Meli ya thamani inateketea, wanamsaliti Nyerere

Time will tell
Mbaya zaidi nahodha hajui kusoma dira🙄
 
Wakumlaumu ni huyo huyo Nyerere. Alikuwa na kiherehere cha kuongoza kabla ya nchi kuwa tayari. Matatizo mnayoyaona sasa hivi ni matunda ya kujitawala kabla hatujawa tayari.
Naunga mkono hoja.huyo nyerere ndo chanzo matatizo haya
 
Sawa hongera sana Kalamu1 kwa kuwa mtanzania msomi mwenye akili kubwa ya ugunduzi. Japo sijajua ulichogundua
Nadhani huelewi ninachokieleza mkuu Stuxnet, na pengine siyo kosa lako.
Tuachane na mchango nilioweka katika nyanja yangu ya kitaaluma, kwa sababu hiyo siyo hoja hata kidogo katika mjadala kati yangu na wewe.

Turudi kwenye yale uliyoandika wewe huko mwanzo, yaliyonisikitisha na kunisononesha moyo kujuwa kwamba hadi hii leo bado kuna waTanzania wenye aina ile ya mawazo?
Hapana, huenda unatania, ni kawaida ya watu kuja hapa JF na kujifurahisha tu kwa kuweka michango ya ajabu ajabu sana wakijuwa kwamba itaamsha mizozo. Hiyo ndiyo furaha yao.

Kiufupi nikuulize: Hivi Tanzania hatutaweza kuendelea bila sisi wenyewe kugundua vitu vyetu vya kipekee ambavyo itabidi ndivyo vituletee maendeleo?

Hivi hatuwezi kuwa na mahospitali mazuri yenye kutoa huduma nzuri kwa wananchi wetu bila ya sisi kugundua yote yanayohitajika kwenye mahospitali hayo?

Hivi wakulima wetu huko vijijini haiwezekani kabisa tukawasaidia wakawa na kilimo kinacholeta tija hadi tugundue mahitaji yote yanayotakiwa kuwasaidia katika kazi zao za kila siku?

Ninaweza kuendelea kukuuliza maswali ya namna hiyo hiyo katika nyanja zote na sekta zote tunazozitegemea kuzitumia kuiletea maendeleo nchi yetu.

Maana yako ni kwamba, maadam hatujagundua chochote, na pengine hatuwezi kutumia kilichogunduliwa na wengine (na siyo lazima wawe ni wazungu), basi hatutaweza kupata maendeleo?

Ngoja nimalize haraka kabla sijaandika gazeti hapa kwa haya yafuatayo.

Hapa tulipofikia sasa hivi kama waTanzania, kitu pekee tunachokosa ili tuweze kuibadilisha Tanzania ni uongozi tu; uongozi ambao hauna dira nchi yetu inapaswa kwenda wapi. Tunao wasomi wa kutosha kabisa ambao kama wanaweza kupangwa vyama na kupewa nyanja za kufanya kazi zao na mipango madhubuti ikawepo, hawa watu tulionao sasa hivi wanatosha kabisa kuleta mabadiliko makubwa sana katika kila nyanja.
Kwa bahati mbaya sana, hatuwatumii ipasavyo, kwa kuwanyima fursa ya kutumia elimu yao kuifaidisha nchi hii.

Leo hii watawala wakisema tunataka tuwatumie watu wetu (wataalam) tulionao na tusimamie kilimo chetu barabara, kilimo chetu kitakuwa ni tofauti na kilivyo sasa.
Leo hii serikali wakisema tunaweka mkakati wa kuwatumia wataalam wetu wa madawa tulio nao tuimarishe ujuzi wetu na uzalishaji katika eneo hilo, na kusimamia kazi hiyo, hali ya uzalishaji wa madawa nchini utakuwa ni tofauti kabisa na ilivyo sasa.
Na usije ukafikiri nahimiza serikali ifanye kila kitu, bila kushirikisha sekta binafsi, hapana; lakini huo ni mjadala mwingine. Kinachotakiwa ni serikali kuweka mikakati, na kuisimamia mipango inayohusika.

India, China, Korea (zote mbili), Vietnam, na nchi nyingi tu nyingine, wamelazimika kuwaleta wazungu na elimu yao kufanya waliyofanya walipoamua kufanya? India wakatengeneza bomu la nuclear, na sasa mambo mengi mengine.

Basi bhwanah, kama hatuelewani, hatuwezi tukaelewana hata nikiandika kitabu.

Nimetiririka tu, sikurudi nyuma kusahihisha. Kama utaona makosa ya kiuandishi, juwa sikusahihisha.
 
Tuna mali lkn hatuna teknolojia hyo ndyo laa a pekee inatutesa waafrika hata atawale nan tutaishia propaganda tu hakuna kinachoweza kubadilika bila mkono wa mzungu
Teknolojia ya namna gani mkuu?

Hata hii ya kuzalisha mbegu bora kwa wakulima wetu ili waweze kupata tija katika kilimo chao, hatuna?

Teknologia ya namna gani, hata ya kutengeneza vidonge na kapsules ili wananchi wetu wapate dawa muhimu?

Teknologia gani, ya kuwafundisha vijana wetu mashuleni ili wapate elimu bora ya kujuwa teknologia iliyopo sasa na ijayo waweze kuitumia ipasavyo?
Haya na mengi mengine kweli kwa wakati huu hatuwezi kuyafanya sisi wenyewe?

Sikubaliani kamwe na dhana hii.

Tunachokosa ni uongozi wa kutupanga na kutumia vyema tuliyonayo sasa hivi ili yalete maendeleo.
Tunahitaji teknologia gani ili tuweze kujenga vyoo safi na imara vya mashimo huko vijijini?
 
Mkuu umenena ipasavyo kunenwa juu ya watawala heshima kwako mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…