Mdude Nyagali, muungwana akivuliwa nguo huchutama

Mdude Nyagali, muungwana akivuliwa nguo huchutama

Rais siyo mama ni rais wa nchi kumuita mama ni kutuondolea moral obligation ya kukosoa na kumuonya anaposhindwa kutekeleza wajibu wake.

Rais hatuongozi kama mama anatuongoza kama rais wa nchi.

Umama usiwe kivuli cha kujificha asikosolewe.

Acheni uzwazwa
Rais alisema hana shida ya kukoselewa ila inatakiwa kukosolewa kwa staha.
Hata nyumbani mama anakosea na kuelezwa kwa nidhamu.
 
Pumbavu kabisa! Unataka uungwana wa kulamba nyayo! Shenzi!
Wahenga walisema “Muungwana akivuliwa nguo huchutama” na “asiyefunzwa na mamaye atafunzwa na ulimwengu.“

Tarehe 01 Julai 2021 Mdude Nyagali (Mdude CHADEMA) akiwa katika kongamano la kudai katiba mpya alitoa matamshi yasiyokuwa na staha yenye kuleta ukakasi na kichefuchefu kwa kila anayeyasikia na kuyasoma ambayo yaliyomlenga moja kwa moja Rais wa JMT na Mwenyekiti wa CCM. Naomba kumnukuu Mdude; “mwambieni huyo mama yenu wembe niliotumia kumnyoa mtangulizi wake nitamnyolea yeye akileta jeuri” mwisho wa nukuu.

Ni aibu kwa kijana wa kitanzania na Chama anachotoka kutokuwa na adabu mbele ya Rais wa nchi na ambaye pia ni mama katika jamii. Pongezi kwa wachangiaji wote katika mitandao ya kijamii hapa jukwaani (Jamii Forums) na kwingineko hasa wale wa kutoka upinzani na CHADEMA walioneshwa kuchukizwa na kutokulizishwa na lugha aliyoitumika Mdude; Tunasimama kwa pamoja na kumueleza Mdude kuwa Rais kama mama anastahili heshima na anatakiwa kukosolewa kwa adabu. Mdude anatakiwa kukemewa kwa nguvu na watu wa kada na vyama vyote na wale wasio na vyama nchini. Sambamba na hilo tumkumbushe kijana huyu kuwa dunia hadaa ulimwengu shujaa.

Ni wakati sahihi wa Mdude kujitokeza mbele ya umma na kuomba radhi kutokana na matamshi yake yaliyoleta hisia mseto katika jamii kama ambavyo ameaswa/ameonywa na wanajamii. Rais wa JMT alisema tumkosee yeye na Serikali kwa lugha yenye heshima na tutoe ushauri nini kifanyike kwa sababu kila mtu ana doa.

Mdude popote ulipo kumbuka kuwa hauwezi kuacha alama kama unavyojimbanua kwa siasa za namna hii kwa sababu ganda la muwa la jana chungu kaona kivuno; wakati ukifika utatupa majibu sahihi.

Siasa inahitaji kujibu hoja kwa hoja bora zaidi na sio kuleta vitisho katika jamii.


View attachment 1840961
 
Kwani huyo Mdude aliwahi kumnyoa nani na kwa uwezo wa wembe gani zaidi ya yeye kunyolewa? Laiti kungekuwa na duka la kununua busara huyu angenunuliwa japo kijiko kidogo. Apuuzwe tu.
Analeta ujuaji tu lakini Hana lolote zaidi ya kukosa nidhamu.
 
Wajinga ndio maana wanaumia sana kwa sababu ya kujiona kwao mashujaa.

Wenzao wajanja akina mbowe hayawakuti kwa sababu wanaenda kwa timing saana wanaepukana na mateso makali yanayotokana na matokeo ya vinywa vyao.
MDUDE CHADEMA likija kumuangikia ataona.
 
Wanaompa PLATFORM ya kuongea huo upuuzi ni wapuuzi.
Huyu dogo anapaswa kukaa chini na kutulia, ataumizwa
Wanataka kumpa nafasi kuonekana kama mshindi wa Chama. Lakini kijana Hana hoja.
 
Kabla ya kuandika bandiko hili la kumshutumu huyo Mdude ulishawahi kuwaandikia viongozi was ccm waliowahi kutoa kauli zisizo na staha?
Rejea kauli za Heri James kule Arusha na kwingineko juu ya kumchoma Lissu sindano ya sumu!
Pia rejea kauli ya mh. juu ya askari was ccm kukosa shabaha! Na kauli nyingine nyingi zisizo na staha kutoka Kwa ccm. Hizo kwako zilikuwa kauli njema siyo?
Mdude hajamtaja mtu Kwa jina, ni kitu Gani kikuwashe kumhukumu Kwa utovu was nidhamu?
Neno wembe lipo kwenye nyimbo ya hamasa ya ccm iliyotungwa na tot na huimbwa na wanaccm mara nyingi. Kwanini Mdude akiutaja wembe ninyi ccm mnahamaki na kuona ukosefu was adabu?
Najua ccm mna mbinu chafu za kuchepusha dai la katiba mpya Kwa kujificha nyuma ya Mdude, hamtafanikiwa kuuzima moto wa katiba mpya kirahisi hivi. Jipangeni kwani wanakuja kina Mdude wengi mno!
huwa nasema chadema wengi wao ni mapimbi.Huwezi kumsema vibaya rais kwa staili hii.
unaposema wembe uliyotumia kwa mtu ambaye na marehemu tukisema wewe ndiye uliyemuua tutakuwa tumekosea?

Huyo mama Yenu::: kwa lugha nyengine wewe siyo mama yako,hivyo wewe ni mtoto haramu

utamnyoa ::unaweza kumnyoa mama yako ??

by the way ,huyu jamaa ni kabila gani?
 
huwa nasema chadema wengi wao ni mapimbi.Huwezi kumsema vibaya rais kwa staili hii.
unaposema wembe uliyotumia kwa mtu ambaye na marehemu tukisema wewe ndiye uliyemuua tutakuwa tumekosea?

Huyo mama Yenu::: kwa lugha nyengine wewe siyo mama yako,hivyo wewe ni mtoto haramu

utamnyoa ::unaweza kumnyoa mama yako ??

by the way ,huyu jamaa ni kabila gani?
CHADEMA wazinguaji sana eti kijana anaonekana anajua. Analeta siasa za majitaka.
Inaonekana hajalelewa vizuri kijamii na kisiasa. Ni shida sana kuona kijana kama huyu alisema anataka kuwa rais 2045.
 
Rais alisema hana shida ya kukoselewa ila inatakiwa kukosolewa kwa staha.
Hata nyumbani mama anakosea na kuelezwa kwa nidhamu.
Wakosoaji anataka awapangie namna ya kukosoa ?

Mtu anakosoa utashi wake siyo kwa utashi wa anayekosolewa

Kama hamtaki akosolewe mwondoeni kwenye kiti cha urais ili asikosolewe.
 
Uungwana wa kujibu hoja kwa hoja na siyo hoja kwa matusi.
Shindana kwa kuleta hoja bora.
Tusi nalo ni hoja kwa wapumbavu! Wananchi wote nchi hii ni sawa hakuna cha Rais wala mtwana! Rais na mtwana wataheshimika kwa matendo yao na si nafasi zao katika jamii!
 
Mdude anapaswa ajitafakari, mbona wakosoaji wa serikali walikuwa wengi lakini yalikuwa hayawapati yaliyokuwa yanampata yeye? Wapo wengi tu kama kina Malisa, Kilewo vijana wa Chadema, hawajawahi kupata hata nusu ya madhira yaliyompata Mdude. Mdude ana tatizo, na akiendelea ataondoka "sasa hivi watadili naye kimya kimya yaani unapata maumivu ila hujui aliyekupa maumivu"
Haisaidii !!. Aliyedili na kuwaumiza watu yuko wapi sasa ?!.
 
Wahenga walisema “Muungwana akivuliwa nguo huchutama” na “asiyefunzwa na mamaye atafunzwa na ulimwengu.“

Tarehe 01 Julai 2021 Mdude Nyagali (Mdude CHADEMA) akiwa katika kongamano la kudai katiba mpya alitoa matamshi yasiyokuwa na staha yenye kuleta ukakasi na kichefuchefu kwa kila anayeyasikia na kuyasoma ambayo yaliyomlenga moja kwa moja Rais wa JMT na Mwenyekiti wa CCM. Naomba kumnukuu Mdude; “mwambieni huyo mama yenu wembe niliotumia kumnyoa mtangulizi wake nitamnyolea yeye akileta jeuri” mwisho wa nukuu.

Ni aibu kwa kijana wa kitanzania na Chama anachotoka kutokuwa na adabu mbele ya Rais wa nchi na ambaye pia ni mama katika jamii. Pongezi kwa wachangiaji wote katika mitandao ya kijamii hapa jukwaani (Jamii Forums) na kwingineko hasa wale wa kutoka upinzani na CHADEMA walioneshwa kuchukizwa na kutokulizishwa na lugha aliyoitumika Mdude; Tunasimama kwa pamoja na kumueleza Mdude kuwa Rais kama mama anastahili heshima na anatakiwa kukosolewa kwa adabu. Mdude anatakiwa kukemewa kwa nguvu na watu wa kada na vyama vyote na wale wasio na vyama nchini. Sambamba na hilo tumkumbushe kijana huyu kuwa dunia hadaa ulimwengu shujaa.

Ni wakati sahihi wa Mdude kujitokeza mbele ya umma na kuomba radhi kutokana na matamshi yake yaliyoleta hisia mseto katika jamii kama ambavyo ameaswa/ameonywa na wanajamii. Rais wa JMT alisema tumkosee yeye na Serikali kwa lugha yenye heshima na tutoe ushauri nini kifanyike kwa sababu kila mtu ana doa.

Mdude popote ulipo kumbuka kuwa hauwezi kuacha alama kama unavyojimbanua kwa siasa za namna hii kwa sababu ganda la muwa la jana chungu kaona kivuno; wakati ukifika utatupa majibu sahihi.

Siasa inahitaji kujibu hoja kwa hoja bora zaidi na sio kuleta vitisho katika jamii.


View attachment 1840961
Thread ya kipumbavu kabisa! Nothing more nothing less!
 
Mdude anapaswa ajitafakari, mbona wakosoaji wa serikali walikuwa wengi lakini yalikuwa hayawapati yaliyokuwa yanampata yeye? Wapo wengi tu kama kina Malisa, Kilewo vijana wa Chadema, hawajawahi kupata hata nusu ya madhira yaliyompata Mdude. Mdude ana tatizo, na akiendelea ataondoka "sasa hivi watadili naye kimya kimya yaani unapata maumivu ila hujui aliyekupa maumivu"
Stick to the point and quit being a moron! Mtu akimtukana mwizi ni kosa kwasababu tu mwizi hajafikishwa mahakamani?

On the other hand, hakuna kosa lolote alilofanya mdude kwenye kauli zake.
 
Kitakachoonyesha kuwa ni matusi au siyo matusi ni katiba.Kwani katiba inasemaje?
Sie wananchi tuliyo wengi hatuna kabisa uelewa na katiba, sasa ukiniuliza habari za katiba unakuwa unanipa mtihani labda hiyo katiba mpya ndio tutaielewa.
 
Stick to the point and quit being a moron! Mtu akimtukana mwizi ni kosa kwasababu tu mwizi hajafikishwa mahakamani?

On the other hand, hakuna kosa lolote alilofanya mdude kwenye kauli zake.
Kwani Mdude na Rais Samia hawaelewani? maana sijaelewa sababu ya kutumika kauli kama ile ya "huyo mama yenu..." katika hali ya kawaida kwa mtu ambaye huna tatizo nae.
 
Wakosoaji anataka awapangie namna ya kukosoa ?

Mtu anakosoa utashi wake siyo kwa utashi wa anayekosolewa

Kama hamtaki akosolewe mwondoeni kwenye kiti cha urais ili asikosolewe.
Ukosoaji lazima uwe na hoja na sio maneno yenye uhuni. Tujifunze vizuri siasa za ukosoaji zikoje.
 
Tusi nalo ni hoja kwa wapumbavu! Wananchi wote nchi hii ni sawa hakuna cha Rais wala mtwana! Rais na mtwana wataheshimika kwa matendo yao na si nafasi zao katika jamii!
Ni kweli suala la heshima sio tu kwa Rais bali na wanajamii kwa sababu ada ya mja hunena muungwana ni kitendo. Mtu mwema katika jamii tunamtambua kwa matendo yake lakini domokaya kwa maneno matupu yenye kejeli.
 
Back
Top Bottom