Media ni Mhimili Muhimu kama ile mitatu ila ni dhaifu kiuchumi. Je, imefika wakati wapewe Ruzuku au iachwe ipambane na hali yake?

Yaan waandishi wa habari wamekuwa hovyo haswa...
 
Ruzuku wapewe JF tu

Hiki ni Kisima cha Habari za Dunia nzima kwa kila dakika inayokatika

Vyombo vingine wanasubiri teuzi tu lakini JF Akina Lucas, Mzee Mgaya, Erythrocyte nk wao wako kizalendo zaidi 😂😂
100%
Vilivyobaki viko mfùkoni mwa sisiemu
 
Wakati nasoma hii makala nikawa natafuta ni wapi ungesema hela zipelekwe. Ninachoona hakuna center zaidi ya RTD na TBC. Kwanza hii taasisi hata hivyo inaendeshwa kwa kodi zetu ambapo ni ruzuku tosha. Sasa hapa utatengeneza mtafaruku mkubwa sana wa kimaslahi kwani media imegawanyika sana japo lengo lake ni moja. Hapo itabidi tena iundwe mamlaka ya kusimamia media (au ndio MCT?). Hata ikiwepo hiyo mamlaka ni wazi kwamba focus itaondoka. Kwa hili ibaki tu kusema media tunawapenda ila kwa ishu ya ruzuku, no!
 
BBC ni chombo cha umma, Kama serikali ikiiga utaratibu wa UK ni wazi pesa hizo zitaenda TBC.
Pia iwapo serikali ikianza kutoa ruzuku kwa vyombo vya habari ni wazi ile sifa ya Muhimbili usio rasmi itapotea mifano halisi tunayo.
Wakati vuguvugu la vyama vingi linaanza vyombo vya habari binafsi vilifanya kazi kubwa kufichua maovu magazeti Kama Family mirror, motomoto hata wewe mwenyewe ulikuwa na kipindi kinaitwa kitimoto ingawa ungekuwa nacho Hadi Sasa ingebidi ubadilishe jina.
Hata baba wa Taifa aliwahi kusifia vyombo vya habari vinafanya kazi nzuri kuliko vyama vya siasa.
Sasa hivi vyombo karibia vyote vimepoteza uhuru na vimebaki na kazi ya kusifia. Hata humu ukiandika habari inayogusa viongozi wa serikali hata Kama una ushahidi itaondolewa. Kuwalipa itakuwa matumizi mabaya ya Kodi za wananchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…