Media za Bongo na muendelezo wa Copy & Paste

Kwenye vipindi Clouds ni wabunifu
Kwenye studio set up wasafi ni wabunifu.
Wote set up sasahivi wanaizingatia kutokana na urushaji wa matangazo Online, Kwa Tanzania Redio yenye set up nzuri kwangu mimi ni Lake fm iko Mwanza, kwa Africa Mashariki hakuna wakumfikia NRG Radio Nairobi
 
Radio karibia zote isipokuwa radio one,zilizobak zinaiga kwa clouds fm kwasasa karibia radio zote zna kipind knachofanana na Leo tena
 
Wasafi wana kipindi chaitwa story book, haya tuambie wameiba wapi?

Nafikiri ifike mahali angalau ungechambua kipindi hata kimoja ili uone tofauti na ubunifu uliopo si kuorodhesha vingi ili uonekane mchambuzi mzuri.

Nikupe mfano, kuna segment kwenye block 89 inaitwa group admin, haya niambie inafananaje na segment iliyopo XXL kuanzia jina na content wise?

Hizi kelele tumshazisikia mtaani na kwa washabiki, wewe usipoleta upembuzi makini tutakuona wale wale.
 
Jina linakuwa tofauti ila Maudhui ni yale yale, Mkasi na Bar Tender tofauti ni Location tu na baadhi ya vitu ila Idea ni ile ile
Huo unaoita utofauti ndio ubunifu wenyewe sasa.

Huku kwenye Bar tender mtangazaji ndo muhudumu ama mtoa huduma kule kwenye Mkasi mtangazaji ni mtangazi tu, muhudumu ni mtu mwingine.

Tafsiri ya copy and paste maana yake kitu ni kile kile kwa asilimia nyingi huku vitu ni tofauti na utofauti ndo ubunifu elewa hilo.
 
Tatizo la kukaa kwa shemeji ndio hilo, we kutwa unamind vipindi vya TV tu. Tafuta kazi ya kufanya mkuu, katembeze hata kimachinga.
 
Ukishakuwa umetengeneza kundi la Misukule wewe unakuwa mungu kabisa yaani MR PERFECT hukosei.

Kila Upuuzi Utakaofanya UTAHALALISHWA.

Ukiimba MATUSI utaambiwa SIMBAA hivyo ndio mashabiki wanataka ngoma zinazotrend.

Ukizalilisha Wanawake Huku Unazalisha Huko Huko Kama Nzige, Utaambiwa, Simbaaa Kwani Kwani Kuna Kosa Gani ? Nani Hazini.

Ukianza Kukopi Na Kuimba Nyimbo Za Watu Kama Chatu Mandota Na Mkali Wenu, Wanakwambia Huyo Ndo Simba Kwani Kuna Jipya Gani Duniani ? Kukopi Kawaida Tu !

Ndivyo Ilivyo !

Wanaoabudiwa Huwakosei Mbele Ya Macho Ya Wafuasi Wao!
 
Radio karibia zote isipokuwa radio one,zilizobak zinaiga kwa clouds fm kwasasa karibia radio zote zna kipind knachofanana na Leo tena
nchi nzima, mode ya kipindi cha Leo Tena iko kwenye Redio nyingi
 
The Story book ni Idea wengi wameijua baada ya kwenda hewani, ila wengi sana wanafanya kitu cha namna hiyo nenda You tube huko
mfano mmoja ni huo

Group Admin hiyo idea ilikuwa inafanyika KISS FM kwenye kipindi cha Kiss collabo, kuna vitu vinaletwa hapo vilishafanyika sehemu nyingine ila watu hawakuvijua kwa sababu redio ziko mikoani, Huyo Callipso kuna Idea nyingi kazileta hapo kazitoa sehemu alizoanzia kazi, mtu mwingine anaeleta vitu hapo Ni Mbaba VC (Timotheo Ngalula) ni vitu ambavyo walifanya muda mrefu
 
kweli kabisa
 
Hamtaki kusikia wala kuambiwa ukweli
 
Hahahha hapo kweli kabisa, alianza Zanana na Mak Juice...ila sahizi mji umechafuka vibanda vya kuuza Juice. Kila mtu anafungua lake ndio kaliba ya watanzania πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚!!!

Mtu kuumiza kichwa hataki anachungulia alipowin mwenzie nae anatambaa na chaki!
 
Mafanikio yapi unayoyazungumzia?
Hata kama wamekopi lakini wameboresha na wana identity yao kuliko hao wasafi
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unataka kusema kama kwenye chumba cha mtihani wasafi kakopi majibu yote mpk jina yaani kaokoa muda hajashughulisha ubongo ?
Miaka inavyoenda redio zitakuwa hazina umuhimu kabisa ,kuna itaji ubunifu sana ili redio ziendelee kuwapo.

Ss km mtu ana C&P mtihani majibu mpk jina ndio kufeli huko.
 
Miaka inavyoenda redio zitakuwa hazina umuhimu kabisa ,kuna itaji ubunifu sana ili redio ziendelee kuwapo.

Ss km mtu ana C&P mtihani majibu mpk jina ndio kufeli huko.
redio haziwezi kuishiwa Umuhimu, sema zitashindwa kujiendesha kibiashara kwa kukosa ubunifu
 
Miaka inavyoenda redio zitakuwa hazina umuhimu kabisa ,kuna itaji ubunifu sana ili redio ziendelee kuwapo.

Ss km mtu ana C&P mtihani majibu mpk jina ndio kufeli huko.
Hii pia ni kutokana na watu ulionao katika taasisi kama hawashughurishi vichwa mambo ndio huwa hivo, redio ikikosa matangazo atafutwe mchawi ni nani.
 
Hahahah watu wanashindwa kuiga frequency tu
 
redio haziwezi kuishiwa Umuhimu, sema zitashindwa kujiendesha kibiashara kwa kukosa ubunifu
Ukishaishiwa kibiashara ndio kufilisika kwenyewe,kama matumizi ya internet yatazidi kukua online Tv ndio zitakuwa na soko.
Kitu kingine ni kwamba vipindi vingi havina content za kibunifu kama MTU unafuatilia sana mitandao unaweza ukawa unapata taarifa na burudani zote hakuna aja ya redio .

Ninachokiona watangazaji wanaokoteza okoteza taarifa za mitandaoni ndio wanatangaza hawajitumi,kuandaa vipindi vya kibunifu .

Mwambieni CEO wa wasafi anione nimpe idea za vipindi vya kibunifu sio C&P.
 
Kwa ukuaji wa Teknolojia TV ndio zimekosa soko, matangazo mengi ya TV yamekimbilia Online televisheni kwenye viewers wengi na gharama ndogo, TV station matangazo yana gharama kubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…