Mdogo wa Gwajima amtetea Makonda, asema Josephat apuuzwe vita ya madawa ya kulevya

Mdogo wa Gwajima amtetea Makonda, asema Josephat apuuzwe vita ya madawa ya kulevya

kwani kumuandama sana inaweza kusababisha watu wengine siku zijazo kuogopa kujihusisha kupambana na madawa.

Huu ni mwendelezo wa vibweka vya Daud bashite,watu waogope kupambana na madawa ya kulevya siku zijazo badala ya kuogopa kutumia vyeti feki siku za usoni.
 
Mfa maji haishi kutapatapa,dar es salaam itakuwa na RC mpya very soon
 
Kashapewa chake huyoo,tunataka vyeti tuu..madawa yasitumike kuhailialisha kugushi cheti
Makelele yoote cheti na wala hamjagundua kwamba hayana msaada? Eti bashite aoneshe cheti? Kwa nani? Awaoneshe cheti ili baadaye mmpe nini? Mahitaji ya kijinga yasiyotekelezeka. Na ni nani mwingine iwe kwa wema au ubaya alishaonesha cheti chake kwenye hili jukwaa ambao zaidi ya 80% ni wambeya na wakosa cha kufanya.
 
Kwa ufupi

Mdogo wake na mchungaji Josephat Gwajima wa Kanisa la ufufuo na uzima, amesema mchungaji huyo anatakiwa aache kutumika na kuhoji kuna nani nyuma yake. Amedai mchungaji hawezi kujiingiza kwenye malumbano na mipasho ya kidunia.

Ameendelea kusema vyeti vya Makonda viachiwe mamlaka husika kuchunguza kwani kumuandama sana inaweza kusababisha watu wengine siku zijazo kuogopa kujihusisha kupambana na madawa ya kulevya.

Amesema serikali imemlea sana Gwajima na waziri wa mambo ya ndani anatakiwa amuangalie na ana tuhuma nyingi ikiwemo kadai angemfufua baba wa watoto yatima ilhali yeye anajua hajawahi kufufua hata panya.

Amedai tabia ya kubeza shughuli za maendeleo zinazofanywa na serikali sio tabia njema na haiisadii nchi. Amesema anajua vita ya madawa ya kulevya ni ngumu na hugharimu maisha, atoa wito kwa watanzania wote kuunga mkoni juhudi za kutokomeza madawa ya kulevya hasa Dar es Salaam.

Amesema anafahamu yeyote atakayejitokeza kuunga mkono juhudi za kupambana na madawa ya kulevya ataandamwa tu na hivyo kwa namna ya pekee anamshukuru mkuu wa mkoa wa Dar Paulo Makonda na atakumbukwa na vizazi vyote kwa kujitoa Muhanga kusimamia vita ya madawa ya kulevya Dar es Salaam na kila mmoja amefahamu athari za madawa ya kulevya hadi kwa watoto wadogo ndio maana anaandamwa kila kona na kuhoji walikuwa wapi kuyasema yote kabla ya vita ya madawa ya kulevya.


Acheni kutuyeyusha Ukweli Mchungu kuhusu anayejiita Mdogo wa Gwajima
 
Ukiona mtu mzima analiaa mbele za watu uje kuna jamboooooooo!!!!!!
 
Ahhh!!!!! kumbe ni kadaaaaa!!! nilidhani kitu kingine kumbe kada (Hapo haitakiwi akili ya PHD) y
 
Mbona vita ya dawa za kulevya inaendelea chini ya Kamishna Siang'a,kwa utaalam na kisheria zaidi!Bashite acha kujificha nyuma ya dawa za kulevya weka vyeti mezani.
 
Alafu ona jamaa alivokuwa na wasiwasi usoni hata kuigiza ajui tafuta nyingine hii hapana
 
Duh huyu hamjuwi gwajima angekuwa anamjuwa asingeongea huo ujinga me simwamini gwajima ila kuweka ligi na gwajim lazima uwe mwendawazimu maana gwajima atamchana chana na atapotea kabisa Na bashite wake !!🙂🙂🙂🙂
 
Umepewa ngapi kaka? Madawa ya kulevya na vyeti vya kughushi vinahusiana je?
 
Kosa la kutuhumiwa kushindwa kumfufua mtu ni kosa jipya kabisa katika makosa yaliyowahi kutendwa na wanadamu,hili kosa huyo anayejiita mdogo wake Gwajima atakuwa anelidownload kwenye katiba ya chama cha mapinduzi kwa kuwa amejitambulisha kuwa yeye ni kada wa hicho chama.

Tumbo linatesa sana,ni bora utumie kiungo cha uzazi kufikiri kuliko kutumia tumbo,ukifikiri kwa kutumia tumbo utadharirika tu.Kama hao watoto wakiona wamenyimwa haki yao ya kikatiba,haki ya kufufuliwa kwa baba yao,basi waende mahakamani wafungue kesi ya madai ya kudai baba yao afufuliwe!

Hii ni kali sana,JMT inapaswa iwapeleke mbinguni mawakili na waendesha mashitaka ili wakajifunze namna ya kusimamia na kuitolea maamuzi kesi hii mpya ulimwenguni,kesi ya kutuhumiwa kushindwa kumfufua mtu.
 
Vyeti si hoja, hoja iliopo mezani ni madawa ya kulevya-tuelekeze akili zetu kwenye madawa.
Nawe usiwe kipofu na kujilazimisha kuziba maskio hoja iliyopo ni ya madawa ya kulevya na na suala la kujua jina halisi la mkuu wetu Wa mkoa ni makonda au ni bashite aweke vyeti kwanza
 
Dah! huyu ndiye ndugu yake anayemfahamu in and out " hajawaki kufufua hata panya" ila waliokutana naye bongo ndio wanajifanya kumuamini. Kamrarua ile mbaya
masikitiko yangu ni kwa hao 15 walio kupa like hadi sasa.
 
Kwa ufupi

Mdogo wake na mchungaji Josephat Gwajima wa Kanisa la ufufuo na uzima, amesema mchungaji huyo anatakiwa aache kutumika na kuhoji kuna nani nyuma yake. Amedai mchungaji hawezi kujiingiza kwenye malumbano na mipasho ya kidunia.

Ameendelea kusema vyeti vya Makonda viachiwe mamlaka husika kuchunguza kwani kumuandama sana inaweza kusababisha watu wengine siku zijazo kuogopa kujihusisha kupambana na madawa ya kulevya.

Amesema serikali imemlea sana Gwajima na waziri wa mambo ya ndani anatakiwa amuangalie na ana tuhuma nyingi ikiwemo kadai angemfufua baba wa watoto yatima ilhali yeye anajua hajawahi kufufua hata panya.

Amedai tabia ya kubeza shughuli za maendeleo zinazofanywa na serikali sio tabia njema na haiisadii nchi. Amesema anajua vita ya madawa ya kulevya ni ngumu na hugharimu maisha, atoa wito kwa watanzania wote kuunga mkoni juhudi za kutokomeza madawa ya kulevya hasa Dar es Salaam.

Amesema anafahamu yeyote atakayejitokeza kuunga mkono juhudi za kupambana na madawa ya kulevya ataandamwa tu na hivyo kwa namna ya pekee anamshukuru mkuu wa mkoa wa Dar Paulo Makonda na atakumbukwa na vizazi vyote kwa kujitoa Muhanga kusimamia vita ya madawa ya kulevya Dar es Salaam na kila mmoja amefahamu athari za madawa ya kulevya hadi kwa watoto wadogo ndio maana anaandamwa kila kona na kuhoji walikuwa wapi kuyasema yote kabla ya vita ya madawa ya kulevya.


Huyo mdogowa gwajima atambue kakayake anajitetea kwa kutajwa anatumia madawa so let him talk what he know!%
 
Back
Top Bottom