Mdee: Sina hizo bilioni 10 nilikuwa nafikisha ujumbe tu kwa Serikali

Mdee: Sina hizo bilioni 10 nilikuwa nafikisha ujumbe tu kwa Serikali

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Hoja ya mbunge wa viti Maalumu Halima Mdee kuhusu Sh10 bilioni imeendelea kutikisa katika mitandao ya kijamii wengi wakihoji alipata wapi kiasi hicho.

Hata hivyo jana Mdee alizungumzia jambo hilo na kukanusha kuwa hana kiasi hicho kwenye akaunti yake bali amesema kwa maana ya kufikisha ujumbe kwa Serikali.

“Ni kweli nilisema, lakini kwa namna nyingine watu wasingenielewa bali nilikuwa natumia njia hiyo kufikisha ujumbe kwa Serikali, hivi katika usawa huu mtu uwe na kiasi hicho si mambo yatakuwa mazuri sana, ule ulikuwa utani,” alisema Mdee akiwa nje ya ukumbi wa bunge.
 
Vijana wengi humu ni vi.laza sana! Waling'ang'ania eti Halima Mdee anazo bilioni 10!

Hawajui kabisa maana ya bilioni 10, ! Eti wanajumlisha laki 5 wanazochangiana kina Halima Mdee na wenzake ( 18) eti wamekusanya bilioni 10!

Ni hivi mtu anayepata Laki 5 kwa mwezi bila kuitumia anahitaji miaka 167 kuweza kufikisha bilioni 1.

Halima Mdee au Ester Bulaya wangekuwa hata na bilioni 1 acha 10 wasingekomalia ubunge wa viti maalumu!

Kuna Wabunge hadi leo wanadaiwa na mawakala waliowasimamia majimboni kwani baada ya kubwagwa wakakimbia !
 
Ni lopolopo sana huyu mwanamke, na anaongea kwa makelele sana.
Haya na kuropoka lukuvi anazo ilikuwaje?
 
Hivi huu nao ni mjadala, angekuwa nazo angetumia nguvu zote hizo kubaki Mjengoni jameni?.
 
“Ni kweli nilisema, lakini kwa namna nyingine watu wasingenielewa bali nilikuwa natumia njia hiyo kufikisha ujumbe kwa Serikali, hivi katika usawa huu mtu uwe na kiasi hicho si mambo yatakuwa mazuri sana,ule ulikuwa utani,” alisema Mdee akiwa nje ya ukumbi wa bunge.
I've always believed that this feminine personality is overrated.
 
Hata mlevi anaongea ukweli, pombe zikiisha kichwani anakataa,
Siamini kwa jinsi Halima yuko smat kichwani angeongea vitu kama hivyo,
Katoa siri anjistukia
 
Hivi huu nao ni mjadala, angekuwa nazo angetumia nguvu zote hizo kubaki Mjengoni jameni?.
The more you get, the more you want. Mbona kanuni rahisi sana hiyo!

It's very unfortunate if your parents failed to teach (instruct) you on this.
 
Hoja ya mbunge wa viti Maalumu Halima Mdee kuhusu Sh10 bilioni imeendelea kutikisa katika mitandao ya kijamii wengi wakihoji alipata wapi kiasi hicho.

Hata hivyo jana Mdee alizungumzia jambo hilo na kukanusha kuwa hana kiasi hicho kwenye akaunti yake bali amesema kwa maana ya kufikisha ujumbe kwa Serikali.

“Ni kweli nilisema, lakini kwa namna nyingine watu wasingenielewa bali nilikuwa natumia njia hiyo kufikisha ujumbe kwa Serikali, hivi katika usawa huu mtu uwe na kiasi hicho si mambo yatakuwa mazuri sana, ule ulikuwa utani,” alisema Mdee akiwa nje ya ukumbi wa bunge.
Utani wa pesa siyo mzuri, tubaki tu kwenye utani wa ngumi!
 
Mambo mengine tuwe tunayapotezea tu jamani,tabia zetu watanzania zinaakisi tabia za kijamaa ambazo tulirithi kutoka awamu ya kwanza na hii ipo kwenyw damu haitoki,ninachomaanisha ni kwamba hizi tabia za nongwa nongwa kwa walionazo ni tabia ambazo zinatokana na sera ya ujamaa kwamba kumiliki ukwasi ni evil either kwa wanasiasa,watumishi or anyone else!!!..Nchi za watu wanaojielewa huwezi kukuta mijadala kama hii hasa kwenye kipindi hiki ambacho Capitalism imeota mizizi mirefu sana
 
Ukielwa msemo kwamba wanawake uchumi wameukalia, huwezi kumshangaa kuwa na 10 bil.....mnaweza kutokea wote nyumba ya nyasi baada ya mwaka ukamkuta anasukuma viiieite wewe ukiendelea na sterling kiuno, hapo napo utashangaa?
 
Wewe ulipewa bil moja ili u mobilize deal.. sana sana ulibaki na mil 500, pamoja na hizi posho posho kwa sasa utakuwa na mil 600 - acha fix.
 
Back
Top Bottom