wasio na vyama katika nchi isiyo na wagombea binafsi ni kituko zaidi.
 
Unamuacha wapi mbowe ambae alihongwa na Lowassa akamtimua Slaa?

Wanasiasa wa upinzani nchi hii ni wachumia tumbo tu hawana msaada ama nia ya kutusaidia kuiondoa ccm.

Wanataka demokrasia huku wao vi wenyeviti wa maisha wa vyama vyao.

Umemaliza yote mkuu
Baada ya kuusoma mchezo na kugundua hakuna ukweli hata kwa boss wao Kina Halima wamejiongeza
 
Tumia akili hizi hizi kuhoji ccm ubora wa elimu huduma za afya kupungua kwa umaskini kuongezeka gharama ya maisha
 
Kweli kabisa,msimamo wake wa kumkataa Lowasa ambae miaka yote yeye Slaa alimtanabaisha kama mmoja wa mafisadi. alafu anakaribishwa eti kwasababu kaweza kumnunua Mbowe mmiliki wa chama!,mzee wa watu akajiondokea chama kikafa kimikakati na weredi.
Na kwa Sasa slaa Yuko na kina lowasa chama kimoja ccm.Siasa kwa kweli ni mchezo mchafu
 

Usisahau katika safari ya mamba na Kenge wapo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…