Mechi ya Taifa Stars na Uganda yasimama kwa muda kutokana na taa za uwanjani kupungua mwanga. Taa ziliwaka ikaendelea

Mechi ya Taifa Stars na Uganda yasimama kwa muda kutokana na taa za uwanjani kupungua mwanga. Taa ziliwaka ikaendelea

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Mechi ya Taifa Stars na Uganda yasimama kwa muda kutokana na taa za uwanjani kupungua mwanga, mwamuzi wa mchezo amesimamisha mechi akifanya mawasiliano na meneja wa mchezo kuona ni mamuzi gani yafanyike.

====

Sasisho: Taa zilizokuwa zimepoteza mwanga zimewaka na mchezo unaendelea ili kukamilisha kipindi cha kwanza.

1680028036218.png
 
Tukienda tu kwa kubembelezana kama ilivyo kwa Waziri wa Nishati! Iko siku tutapata bonge la Aibu zaidi ya hili la umeme kuwa mdogo kwenye uwanja wa Mkapa mechi ya kimataifa ya Tanzania na Uganda!

Halafu sijui ni kwa nini huwa inakuwa hivi!

Kila mtu aliyewahi kulalamikiwa sana na wananchi kwenye tawala hizi, mtu huyo huja kuwa sababu ya serikali kufeli vibaya na kuwa ya hovyo hovyo tu

Nchi nzima kwani imekosa watu makini hadi iwe yuleyule tu aliyefeli hata kabla ya kuanza?

Hivi majuzi kwenye ziara ya Rais kabisa kule Arusha! Umeme ulikatika mbele yake na bado mh Januar Makamba bado aliendelea kuwa waziri

Mfano

Makonda!
 
Ni aibu aisee uko duniani mechi za usiku ni Tamuu kuangalia uwanja safi,mwanga wa kutosha unaweza sema ni mchana huku kwetu sasa TV haiwaki,Mataa yanasinzia sasa iyo VAR itaweza kuendeshwa kweli?

Uwanja upumue
 
Sijui meneja wa uwanja wa Taifa huwa anakazi gani km kila siku kunakuwa na mapungufu.Mara vyoo vichafu, mara pitch kuharibika, mara viti vimeng'olewa, leo baadhi ya taa zimegoma kuwaka. Kama hatuwezi kuuendesha uwanja basi tuwarudishe wachina wauendeshe kuliko kutia aibu namna hii. Huge disappointment!
 
Back
Top Bottom