Mdude Nyagali, muungwana akivuliwa nguo huchutama

Mdude Nyagali, muungwana akivuliwa nguo huchutama

Baraka Mina

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2020
Posts
586
Reaction score
590
Wahenga walisema “Muungwana akivuliwa nguo huchutama” na “asiyefunzwa na mamaye atafunzwa na ulimwengu.“

Tarehe 01 Julai 2021 Mdude Nyagali (Mdude CHADEMA) akiwa katika kongamano la kudai katiba mpya alitoa matamshi yasiyokuwa na staha yenye kuleta ukakasi na kichefuchefu kwa kila anayeyasikia na kuyasoma ambayo yaliyomlenga moja kwa moja Rais wa JMT na Mwenyekiti wa CCM. Naomba kumnukuu Mdude; “mwambieni huyo mama yenu wembe niliotumia kumnyoa mtangulizi wake nitamnyolea yeye akileta jeuri” mwisho wa nukuu.

Ni aibu kwa kijana wa kitanzania na Chama anachotoka kutokuwa na adabu mbele ya Rais wa nchi na ambaye pia ni mama katika jamii. Pongezi kwa wachangiaji wote katika mitandao ya kijamii hapa jukwaani (Jamii Forums) na kwingineko hasa wale wa kutoka upinzani na CHADEMA walioneshwa kuchukizwa na kutokulizishwa na lugha aliyoitumika Mdude; Tunasimama kwa pamoja na kumueleza Mdude kuwa Rais kama mama anastahili heshima na anatakiwa kukosolewa kwa adabu. Mdude anatakiwa kukemewa kwa nguvu na watu wa kada na vyama vyote na wale wasio na vyama nchini. Sambamba na hilo tumkumbushe kijana huyu kuwa dunia hadaa ulimwengu shujaa.

Ni wakati sahihi wa Mdude kujitokeza mbele ya umma na kuomba radhi kutokana na matamshi yake yaliyoleta hisia mseto katika jamii kama ambavyo ameaswa/ameonywa na wanajamii. Rais wa JMT alisema tumkosee yeye na Serikali kwa lugha yenye heshima na tutoe ushauri nini kifanyike kwa sababu kila mtu ana doa.

Mdude popote ulipo kumbuka kuwa hauwezi kuacha alama kama unavyojimbanua kwa siasa za namna hii kwa sababu ganda la muwa la jana chungu kaona kivuno; wakati ukifika utatupa majibu sahihi.

Siasa inahitaji kujibu hoja kwa hoja bora zaidi na sio kuleta vitisho katika jamii.


 
Well said Brother...cha kushangaza hata viongozi wake wamekaa kimya kabisa...Pumbavu kabisa huyu kijana...ashukuru Mungu tu alimchukua Magu hata kama alikuw hana makosa ..kwa kauli hizi za kipumbavu angeendela kukaa huko jela..na ashukuru Mungu uongozi wa Samia umeingia na leo yeye yuko nje kwa juhudi za Rais Samia afu anakuja kutoa kauli ambazo hazina adabu...hapo hata Rais sijui anajisikiaje.Siasa za kipumbav kama hizi ndio huwa zinawafanya watu wawe na second thoughts abt Chadema...so immature..
 
Well said Brother...cha kushangaza hata viongozi wake wamekaa kimya kabisa...Pumbavu kabisa huyu kijana...ashukuru Mungu tu alimchukua Magu hata kama alikuw hana makosa ..kwa kauli hizi za kipumbavu angeendela kukaa huko jela..na ashukuru Mungu uongozi wa Samia umeingia na leo yeye yuko nje kwa juhudi za Rais Samia afu anakuja kutoa kauli ambazo hazina adabu...hapo hata Rais sijui anajisikiaje.Siasa za kipumbav kama hizi ndio huwa zinawafanya watu wawe na second thoughts abt Chadema...so immature..
Ndiyo Mkuu, siasa za namna hii hazina tija kwa taifa na ustawi wa jamii yetu.
Inasikitisha kuona uozo wa namna hii unakumbatiwa, vijana wa taifa hili wanatakiwa kujiandaa vema kisiasa wakiwa na hoja na sio vioja.
Mdude labda apewe kwanza ushauri kabla ya kurejea katika majukwaa ya kisiasa.
 
Samia ajitokeze kuomba radhi watanzania kwa kauli hii ya kifedhuli.

 
Magufuli alivyokuwa anatukana watanzania kuwa wabaki na mavi yao nyumbani yalikuwa ni maneno yenye staha?Kheri James alivyokuwa anatukana watu hovyohovyo yalikuwa ni maneno yenye staha?Uliwahi kukemea mambo haya?
5tfvce11.png
 
Kabla ya kuandika bandiko hili la kumshutumu huyo Mdude ulishawahi kuwaandikia viongozi was ccm waliowahi kutoa kauli zisizo na staha?

Rejea kauli za Heri James kule Arusha na kwingineko juu ya kumchoma Lissu sindano ya sumu!

Pia rejea kauli ya mh. juu ya askari was ccm kukosa shabaha! Na kauli nyingine nyingi zisizo na staha kutoka Kwa ccm. Hizo kwako zilikuwa kauli njema siyo?

Mdude hajamtaja mtu Kwa jina, ni kitu Gani kikuwashe kumhukumu Kwa utovu was nidhamu?

Neno wembe lipo kwenye nyimbo ya hamasa ya ccm iliyotungwa na tot na huimbwa na wanaccm mara nyingi. Kwanini Mdude akiutaja wembe ninyi ccm mnahamaki na kuona ukosefu was adabu?

Najua ccm mna mbinu chafu za kuchepusha dai la katiba mpya Kwa kujificha nyuma ya Mdude, hamtafanikiwa kuuzima moto wa katiba mpya kirahisi hivi. Jipangeni kwani wanakuja kina Mdude wengi mno!
 
Wahenga walisema “Muungwana akivuliwa nguo huchutama” na “asiyefunzwa na mamaye atafunzwa na ulimwengu.“

Tarehe 01 Julai 2021 Mdude Nyagali (Mdude CHADEMA) akiwa katika kongamano la kudai katiba mpya alitoa matamshi yasiyokuwa na staha yenye kuleta ukakasi na kichefuchefu kwa kila anayeyasikia na kuyasoma ambayo yaliyomlenga moja kwa moja Rais wa JMT na Mwenyekiti wa CCM. Naomba kumnukuu Mdude; “mwambieni huyo mama yenu wembe niliotumia kumnyoa mtangulizi wake nitamnyolea yeye akileta jeuri” mwisho wa nukuu.

Ni aibu kwa kijana wa kitanzania na Chama anachotoka kutokuwa na adabu mbele ya Rais wa nchi na ambaye pia ni mama katika jamii. Pongezi kwa wachangiaji wote katika mitandao ya kijamii hapa jukwaani (Jamii Forums) na kwingineko hasa wale wa kutoka upinzani na CHADEMA walioneshwa kuchukizwa na kutokulizishwa na lugha aliyoitumika Mdude; Tunasimama kwa pamoja na kumueleza Mdude kuwa Rais kama mama anastahili heshima na anatakiwa kukosolewa kwa adabu. Mdude anatakiwa kukemewa kwa nguvu na watu wa kada na vyama vyote na wale wasio na vyama nchini. Sambamba na hilo tumkumbushe kijana huyu kuwa dunia hadaa ulimwengu shujaa.

Ni wakati sahihi wa Mdude kujitokeza mbele ya umma na kuomba radhi kutokana na matamshi yake yaliyoleta hisia mseto katika jamii kama ambavyo ameaswa/ameonywa na wanajamii. Rais wa JMT alisema tumkosee yeye na Serikali kwa lugha yenye heshima na tutoe ushauri nini kifanyike kwa sababu kila mtu ana doa.

Mdude popote ulipo kumbuka kuwa hauwezi kuacha alama kama unavyojimbanua kwa siasa za namna hii kwa sababu ganda la muwa la jana chungu kaona kivuno; wakati ukifika utatupa majibu sahihi.

Siasa inahitaji kujibu hoja kwa hoja bora zaidi na sio kuleta vitisho katika jamii.


View attachment 1840961
Nini maoni yako juu ya haya maneno kutoka kwa mkuu wa wilaya.
IMG_20210704_181048.jpg
 
Mdude anahitaji counseling ya kutosha. Amepitia mengi na ya kuumiza. Lakini hiyo isiwe sababu ya yeye kutoa matamshi yasiyo na heshima na ambayo hayaleti tija. Chadema wasipokuwa serious, ita wa cost sana kauli kama hizi za Mdude. Siasa siyo matusi wala kukoseana heshima, bali ni kuelezana na kurekebishana pale penye challenges kwa manufaa ya wananchi wote. Hakuna aliyekataa kwamba Mdude amepitia mengi. Pamoja na yote hayo, isiwe sababu ya kutoa kauli zinazokosa heshima. Lazime afikiri kwanza kabla ya kutoa kauli zake. I hope kauli aliyoitoa hivi karibuni does not define him, na kama binadamu ajirudi. La sivyo naona kama trend ndiyo hii, anapoelekea itamuharibia sana.
 
Nini maoni yako juu ya haya maneno kutoka kwa mkuu wa wilaya. View attachment 1841105
Hata huyo ndugu James alivyoona hali ya hewa imebadilika alijitokeza hadharani akaomba msamaha kwa kauli zake za kujua au kutokujua. Labda nikuulize: katka utaeala huu wa awamu ya 6 ni kauli gani chafu imewahi kutolewa na viongozi ukiachana na ile ya kasesera (ambae uteuzi wake ulitenguliwa)?
 
Hata huyo ndugu James alivyoona hali ya hewa imebadilika alijitokeza hadharani akaomba msamaha kwa kauli zake za kujua au kutokujua. Labda nikuulize: katka utaeala huu wa awamu ya 6 ni kauli gani chafu imewahi kutolewa na viongozi ukiachana na ile ya kasesera (ambae uteuzi wake ulitenguliwa)?
Sasa mkuu, kusema wembe atakao aliotumia kumnyolea mzee Magu ndio atamnyolea na Samia unaona ni kauli chafu kweli? Be seriously, after all Ccm wana wimbo kabisa unasema wembe ni ule ule.
 
Mdude anapaswa ajitafakari, mbona wakosoaji wa serikali walikuwa wengi lakini yalikuwa hayawapati yaliyokuwa yanampata yeye? Wapo wengi tu kama kina Malisa, Kilewo vijana wa Chadema, hawajawahi kupata hata nusu ya madhira yaliyompata Mdude. Mdude ana tatizo, na akiendelea ataondoka "sasa hivi watadili naye kimya kimya yaani unapata maumivu ila hujui aliyekupa maumivu"
 
Mamlaka husika zinatakiwa kuchukua hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa watu wengine. Ofisi ya Rais ni taasisi.
 
Chadema hawabebeki ,ukiwabeba watakunyea kweupe.usisahau ya lisu kwamba mama ni magu wa kike.
Viongozi na wanachama wa CHADEMA wanafanya tutafakari sana juu ya uwezo wao wa kiuongozi. Jambo dogo kama hili wanashindwa kujua ni lugha gani inafaa. Wakipewa dola watatukana wananchi na kuwadharau sana.
 
Magufuli alivyokuwa anatukana watanzania kuwa wabaki na mavi yao nyumbani yalikuwa ni maneno yenye staha?Kheri James alivyokuwa anatukana watu hovyohovyo yalikuwa ni maneno yenye staha?Uliwahi kukemea mambo haya?
View attachment 1841099
Mkuu CCM imejengwa chini ya misingi ya kujisahihisha.
Soma zaidi hapa:
 
Kabla ya kuandika bandiko hili la kumshutumu huyo Mdude ulishawahi kuwaandikia viongozi was ccm waliowahi kutoa kauli zisizo na staha?
Rejea kauli za Heri James kule Arusha na kwingineko juu ya kumchoma Lissu sindano ya sumu!
Pia rejea kauli ya mh. juu ya askari was ccm kukosa shabaha! Na kauli nyingine nyingi zisizo na staha kutoka Kwa ccm. Hizo kwako zilikuwa kauli njema siyo?
Mdude hajamtaja mtu Kwa jina, ni kitu Gani kikuwashe kumhukumu Kwa utovu was nidhamu?
Neno wembe lipo kwenye nyimbo ya hamasa ya ccm iliyotungwa na tot na huimbwa na wanaccm mara nyingi. Kwanini Mdude akiutaja wembe ninyi ccm mnahamaki na kuona ukosefu was adabu?
Najua ccm mna mbinu chafu za kuchepusha dai la katiba mpya Kwa kujificha nyuma ya Mdude, hamtafanikiwa kuuzima moto wa katiba mpya kirahisi hivi. Jipangeni kwani wanakuja kina Mdude wengi mno!
Suala la Lissu Nani ni mhusika wa tukio lile?
Pia kuna utofauti mkubwa sana wa kauli hizi mbili na matukio haya.
Mhusika aliambiwa afike uchunguzi ukamilike ukweli uwekwe sio kuishtumu dola.
Ishu ya Kheei James UVCCM ilitoa ufafanuzi.
Soma zaidi hapa:
 
Back
Top Bottom